NYENJENKURU
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 1,067
- 299
Enzi hizo FOE mwaka wa pili na wanafanya mashambulizi kwa Ngwini..hasa wala wa ME baada ya kupewa michoro migumu ya ME 202..
Exactly mkuu ila nadhani Oldonyo ilikithiri zaidi, kuna wakati zile cubics za mwishoni kabisa (kama unakumbuka Oldonyo haina partitions kama Meru, Mawenzi, Kibo au Hanang) watemi walizigeuza zikawa kama gym vile.
Huko ni mwendo wa kuwasha bangi na kupiga chuma (makopo ya zege).
Mabweni yaliyokithiri kwa bangi Ilboru yalikuwa Meru na Oldonyo. Ilikuwa ukipangiwa kuishi ktk mabweni haya ni sawa na jehanam.
Yaah! Nilishi Oldonyo O-level. Ilikuwa inaitwa wodi kwa sababu hakukuwa na partion. Cubics zilikuwa ni store za bangi na hakuna alikuwa anasuruhusiwa kuingia mle except wavutaji tu. Form one unaweza kuingia mle kama walikutuma kuwachukulia maji ya moto kwa mzee Alfayo (jikoni) short of that utaumia. Anyway, maisha ni magumu katikal evel ya ordinary. Too much bulling. Yale mavuta bangi mengi yanafeligi mitahani ya mwisho, sijui yanaendaga wapi baada ya hapo na bangi zao.
huyu jamaa mwandishi kakosea jina tu, alikua anaitwa Omary Sarota ni mwenyeji wa Mara, kwao ni Musoma mjini sehemu inaitwa Kamunyonge ..
Nakubaliana na wewe. Damu ya mwanadamu haipotei bure. Ndio maana nimeomba wanaomjua huyo Sarota waweke picha yake hapa jamviniInasikitisha sana, naamini waliosababisha hilo inawahaunt na they will take this kaburini.
Maskini Levina, l hope Mungu kamsamehe makosa yake na amepumzika kwa amani.
Mwenye picha ya huyu Sarota aianike hapa.
Nataka kuweka bounty on his head................
Picha ya Omary Sarota kwa sasa kuipata ni shida...alikua bonge la braza man kipindi hicho,nafikiri sasa hivi atakua mtu mzima sana maana mimi nilisoma na mdogo wake shule moja pale musoma mjini ambae pia kwangu ni mkubwa ..sarota kwa sasa atakua kwenye late fifties au early sixties siko sure sana na hilo ila nina uhakika atakua yuko huko kwao kamunyonge, musoma mjini.
Mama yangu! Nashukuru bado nilikuwa ni mdogo kipindi hicho labda na miye yangenikuta
oldonyo mkuu oldonyoo............na rungwe wacha kabisa...........
Mkuu EMT nashukuru kuni copy memo yako juu ya kifo cha huyu dada Lavina Mukasa.Inasikitisha sana, hao punch nadhani nafsi inawasuta sasa
Rest in peace levina
Walaaniwe maisha,R.I.P dada Levina hii thread imenisikitisha na kunisononesha sana,wahusika wa PUNCH bado wako hai kweli?
Mbona mimi nakumbuka kama huyu alijirusha ghorofani? Ilitangazwa kwenye vyombo vya habari enzi zile ni radio tanzania.
Vile vile ilikuwa ni hot issue na kulikuwa na discussion kwenye magazeti (sina uhakika kama ni lile la mfanyakazi) kuhusu role ya punch pale chuo kikuu.
Kwa kweli hili tukio lilishtua watu wengi miaka ile na ilionyesha jinsi gani wanawake walikuwa wanadhalilishwa pale chuoni.
Wale vijana waliosababisha hiyo walifanywa nini, au waliachiwa kuendelea na degree zao bila zahama?
Tena enzi hizo nauli ya daladala kwa mwanafunzi ilikua shilingi moja basi makonda walitunyanyasaje wanafunzi, lkn wanafunzi wa tambaza walikua wanawapa kichapo makonda acha tu. kuna jina lilikua linavuma kama nakumbuka ni PUZA or something like that huyo alikua tishio.