Kwanini Canaan alilaaniwa na sio Ham?!

Mkuu zitto junior ili uweze kuelewa ni kwanini Nuhu alimlaani Caanan na siyo Ham aliyetenda kosa, kwanza unatakiwa ulielewa na kuliamini NENO la MUNGU. Ili ulielewe NENO la MUNGU, kwanza lazima uliamini. Binadamu hatuwezi kumwelewa MUNGU, lakini tunaweza kulielewa NENO lake ambalo ametupa ili litusaidie katika maisha ya sasa na yale yajayo.

Tatizo linakuja pale ambapo watu walio wengi hawataki kuielewa Biblia wala kuiamini, wengi wanaona kile kilichoandikwa kwenye Biblia ni kama hadithi tu, ni kama porojo tu ambazo hazina maana. Ukweli ni kwamba, Biblia ni zaidi ya hadithi, ni zaidi ya Historia, na ni zaidi ya Unabii ambao umekuwa ukitimia kila siku. Kwa kulitambua hili, mimi nitakupa majibu ya Kibiblia ni kwanini Nuhu alimlaani Caanani badala ya Ham. Majibu yote yapo ndani ya Biblia na nje ya Biblia huwezi kupata majibu.

Iko hivi; zamani zile Wazazi hasa baba walikuwa wanatoa baraka au laana kwa kizazi cha watoto wao na siyo kwa mtu mmoja peke yake. Kama ni baraka, baba alikuwa anatoa baraka hizi kwa watoto wake wa kiume na vizazi vyao vyote vinavyofuata kwa sababu walikuwa wanaamini kuwa kizazi hakiishii kwa watoto, bali kinaendelea na kuendelea. Pia huu ndiyo ulikuwa utaratibu waliojifunza kutoka kwa BWANA MUNGU, pale alipotoa laana ya kwanza kwa mwanadamu na nyoka;

"nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa na wewe utamponda kisigino". MWANZO 3:15

Hapo juu utaona hiyo laana siyo kwa Eva na nyoka peke yao, bali ni kwa uzao wao wote utakaotokea duniani. Hii inaonekana kuwa wazee wale wa kale walijifunza pia kutoa laana au baraka kwa kizazi na kizazi. Hebu tuone baraka ya Isaka kwa Yakobo.

"Mataifa na wakutumikie, na makabila wakusujudie. Uwe bwana wa ndugu zako, na wana wa mama yako na wakusujudie. Atakaye kulaani, alaaniwe na atakayekubariki, abarikiwe". MWANZO 27:29

Hapa pia utaona Yakobo anabarikiwa na baba yake, tena siyo baraka kwa ajili yake tu katika maisha yake yeye kama Yakobo, bali ni kwa ajili yake na uzao wake wote utakaofuatia baada yake. Hivi ndivyo ilivyokuwa, hivi ndivyo wanadamu walijifunza kutoa baraka kwa wana wao au laana. Pia unaweza ukasoma kitabu hicho cha MWANZO sura ya 49, na utaona jinsi ambavyo na yeye Yakobo alivyotoa baraka kwa watoto wake 12.

Tukirudi upande wa BWANA MUNGU, pia tutaona jinsi alivyombariki mzee Ibrahimu, hakumbariki yeye tu kwa wakati ule, bali alimbariki yeye na uzao wake wote utakaofuatia baadaye.

"Nami nitakufanya wewe kuwa Taifa kubwa na kukubariki, na kulikuza jina lako nawe uwe baraka. Nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia zitabarikiwa". MWANZO 12:2-3

Mpaka hapa tutakuwa tumeona jinsi baraka na laana zilivyokuwa zinatolewa na inaonekana wazi kabisa namna ya kutoa baraka au laana, Wanadamu wa kale akiwemo mzee Nuhu walijifunza kutoka kwa MUNGU. Tukumbuke kuwa Nuhu alikuwa ni Nabii wa MUNGU, na aliongea na MUNGU mara nyingi tu katika njozi na maono. Hivyo basi Hamu alipokosea kwa kumwangalia baba yake akiwa uchi na kumcheka, alilaaniwa Caanani ambaye alikuwa ni uzao wa Hamu, yaani kizazi chote cha Hamu kikawa kimelaaniwa.

Huo ndiyo ulikuwa utaratibu wa kutoa laana au baraka, tena ni utaratibu ambao ulikuwa na baraka zote toka kwa MUNGU. Caanan hakumcheka Nuhu, lakini alilaaniwa sababu yeye alikuwa ni uzao wa Hamu, Caanan alikuwa anabeba damu ya Hamu ndani yake na alipaswa kulaaniwa. Pia tukumbuke jinsi MUNGU alivyosema katika zile Amri kumi;

".........nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao na kuzishika amri zangu". KUTOKA 20:5-6

Nuhu hakukosea kumlaani Caanan, nasema hakukosea sababu Nuhu alifuata utaratibu uliokuwepo. Utaratibu ambao hata BWANA MUNGU aliutumia kwa mara ya kwanza pale Eva alipokula matunda ya mti aliokatazwa asile. Tukihoji kwanini Nuhu Nabii wa MUNGU alimlaani Caanan kwa makosa ya baba yake, itakuwa kama tunataka kuhoji pia ni kwanini sisi leo hii tunabeba laana ya Eva na Adamu wakati siyo sisi tuliokula tunda. Nafikiri hakuna mwanadamu anayeweza kusimama na kumuuliza MUNGU kwanini ulifanya hivyo, kwanini ulitulaani sisi? (Soma ISAYA 45:9 au WARUMI 9:14-21)

MUNGU hakosei na wala MUNGU hamuonei mtu wala kumpendelea mtu. Nuhu alikuwa ni Nabii wa MUNGU, hivyo basi laana ya Nuhu kwa Caanan ilipata baraka zote toka kwa MUNGU. Kama Nuhu angekuwa ametoa laana kwa uonevu bila kufuata utaratibu unaokubalika na MUNGU; basi MUNGU asingekubali Caanan alaanike, angeizuia hiyo laana isitokee.

Nina imani kwa maelezo hayo, utakuwa umeelewa ni kwanini Caanan alibeba laana ya baba yake, tena siyo Caanan tu, bali ni yeye na uzao wake wote uliofuatia. Hata sisi Waafrika tunabeba laana hiyo mpaka leo, lakini tukumbuke kwamba MUNGU aliyetupiga kwa laana, ndiye YEYE huyo huyo aliyetuletea UKOMBOZI kupitia kwa Mwanawe YESU KRISTO.


"Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam Mimi ndiye, wala hapana MUNGU mwingine ila Mimi; naua Mimi, naponya Mimi, nimejeruhi tena nimeponya; wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu". KUMBUKUMBU LA TORATI 32:39
Mkuu zitto junior hatuwezi kumwelewa MUNGU hata siku moja, akili zake, wala mawazo yake, hayachunguziki na Mwanadamu wala Malaika. Lakini tunaweza kulielewa NENO lake, kuliamini na kumtii Yeye kama MUUMBA wetu.
Asante Sana. Naendelea kupata elimu zaidi.

Barikiwa
 
Mkuu Son of Gamba nashukuru kwa hoja yako iliyoshiba madini nimekuelewa sana tu ingawa ntarudi na swali ila kuna mtoa mada mmoja hapo juu alihoji JE NI HAKI Kosa kufanywa na mtu mmoja alafu laana kwa ukoo mzima?? Akaenda mbali na kusema huo ni uonevu na kadhalika

Hivyo basi kwa hekima yako unafkiri nini chanzo cha Mungu akilaani ni mpaka vizazi na akibariki ni vizazi kwanini haangalii mtu na mtu !!

Barikiwa

Cc Doto Dotto
Nikisoma maandiko hayo huwa napata mawazo sana. Yaani laana hadi kizazi cha 3 ama cha 4.
 
Okay upo sahihi kwa mtazamo wako ila inakuwa haijibu swali letu kwamba kwanini laana iende kwa canaan kma kwenye hilo kosa hausiki popote.... Tukijua sababu basi nadharia hizi zinakuwa hazina maana

Ok, mimi nilikiwa namuuliza namuuliza Mshana Jr na Jamaa mwingine aliyesema, Laana inaenda mpaka kizazi cha nne, ndio nikauliza hiyo laana ya kizazi cha nne anaitoa nani?, Mungu au mtu, Kama ni Mungu iweje Noah atoe laana kwa mjukuu wake?,

Back kwenye Swali lako au hoja yako, ni hoja fikirishi sana na tunasemaga mara nyingi Biblia iko coded, yaani ni fumbo so vitu vingi vinahitaji tafakari na pia kujua mapokeo ambayo mara nyingi yanasimamia kwenye tamaduni na historia ya eneo husika,

Swali la msingi nadhani linasimama pamoja na hoja yako ni kuwa, wakati Ham anamwona Baba yake akiwa uchi hakuwa mtoto mdogo, alikuwa ni mtu mwenye Mke na watoto wanne, so ni mtu mkomavu ambaye kwake isingekuwa rahisi kucheka uchi wa babake na kuwaadithia nduguze kama mambo ya kitoto vile, kitendo kilichofanywa na Kakaze cha kumfunika uchi babaye hata yeye angeweza kukifanya, iweje amwone uchi na atoke nje akimwacha uchi?

So lazima uncode filosofia iliyotumika hapo, Na kufanya hivyo kunaendana na kusoma Biblia pamoja na mapokeo mbalimbali ya kukuwezesha kujua tamadani za hayo maeneo wakati wa Noah

Ni vizuri umeiweka hapa kuna watu wanweza kiwa na uelewa wa habari ya laana ya kaanani, lakini mpaka sasa naona swali liko palepale na zinatoka haya nyingi zisizo na jibu la swali husika
 
Mkuu zitto junior ili uweze kuelewa ni kwanini Nuhu alimlaani Caanan na siyo Ham aliyetenda kosa, kwanza unatakiwa ulielewa na kuliamini NENO la MUNGU. Ili ulielewe NENO la MUNGU, kwanza lazima uliamini. Binadamu hatuwezi kumwelewa MUNGU, lakini tunaweza kulielewa NENO lake ambalo ametupa ili litusaidie katika maisha ya sasa na yale yajayo.

Tatizo linakuja pale ambapo watu walio wengi hawataki kuielewa Biblia wala kuiamini, wengi wanaona kile kilichoandikwa kwenye Biblia ni kama hadithi tu, ni kama porojo tu ambazo hazina maana. Ukweli ni kwamba, Biblia ni zaidi ya hadithi, ni zaidi ya Historia, na ni zaidi ya Unabii ambao umekuwa ukitimia kila siku. Kwa kulitambua hili, mimi nitakupa majibu ya Kibiblia ni kwanini Nuhu alimlaani Caanani badala ya Ham. Majibu yote yapo ndani ya Biblia na nje ya Biblia huwezi kupata majibu.

Iko hivi; zamani zile Wazazi hasa baba walikuwa wanatoa baraka au laana kwa kizazi cha watoto wao na siyo kwa mtu mmoja peke yake. Kama ni baraka, baba alikuwa anatoa baraka hizi kwa watoto wake wa kiume na vizazi vyao vyote vinavyofuata kwa sababu walikuwa wanaamini kuwa kizazi hakiishii kwa watoto, bali kinaendelea na kuendelea. Pia huu ndiyo ulikuwa utaratibu waliojifunza kutoka kwa BWANA MUNGU, pale alipotoa laana ya kwanza kwa mwanadamu na nyoka;

"nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa na wewe utamponda kisigino". MWANZO 3:15

Hapo juu utaona hiyo laana siyo kwa Eva na nyoka peke yao, bali ni kwa uzao wao wote utakaotokea duniani. Hii inaonekana kuwa wazee wale wa kale walijifunza pia kutoa laana au baraka kwa kizazi na kizazi. Hebu tuone baraka ya Isaka kwa Yakobo.

"Mataifa na wakutumikie, na makabila wakusujudie. Uwe bwana wa ndugu zako, na wana wa mama yako na wakusujudie. Atakaye kulaani, alaaniwe na atakayekubariki, abarikiwe". MWANZO 27:29

Hapa pia utaona Yakobo anabarikiwa na baba yake, tena siyo baraka kwa ajili yake tu katika maisha yake yeye kama Yakobo, bali ni kwa ajili yake na uzao wake wote utakaofuatia baada yake. Hivi ndivyo ilivyokuwa, hivi ndivyo wanadamu walijifunza kutoa baraka kwa wana wao au laana. Pia unaweza ukasoma kitabu hicho cha MWANZO sura ya 49, na utaona jinsi ambavyo na yeye Yakobo alivyotoa baraka kwa watoto wake 12.

Tukirudi upande wa BWANA MUNGU, pia tutaona jinsi alivyombariki mzee Ibrahimu, hakumbariki yeye tu kwa wakati ule, bali alimbariki yeye na uzao wake wote utakaofuatia baadaye.

"Nami nitakufanya wewe kuwa Taifa kubwa na kukubariki, na kulikuza jina lako nawe uwe baraka. Nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia zitabarikiwa". MWANZO 12:2-3

Mpaka hapa tutakuwa tumeona jinsi baraka na laana zilivyokuwa zinatolewa na inaonekana wazi kabisa namna ya kutoa baraka au laana, Wanadamu wa kale akiwemo mzee Nuhu walijifunza kutoka kwa MUNGU. Tukumbuke kuwa Nuhu alikuwa ni Nabii wa MUNGU, na aliongea na MUNGU mara nyingi tu katika njozi na maono. Hivyo basi Hamu alipokosea kwa kumwangalia baba yake akiwa uchi na kumcheka, alilaaniwa Caanani ambaye alikuwa ni uzao wa Hamu, yaani kizazi chote cha Hamu kikawa kimelaaniwa.

Huo ndiyo ulikuwa utaratibu wa kutoa laana au baraka, tena ni utaratibu ambao ulikuwa na baraka zote toka kwa MUNGU. Caanan hakumcheka Nuhu, lakini alilaaniwa sababu yeye alikuwa ni uzao wa Hamu, Caanan alikuwa anabeba damu ya Hamu ndani yake na alipaswa kulaaniwa. Pia tukumbuke jinsi MUNGU alivyosema katika zile Amri kumi;

".........nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao na kuzishika amri zangu". KUTOKA 20:5-6

Nuhu hakukosea kumlaani Caanan, nasema hakukosea sababu Nuhu alifuata utaratibu uliokuwepo. Utaratibu ambao hata BWANA MUNGU aliutumia kwa mara ya kwanza pale Eva alipokula matunda ya mti aliokatazwa asile. Tukihoji kwanini Nuhu Nabii wa MUNGU alimlaani Caanan kwa makosa ya baba yake, itakuwa kama tunataka kuhoji pia ni kwanini sisi leo hii tunabeba laana ya Eva na Adamu wakati siyo sisi tuliokula tunda. Nafikiri hakuna mwanadamu anayeweza kusimama na kumuuliza MUNGU kwanini ulifanya hivyo, kwanini ulitulaani sisi? (Soma ISAYA 45:9 au WARUMI 9:14-21)

MUNGU hakosei na wala MUNGU hamuonei mtu wala kumpendelea mtu. Nuhu alikuwa ni Nabii wa MUNGU, hivyo basi laana ya Nuhu kwa Caanan ilipata baraka zote toka kwa MUNGU. Kama Nuhu angekuwa ametoa laana kwa uonevu bila kufuata utaratibu unaokubalika na MUNGU; basi MUNGU asingekubali Caanan alaanike, angeizuia hiyo laana isitokee.

Nina imani kwa maelezo hayo, utakuwa umeelewa ni kwanini Caanan alibeba laana ya baba yake, tena siyo Caanan tu, bali ni yeye na uzao wake wote uliofuatia. Hata sisi Waafrika tunabeba laana hiyo mpaka leo, lakini tukumbuke kwamba MUNGU aliyetupiga kwa laana, ndiye YEYE huyo huyo aliyetuletea UKOMBOZI kupitia kwa Mwanawe YESU KRISTO.


"Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam Mimi ndiye, wala hapana MUNGU mwingine ila Mimi; naua Mimi, naponya Mimi, nimejeruhi tena nimeponya; wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu". KUMBUKUMBU LA TORATI 32:39
Mkuu zitto junior hatuwezi kumwelewa MUNGU hata siku moja, akili zake, wala mawazo yake, hayachunguziki na Mwanadamu wala Malaika. Lakini tunaweza kulielewa NENO lake, kuliamini na kumtii Yeye kama MUUMBA wetu.
Mtoto wa Gamba.

Kwanza sidhani asomae kama kitabu cha hadithi anaweza fikirisha akili akapata maswali ambayo hana majibu kupelekea kushirikisha wenziwe ili aeleweshwe..

Ukiona msomaji kaleta hoja kama hizi ujue hakusoma kama kitabu cha hadithi..

...
Kutokana na maelezo/hoja hizi ulizoweka hapa, Pia kuna maswali/hoja zinahitaji ufumbuzi zaidi..

Kwa Mfano:
Tumeona Ibrahim/Abraham akibarikiwa na kizazi chake.

Pia Isaka akambariki Yakobo na kizazi chake.

Swali/Hoja.
Inawezekana mtu atokae na kizazi cha Ibrahim/Abraham aje kulaaniwa na Mwanadamu au Mungu huko mbele?..
Sababu Mungu alishabariki hiki kizazi na kusema kwamba "Alaaniwe atakae Kulaani"..

....

Pia nikufahamishe kuwa watu hawana shaka na laana katika mkasa wa huu wa Nuhu..
Tatizo linakuja kwanini isianze kwa Ham na kuendelea mbele kwa uzao wake wote?..
Kwanini Canaan tu?..

Hapo ndipo panapohitaji Hekima..
Aliesoma na kufahamu, Atujuze nasi tupate kufahamu..
 
Ok, mimi nilikiwa namuuliza namuuliza Mshana Jr na Jamaa mwingine aliyesema, Laana inaenda mpaka kizazi cha nne, ndio nikauliza hiyo laana ya kizazi cha nne anaitoa nani?, Mungu au mtu, Kama ni Mungu iweje Noah atoe laana kwa mjukuu wake?,

Back kwenye Swali lako au hoja yako, ni hoja fikirishi sana na tunasemaga mara nyingi Biblia iko coded, yaani ni fumbo so vitu vingi vinahitaji tafakari na pia kujua mapokeo ambayo mara nyingi yanasimamia kwenye tamaduni na historia ya eneo husika,

Swali la msingi nadhani linasimama pamoja na hoja yako ni kuwa, wakati Ham anamwona Baba yake akiwa uchi hakuwa mtoto mdogo, alikuwa ni mtu mwenye Mke na watoto wanne, so ni mtu mkomavu ambaye kwake isingekuwa rahisi kucheka uchi wa babake na kuwaadithia nduguze kama mambo ya kitoto vile, kitendo kilichofanywa na Kakaze cha kumfunika uchi babaye hata yeye angeweza kukifanya, iweje amwone uchi na atoke nje akimwacha uchi?

So lazima uncode filosofia iliyotumika hapo, Na kufanya hivyo kunaendana na kusoma Biblia pamoja na mapokeo mbalimbali ya kukuwezesha kujua tamadani za hayo maeneo wakati wa Noah

Ni vizuri umeiweka hapa kuna watu wanweza kiwa na uelewa wa habari ya laana ya kaanani, lakini mpaka sasa naona swali liko palepale na zinatoka haya nyingi zisizo na jibu la swali husika
nakufuatulia mkuu"" umechambua vyema "" kwa upande wangu " mimi hayo mambo ya laana mpaka kizazi cha 4 siyaamini "" na subiri wenye imani ya hivyo vitu " wake watudadavulie lakini iwe ni kwa essay za kueleweka ""
 
Uko utaratibu wa Kiutendaji wa Kimungu. Mungu hatendi kiholela holela tu.

Mungu alimbariki Nuhu na watoto wake watatu. Na Nuhu akamlani Caanan na kusema kuwa atakua mtumwa kwa nduguze.

Kaanani alikuwa ndio lango la baraka katika uzao wa Ham. Utasema kwa nini? Jiulize kwa nini? hakuna nchi ya Ham ila iko nchi ya Kaanani? Wakati Ham ndio Baba wa uzao wake.

Ndio maana hata kwa Abraham Mtoto aliyebeba lile agano/baraka za kiroho alikuwa ni Isihaka. Tena kwa sababu hiyo Bwana Yesu/Mungu akaja ulimwenguni kupitia uzao wa Daudi ambaye ukirudi nyuma utamkuta Isack. Hakuna ukombozi mwingine kwa mwanadamu kutokana na dhambi bila kupitia kwa Bwana Yesu. Ndio ukweli mchungu huo. Huko kwengine ni kujidanganya tu, utaishia jehanamu na mabilioni tayari wamesha potelea jehanamu.
 
Uko utaratibu wa Kiutendaji wa Kimungu. Mungu hatendi kiholela holela tu.

Mungu alimbariki Nuhu na watoto wake watatu. Na Nuhu akamlani Caanan na kusema kuwa atakua mtumwa kwa nduguze.

Kaanani alikuwa ndio lango la baraka katika uzao wa Ham. Utasema kwa nini? Jiulize kwa nini? hakuna nchi ya Ham ila iko nchi ya Kaanani? Wakati Ham ndio Baba wa uzao wake.

Ndio maana hata kwa Abraham Mtoto aliyebeba lile agano/baraka za kiroho alikuwa ni Isihaka. Tena kwa sababu hiyo Bwana Yesu/Mungu akaja ulimwenguni kupitia uzao wa Daudi ambaye ukirudi nyuma utamkuta Isack. Hakuna ukombozi mwingine kwa mwanadamu kutokana na dhambi bila kupitia kwa Bwana Yesu. Ndio ukweli mchungu huo. Huko kwengine ni kujidanganya tu, utaishia jehanamu na mabilioni tayari wamesha potelea jehanamu.
Mkuu nmekuelewa ila hoja yako inazidisha maswali kuliko majibu..... Sawa alilaaniwa Canaan je swali inakuja kwanini canaan na sio cush mizraim na phut??

Okay umesema mwenye taifa ni canaan ambayo si kweli..... Misri imetoka kwa mizraim na phut ilianzisha nchi ya libya na pia cush alianzisha taifa la ethiopia sasa mbona wote walikuwa na mataifa why canaan ana kipi hasa cha ajabu kuliko hao kaka zake

Hatuna shida na laana wala Yesu ila tunajiuliza Why canaan?? Tusaidie hapo kwanni unasema canaan ni mlango wa baraka
 
Tafuta semina za Mwl Mwakasege kuhusu "malango na baraka" katika ulimwengu wa Kiroho. Nimezunguza kwa Misingi ya Ukristo na Biblia tu.

Halafu unasema, "Hakuna nchi ya Caanan?" Are you kidding?

Hujui kinyume cha baraka ni laana? Baraka za watoto wa Ham zilikuwa zipitishiwe kwa Caanan. Soma Kuhusu Yusuph na Nduguze 11 Watoto wa Yakobo/Israel utaelewa maanaya mlango wa baraka. Wao 11 Acha hao 3 wa Ham, 11 na Baba yao Yakobo hawakuwa na jinsi walimfata Yusuph Misri ili waponywe na Njaa.

Mkuu nmekuelewa ila hoja yako inazidisha maswali kuliko majibu..... Sawa alilaaniwa Canaan je swali inakuja kwanini canaan na sio cush mizraim na phut??

Okay umesema mwenye taifa ni canaan ambayo si kweli..... Misri imetoka kwa mizraim na phut ilianzisha nchi ya libya na pia cush alianzisha taifa la ethiopia sasa mbona wote walikuwa na mataifa why canaan ana kipi hasa cha ajabu kuliko hao kaka zake

Hatuna shida na laana wala Yesu ila tunajiuliza Why canaan?? Tusaidie hapo kwanni unasema canaan ni mlango wa baraka
 
Tafuta semina za Mwl Mwakasege kuhusu "malango na baraka" katika ulimwengu wa Kiroho. Nimezunguza kwa Misingi ya Ukristo na Biblia tu.

Halafu unasema, "Hakuna nchi ya Caanan?" Are you kidding?
Nasema nchi ilikuwepo ila hata watoto wengine wote na Ham walikuwa na nchi ambazo kwa nyakati tofauti ziliwahi kutawala dunia hii kuanzia misri mpaka ethiopia so sioni big deal canaan kuwa na nchi

Kuhusu malango ya baraka ni vzuri ungeeleza ulichoelewa kuishia katikati hautusaidii kma unalink au pdf ama unakumbuka tuwekee hapa tujifunze zaidi mkuu

Ubarikiwe
 
Hizo nyingine unazo sema zinaitwa taifa la Mungu? BWANA YESU/MUNGU alipokuja dunuani alizaliwa wapi? BETHLEHEM na YERUSALEMU ziko Misri AU MAKKA. Iko ISRAEL? Hekalu la Nabii Selemani? Liko SAUDIA? Mtume Muhamad SAW kwa nini hakushushiwa Quran Makka AU Madina? Akasema alishushiwa hapo JERUSALEM?

Nasema nchi ilikuwepo ila hata watoto wengine wote na Ham walikuwa na nchi ambazo kwa nyakati tofauti ziliwahi kutawala dunia hii kuanzia misri mpaka ethiopia so sioni big deal canaan kuwa na nchi

Kuhusu malango ya baraka ni vzuri ungeeleza ulichoelewa kuishia katikati hautusaidii kma unalink au pdf ama unakumbuka tuwekee hapa tujifunze zaidi mkuu

Ubarikiwe
 
Hizo nyingine unazo sema zinaitwa taifa la Mungu? BWANA YESU/MUNGU alipokuja dunuani akizaliwa wapi? YERUSALEMU iko Misri AU MAKKA. Iko ISRAEL? Hekalu la Nabii Selemani? Liko SAUDIA? Mtume Muhamad SAW kwa nini hakushushiwa Quran Makka AU Madina? Akasema alishushiwa hapo JERUSALEM?
Labda nikukisoe hapo mkuu canaan ya sasa sio canaan ya kale kumbuka kibiblia nchi ya ahadi kwa waisraeli ilikuwa inafika hadi River tigris na Euphrates kwahiyo una maana syria na iraq pia ni taifa la Mungu kwa definition hiyo unayotaka kutuaminisha???

Alafu nachotaka tufahamu ni kwamba Canaan walienda wayahudi sababu ya kutimiza laana hii ila kama Nuhu asingemlaani Canaan Mungu angewapeleka kwingine sio CANAAN na ndio maana bado kuna mjadala mkubwa sana hadi leo kuwa huenda Canaan aliwekwa kwenye laana ili kuhalalisha uvamizi huu wa wayahudi canaan!! Hivyo huenda Ethiopia ingekuwa taifa teule kma sio laana ya Ham so bado haijibu hoja kwanni Canaan ana utofauti

Alafu mkuu haya mambo yaliisha Yesu alipokuja wote tupo sawa mbele za Mungu hakuna kitu kama taifa la Mungu or what wayahudi walimkataa Yesu na hivo Mungu alitugeukia sisi wengine sasa hayo ya taifa teule yametoka wapi tena?? Wanaenda kuzimu kama kawaida so tuachage kuaminishana kuwa kuna taifa teule na israel ya sasa sio israel ya kale

Ni mawazo tu
 
Yesu alikuja kwao "wale walio kuwa wake hawakumpokea" (Wayahudi Taifa teule la Mungu), bali waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika wana wa Mungu wa aminio Jina lake. (Ndio watu wote wa dunia walio mpokea Bwana Yesu wakiwemo wakina Petro-Wayahudi).

Unajua maana ya Taifa Teule la Mungu?

Sio huenda Caanan aliwekwa katika laana ndivyo hivyo ilivyo. Ndio maana kuna taifa teule la Mungu ili kupitia hilo Mungu afanye ukuhani wake hapa duniani. Matendo ya Mungu hayo, ni makuu na ya ajabu.

Labda nikukisoe hapo mkuu canaan ya sasa sio canaan ya kale kumbuka kibiblia nchi ya ahadi kwa waisraeli ilikuwa inafika hadi River tigris na Euphrates kwahiyo una maana syria na iraq pia ni taifa la Mungu kwa definition hiyo unayotaka kutuaminisha???

Alafu nachotaka tufahamu ni kwamba Canaan walienda wayahudi sababu ya kutimiza laana hii ila kama Nuhu asingemlaani Canaan Mungu angewapeleka kwingine sio CANAAN na ndio maana bado kuna mjadala mkubwa sana hadi leo kuwa huenda Canaan aliwekwa kwenye laana ili kuhalalisha uvamizi huu wa wayahudi canaan!! Hivyo huenda Ethiopia ingekuwa taifa teule kma sio laana ya Ham so bado haijibu hoja kwanni Canaan ana utofauti

Alafu mkuu haya mambo yaliisha Yesu alipokuja wote tupo sawa mbele za Mungu hakuna kitu kama taifa la Mungu or what wayahudi walimkataa Yesu na hivo Mungu alitugeukia sisi wengine sasa hayo ya taifa teule yametoka wapi tena?? Wanaenda kuzimu kama kawaida so tuachage kuaminishana kuwa kuna taifa teule na israel ya sasa sio israel ya kale

Ni mawazo tu
 
Asingeachwa na wanadamu lakini kwa Mungu angehesabika haki

39 Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.
Luka 23 :39

40 Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
Luka 23 :40

41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
Luka 23 :41

42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
Luka 23 :42

43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.
Luka 23 :43

Hapa nadhani umeelewa
Sijakuelewa hata kidogo hebu soma hii:

Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake. Ezekiel 18:20

Sasa iweje Canaan abebe uovu wa baba yake Ham?

Iweje Watoto wa Akani waangamizwe kisa uovu wa baba yao?

Iweje ardhi ilaaniwe kwa uovu wa Adam?
 
Yesu alikuja kwao "wale walio kuwa wake hawakumpokea" (Wayahudi Taifa teule la Mungu), bali waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika wana wa Mungu wa aminio Jina lake. (Ndio watu wote wa dunia walio mpokea Bwana Yesu wakiwemo wakina Petro-Wayahudi).

Unajua maana ya Taifa Teule la Mungu?

Sio huenda Caanan aliwekwa katika laana ndivyo hivyo ilivyo. Ndio maana kina taifa teule la Mungu ili kupitia hilo Mungu afanye ukuhani wake hapa duniani. Matendo ya Mungu hayo, ni makuu na ya ajabu.
Hapana hapa nitofautiane na wwe tena....Canaan haikuwa taifa teule mkuu ila mpaka pale ilipotumika kutimiza laana ya Nuhu hivyo bila laana ya Nuhu wasingepelekwa Canaan sababu jiulize kwanini Abraham alipotolewa nchi yake aelekezwe Kwenda huko na sio Nigeria au china??? Kipi kinaashiria canaan ni taifa teule kiasi kwamba ilikuwa meant ikaliwe na wayahudi?? Embu tusaidie hapo maana ndipo tunapopishana

Na taifa teule haikuwa Israel mkuu ni kwamba Zilianza kwa shem na zikaenda throughout bloodline yake huyo Yakobo aliiba tu lakini Baraka ya Abraham ilikuwa kwa mataifa yote yaliyotokana kwake ila sio kwa Israel tu hivyo hata semites wengine wengi tu na edomites walipokea baraka hizi sio jews pekee kama mnavyotaka kutuaminisha

Mtazamo tu
 
Sijakuelewa hata kidogo hebu soma hii:

Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake. Ezekiel 18:20

Sasa iweje Canaan abebe uovu wa baba yake Ham?

Iweje Watoto wa Akani waangamizwe kisa uovu wa baba yao?

Iweje ardhi ilaaniwe kwa uovu wa Adam?
Aiseee hoja nzito sana hii ngoja wataalam waje tikakami wa lopelope mitale na midimu
 
Swali/Hoja.
Inawezekana mtu atokae na kizazi cha Ibrahim/Abraham aje kulaaniwa na Mwanadamu au Mungu huko mbele?..
Sababu Mungu alishabariki hiki kizazi na kusema kwamba "Alaaniwe atakae Kulaani"..

Hakuna mwanadamu anayeweza kuwalaani wana wa Israeli na laana hiyo ikatokea au ikafanyakazi, hakuna... Lakini, MUNGU peke yake anaweza kuwalaani Waisraeli wale ambao hawatafuata amri zake na maagizo yake na sheria zake. Ukisoma KUMBUKUMBU LA TORATI 28:15-19, utaona jinsi ilivyo.

Pia nikufahamishe kuwa watu hawana shaka na laana katika mkasa wa huu wa Nuhu..
Tatizo linakuja kwanini isianze kwa Ham na kuendelea mbele kwa uzao wake wote?..
Kwanini Canaan tu?..
Hili swali lako nimeshalijibu kwa kirefu sana, tafuta comment [HASHTAG]#103[/HASHTAG] katika uzi huu na ujisomee.

Unajua nini mkuu Babu Kivu kuna kitu watu wengi wanakosea sana bila kujua, kitu hicho ni pale watu wanapotaka "kumwelewa" BWANA MUNGU. Hakuna Mwanadamu wala Malaika mwenye uwezo wa kumwelewa MUNGU. Sisi Wanadamu na Malaika, tunao uwezo wa "kumwamini" na "kumtii" MUNGU, lakini hatuna uwezo, wala akili za "kumwelewa". Hata Biblia haikupi nafasi ya "kumwelewa" MUNGU, isipokuwa inakupa uwezo wa kumwamini na kumtii basi. Tena kuamini na kutii ni hiari, wala BWANA MUNGU hamlazimishi yeyote.

Watu wengi wanaisoma Biblia ili "wamwelewe" MUNGU, wanapogundua Biblia haiwaeleweshi kuhusu MUNGU, wanakata tamaa, wanasema MUNGU ni muonevu, mara ooh, anaupendeleo, mara ooh, Biblia inaji-contradict, n.k. Wanakosa imani, mwishowe wanasema MUNGU hayupo.

Lakini ukweli ni kwamba MUNGU yupo sana, sema tu hajatupa nafasi ya sisi kumwelewa, yaani hajavipa nafasi viumbe vyake vyote kumwelewa. Isipokuwa ametoa nafasi kubwa sana ya viumbe vyake vyote kumwamini na kumtii. Na hilo ndilo jambo muhimu kuliko yote, kuamini na kutii.
 
Uko utaratibu wa Kiutendaji wa Kimungu. Mungu hatendi kiholela holela tu.

Mungu alimbariki Nuhu na watoto wake watatu. Na Nuhu akamlani Caanan na kusema kuwa atakua mtumwa kwa nduguze.

Kaanani alikuwa ndio lango la baraka katika uzao wa Ham. Utasema kwa nini? Jiulize kwa nini? hakuna nchi ya Ham ila iko nchi ya Kaanani? Wakati Ham ndio Baba wa uzao wake.

Ndio maana hata kwa Abraham Mtoto aliyebeba lile agano/baraka za kiroho alikuwa ni Isihaka. Tena kwa sababu hiyo Bwana Yesu/Mungu akaja ulimwenguni kupitia uzao wa Daudi ambaye ukirudi nyuma utamkuta Isack. Hakuna ukombozi mwingine kwa mwanadamu kutokana na dhambi bila kupitia kwa Bwana Yesu. Ndio ukweli mchungu huo. Huko kwengine ni kujidanganya tu, utaishia jehanamu na mabilioni tayari wamesha potelea jehanamu.
Ndugu unataka uholela gan tena zaidi ya huu wakutoa laana adi kizazi cha nne
 
Ni
Sijakuelewa hata kidogo hebu soma hii:

Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake. Ezekiel 18:20

Sasa iweje Canaan abebe uovu wa baba yake Ham?

Iweje Watoto wa Akani waangamizwe kisa uovu wa baba yao?

Iweje ardhi ilaaniwe kwa uovu wa Adam?
niajabu mkuu haki yake mwenye haki na uovu wake mwenye uovu kila mtu ahukumiwe kwa matendo yake laana mpaka kizazi ni hadaa tupu
 
Ni
Sijakuelewa hata kidogo hebu soma hii:

Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake. Ezekiel 18:20

Sasa iweje Canaan abebe uovu wa baba yake Ham?

Iweje Watoto wa Akani waangamizwe kisa uovu wa baba yao?

Iweje ardhi ilaaniwe kwa uovu wa Adam?
niajabu mkuu haki yake mwenye haki na uovu wake mwenye uovu kila mtu ahukumiwe kwa matendo yake laana mpaka kizazi cha nne ni hadaa tupu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom