KWA WAHENGA TU: Mara ya kwanza kuona TV/ Video/ Sinema ilikuwa mwaka gani na ulijisikiaje?

Kinengunengu

JF-Expert Member
May 3, 2021
1,719
4,309
Binafsi nakumbuka mara ya kwanza kuona video ilikuwa ni Late 1980"s na ilikuwa ni Sinema. Walikuja uwanjani kijijini kwetu wakihamasisha maendeleo. Waliwasha Sinema na Waliweka wimbo wa "Remmy Ongala" sikumbuki Jina ila Binafsi sikuwa najua tofauti ya Sinema na Muziki. Nikawa nacheza nikiamini ndio mziki na sio Sinema.

Baadae, Early 1990"s nikaja kuona video kwa mara ya kwanza. Kuna Askari mmoja alienda kusoma South Afrika akaja na TV/Video akawa anaweka Mikanda nasi tunaangalia kwa masharti ya kufanya/kusaidia kazi ndogondogo nyumba kwake kama kulima, kuosha vyombo n.k. Nakumbuka Mkanda wangu wa kwanza kuona ni Anord Shwazniger kuna picha moja amecheza anaenda mkomboa mwanae "Jane". Humo Anord anatumia Mabomu, Visu, Bunduki na Ndege kuangusha mabomu.

Sasa yale mabunduki na Jinsi alivyokuwa anaua watu nilijua ni kweli. Ile Jioni nimetoka angalia mkanda huo, Ndege iliyokuwa inamwaga Sumu kwa ajili ya kuua "quelea quelea " kwenye mashamba ya Mpunga ikapita. Hahaaa, nililia na kukimbia sana nikipiga kelele "Anord ananilipua/Ananiua"

Video yangu ya Pili kuangalia ni Marudio ya mechi ya Simba na Stela Abidjan.

Wewe je Mhenga, unakumbuka nini?
 
2001 nikiwa darasa la 1.
Nilihisi kama mazingaombwe vile.
★Kwaya ya mapigano ulyankulu
★ Mbutalikaso😂
★Halafu usiku wakaweja Movie ya Rambo 😂
 
Delta Force - 1980
IMG_20220725_111131.jpg
IMG_20220725_111206.jpg
 
Asante Afande Hemed RPC Arusha, Late 80s watoto wa kota tuliponea hapo kila jioni tunakusanyika kuangalia sinema!
 
Nimezaliwa nimeikuta nyumbani ila nilipokuja Tz bara hakukuwa naTv miaka ya 90 ukitaka kutazama video unaenda chuo cha mipango Area C kwa sasa ni K/Ndege Secondary au kwa Hayati Harold Jaffu almaarufu BABA VIDEO R.I.P
 
Mwishoni mwa 93 nilikuwa naangalia TV na sinema na muziki za akina Yondo Sista, Mabele, Pepe Kale, Ghatto nk.Kulikuwa na mashine ya kukoboa mpunga na inazalisha umeme kwa hiyo ndio tulikuwa tukiangalia nyakati za usiku.

Miaka hiyo huko Malinyi, Morogoro.
 
Tv: 1975 - TVZ(Z’bar)
Betamax: 1980’s - Arusha
VHS: 1980’s - Arusha

Sinema: 1970’ - Majestic, Metropol (Znz &Ar)
 
TV 1976 Jengo la Vijana Morogoro Road Dsm ilikuwa TvZanzibar,,,Sinema 1960's kwenye magari ya sinema yalikuwa yanakuja vijijini enzi za 'Mhogo mchungu"

Mkuu enzi hizo Tv Znz ilikuwa inapatikana live Dar au walikuwa wanaonyesha recorded
Nauliza tu
 
Yaani maisha haya watu tumetoka mbali....Mzee Reginald Mengi kweli alikuwa mkombozi..apumzike kwa Amani...maana aliweka kontena mji mzima mnakusanyika hapo uwanjani then kontena linafunguliwa tunaanza kuona ITV Hadi usiku...

Kimbembe ilikuwa siku ya pambano la Tyson mbona watu walilala uwanjani kusubiri.
 
Mara ya kwanza kuona video ilikuwa Niko STD 1 au 2 kule Sumbawanga ilikuwa kila saa 2 usiku tunaenda maeneo ya National Housing kulikuwa na open space kubwa, tunaangalia taarifa mpka saa 2;30.

Badae Drs la 3 Kuna Kuna mzee m1 aliitwa mzee Sikanda(RIP) alinununua video, tukaanza kuona Comando ya Anord Swazneger, na Watoto 12, Comando 3.
 
Yaani maisha haya watu tumetoka mbali....Mzee Reginald Mengi kweli alikuwa mkombozi..apumzike kwa Amani...maana aliweka kontena mji mzima mnakusanyika hapo uwanjani.then kontena linafunguliwa tunaanza kuona ITV Hadi usiku...kimbembe ilikuwa siku ya pambano la Tyson mbona watu walilala uwanjani kusubiri.
Na sisi alitukomboa Sumbawanga bana
 
Binafsi nakumbuka mara ya kwanza kuona video ilikuwa ni Late 1980"s na ilikuwa ni Sinema. Walikuja uwanjani kijijini kwetu wakihamasisha maendeleo. Waliwasha Sinema na Waliweka wimbo wa "Remmy Ongala" sikumbuki Jina ila Binafsi sikuwa najua tofauti ya Sinema na Muziki. Nikawa nacheza nikiamini ndio mziki na sio Sinema.

Baadae, Early 1990"s nikaja kuona video kwa mara ya kwanza. Kuna Askari mmoja alienda kusoma South Afrika akaja na TV/Video akawa anaweka Mikanda nasi tunaangalia kwa masharti ya kufanya/kusaidia kazi ndogondogo nyumba kwake kama kulima, kuosha vyombo n.k. Nakumbuka Mkanda wangu wa kwanza kuona ni Anord Shwazniger kuna picha moja amecheza anaenda mkomboa mwanae "Jane". Humo Anord anatumia Mabomu, Visu, Bunduki na Ndege kuangusha mabomu.

Sasa yale mabunduki na Jinsi alivyokuwa anaua watu nilijua ni kweli. Ile Jioni nimetoka angalia mkanda huo, Ndege iliyokuwa inamwaga Sumu kwa ajili ya kuua "quelea quelea " kwenye mashamba ya Mpunga ikapita. Hahaaa, nililia na kukimbia sana nikipiga kelele "Anord ananilipua/Ananiua"

Video yangu ya Pili kuangalia ni Marudio ya mechi ya Simba na Stela Abidjan.

Wewe je Mhenga, unakumbuka nini?
Mkuu ni kama umechanganya mada. Kuna cinema na video!

Cinema ni yale ma screen ya vitambaa ambayo yalikuwepo miaka na miaka.

Lakini video kwa Tanzania teknolojia hii imeanza kuigia nchini miaka ya '80+ na Tv miaka ya '90.
Mara ya kwanza kuona video ilikuwa Niko STD 1 au 2, kule Sumbawanga ilikuwa kila saa 2 usiku tunaenda maeneo ya National Housing kulikuwa na open space kubwa, tunaangalia taarifa mpka saa 2;30.
Badae Drs la 3 Kuna Kuna mzee m1 aliitwa mzee Sikanda(RIP) alinununua video, tukaanza kuona Comando ya Anord Swazneger, na Watoto 12, Comando 3.
 
1978 Middle East ila sikushangaa kwa sababu nilikuwa najua kuna duniani zimetengenezwa
Nilishangaa maendeleo yao mengine tu kama miundombinu na maduka yao makubwa Malls na supermarkets zao

Mimi sio wa kishua ila nilipaa na dege miaka hiyo
Mungu mwema
Shikamoo baba!
 
Back
Top Bottom