Kwa Katiba hii, Tanzania imefikia mwisho wa kupiga hatua za maendeleo, kama hatutatumia hiari tutakaribisha tunakaribisha mapinduzi

Landson Tz

JF-Expert Member
May 8, 2011
295
221
Katiba ya sasa ina mapungufu makubwa sana ambayo yanazuia nchi yetu kupiga hatua za maendeleo na kufanya watanzania wengi kuishi katika ufukara wa kutisha. Takwimu zinaonyesha kuwa 96.6% ya watanzania wanaishi chini ya $2 (TSH.4600) na zaidi ya 86% wanaishi chini ya msitari wa umaskini yaani dola 1.25 (2,875).

Turudi kwenye katiba, katiba hii imenyakua madaraka karibia yote na kuyapachika kwa Rais na wateule wake. Lakini kwa bahati mbaya wateule wa Rais walio wengi bado wana angalia matumbo yao na familia zao wanaacha wananchi wakijihangaikia kwa njia za asili kama wanyama pori wasio kuwa na mchungaji!

Ukiacha madaraka, nchi inanuka rushwa na wizi. Kama hadi tume ya uchaguzi inashiriki kuiba (rushwa) kura tutawezaje kupata viongozi wa kutuvusha hapa tulipo. Katiba yetu kupitia tume mbovu ya uchaguzi imezuia mfumo wa vyama vingi kutupatia viongozi mahili mbadala wa chama tawala kwa kuendekeza wizi wa kura pamoja na vitisho vya dola. Na huko chama tawala rushwa imetamalaki na kuzalisha viongozi wabovu .

Imefika hatua hata vijana wetu wasomi wanakosa ajira, wakati hata serikalini upungufu wa wafanyakazi ni mkubwa! Kisingizio ni ukosefu wa fedha kama huna uwezo wa kutafuta fedha za kulipa wafanyakazi kwa nini uchukue fomu kugombea nafasi ya uongozi wakati hauna uwezo wa kutatua changamoto zao!!

Kwa leo naishia hapa nitaendelea ………
 
Mapinduzi yaliyoshamiri Kila pande ya Africa Tanzania siyo nchi ya Mbinguni isipate wanachopata wenzao.

Abiy Ahmed Ali Pm wa Ethiopia alikuwa na dharau sana dhidi ya Chama cha TPLF amekuwa akituma vikosi vyake vya kijeshi kukamata, kufunga, kutesa na kuua wafuasi wa TPLF na OLA.

Sasa matendo yake yanamtoka puani. Haamini kama ni kikundi kidogo tu kinamnyima usingizi. Na awamu hii akipona basi ashukuru Mungu.

Tanzania tunapaswa kuona mbali tusisubiri yanayotokea Sudani, Mali, Guinea, Gaboni, Ivory Coast, Zambia na Zimbabwe yatokee.

Katiba Mpya haina mbadala.
 
Mkuu umetumwa na mabeberu. Cha msingi katiba hii inatusaidia kushinda uchaguzi ambao ndo kipaumbele cha nchi au hujui
Tunaangalia vitu vinaleta ushindi
 
Hizi ndiuo huitwa hoja za kijinga. Yakitokea mapinduzi unafikiri vijana wote ndiyo watapata ajira? Katiba hata ya leo inasema kila mtu a astahili ajira, lakini mbona haitekelezeki? Ukitaka kuibadilisha utaiandikaje? Hiyo idadi yako ya vijana ubaitumia vibaya, ubafikiri vijana wote ni wakorofi au ni chadema. Nchi ya vyama vingi inayotawala ni Ilani, watu wataipigia kura Ilani inayowapa matumaini.
 
Back
Top Bottom