Acha kupotosha watu, kanisa katoriki lina sheria zake, ukiwa mtawa/Padre unaruhusiwa kuendelea na huduma maisha yako yote au unaruhusiwa kuomba kumpumzika na kuendelea maisha ya kawaida kama muumini mwingine wa kawaida. Dr Slaa aliomba kustaafu upadre kabla ya ujio wa Papa John II kuja tanzania miaka ya 1999 wakati huo akiwa na katibu wa TEC lkn kanisa lilimwomba asipumzike mpaka ziara ya PAPA ikamilike, kama ingekuwa ni dhambi basi kanisa lisinge mwomba kuendelea. baada ya ziara ya PAPA nchini Dr Slaa alikubaliwa na makao makuu kustaafu na kuagwa na kanisa kwa sherehe kubwa. Baada ya kustaafu Dr. Slaa alirudi kwao Karatu na kuanzisha miradi ya jamii, aliweza kupata wafadhiri mbalimbali hivyo kufanikiwa kuleta maendeleao Karatu. Baada ya wananchi kuona mafanikio yake, walimwomba agombee ubunge, na kweli akagombea kupitia CCM, CCM waliona kama ni mgeni katika siasa wakakata jina lake na kumpa mshindi wa tatu aliyekuwa mbunge wakati huo. Hivyo basi wananchi wakamshawishi kuhamia chama cha upinzani na kuwa wangempa kura, Dr Slaa akahamia CHADEMA wakati huo CHADEMA hakina umaarufu kama sasa, chama kilichikuwa maarufu kilikuwa ni NCCR mageuzi. Dr Slaa akashinda kwa kishindo na kuwa mbunge wa kwanza kutoka CHADEMA na Dr Warid Kabour kutoka jimbo la Kigoma mjini.
Kwa wasio jua Dr Slaa ndiye aliyeanziasha taasisi ya tiba ya CCBRT na ni mkurugenzi wa board. Nafikiri ni taasisi peke hapa nchini inayotoa tiba ya ulemavu wa viungo na macho kwa gharama nafuu.
In 1994: With the support of CBM, Dr. Willbrod Slaa, (still on the CCBRT Board) and Geert Vanneste founded CCBRT. Their mission was to contribute towards poverty alleviation by making rehabilitative services accessible and affordable to people with disabilities. In 1994, CCBRT was registered as a private Non-Governmental Tanzanian Society (NGO), under the Tanzanian Societies Act, No SO8261.