Kwa hili, Rostam Aziz hutasameheka

Kwa hili, Rostam Aziz hutasameheka

dada yangu regia umesema vyema lakini hivi hakuna matatizo kwenye majimbo yenu wapendwa wapinzani?

Yapo,tunayapigia kelele ndani na nje ya Bunge!tunajitahidi kuyatatua kadiri tunavyoweza!
 
unaweza kurudia ulichokiandika ukakumbuka kweli kama haujatazamia

Hivi huko uliko kilombero ndio kuna miundo mbinu mizuri kuliko Igunga? don't fool people

Kilombero wamechoka the same way like igunga..anza kutengeneza huko kwenu kabla ya kuja na hoja nyepesi

Unatafuta emotional support than realiaties on the ground!!
 
Hivi huko uliko kilombero ndio kuna miundo mbinu mizuri kuliko Igunga? don't fool people

Kilombero wamechoka the same way like igunga..anza kutengeneza huko kwenu kabla ya kuja na hoja nyepesi

Unatafuta emotional support than realiaties on the ground!!

Kilombero matatizo yapo,ninayajua yote na ninaendelea kuyapigia kelele nje na ndani ya Bunge na mengine ninayatua Mimi mwenyewe Yale ninayoyaweza...ila huwezi kulinganisha Igunga na Kilombero kwa chochote!Kilombero is 1000 miles away compared to Igunga lakini hata hivyo Wabunge wa CHADEMA ni watetezi wa wanyonge wa nchi nzima sio kwa maeneo tunayotoka tu!
 
Ndumba naomba nijue kitu kimoja tu,umewahi fika igunga?na karatu?kama bado tembelea hizi wilaya halafu urudi hapa utueleze ulichokiona personally i have been to both districts




Mimi niko jkaratu,umasikini hapa ni kama igunga hakuna cha kudanganya mtu.wapo watu hawna nyumba wanaishi kama mbuzi,hawana maji na hawana chakula asikudanganye mtu hali ya Tanzania inafanana hakuna cha Igunga wala urambo wala karatu.
 
Kabisa binti yangu. Nilikuwa mlevi sana enzi hizo. sikujenga nyumba. Sikulipa karo wanangu wasome vizuri. Nyumbani hawakula vizuri. Mama yangu kule kijijini alitaabika sana. Tangu ni meacha ulevi alihamdulilah mambo yamerekebika mengi. Ruzuku kwa vyama vya siasa ni wizi uliohalalishwa na CCM itaendelea kututesa sana kwa ruzuku hii.

Mkuu mimi nadhani hoja si kuacha ulevi wa pombe tu,bali namna ya kuzitumia hizo pesa ulizokuwa unazimimina kwenye kilaji, baada ya kuacha kukata kilaji unazielekeza wapi?
Mara ngapi tumeshuhudia bunge likipitisha bajeti kwa matumizi fulani lakini serikali inabadilisha na kufanya kitu kingine? kwahiyo utaona kwamba tunaweza kukubaliana kuondoa ruzuku za vyama vya siasa kwa lengo la mkuzielekeza fedha hizom kwenye maendeleo ya wananchi lakini tuna uhakika kwamba zitafika huko chini kabisa na kununua madawati kama unavydhani?

Mara ngapi tumeshuhudia serikali ikishindwa kupeleka fedha kwenye local government hadi dakika za mwisho mwezi wa nne ama wa tano na hatimaye fedha hizo kushindwa kutumika na kurudishwa hazina? mara ngapi tumeshuhudiwa fedha za maendeleo zikipelekwa huko kwenye halmashauri lakini hazitumiki hadi mwisho wa mwaka zinarudishwa hazina wakati shughuli nyingi za maendeleo ya wananchi zimelala kwa kukosa fedha?

Kwahiyo mkuu tataizo sio kuondoa ruzuku kwenye vyama vya siasa, bali usimamizi. Hata hicho kidogo tulichonacho tumeshindwa kukisimamia, tukipata kikubwa tuna uhakika kwamba tutaweza kukisimamia vizuri? na msimamizi ni huyo huyo ccm?? just thinking aloud!
 
dada yangu regia umesema vyema lakini hivi hakuna matatizo kwenye majimbo yenu wapendwa wapinzani?

Yapo lakini kwani unafikiri ni kazi ya mbunge kuyatatua, wabunge wa Chadema waichana Serikali bungeni na kueleza matatizo ya nchi hii, sasa serikali ikisikia iondoe hayo matatizo na kama serkali haisikii wao wabunge wanaishia hapo sasa tunabaki sie wananchi tuiondoe seriakli zembe na kujaribu nyingine.
 
Kilombero matatizo yapo,ninayajua yote na ninaendelea kuyapigia kelele nje na ndani ya Bunge na mengine ninayatua Mimi mwenyewe Yale ninayoyaweza...ila huwezi kulinganisha Igunga na Kilombero kwa chochote!Kilombero is 1000 miles away compared to Igunga lakini hata hivyo Wabunge wa CHADEMA ni watetezi wa wanyonge wa nchi nzima sio kwa maeneo tunayotoka tu!

1000 miles you must be joking!

Kupiga kelele ndani na nje ya bunge ndiyo kuleta maendeleo?

Unaonaje ukawashauri chama chako wangetumia "strategies +pesa" mlizotumia kutafuta ubunge katika kuharakisha maendeleo?

Mfano mngetumia 30% ya hela mlizotumia kutafuta madaraka (ili mpige kelele) kule igunga mngeweza kujenga zahanati ngapi igunga?

Hivi nyie mnaabudu madaraka au maendeleo ya wananchi?
 
Well said Mkuu!tatizo la WildCard ameangalia upande mmoja tu wa shilingi,anachokisema nikweli lakini lipotatizo la msingi Kama ulibyoainisha!


Mkuu mimi nadhani hoja si kuacha ulevi wa pombe tu,bali namna ya kuzitumia hizo pesa ulizokuwa unazimimina kwenye kilaji, baada ya kuacha kukata kilaji unazielekeza wapi?
Mara ngapi tumeshuhudia bunge likipitisha bajeti kwa matumizi fulani lakini serikali inabadilisha na kufanya kitu kingine? kwahiyo utaona kwamba tunaweza kukubaliana kuondoa ruzuku za vyama vya siasa kwa lengo la mkuzielekeza fedha hizom kwenye maendeleo ya wananchi lakini tuna uhakika kwamba zitafika huko chini kabisa na kununua madawati kama unavydhani?

Mara ngapi tumeshuhudia serikali ikishindwa kupeleka fedha kwenye local government hadi dakika za mwisho mwezi wa nne ama wa tano na hatimaye fedha hizo kushindwa kutumika na kurudishwa hazina? mara ngapi tumeshuhudiwa fedha za maendeleo zikipelekwa huko kwenye halmashauri lakini hazitumiki hadi mwisho wa mwaka zinarudishwa hazina wakati shughuli nyingi za maendeleo ya wananchi zimelala kwa kukosa fedha?

Kwahiyo mkuu tataizo sio kuondoa ruzuku kwenye vyama vya siasa, bali usimamizi. Hata hicho kidogo tulichonacho tumeshindwa kukisimamia, tukipata kikubwa tuna uhakika kwamba tutaweza kukisimamia vizuri? na msimamizi ni huyo huyo ccm?? just thinking aloud!
 
Huamini kuwa huwezi kulinganisha Igunga na Kilombero?
1000 miles you must be joking!

Kupiga kelele ndani na nje ya bunge ndiyo kuleta maendeleo?

Unaonaje ukawashauri chama chako wangetumia "strategies +pesa" mlizotumia kutafuta ubunge katika kuharakisha maendeleo?

Mfano mngetumia 30% ya hela mlizotumia kutafuta madaraka (ili mpige kelele) kule igunga mngeweza kujenga zahanati ngapi igunga?

Hivi nyie mnaabudu madaraka au maendeleo ya wananchi?
 
Bi. Regia,

Mimi kusema kweli nimekusoma ktk hali ambao yanishangaza mimi kwamba wewe hukuyajua haya..Ni hali halisi ya sehemu kubwa ya Tanzania na inasikitisha zaidi pale Wabunge wetu waliopewa dhamana ya kupeleka maendeleo vijijini wanapata muda wa kuwalaghai wananchi kwa Takrima na fedha. Rostam anasifika Igunga kwa kutoa fedha kama vile masikini wanavyoweza kumsifia mtu anayewapa Tsh1,000 kila siku anaposimamisha gari lake...

Ningekuomba sana ulitazame swala hili kwa mapana zaidi kwa sababu Tanzania leo ni maskini kuliko hata wakati wa Uhuru na hesabu ya maskini inazidi kuongezeka kila siku. Kama nchi nzima asilimia 14 ndio wenye umeme tena wa mgao, tunayo maji lakini maji safi ni chini ya asilimia 10 au hakuna kabisa! Hatuna walimu na madktari wa kutosha shule na zahanati zilizojengwa ni sawa na magofu au kiwanda kisichozalisha. Kumbuka pia Wadanganyika wengi hawajaona maendeleo na wengi zaidi hawajui maendeleo zaidi ya yale wanayoyaona ktk maisha yao hivyo sii rahisi kabisa kumshawishi mwana Igunga akuelewe ktk muda mfupi kiasi hicho...

CCM walikuwa wanataka ku prove kitu hivyo msinde msishinde Igunga lazima waichukue. Hivyo kwa ujumla wa yote haya wananchi wa Igunga hawakutendewa haki hata kidogo. Kilichofanyika pale ni kupeleka fahgari wawili wakagombane wakati nyasi hao wanaIgunga ndio waathirika. Kweli Chadema kimeweza kujijenga, lakini hii kweli ni haki?..Kweli chama kinatakiwa kujijenga wakati wa uchaguzi ambao wananchi wake wana nafasi moja tu ktk miaka mitano kufanya maamuzi magumu.

Ushauri wangu kwenu, tembeleeni sana majimbo, vijiji mkajionee wenyewe jinsi nchi yetu ilivyokuwa nyuma ktk maendeleo kwani sii Igunga peke yake, sehemu kubwa ya Taifa letu ni Igunga ya Rostam. Mbunge anachaguliwa na kusifikia sii kwa kuwapelekea maendeleo bali kwa kutoa misaada na sadaka zaidi kama Taifa letu linavyoomba misaada nje...Ni Mataifa gani marafiki zetu zaidi kama sii yale yanayotupa misaada kuliko Wawekezaji waliokuja kutupa ajira na kuinvest nchini..
 
Huamini kuwa huwezi kulinganisha Igunga na Kilombero?

Wote ni wagonjwa moja ni mahututi mwingine yuko ICU...

Igunga ni maskini sana na kilombero ni maskini..

miundombinu ni mibovu na watu hawapati maji safi, barabara, umeme na nyumba bora...

Usisahau elimu pia..

Labda ni wewe na wabunge wenzako na familia zenu..
 
Mkuu,nakubaliana na wewe kwa asilimia kadhaa na aslimia kadhaa sikubaliani na wewe.Hoja hapa inamzungumzia Rostam na nimeainisha sababu.Ninatambua kabisa matatizo haya yapo pia sehemu nyingine lakini mimi nimeamua Igunga kwakuwa ndio tumetoka Jana tu kwenye uchaguzi mdogo na uchaguzi wake sio Kama chaguzi ndogo tulizoazizoea za Mbunge kufariki lakini pia nikutokana na status au jina la Rostam katika Taifa hili..

Kuhusu vyama kukijenga wakati wa uchaguzi mdogo nadhani hii ungeianzishia sredi yake ili tudebate kwa mapana yake..tukianza kuijadili hapa tutaharibu utamu wa sredi yangu..au unasemaje Kamanda?

Bi. Regia,

Mimi kusema kweli nimekusoma ktk hali ambao yanishangaza mimi kwamba wewe hukuyajua haya..Ni hali halisi ya sehemu kubwa ya Tanzania na inasikitisha zaidi pale Wabunge wetu waliopewa dhamana ya kupeleka maendeleo vijijini wanapata muda wa kuwalaghai wananchi kwa Takrima na fedha. Rostam anasifika Igunga kwa kutoa fedha kama vile masikini wanavyoweza kumsifia mtu anayewapa Tsh1,000 kila siku anaposimamisha gari lake...

Ningekuomba sana ulitazame swala hili kwa mapana zaidi kwa sababu Tanzania leo ni maskini kuliko hata wakati wa Uhuru na hesabu ya maskini inazidi kuongezeka kila siku. Kama nchi nzima asilimia 14 ndio wenye umeme tena wa mgao, tunayo maji lakini maji safi ni chini ya asilimia 10 au hakuna kabisa! Hatuna walimu na madktari wa kutosha shule na zahanati zilizojengwa ni sawa na magofu au kiwanda kisichozalisha. Kumbuka pia Wadanganyika wengi hawajaona maendeleo na wengi zaidi hawajui maendeleo zaidi ya yale wanayoyaona ktk maisha yao hivyo sii rahisi kabisa kumshawishi mwana Igunga akuelewe ktk muda mfupi kiasi hicho...

CCM walikuwa wanataka ku prove kitu hivyo msinde msishinde Igunga lazima waichukue. Hivyo kwa ujumla wa yote haya wananchi wa Igunga hawakutendewa haki hata kidogo. Kilichofanyika pale ni kupeleka fahgari wawili wakagombane wakati nyasi hao wanaIgunga ndio waathirika. Kweli Chadema kimeweza kujijenga, lakini hii kweli ni haki?..Kweli chama kinatakiwa kujijenga wakati wa uchaguzi ambao wananchi wake wana nafasi moja tu ktk miaka mitano kufanya maamuzi magumu.

Ushauri wangu kwenu, tembeleeni sana majimbo, vijiji mkajionee wenyewe jinsi nchi yetu ilivyokuwa nyuma ktk maendeleo kwani sii Igunga peke yake, sehemu kubwa ya Taifa letu ni Igunga ya Rostam. Mbunge anachaguliwa na kusifikia sii kwa kuwapelekea maendeleo bali kwa kutoa misaada na sadaka zaidi kama Taifa letu linavyoomba misaada nje...Ni Mataifa gani marafiki zetu zaidi kama sii yale yanayotupa misaada kuliko Wawekezaji waliokuja kutupa ajira na kuinvest nchini..
 
Hivi Kilombero iko chini ya nani vile for 50 years???


Wote ni wagonjwa moja ni mahututi mwingine yuko ICU...

Igunga ni maskini sana na kilombero ni maskini..

miundombinu ni mibovu na watu hawapati maji safi, barabara, umeme na nyumba bora...

Usisahau elimu pia..

Labda ni wewe na wabunge wenzako na familia zenu..
 
Haya ni matatizo ya takriban nchi nzima, kwa hili inatakiwa ujadili upana wake na si kumuona rostam pekee.
 
wajemeni shida hizo ziko kila mahali hata kule karatu. Rostam alikuwa mbunge tu, kazi ya kuondoa kero hizo ni ya serikali.... aghh!

Acha ujinga, kwa hiyo tunapopeleka wabunge bungeni tunapoteza muda na mali zetu bure. Nani kakwambia serikali ndo inaweza kuondoa kero isizozijua? Nani anayeweza kuisimamia serikali isifanye yale ya Deep Green, Meremeta, Mikataba mibovu ili ipate fedha za kuondolea kero?

Narudia tena, "ACHA UJINGA, HUNA CHA KUCHANGIA KAMWOMBE ROSTAM HELA UKANYWE POMBE"
 
Mkuu umesema vyema lakini hujaconclude...Nini sasa kifanyike ili kuondoa hicho ulichokizunhumza?

Utashauri nini wakati Watanzania hawako tayari kubadilika? Kwa mfano, Rostam Aziz ndiye Mbunge aliyekuwa na ushiriki mdogo zaidi kati ya wabunge wa kawaida. Rostam ndiye mbunge pekee ambaye hakuchangia kwa namna yoyote ile kaika kipindi chake chote cha miaka mitano bungeni lililopita. Kama maendeleo uliyoghusia ndio hayo, wapiga kura wake walishawahi kumshikilia bango? Pia wabunge wa kuchaguliwa ndio wanaongoza kwa ushiriki zaidi ya wale wa kuteuliwa. Don't take personally, b'se this is in according to utafiti uliofanywa.

Nilichoongelea hakiwezi kubadilika mpaka pale Watanzania kwa ujumla watakapoamua kubadilika. Otherwise ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa. Hata hivyo, kila chama cha siasa na kwa kila Mbunge inabidi kufafanua zaidi ni kwa namna gani wamekuwa wakitumika kwa maslahi ya majimbo yao. Mijadala ya wazi ni muhimu kwa kukuza sio tuu demokrasia bali pia uwajibikaji. "Wabunge" wachache sana ni wabunge Tanzania. Hakuwa na hatakuwa Rostam tuu. Hili ni tatizo la kitaifa na sio tatizo la Igunga tuu.
 
THE NEW ROSTAM AZIZ AND THE IMAGINERY GOAL IN BARTER TRADE WITH CCM TODAY AND ON

Da Regia, what Rostam are you talking about here?? You must understand that at no time did Rostam Aziz go to parliament for the benifit of Tanzanians in Igunga.

Rostam Aziz, a defacto leader of terrorist networks in East Coast of Africa and South of Sahara had only moved into politics to get a bargaining advantage with many governments in the region from a legitimate vintage point of being a member of parliament.

This leading wholeseller in religious extremism, facilitator establishmend of illegitimate government through the backdoors, a first-rate merchandiser of uranium from the great lakes region, had only gone into politics to further the Iranian agenda as he gets paid in multibillion corruption deals.

Periods in the run to Igunga elections, a cheque had been rush in the name of DOWANS that was ultimately used partly to help oil the the daily failing CCM campaign machine that this time round had to assemble a bunch of political heavyweights of yerteryears who has since lost touch with reality on the ground.

Ooh no, who says thay Rostam Aziz' handout to CCM a few weeks ago was a sign of love for the party, the man has since been asked by the ruling party to play the devil from outside parliament in return for A FALSE PROTECTION by our government in order that the now dangerously hovering eagles DO NOT claw him up from the thickets of Igunga just the same way similar greatings had to be delivered to one of his compartriots in Yemen the other day.

Soon after the very many pieces out there coul perfectly be pieced together, sooner than later, to understand his mission wave-lengths all over, perhaps, the CCM-promised protection shall have withered to a tiny-small cristal of sugar. And soonafter that, a new Tanzania which is freer and more people-centred shall have been on the path to be born for once.

Aziz and ilks, the lences are drawing closer today than yesterday. Igunga pray for a people's power and you will be free and you will be on the driver's seat to chart your own development destinies - more NGOs may start streaming in even tomorrow after all.

Tanzania will be back to our long cherished love fo one another alongside all divides; real or imagined. And that could be no better a bit anyway.
 
Mkuu,nakubaliana na wewe kwa asilimia kadhaa na aslimia kadhaa sikubaliani na wewe.Hoja hapa inamzungumzia Rostam na nimeainisha sababu.Ninatambua kabisa matatizo haya yapo pia sehemu nyingine lakini mimi nimeamua Igunga kwakuwa ndio tumetoka Jana tu kwenye uchaguzi mdogo na uchaguzi wake sio Kama chaguzi ndogo tulizoazizoea za Mbunge kufariki lakini pia nikutokana na status au jina la Rostam katika Taifa hili..

Kuhusu vyama kukijenga wakati wa uchaguzi mdogo nadhani hii ungeianzishia sredi yake ili tudebate kwa mapana yake..tukianza kuijadili hapa tutaharibu utamu wa sredi yangu..au unasemaje Kamanda?
Nakupata sana, isipokuwa mimi nazungumza kama raia mwenye uchungu na maendeleo na nimeona wabunge wengi sana wakifanya wasiyotakiwa kuyafanya kisiasa. Kwa maana kwamba kwa kila jema wanalolifanya ni kujihakikishia wao nafasi ya kuchaguliwa tena na sii kuwapelekea maendeleo. Hili neno maendeleo halipo ktk msahafu wa Wabunge na serikali yenyewe! huwezi kujisifia maendeleo wakati takwimu zinaonyesha asilimia 14 ya umeme nchini na maji safi ni zero!.. ni sifa ipo unaweza kumpa hata mbunge mmoja..Na hata kama kaweza kufanya katika jimbo lake kweli ni haki kwa mbunge kufanya hayo toka mfukoni mwake?.

Na CCM ya leo, hao wasomi wetu hawana lolote jema, huwezi kuweka Umeme ukawa wa mgao masaa 12 ya mchana hakuna umeme wakati ndio wakati wa Uzalishaji! Na kwa upumbavu wa wananchi wengi wanalalamika umeme unapokatika usiku majumbani kwao wakati wabunge na mawaziri nyumba zao zina Umeme!. Ukitazama picha hii ktk fikra za kimaendeleo utajua kwamba Tanzania bado kabisa hatufahamu nini maendeleo na yanapatikana vipi..

Jingine hakuna maji safi isipokuwa ya chupa, sasa jiulize huko viwandani wanakotengeneza vyakula inakuwaje?..Sii ndio ya JK kugawa viandarua hali mbu wakizaana na kueneza malaria ili mashirika ya nje ya kuuza madawa wapate kufanya biashara zaidi!. Kama tunashindwa kuelewa matatizo yetu wenyewe, tunatembelea Mahospital na kushangaa hali ya wagonjwa wakati sisi wenyewe ndio tunazalisha magonjwa inanipa wasiwasi mkubwa na kuelewa kwa viongozi wetu.


Binafsi Rostam namchukia zaidi ktk UFISADI mkubwa aloufanya kwa Taifa hili, huyu hana huruma na yanayotokea Igunga ni sehemu ndigo sana na ushenzi wa utawala mzima wa CCM kwa wananchi wake. Ni dhulma na kuibia wananchi UHURU wao pale serikali inaposhindwa kuthamini UTU wa wananchi wake. Rostam ni sehemu ya utawala mzima wa CCM na wala sintoweza kumtofautisha na viongozi walio wengi kwa sababu wote wamekumbatia ulimbukeni na IGNORANCE - wanazidiana kimatendo tu..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom