Dah! hii habari imenishtua sana, pia siwezi kushangaa kwani siyo Igunga peke yake ukitembelea baadhi ya majimbo kadhaa utakutana na hali kama hii... Hii hali haikupaswa kuwa sehemu ambayo tajiri mkubwa na kifisadi wa kimataifa Rostam anatoka, nilitegemea wananchi wa huko wangekuwa na maendeleo kwa kiasi flani hivi....
Kwenye hii dunia ya sasa ukiwa hauna elimu ni taabu sana, sasa sipati picha hao vijana na watoto wasiyo jua kusoma wala kuandika hatima yao itakuwa je? Hizi lawama pia serikali inahusika moja kwa moja, maana kwa kushindwa kuwapa wananchi wake haki zao muhimu kama elimu na Afya...
Hii mdio miaka 50 ya uhuru tunajivunia? hakika tumepiga hatua kubwa kwa kufanya wananchi wake mbumbumbu..... Ili tatizo alitoisha kama wananchi wenyewe hatuta amka na kuwapigania wenzitu ambao wanakandamizwa kwa kuto kujua haki zao.