Kwa hili, Rostam Aziz hutasameheka

Kwa hili, Rostam Aziz hutasameheka

Hivi unajua Mnyika aliwahi kumuita JK dhaifu bungeni,lakini alipokutana naye walisalimiana na kucheka na hata ikulu pia alipokelewa bila kinuniwa.

Hiyo kauli ya kawaida sana sio shombo za kama wabunge flani wa upinzani. Hao ni kauli kali na za ovyo sana kama wana ugomvi binafsi na mpinzani wao.
 
Unaweza ukawa Sawa au Usiwe Sawa Mtoa mada r.i.p. Pengine alishikwa na Jazba tu but Mtu yeyote akiomba msamaha husamehewa so hii itabakia kama ilivyo sababu Rostam hakuwahiOmba Msamaha kwa Wananchi yawezekana kwa Mungu wake alishaomba au anaendelea Kuomba Samehe Saba mara Sabini.. Ukisamehe na Mungu Anasamehe..

Na Pia Usilaani kwani nawe Utalaaniwa
Dogo kumbe wewe wa kitambo humu
 
Namba tisa hatari sana! Ningepata fursa ya kufika hicho kijj na kuishi hapo ninge enjoy sana... Japo Inasikitisha 😔
 
Dada Regia umesema kweli,kama mtu umefika igunga hali inasikitisha sana,hao wanaotembea uchi ni wataturu na wanalalia ngozi,nilishawahi kushuhudia mama mjamzito anaumwa amebebwa kwenye tela linalokokotwa na ng'ombe pale simbo.Kiufupi hali ya igunga ni mbaya na zaidi inachangiwa na ukosefu wa elimu
naamini mambo yatakuwa yamebadilika sio lazima iwe kwa kiasi kikubwa hata kwa kiasi fulani
 
Si huko igunga pekee ndo unadhani raia ni masikini. Ni maeneo mengi tuu na ni kama asilimia kama 40 ya watanzania wanaishi katika mazingira kama hayo.
Cha ajabu ni kwamba, unaweza sema wao wana shida wakati wao wanaona kawaida tuu. Kwa sababu hali kama hiyo anaikuta tangu akiwa mtoto, anakuwa nayo hadi kuwa mtu mzima, hivyo haoni kama ni shida.
Cdm na wana harakati mbalimbali tuna budi kuwaelimisha wananchi ili watambue haki zao. Hiyo ndo itakuwa suluhisho la matatizo. Lakini ni jambo lisilo rahisi kubadili fikra za watu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom