Kwa hili, Rostam Aziz hutasameheka

Kwa hili, Rostam Aziz hutasameheka

Na wewe umenielewa kweli?Kuondoa ruzuku kutausambaratisha upinzani lakini siyo ccm,kwasababu wana mbinu za kuziba gap.Nilikuuliza mtaliziba vipi kwasababu mmeshauza nchi.Nadhani hamtashindwa maana punda bora afe,Igunga ni mfano.Mbona jamaa yako katajirika na huku jimbo umasikini ukizidi?Sasa unasema ni kwasababu hizo pesa alizisave kwenye akaunti yake badala ya kuzipeleka kwenye maendeleo na sasa waambiwe wasizitoe wakati wa kampeni bali waziache kwenye akaunti?Hapo nimekuelewa.
Labda Mushi haupo hapa nchini! Ruzuku ikiondoka leo, jioni hii, kesho CCM haipo. Hawajawahi kuishi bila ruzuku tangu uhuru. Tutafute namna kupunguza kuigharamia SIASA. Usimamizi wa dhati wa BUNGE uwepo. CAG awe huru. TAKUKURU iwe huru. Tume ya MAADILI kwa VIONGOZI iimarishwe. Matatizo kwa MTANZANIA wa kawaida hayatakwisha lakini yatapungua sana tu.
 
Mkuu umesema vyema lakini hujaconclude...Nini sasa kifanyike ili kuondoa hicho ulichokizunhumza?



Kazi za mbunge zimegawanyika katika makundu matatu. Mbunge anawajibika jimboni kwake, bungeni na kwenye chama chake. Bungeni ana wajibu wa kushiriki kwenye debates, kupitisha sheria, n.k. Kwenye chama, anaunga mkono chama chake na kukisaidia katika nyanja mbali mbali kama ku advocate polices zake, msemaji wa chama, nk. Kwenye jimbo lake, mbunge ana jukumu la kushauri jinsi ya kutatua matatizo yanayowakabili wanajimbo hasa yale yanayotakiwa kutatuliwa na serikali, kuwakilisha concerns za wanajimbo bungeni na ku act as a figurehead wa jimbo lake.

Tatizo tulilonalo ni kuwa wabunge wetu wamejikita zaidi kwenye kusaidia vyama vyao kwa njia yoyote ile. Wabunge wengi tuu hawajishughulishi na majadiliano yanayokuwa yanaendelea bungeni. Wengine mpaka wanapigwa picha wakiwa wamelala wakati majadiliano makali yakiendelea. Kubwa zaidi wabunge wengi hawatekelezi majukumu yao kwenye majimbo yao.

Rostam Aziz ni mfano tuu. Sijawahi kumsikia Rostam amesimama bungeni akitetea jambo fulani linalohusu jimbo lake. Wengine walidhani hana haja ya kufanya hivyo kwa vile jimbo lake tayari lina maendeleo ya kutosha. Igunga ni mfano tuu. Kwa wale ambao wamebahatika kutembelea vijijini utalia na roho yako. Hali ni mbaya. Hawa watu wana wawakilishi lakini wanaishi Dar. Wakati Rostam anajiuzuli ilimbidi apande ndege aende Igunga kujiuzulu. Wengine wakijiuzulu watafanya hivyo hivyo.

Lakini the root cause ni sisi wenyewe Watanzania. Politicians use us for their own benefits because we Tanzania don't really bother anymore. Ili mradi tunaenda haja kubwa, that's what matter to us now. Our future generation tumeisahau kabisa. And we will be punished for this. Asha Dii alianzisha thread moja muhimu sana juu ya trend ya African Politics (https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-politics-historia-itajirudia-tanzania-5.html) ambapo nilisema: We create problems, which in turn we use them to buy votes from voters. Whether wangeshinda Chadema, CUF au walivyoshinda CCM, by 2015 hali mbaya ya maendeleo jimbo la Igunga itaendelea kuwa vile vile. Trust me on this.

Our political game is based on manipulating the poor and illiterate. We create opportunities of dependency to the government and this way the poor always put the same leader, leadership style in power. We the people make our leaders whether new or old what they are. Our leaders in a large measure a reflection of the totality of our attitude to everything. Leadership is sustained by fellowship.
 
Dada yote unayosema hapa ni kweli kabisa lakini mbona hamkuyasema wakati mkiwa Igunga?

Wewe vipi? Si kasema hakuwahifika Igunga? Umesahau no research, no right to speak
 
WC unafikiri fedha hizi zikiachwa kupelekwa kwenye vyama vya siasa ndio Maendeleo yatapatikana?hivi unadhani mtu aliyekuwa nakunywa pombe zamani then akaacha basi baada ya kuacha fedha zile alizokuwa ananunulia pombe zitaleta mabadiliko nyumbani kwake?
Kabisa binti yangu. Nilikuwa mlevi sana enzi hizo. sikujenga nyumba. Sikulipa karo wanangu wasome vizuri. Nyumbani hawakula vizuri. Mama yangu kule kijijini alitaabika sana. Tangu ni meacha ulevi alihamdulilah mambo yamerekebika mengi. Ruzuku kwa vyama vya siasa ni wizi uliohalalishwa na CCM itaendelea kututesa sana kwa ruzuku hii.
 
Siyo fair kabisa kumlaumu Rostam hata kidogo,

Yeye ni mfanyabiashara na kwa kanuni tukufu za biashara na uchumi, hakuna hata coin moja inaweza kutupwa barabarani labda kama hiyo sehemu itaweza kuzaa nyingine mbili au tatu.

Walaaniwe wale waliorumruhusu RA kuwatumia watu naive kama machela ya kufanyia uchuuzi!!
 
Labda Mushi haupo hapa nchini! Ruzuku ikiondoka leo, jioni hii, kesho CCM haipo. Hawajawahi kuishi bila ruzuku tangu uhuru. Tutafute namna kupunguza kuigharamia SIASA. Usimamizi wa dhati wa BUNGE uwepo. CAG awe huru. TAKUKURU iwe huru. Tume ya MAADILI kwa VIONGOZI iimarishwe. Matatizo kwa MTANZANIA wa kawaida hayatakwisha lakini yatapungua sana tu.

Unasema CAG awe huru,unafikiri tatizo la matumizi mabaya ya fedha ni kwakuwa CAG hayuko huru?
 
Bana eeh,tunajuwa wabunge wanavyofanya kazi bana.Huo umasikini wa Igunga unaonyesha wazi kabisa kuwa haungetatuliwa na haya unayosema ya ruzuku.Hapa tatizo la msingi siyo hilo.Umeelewa mkuu?Kuna wabunge ambao hawakupata utajiri kama yeye na wamesaidia majimbo yao.Ni mapenzi ya mtu kwa taifa na wananchi na si eti mambo ya kuwanyima upinzani na ccm ruzuku.Kwanza nimeshakwambia kuwa ccm hawataathirika.Usizungushe mkuu,mbona husomi posti vyema?Hilo la kutokupewa ruzuku ni debatable lakini halina nafasi kwenye issue hii.Trust me,nionyeshe kivipi lingemsaidia RA kuwaletea maendeleo masikini wa Igunga aliotumia migongo yao na bado kuwaacha masikini wa kutupwa!Bila hata yale mahitaji muhimu ya kibinadamu?Aargh!
Wewe unamwangalia Rostam tu. Ninachosema ni kwamba ondoa ruzuku kwenye vyama hivi kisha peleka pesa yote hiyo kwenye madawati kila mwezi. Ndani ya miezi sita tu nchi nzima hakuna mwanafunzi wa shule ya msingi atakaa chini. USIMAMIZI na UWAJIBIKAJI wa nguvu hata kutwangana risasi uwepo basi.
 
Kabisa binti yangu. Nilikuwa mlevi sana enzi hizo. sikujenga nyumba. Sikulipa karo wanangu wasome vizuri. Nyumbani hawakula vizuri. Mama yangu kule kijijini alitaabika sana. Tangu ni meacha ulevi alihamdulilah mambo yamerekebika mengi. Ruzuku kwa vyama vya siasa ni wizi uliohalalishwa na CCM itaendelea kututesa sana kwa ruzuku hii.
Ni asilimia ngapi ya walioacha pombe fedha zile za pombe zimeleta Maendeleo?CCM ikinyimwa ruzuku Leo watatengeneza njia nyingine za kuiba kama zile za EPA n.k and will survive,CCM ni smart kwa wizi..Wakati wewe unawaza vyama vya siasa viondolewe ruzuku think tank wao wanafikiri njia mbadala ya kukipatia fedha chama chao...
 
Unasema CAG awe huru,unafikiri tatizo la matumizi mabaya ya fedha ni kwakuwa CAG hayuko huru?
Hayuko huru. Hata Regia unajua. Si uliona ile ya juzi ya Jairo? Halafu, mimi niko against kabisa taasisi ya UMMA kama ofisi ya CAG kufanya ukaguzi kwenye taasisi nyingine za umma kama mawizara, mashirika ya umma. Unaikumbuka TAC ya enzi hizo na mashirika ya UMMA? Au COASCO na vyama vya USHIRIKA?
 
Ni asilimia ngapi ya walioacha pombe fedha zile za pombe zimeleta Maendeleo?CCM ikinyimwa ruzuku Leo watatengeneza njia nyingine za kuiba kama zile za EPA n.k and will survive,CCM ni smart kwa wizi..Wakati wewe unawaza vyama vya siasa viondolewe ruzuku think tank wao wanafikiri njia mbadala ya kukipatia fedha chama chao...
Mkiwaruhusu watengeneze njia nyingine na ninyi WABUNGE mpo mnaangalia tu, tutawageuka vibaya. Hawana njia mbadala wakibanwa kisawasawa. Peleka hoja bunge lijalo ruzuku kwa vyama vya siasa iende kwenye madawati angalau kwa mwaka mmoja tu.
 
Binafsi napenda nilingalie hili kwa jicho la tofauti,...tatizo sio rostam,...tatizo ni sera za chama chake.
Hakuna jimbo katika tanzania hii utaenda ukose kuyaona uliyo yaona Igunga,..haijalishi jimbo
hilo linaongozwa na mbunge tajiri wa ccm au mbunge maskini wa chama cha upinzani,...kote hali ni sawa kabisa.

Nimeona picha hapo juu ya watoto wakiwa darasani wamekaa chini wanajifunza kuandika....
Well,hainishtui hata kidogo,...trust me.

Nimesoma shule za serikali,kwanzia vidudu hadi chuo kikuu.
Nasoma UDSM,lakini hakuna tofauti ha hayo unayo yaona kwa watoto kukaa chini.
Labda tofauti tu ni kwamba udsm wanaosoma ni watu wazima kwahiyo hata wakikaa chini watakaa katika
hali ya ku-maintain usafi na unadhifu wao.
Lakini ukweli ni kwamba hata chuo kikuu na kikongwe kabisa Tanzania wasomi wake wanakaa chini wakiwa
wana sikiliza lecture.
(Nikipata nafasi nitatoa picha hapa siku moja)

Sasa kama chuo kikuu katika Tanzania kiko hivo unategemea nini kwa watoto wa shule ya msingi
walio vijijini kabisa?
Ni kawaida kabisa.

Mjini hapa watu wengi wamepanga,wapo wenye hela lakini hazitoshi kujenga,...
tatizo ni sera mbovu za ccm zinazo sababisha bei za bidhaa ya ujenzi kuwa juu.

Tofauti kati ya hawa wa mjini walio panga (nikiwemo mimi) na wale wa vijijini wanao onekana
kanika nyumba za tembe ni kwamba wao wameweza kujenga zao kutokana na kipato chao
hata kama tunaziita mbovu na sisi tumeshindwa kujenga ingawa tunawazidi kipato.

Chimbuko la haya yote ni sera mbovu za CCM,...lakini swali ni je,....
Kuna chama chenye sera nzuri za kuleta maisha mazuri kwa watanzania kweli?
Sidhani

Clemmy,

Sidhani kama umeweza kujua ni nini Regia anasema. Anamlaumu kuwa pamoja na kuwa na influence hakuweza kuzitumia ili kuwekeza Igunga ili angalau pawe na mzunguko wa pesa kiasi kwamba watu wangebadilika.
 
Mi nimesoma Igunga jamani
Kuna shule za msingi madawati yao ni matuta ya udongo
Maji tulikuwa tunafuata km 8 mpaka 10 hivi
Maji hayo tulikuwa tunashare na ng'ombe
Mara nyingi vipindi vya jioni wadada kutokana na asili yao walikuwa hawahudhurii maana walienda kuyasaka maji ili waoge
Wavulana enzi hizo tulikuwa tunaoga mara 2 au 3 ukijitahidi kwa wiki hivi. Yaani siku ya jumamosi na jumatano tu.
Connection ya vijiji ni njia za ng'ombe ati, hizo nimezitumia sana kwa njia ya baiskeli au wakati mwingine miguu
 
Nimeamua kuandika habari hii baada ya kujishauri tangu nikiwa Igunga!

Rostam Aziz amekuwa Mbunge wa Igunga tangu mwaka 1994 ambapo mpaka sasa ni takribani miaka 17 chini ya uongozi wake. Nilikuwa sijawahi kufika Igunga kabla hivyo sikuifahamu ilivyo.Siku Rostam anajiuzulu alieleza mafanikio mengi aliyoyafanya Igunga nikadhani Igunga hali ni shwari na watu wanamaendeleo mazuri,nilivyofika sikuamini nilichokiona. Rostam alitudanganya. Katika tembea yangu yote hapa nchini sijawahi kuona Wananchi wanashida kama wa Igunga.

Mambo yafuatayo nimeyagundua katika jimbo la Igunga;

1. Wananchi wengi wa Jimbo la Igunga hawajui kusoma na kuandika mpaka vijana wadogo

2. Wananchi wengi wa Igunga wanatembea hadi Kilomita 13 kufuata maji kwenye Makomero tena maji yenyewe sio safi wala salama

3. Wananchi wengi wa Igunga wanatembea hadi Kilomita 10 kufuata shule,wengine wanaenda hadi 20

4. Kwenye kata nilizopita hawaelewi wala kuzijua shule za awali.

5. Wananchi wengi wanatembea umbalimrefu kufuata Zahanati na hayo majengo yenyewe ya Zahanati unaweza kulia.

6. Hakuna barabara za kuunganisha kijiji kimoja na kingine,njia zilizopo ni mapitio ya ng'ombe.

7. Wananchi wengi hawana vyoo wala hawana mpango wa Kujenga vyoo,wao wajenga mabafu tu yanayotumika kuogea na kujisadia haja ndogo,haja kubwa utajua mwenyewe.

8. Zipo Kata ambazo hazing mawasiliano ya simu

9. Lipo Kabila mpaka leo wanatembea uchi kama kwa King Muswati.

10. Wapo wanaotembea karibu Kilomita 13 kufuata TV waone taarifa ya habari na mambo mengine. Hii ni Kata anayotoka Dr. Kafumu

11. Na mengine mengi madogo madogo.

Rostam alikuwa na uwezo wa kupunguza hayo niliyoyataja kwasababu zifuatazo

1. Alikuwa ni Mbunge hivyo alikuwa na fursa ya kupiga kelele ndani na nje ya Bunge na akasililizwa.
2. Alikuwa Mbunge mwenye ushawishi ndani ya chama chake hivyo angeweza kushawishi Mawaziri ili miradi iende Jimboni kwake.
3. Alikuwa Mbunge tajiri sana,kama aliweza kuipa CCM,Mabilioni ya shillingi,Kama aliweza kuhonga watu mbalimbali mamilioni ya shilingi alishindwaje kusaidia Jimboni kwake? aliishia kuwanunulia tu simu Mabalozi wa Nyumba Kumi ili wamfanyie Kampeni.
4. Alikuwa anafahamiana na wafadhili wengi tu wa Maendeleo wa ndani na nje ya nchi alishindwaje kuwashawishi wawekeze kwake?

Rostam aliyaweza haya yote lakini hakujali kwakuwa hakuwa na lengo la kuwatumikia Wananchi wa Igunga. Kwasababu hizo basi nashawishika kusema kuwa Rostam ni zaidi ya DUBWANA ni mtu anayeongoza kwa roho mbaya hapa nchini. Hana huruma hata kidogo, anajali maslahi yake tu.. Bora ulivyojiuzulu, ungejiuzulu na utanzania kabisa, ukaombe uraia wa nchi nyingine huko ughaibuni sio Afrika!

Nawasilisha!

Chadema mngetumia 30% ya hela mliyotumia kugombea madaraka ya ubunge mgeweza kusaidia mojawapo la matatizo uliyoyataja hapo juu!

Je mko tayari kama chama kuhMIAH resources zenu katika kuleta maendeleo na siyo kugmbea madaraka by any means necessaary?
 
Hayuko huru. Hata Regia unajua. Si uliona ile ya juzi ya Jairo? Halafu, mimi niko against kabisa taasisi ya UMMA kama ofisi ya CAG kufanya ukaguzi kwenye taasisi nyingine za umma kama mawizara, mashirika ya umma. Unaikumbuka TAC ya enzi hizo na mashirika ya UMMA? Au COASCO na vyama vya USHIRIKA?

Nadhani hujanielewa sijapinga kuwa CAG yuko huru nilichosema je kwakuwa CAG hayuko huru ndio sababu ya matumizi mabaya ya fedha za umma?
 
Mkiwaruhusu watengeneze njia nyingine na ninyi WABUNGE mpo mnaangalia tu, tutawageuka vibaya. Hawana njia mbadala wakibanwa kisawasawa. Peleka hoja bunge lijalo ruzuku kwa vyama vya siasa iende kwenye madawati angalau kwa mwaka mmoja tu.

Sijasema kuwa tutawaruhusu nilichosema kuwa wanaweza kutengeneza njia za kuiba ili wapate fedha kwenye chama chao!
 
Nimeamua kuandika habari hii baada ya kujishauri tangu nikiwa Igunga!

Rostam Aziz amekuwa Mbunge wa Igunga tangu mwaka 1994 ambapo mpaka sasa ni takribani miaka 17 chini ya uongozi wake. Nilikuwa sijawahi kufika Igunga kabla hivyo sikuifahamu ilivyo.Siku Rostam anajiuzulu alieleza mafanikio mengi aliyoyafanya Igunga nikadhani Igunga hali ni shwari na watu wanamaendeleo mazuri,nilivyofika sikuamini nilichokiona. Rostam alitudanganya. Katika tembea yangu yote hapa nchini sijawahi kuona Wananchi wanashida kama wa Igunga.

Mambo yafuatayo nimeyagundua katika jimbo la Igunga;

1. Wananchi wengi wa Jimbo la Igunga hawajui kusoma na kuandika mpaka vijana wadogo

2. Wananchi wengi wa Igunga wanatembea hadi Kilomita 13 kufuata maji kwenye Makomero tena maji yenyewe sio safi wala salama

3. Wananchi wengi wa Igunga wanatembea hadi Kilomita 10 kufuata shule,wengine wanaenda hadi 20

4. Kwenye kata nilizopita hawaelewi wala kuzijua shule za awali.

5. Wananchi wengi wanatembea umbalimrefu kufuata Zahanati na hayo majengo yenyewe ya Zahanati unaweza kulia.

6. Hakuna barabara za kuunganisha kijiji kimoja na kingine,njia zilizopo ni mapitio ya ng'ombe.

7. Wananchi wengi hawana vyoo wala hawana mpango wa Kujenga vyoo,wao wajenga mabafu tu yanayotumika kuogea na kujisadia haja ndogo,haja kubwa utajua mwenyewe.

8. Zipo Kata ambazo hazing mawasiliano ya simu

9. Lipo Kabila mpaka leo wanatembea uchi kama kwa King Muswati.

10. Wapo wanaotembea karibu Kilomita 13 kufuata TV waone taarifa ya habari na mambo mengine. Hii ni Kata anayotoka Dr. Kafumu

11. Na mengine mengi madogo madogo.

Rostam alikuwa na uwezo wa kupunguza hayo niliyoyataja kwasababu zifuatazo

1. Alikuwa ni Mbunge hivyo alikuwa na fursa ya kupiga kelele ndani na nje ya Bunge na akasililizwa.
2. Alikuwa Mbunge mwenye ushawishi ndani ya chama chake hivyo angeweza kushawishi Mawaziri ili miradi iende Jimboni kwake.
3. Alikuwa Mbunge tajiri sana,kama aliweza kuipa CCM,Mabilioni ya shillingi,Kama aliweza kuhonga watu mbalimbali mamilioni ya shilingi alishindwaje kusaidia Jimboni kwake? aliishia kuwanunulia tu simu Mabalozi wa Nyumba Kumi ili wamfanyie Kampeni.
4. Alikuwa anafahamiana na wafadhili wengi tu wa Maendeleo wa ndani na nje ya nchi alishindwaje kuwashawishi wawekeze kwake?

Rostam aliyaweza haya yote lakini hakujali kwakuwa hakuwa na lengo la kuwatumikia Wananchi wa Igunga. Kwasababu hizo basi nashawishika kusema kuwa Rostam ni zaidi ya DUBWANA ni mtu anayeongoza kwa roho mbaya hapa nchini. Hana huruma hata kidogo, anajali maslahi yake tu.. Bora ulivyojiuzulu, ungejiuzulu na utanzania kabisa, ukaombe uraia wa nchi nyingine huko ughaibuni sio Afrika!

Nawasilisha!

Huyu burushi aliyeigia bungeni kwa ticket ya CCM alikuwa amekaa kibiashara zaidi. Haya mambo ya maendeleao ya wananchi mnamuonea bure tu. Ndiyo maana alikuwa ananunua kura kwa kutoa rushwa na kimsingi bishara na wapiga kura ilikuwa ikikamilika mara anapochaguliwa kwenda bungeni. Ni kweli haya matatizo ya wananchi na mambo ya maendeleo uliyoyaongea hapo juu yanamhusu mbunge, lakini siyo kitu cha msingi kilichomsukuma Rostam kuingia kwenye siasa za nchi hii. Kilichompeleka CCM na hatimaye kwenye ubunge/uraisi ni vitu kama Kagoda, Richmond, Dowans na mengine kama hayo ambayo mimi nadhani amefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana.
 
dada yangu regia umesema vyema lakini hivi hakuna matatizo kwenye majimbo yenu wapendwa wapinzani?
 
Mkuu Regia, mafisadi ndivyo walivyo...hutoa vijisenti vichache tu hapa na pale ili waonekane wanasaidia wananchi majimboni na huku wao wakineemeka kwa mabilioni.
 
Nadhani hujanielewa sijapinga kuwa CAG yuko huru nilichosema je kwakuwa CAG hayuko huru ndio sababu ya matumizi mabaya ya fedha za umma?

Hivi huko uliko kilombero ndio kuna miundo mbinu mizuri kuliko Igunga? don't fool people

Kilombero wamechoka the same way like igunga..anza kutengeneza huko kwenu kabla ya kuja na hoja nyepesi

Unatafuta emotional support than realiaties on the ground!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom