Kwa biti la Kagame wasithubutu tena kupeleka vikosi Goma

Kwa biti la Kagame wasithubutu tena kupeleka vikosi Goma

Kama kawaida yake jana Kagame ametoa biti nzito sana kwa wanaoitishia Rwanda kupitia mgoggoro wa Congo.

Kwa dharau sana kawaita nchi za SADC zilizopeleka vikosi vyake Bukavu na Goma " Confused brothers and Sisters" yaaani kaka zetu na dada zetu waliochanganyikiwa.

Hakuwaacha hapo tu, kawaambia mlichokipata safari hii ni sehemu ndogo tu ya mtakachokipata mkijaribu tena kuleta vikosi vyenu kupambana na Rwanda.

Maneno haya ya Kagame ni ujumbe tosha kwa JWTZ kuwa wajikite kwenye professionalism maana CCM wanavyowaingilia mpaka saivi wamekuwa kituko hadi kwa majirani zetu.

Hongereni CCM kwa kuifanya Tanzania saivi kuwa kituko cha karne.
Wakati huo huo KDF imeanza mazungumzo na kampuni moja bora ya Israel inayotengeneza Air defense system....
Sisi tuendelee tu kufungua viwanda vya kuponda kokoto na kujitapa kuwa jeshi la sita kwa ubora Duniani.
 
Kama kawaida yake jana Kagame ametoa biti nzito sana kwa wanaoitishia Rwanda kupitia mgoggoro wa Congo.

Kwa dharau sana kawaita nchi za SADC zilizopeleka vikosi vyake Bukavu na Goma " Confused brothers and Sisters" yaaani kaka zetu na dada zetu waliochanganyikiwa.

Hakuwaacha hapo tu, kawaambia mlichokipata safari hii ni sehemu ndogo tu ya mtakachokipata mkijaribu tena kuleta vikosi vyenu kupambana na Rwanda.

Maneno haya ya Kagame ni ujumbe tosha kwa JWTZ kuwa wajikite kwenye professionalism maana CCM wanavyowaingilia mpaka saivi wamekuwa kituko hadi kwa majirani zetu.

Hongereni CCM kwa kuifanya Tanzania saivi kuwa kituko cha karne.
Andiko lako halina hoja.
 
Hayo ni maneno tu kamwe hawezi chezea jeshi imara na lenye nguvu kama jwtz,akumbuke lilikwenda kulinda Amani kwa kivuli cha SADC na sio kwamba maamuzi yalikuwa yanatokea Lugalo,ajaribu kuingia Karagwe au Ngara hata robo kilomita athibitishe maneno yake aone,Ushauri hapa tujihadhari sana kwenye mfumo wa jeshi letu na wanasiasa waliache kabisa lifanye utaratibu wa Ajira zake lenyewe isije ikawa kama Jeshi la Irani ndani yake Kuna MOSSAD,tujihadhari sana na hilo
Wanasiasa wameshalifikia pia Tiss nao Inatakiwa wabadilike baada ya kulinda kikundi cha watu wa chache ambao ni wanasiasa wawe wazalendo kwa nchi
 
Wanasiasa wameshalifikia pia Tiss nao Inatakiwa wabadilike baada ya kulinda kikundi cha watu wa chache ambao ni wanasiasa wawe wazalendo kwa nchi
Haya ndo matokeo ya vyombo vya ulinzi na usalama kugeuka kuwa vikaragosi vya Wanasiasa.

Tiss na JWTZ saivi ni mwendo wa kujipendekeza kwa viongozi wa CCM ili wapate ulaji. Hawawazi chochote kuhusu maslahi mapana ya Taifa. Wao maslahi mapana ya Taifa ni kukandamiza upinzani na wananchi ili CCM waendelee kulila hili Taifa na kuneemeka.
 
Unajigambq wakati kawatia adabu hapo Goma

Heb nielekez3 vizuri with reference and citation where necessary, 1. wale M23 ni kagame ??

2. JWTZ imekabliqna wapi na jeshi la RWANDA. ??
au Kikosi cha SADEC cha SAMI ni cha JWTZ .??

heb nielekeze kama ni cha JWTZ. unambie battalion gani na kambi GANI. . With reference of Numbers mana kila battalion na kambi zinajylikanq kwa namba mkuu.

Yani kikosi kipigwe af kombania yake imepoa tu. Why hawakwenda kutoa msaada .....
 
JWTZ Ipo imara mno

Hakuna jeshi east and central afrika la kuikoromea JWTZ!!

Naongea by experience in side!!
Experience gani mkuu,Hao wametandikwa vibaya sana hapo congo

Vita ni silaha na teknolojia sio kelele,Rwanda amewekeza silaha za kisasa na drones za kisasa

Ana uwezo wa kukupiga toka kigali mpaka Dar es Salaam kwa tech tu

Huko congo waliomba msamaha akawaambia JWTZ waondoke maana walikuwa tayari mateka na akawakagua wakati wa kuondoka ,Clip zipo
 
Heb nielekez3 vizuri with reference and citation where necessary, 1. wale M23 ni kagame ??
M23 ni Wakongo ila wanapewa Nguvu na askari wa Kagame, chini ya Kagame kwa silaha, biashara na kila kitu kama alivyowapa nyie nafasi ya kupita kwake baada ya kupigika huko DRC baada ya kuwakagua mpaka CHUPI..
2. JWTZ imekabliqna wapi na jeshi la RWANDA. ??
au Kikosi cha SADEC cha SAMI ni cha JWTZ .??
Kwani askari wa JWTZ wanaozikwa kila mwaka wanatoka wapi?

Whatever ilikuwa SAMIDRC au SADC, JWTZ walikuwemo
heb nielekeze kama ni cha JWTZ. unambie battalion gani na kambi GANI. . With reference of Numbers mana kila battalion na kambi zinajylikanq kwa namba mkuu.
Askari wa JWTZ wanaokufa kila mwaka huko Congo wanatoka battalion ipi?
Yani kikosi kipigwe af kombania yake imepoa tu. Why hawakwenda kutoa msaada .....
Unapoa kwasababu unayepigana naye anakujua nje ndani, maana silaha zako unanunua kwa Lugumi ambaye ni mtu wake
 
Kama alijuwa sadc itafeli hakutakiwa kulipeleka jeshi kule

Na huo ndio ulikuwa ushauri wa JWTZ

Aliupuuza!.
Hivi wewe unafahamu kazi za Jeshi kweli kwa katiba yetu.?Na unafahamu kofia ya Rais kama amiri jeshi mkuu?

Jirani ana angamia na wewe unapakana nae lazima umsaidie kwani yakiharibika yatahamia upande wako ni hesabu za kawaida kabisa kwenye uchumi au siasa

Athari za wakimbizi ni mbaya zaidi kuliko kumsaidia jirani

Jeshi letu lilishindwa huko kongo,Walienda kwa mbwmbwe za kupiga kunguru mweusi wakarudi mateka kupitia Rwanda
 
Kagame kachanganyikiwa.Kwanza alitaka kugomea kusaini ule mkataba wa Amani na Congo kule Marekani,Trump akamwambia hutokuwa na nafasi ya kujificha hata msituni tutakufyeka asubuhi tu, Rwanda ikabidi isaini,juzi kiongozi wa M23 kapishana na Rwanda juu ya huo mkataba jamaa ana ambition za kufika Kishansa Rwanda wanasema hapana Kuna mkataba na jamaa kakaza,alipoona M23 wamekaza akaleta ujuaji kwa Congo Tena Congo wamemjibu tuna utekelezaji wa mkataba vinginevyo tunamwambia bwana mkubwa umegoma.Rwanda imepoteza Congo imeshinda.Kagame analia Tishekedi anacheka.Kagame yuko kwenye Destination haelewi hatima yake. Tishekedi aliweka mawazili diaspora ndio waliomsaidia kumzidi maarifa Kagame.Muacheni abweke.
Umeandika utumbo sijui kama unaelewa, yani mtu kashavamia nyumbani kwako akachukua vyumba kadhaa akawa anaishi kama kwake, anakuja kutaka kukutoa chumbani kwako unamwambia heshimu mkataba ukiingia chumbani kwangu naenda kukusemea alafu unasema umeshinda?
 
Dhaifu wakati kawapiga mkong'oto hadi mkaomba poo. Kasema hadi akaamua kuwaruhusu mpitishe mizigo yenu na silaha zenu kupitia nchini kwake maana la sivyo mngeuwawa wote
Wameondoka hadi wakasahau viatu...naona makorokoro ya JWTZ huko Chato na majuzi nimewapita hapo Nyakanazi na makontena yao wanatafuta pa kwenda.
 
M23 ni Wakongo ila wanapewa Nguvu na askari wa Kagame, Kagame kwa silaha, biashara na kila kitu kam.alivyowapa nyie nafasi ya kuoita kwake baada ya kupigika huko DEC.

Kwani askari wa JWTZ wanaozikwa kila mwaka wanatoka wapi?

Whatever ilikuwa SAMIDEC au SADC, JWTZ walikuwemo

Askari wa JWTZ wanaokufa kila mwaka huko Congo wanatoka battalion ipi?

Unapoa kwasababu unayepigana naye anakujua nje ndani, maana silaha zako unanunua kwa Lugumi ambaye ni mtu wake
Umemjibu vizuri sana. Asipoelewa basi yeye ni kilaza wa mwisho kabisa duniani.
 
Kama kikosi kinachopigwa kina baadh ya askance wa tz basi hilo sio jesh la tz.... hizo ni fursa tu zinatolewa kwa vijana waende kama ajira... sheria na myenendo ya huko haigusiani na tz moja kwa moja..

Ukiongelea JWTZ kama ni kikosi basi Sema
Kikosi gani kilipigana na rwanda – kipo chini ya Koplo / Sajenti nani ??.. Kama sio chetu ila kina baadh ya Ascari wetu basi sio chetu.

kiliposhindwa ilipaswa kisaidiwe moja kwa moja na sasa inapaswa tujue ni Kombania gani ilienda ku backup – na ipo chini ya Kapteni / Meja gani ?? Mzembe mzembe

Ikiwa kombania ilishindwa nambie inatokea kwenye Batalioni gani na ipo chini ya Kanali Gani ? asokuwa mwajibikaji hivyo ??

heb nipe taarifa za Brigedi ya hiyo battalion ilofeli kumchqpq mranda walipokutana na usisaha Brigedia Jenerali Anaeiongoza. Ongeza na taarifa za Divisheni na Meja Jenerali pia kwa hapa TZ tuna
Kundi la Majeshi (Corps) ambalo lipo chini ya Luteni Jenerali
Acha kulisema Jeshi Kuu (Army) na Jenerali wake kiboya boyq mze.

JESHI SIO WANA SIASA WENU WAIMBA TAARAB HAO.
 
Wameondoka hadi wakasahau viatu...naona makorokoro ya JWTZ huko Chato na majuzi nimewapita hapo Nyakanazi na makontena yao wanatafuta pa kwenda.
Kuna neno kaliongea walitafakari. Kasema sie tuna uwezo wa kupigana na kutembea kilometres zaidi ya 2000 kufika mlipo na kuwafanyizia.

Ukiangalia kilomita 2000 ni umbali wa Kigali hadi Dar es Salaam.
 
Jeshi letu limegeuzwa kituko. Mbona mambo hayakuaga hivi huko nyuma.
 
Back
Top Bottom