Kwa biti la Kagame wasithubutu tena kupeleka vikosi Goma

Kwa biti la Kagame wasithubutu tena kupeleka vikosi Goma

Kama kikosi kinachopigwa kina baadh ya askance wa tz basi hilo sio jesh la tz.... hizo ni fursa tu zinatolewa kwa vijana waende kama ajira... sheria na myenendo ya huko haigusiani na tz moja kwa moja..

Ukiongelea JWTZ kama ni kikosi basi Sema
Kikosi gani kilipigana na rwanda – kipo chini ya Koplo / Sajenti nani ??.. Kama sio chetu ila kina baadh ya Ascari wetu basi sio chetu.

kiliposhindwa ilipaswa kisaidiwe moja kwa moja na sasa inapaswa tujue ni Kombania gani ilienda ku backup – na ipo chini ya Kapteni / Meja gani ?? Mzembe mzembe

Ikiwa kombania ilishindwa nambie inatokea kwenye Batalioni gani na ipo chini ya Kanali Gani ? asokuwa mwajibikaji hivyo ??

heb nipe taarifa za Brigedi ya hiyo battalion ilofeli kumchqpq mranda walipokutana na usisaha Brigedia Jenerali Anaeiongoza. Ongeza na taarifa za Divisheni na Meja Jenerali pia kwa hapa TZ tuna
Kundi la Majeshi (Corps) ambalo lipo chini ya Luteni Jenerali
Acha kulisema Jeshi Kuu (Army) na Jenerali wake kiboya boyq mze.

JESHI SIO WANA SIASA WENU WAIMBA TAARAB HAO.
Endelea kuleta siasa za ki CCM kwenye masuala ya msingi.

Wenzetu wameuwawa, wamedharirishwa saivi wamepewa hadi njia ya kurudi nyumbani kwa huruma tu wewe unaleta tantalila zako za ki uvccm hapa.

Huo upumbavu wenu ndo mana Taifa linazidi kuwa kituko.
 
Wameondoka hadi wakasahau viatu...naona makorokoro ya JWTZ huko Chato na majuzi nimewapita hapo Nyakanazi na makontena yao wanatafuta pa kwenda.
Ni aibu. Kagame kawadhalilisha vibaya mno.
 
Wakati huo huo KDF imeanza mazungumzo na kampuni moja bora ya Israel inayotengeneza Air defense system....
Sisi tuendelee tu kufungua viwanda vya kuponda kokoto na kujitapa kuwa jeshi la sita kwa ubora Duniani.
Hiyo takwimu ya kuwa Jwtz ni jeshi la 6 bora duniani mmeitoa wapi?
 
Trump kesha maliza vita. Kagame asipo jiangalia Trump atatuma ndege.
Labda Kagame anataka kuwadanganya watu wake huo mgogoro ameumaliza yeye kwa kuwashikisha adabu vikosi alivyovisema. Watu wa aina yake huwa janjajanja sana.
 
Endelea kuleta siasa za ki CCM kwenye masuala ya msingi.

Wenzetu wameuwawa, wamedharirishwa saivi wamepewa hadi njia ya kurudi nyumbani kwa huruma tu wewe unaleta tantalila zako za ki uvccm hapa.

Huo upumbavu wenu ndo mana Taifa linazidi kuwa kituko.

Ujinga wenu wa kuwa na wrong approaches na wrong corners to attack msitake kuwatwisha wengine.
 
Kuna neno kaliongea walitafakari. Kasema sie tuna uwezo wa kupigana na kutembea kilometres zaidi ya 2000 kufika mlipo na kuwafanyizia.

Ukiangalia kilomita 2000 ni umbali wa Kigali hadi Dar es Salaam.
Kutoka Kigali hadi Kinshasa, ndicho anachomaanisha, SADC kwa kimbele mbele chao walijikuta wamenunua ugomvi usiowahusu.
 
Hiyo takwimu ya kuwa Jwtz ni jeshi la 6 bora duniani mmeitoa wapi?
Muulize msemaji wa jeshi hizo ranking za majeshi alizitoa wapi hadi kuzitangaza hadharani.
 
Kagame ni sisimizi tu.

Anatumia propaganda dhaifu za vitisho, kwanza yule tunamtumia MIGAMBO tu wamnyooshe na kakijiji chake cha Rwanda.

JWTZ ni jeshi lenye hadhi ya juu sana haliwezi kushindanishwa na huyo KIJITI mwenye afya GOIGOI.

Huu ndio wakati wa akina Lucas Mwashambwa na migambo wenzake akina ChoiceVariable kuchangamkia fursa na kwenda kumtwanga huyo KIJITI WA RWANDA.
Alifanya makosa kuwaleta mateka wakiwa hai.. ndiyo maana machawa mnaongea,mngeletewa masanduku..mngepata akili
 
Kama kawaida yake jana Kagame ametoa biti nzito sana kwa wanaoitishia Rwanda kupitia mgoggoro wa Congo.

Kwa dharau sana kawaita nchi za SADC zilizopeleka vikosi vyake Bukavu na Goma " Confused brothers and Sisters" yaaani kaka zetu na dada zetu waliochanganyikiwa.

Hakuwaacha hapo tu, kawaambia mlichokipata safari hii ni sehemu ndogo tu ya mtakachokipata mkijaribu tena kuleta vikosi vyenu kupambana na Rwanda.

Maneno haya ya Kagame ni ujumbe tosha kwa JWTZ kuwa wajikite kwenye professionalism maana CCM wanavyowaingilia mpaka saivi wamekuwa kituko hadi kwa majirani zetu.

Hongereni CCM kwa kuifanya Tanzania saivi kuwa kituko cha karne.
Kagame kwa kweli amekuwa mtu wa kelele nyingi siku hizi, sijui ana shida gani hasa. Wanasema debe tupu hupiga kelele sana, na binafsi sidhani kama ana jeshi imara kama anavyotaka watu waamini. Badala yake, anazidi kujenga hofu isiyo na msingi, akionekana kuwa na woga hata wa kivuli chake mwenyewe. Sasa, anapowaita members wa SADC 'confused', anamaanisha nini hasa? Je, amejigeuza kuwa msemaji rasmi wa M23? Maelezo yake yamejaa kejeli na dharau zisizo na tija kwa ukanda huu.
 
Labda Kagame anataka kuwadanganya watu wake huo mgogoro ameumaliza yeye kwa kuwashikisha adabu vikosi alivyovisema. Watu wa aina yake huwa janjajanja sana.
Kwani vikosi vya SADC wakiwemo JWTZ hawajashikishwa adabu?
 
Kagame kwa kweli amekuwa mtu wa kelele nyingi siku hizi, sijui ana shida gani hasa. Wanasema debe tupu hupiga kelele sana, na binafsi sidhani kama ana jeshi imara kama anavyotaka watu waamini. Badala yake, anazidi kujenga hofu isiyo na msingi, akionekana kuwa na woga hata wa kivuli chake mwenyewe. Sasa, anapowaita members wa SADC 'confused', anamaanisha nini hasa? Je, amejigeuza kuwa msemaji rasmi wa M23? Maelezo yake yamejaa kejeli na dharau zisizo na tija kwa ukanda huu.
Kama jeshi lenu na TISS wamegeuka vikaragosi na machawa wa wanasiasa wasio na akili CCM kwa nini asiwadharau?

Katiba tu mnashindwa kuiheshimu mnaiendesha nchi hivyo hovyo tu ndo mtaweza kushindana na watu wanaotumia akili kuishi?
 
Vita haipigani hotubani, Kagame ni bingwa wa hotuba. Hatujanza leo kupeleka wanajeshi walinde amani Congo. Arushe kombora litue tuu hapo Rusumo mlimani, aone kama ipo vipi.
Kuna kila dalili anawamudu.

Nyie kazi yenu kubweka tu.

Pelekeni UVCCM wakapigane basi
 
Naomba kuchangia Uzi huu.

Kwanza mnaoidharau Rwanda kijeshi futeni hiyo mentality, ni nchi ambayo kiongozi wake amejidhatiti kuunda JESHI imara, utii na lenye ufanisi mkumbwa sana.
RDF ni moja ya majeshi ya kisasa kabisa Afrika hii.

Silaha kubwa ya JESHI LA RDF ni intelijensia Bora sana. Mnaweza msiamini hata ndani ya vyombo muhimu vya kiulinzi na kimaamuzi Kuna maajenti wa Rwanda. Serikali ya nchi yenu imefumbia macho ambapo wanyarwanda wameshika madaraka na nyazifa muhimu kwenye serikali ya JMT.

Je, Tanzania mtaweza kipi dhidi Yao? Mmeruhusu rushwa mpaka namna ya ku recruit vijana kuwaingiza kwenye JESHI letu, je, serikali ya Rwanda itasita kutoa mafungu Kwa akili ya maafisa walafi Ili wawaingize vijana wao jeshini?
Mkuu wa majeshi Afande J.J Mkunda alisisitiza kihusu raia wa kigeni kupata teuzi serikalini but who cares?

Tanzania inakuwa nchi kubwa yenye ushabiki wa kijinga katika mpira na siasa chafu zisizo na manufaa kwetu.

Kagame anajua by numbers haiwezi Tanzania lakini yeye kaja na njia ya kujua mmeamkaje, mmekula Nini, mmefanya Nini na mnatarajia kufanya Nini.
Rwanda wako smart kuliko mnavyodhani, JESHI letu tumelifanya butu Kwa sababu ya siasa za kishabiki, haliko huru Tena kiasi kwamba mwenyekiti wa Chama mkoa ana nafasi ya kumpa maagizo kamanda wa kijeshi.

SILAHA
RDF inaendelea kujiimarisha Kwa silaha za kisasa zaidi toka Kwa washirika wake wakubwa Russia na China.
RDF Ina mifumo Bora zaidi ya Air Defense Systems kuliko nchi zote za ukanda wa EAC ukiacha Ethiopia.

RDF ina viwanda vya ndani Kwa ajili ya light weapons na APCs ( magari ya delaya).
RDF ina attack and utility helicopters ambazo Zina uwezo wa kushambulia toka mbali Kwa mvua ya mashambulizi ya risasi na makombora ya masafa madogo.
Nimetaja silaha zao muhimu tu ( na zinazojulikana wazi) ambazo Kwa asilimia kubwa wapinzani wa Rwanda hawana.

Vita na Rwanda siyo sawa na Malawi Bali ni kazi pevu inayoitaka Tanzania kukaa chini na kuvipa uhuru, uwezo vyombo vya ulinzi.

Hitimisho:
Taifa letu🇹🇿 tunalipenda sana, lakini tusijiaminishe Kwa uwezo wetu wenyewe. Tujiimarishe zaidi.
 
Mama Samia ni chombo cha neema kwa Tanzania — uongozi wake ni taa ya matumaini, dira ya maendeleo na alama ya hekima. 2030 tupo tayari
 
Back
Top Bottom