Kwa biti la Kagame wasithubutu tena kupeleka vikosi Goma

Kwa biti la Kagame wasithubutu tena kupeleka vikosi Goma

Kagame ni sisimizi tu.

Anatumia propaganda dhaifu za vitisho, kwanza yule tunamtumia MIGAMBO tu wamnyooshe na kakijiji chake cha Rwanda.

JWTZ ni jeshi lenye hadhi ya juu sana haliwezi kushindanishwa na huyo KIJITI mwenye afya GOIGOI.

Huu ndio wakati wa akina Lucas Mwashambwa na migambo wenzake akina ChoiceVariable kuchangamkia fursa na kwenda kumtwanga huyo KIJITI WA RWANDA.
Hahahahaa eti kijiti, mkuu hii ni too much.
 
Semeni vyoooote, ila Jeshi la TZ ni jeshi imara as up now. Halijawahi shindwa any private major operation na halijawah.

KIKWETE alisema hivi, tutakuwa wa mwisho kufanya kitu chochote kibaya, ....... kipindi kile Kagame akabaki anabweka tu mda wote hakuanzisha shambulio kicha kwamba Kikwete alimwambia anza kupiga sisi hatuta anza mpaka uanze wewe ,

na hata Leo ajarib yeye mana sisi huwa hatuna porojo kama NCHI Bali tuna matendo .... anaeona sisi dhaif aanze kupiga tumwonyesho tulichomfanya DADA.
 
JWTZ Ipo imara mno

Hakuna jeshi east and central afrika la kuikoromea JWTZ!!

Naongea by experience in side!!
Kwa technology ya Sasa hivi naona kama Kambi za jwtz zipo uchi wa mnyama..Hasta drones za kawaida zinaweza teketeza Kambi yote ya Lugalo.Hatujui kagame nyuma yupo nani?Tujifunze Kwa urusi mpaka leo anasumbuliwa na Ukraine 🤔
 
Jeshi ni discipline, kama una jeshi kubwa na vifaa kama huna weledi ni bure. Weledi unajengwa na vitu vidogo kama usiibe, usiseme uwongo, heshima etc
 
Dhaifu wakati kawapiga mkong'oto hadi mkaomba poo. Kasema hadi akaamua kuwaruhusu mpitishe mizigo yenu na silaha zenu kupitia nchini kwake maana la sivyo mngeuwawa wote
Hunaga akili wewe,Unashindwa kutofautisha vita na operation tena ambayo inajumuisha vikosi washirika.Kwa hiizo akili zako ndogo unaona rwanda anakipi chakuisumbua Jwtz.Tumia akili zako zakuzaliwa bila mihemko ulete majibu sahihi.
 
Kama kawaida yake jana Kagame ametoa biti nzito sana kwa wanaoitishia Rwanda kupitia mgoggoro wa Congo.

Kwa dharau sana kawaita nchi za SADC zilizopeleka vikosi vyake Bukavu na Goma " Confused brothers and Sisters" yaaani kaka zetu na dada zetu waliochanganyikiwa.

Hakuwaacha hapo tu, kawaambia mlichokipata safari hii ni sehemu ndogo tu ya mtakachokipata mkijaribu tena kuleta vikosi vyenu kupambana na Rwanda.

Maneno haya ya Kagame ni ujumbe tosha kwa JWTZ kuwa wajikite kwenye professionalism maana CCM wanavyowaingilia mpaka saivi wamekuwa kituko hadi kwa majirani zetu.

Hongereni CCM kwa kuifanya Tanzania saivi kuwa kituko cha karne.
Kile kilikuwa "kipande kidogo" cha Jeshi letu kama mchango kwenye Jeshi la SADC. Na Jeshi lolote lililo kwenye "International Mission" halijihusishi na "Full Combat". Sio mnaelewa ninyi wapuuzi?

Hao sio JWTZ na JWTZ haihangaiki na Kagame wala na Jeshi lake. Kuna mahali katamka JWTZ? Kama mnamwamini sana ( ila msije mkamdanganya akaingia mkenge) mwambieni aitishie Tanzania au Jeshi lake (JWTZ) as an entity! Mwambieni basi wapuuzi nyie tuone huo utemi wake!

Kama hamuwezi kaeni kimya kabisa!
 
Kagame ni sisimizi tu.

Anatumia propaganda dhaifu za vitisho, kwanza yule tunamtumia MIGAMBO tu wamnyooshe na kakijiji chake cha Rwanda.

JWTZ ni jeshi lenye hadhi ya juu sana haliwezi kushindanishwa na huyo KIJITI mwenye afya GOIGOI.

Huu ndio wakati wa akina Lucas Mwashambwa na migambo wenzake akina ChoiceVariable kuchangamkia fursa na kwenda kumtwanga huyo KIJITI WA RWANDA.
unamuita kijiti wakati wakaka na wadada wa sadc wamenyoosha mikono juu na kuondoa vikosi vyake huko goma
 
JWTZ Ipo imara mno

Hakuna jeshi east and central afrika la kuikoromea JWTZ!!

Naongea by experience in side!!
Uimara wa Jeshi ni wananchi wake.

Vita ya Kagera kila mwananchi alishiriki na kila kijana mwenye afya alibeba silaha.

Hata uwe na jeshi bora kiasi gani ila kama wananchi wako hawako na wewe UTAPIGWA VIBAYA sana
 
Kama kawaida yake jana Kagame ametoa biti nzito sana kwa wanaoitishia Rwanda kupitia mgoggoro wa Congo.

Kwa dharau sana kawaita nchi za SADC zilizopeleka vikosi vyake Bukavu na Goma " Confused brothers and Sisters" yaaani kaka zetu na dada zetu waliochanganyikiwa.

Hakuwaacha hapo tu, kawaambia mlichokipata safari hii ni sehemu ndogo tu ya mtakachokipata mkijaribu tena kuleta vikosi vyenu kupambana na Rwanda.

Maneno haya ya Kagame ni ujumbe tosha kwa JWTZ kuwa wajikite kwenye professionalism maana CCM wanavyowaingilia mpaka saivi wamekuwa kituko hadi kwa majirani zetu.

Hongereni CCM kwa kuifanya Tanzania saivi kuwa kituko cha karne.
Kwa yanayo endelea ccm kila kitu kinawezekana... Mtanielewa baada ya Oct2025
 
Kagame kachanganyikiwa.Kwanza alitaka kugomea kusaini ule mkataba wa Amani na Congo kule Marekani,Trump akamwambia hutokuwa na nafasi ya kujificha hata msituni tutakufyeka asubuhi tu, Rwanda ikabidi isaini,juzi kiongozi wa M23 kapishana na Rwanda juu ya huo mkataba jamaa ana ambition za kufika Kishansa Rwanda wanasema hapana Kuna mkataba na jamaa kakaza,alipoona M23 wamekaza akaleta ujuaji kwa Congo Tena Congo wamemjibu tuna utekelezaji wa mkataba vinginevyo tunamwambia bwana mkubwa umegoma.Rwanda imepoteza Congo imeshinda.Kagame analia Tishekedi anacheka.Kagame yuko kwenye Destination haelewi hatima yake. Tishekedi aliweka mawazili diaspora ndio waliomsaidia kumzidi maarifa Kagame.Muacheni abweke.
 
JWTZ Ipo imara mno

Hakuna jeshi east and central afrika la kuikoromea JWTZ!!

Naongea by experience in side!!
Labda miaka 30 iliyopita, sahivi limejaa vimemo tu. Na jeshi sahivi ni technology na air superiority kitu ambacho Rwanda wametuzidi. Jeshi sio kupasua matofali na kichwa hizo vita hazipo tena
 
Uimara wa Jeshi ni wananchi wake.

Vita ya Kagera kila mwananchi alishiriki na kila kijana mwenye afya alibeba silaha.

Hata uwe na jeshi bora kiasi gani ila kama wananchi wako hawako na wewe UTAPIGWA VIBAYA sana
Uko sahihi asilimia 200. Leo hii nani ana uchungu/uzalendo kuifia nchi yake akikumbuka ndugu yake alitekwa, aliuwawa, wasomi hawana ajira, wanatukanwa majukwaani wavivu, wajiajiri. Ajira jeshini ni za vimemo watoto wa wakubwa, hela zinachotwa na watawala, wao wanasota. Enzi za Nyerere, elimu, afya na huduma zote ilikuwa ni bure na watu walikuwa ni wazalendo kupindukia.
 
Uko sahihi asilimia 200. Leo hii nani ana uchungu/uzalendo kuifia nchi yake akikumbuka ndugu yake alitekwa, aliuwawa, wasomi hawana ajira, wanatukanwa majukwaani wavivu, wajiajiri. Ajira jeshini ni za vimemo watoto wa wakubwa, hela zinachotwa na watawala, wao wanasota. Enzi za Nyerere, elimu, afya na huduma zote ilikuwa ni bure na watu walikuwa ni wazalendo kupindukia.
Mfano, hawa hapa vijana waandikishwa mitaani kwenda vitani.

Sasa kuna matapeli, wanafikiri vita wanapigana wanajeshi pekee. Hata hao UVCCM na watoto wa kina Mwigulu wanaovaa bendera mnaowaita wazalendo hamtawaona


View: https://youtu.be/Mn5g8DpRrHk?si=jUpqQrQ_PVDgEKjt
 
Kama kawaida yake jana Kagame ametoa biti nzito sana kwa wanaoitishia Rwanda kupitia mgoggoro wa Congo.

Kwa dharau sana kawaita nchi za SADC zilizopeleka vikosi vyake Bukavu na Goma " Confused brothers and Sisters" yaaani kaka zetu na dada zetu waliochanganyikiwa.

Hakuwaacha hapo tu, kawaambia mlichokipata safari hii ni sehemu ndogo tu ya mtakachokipata mkijaribu tena kuleta vikosi vyenu kupambana na Rwanda.

Maneno haya ya Kagame ni ujumbe tosha kwa JWTZ kuwa wajikite kwenye professionalism maana CCM wanavyowaingilia mpaka saivi wamekuwa kituko hadi kwa majirani zetu.

Hongereni CCM kwa kuifanya Tanzania saivi kuwa kituko cha karne.
Tayari USA amesaini mkataba huo wa kumaliza mgogoro:Na USA atachota madini ya kutosha kutoka huko Congo:Yeye Kagame hana resource yeyote zaidi ya kutaka kuiba kutoka Congo:Kitakacho mpata kwa sasa ni yeye kutumiwa vindege vidogo visivyo na rubani na kummaliza:Tayari wakubwa na wenye dunia wapo Congo:Yeye aendelea kulia lia kama mbwa koko lakini kwa sasa its the end of the road.
 
Back
Top Bottom