Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 617
Wakuu wa JF kidogo sikuelewa nadhani sababu sikuanza mwanzo kuangalia Bunge jana lakini wakati mbunge mmoja wa CUF akichangia mada alimpongeza Spika kwa kupokea kadi tatu za uanachama wa CUF akamuomba ampe moja Chiligati na nyingine Waziri Pinda.
Kulikoni?naomba mnisaidie hapa.
Kevo, kilichowasilishwa kwa Spika hakikua kadi bali ni sarafu ya Sultani wa Zanzibar yenye rangi na nembo ya bendera ya CUF na akaombwa aonyeshe na kadi ya CUF walinganishe akawapa. Kwa kweli yule mbunge alichemsha sana na aliwapa CCM nguvu kwamba chama cha CUF ni cha Sultani na wabunge wa CCM walisikika wakisema "Kumbe CUF ni chama cha Waarabu!!". Mbunge yule alisema watalii wanatembelea kuona mambo mbalimbali akatoa ushahidi wa sarafu akisema ina alama za CUF, wabunge walicheka na Spika alisema michango mingine inachangamsha sana. Sina hakika mbunge yule alifanya kwa nia njema kwa CUF