Jamani Wa-Tz kwa mara nyingine tena tumepatiwa Waziri wa Fedha Bomu! Mh. awajibishwe kwa kulipotosha Bunge. Tujiulize, kama Wabunge wasingekuwa makini si ingepitishwa Bajeti feki (inayoji-contardict)? Hiyo ni aibu kubwa kwa Mh. Mkullo na Rais pia.
Upuuzi wa namna hiyo haujawahi kuwasilishwa na Waziri wa Fedha yoyote kabla yake , hata yule aliyetuambia ikibid WaTz tutalishwa nyasi ili Mkuu wa Nchi apate usafiri wa kumpaisha angani.
Mh. awajibike mwenyewe au awajibishwe ili wengine wawe makini.
Naomba kuwasilisha!
Kweli huyu waziri ni bomu sana....
Seems hakuchukua muda kukaa chini na kuipitia kwa mapana ile bajeti. Mambo ya kukaa ofisini hayo (kama Mwanyika) na kusaini barua na vimemo tu. Unakumbuka Mwanyika naye alivyosema kwenye Tume ya Mwakyembe kwamba yeye kazi yake ofisini ni kupitia makabrasha ya siku na kutia saini, ila yanayoendelea kwenye ofisi technically hausiki navyo......?? Huyu naye ni staili hiyo hiyo.
Inaonesha alivyopewa na speech, yeye akapitia speech tu, si anajua anaenda kusoma tu....kudadadeki, hakujua kuna kina Slaa, Hamad na wengine ambao wataikalia na kuichambua.
Ila kingine, tuna uhakika gani kama miaka mingine haikuwa hivi?? Je wabunge wanasomaga miswada yote inayopitishwa bungeni kiundani???