Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Wabunge sasa hivi komaeni watu wakamatwe na si kulia lia mambo ya uchawi na kukibimbia bungeni halafu kurudi na yale yale!Kama mlikuwa mkijali maisha yenu dhidi ya mauwaji na ushirikina ni kwanini hamkuwakamata MAFISADI?Nilishawahi kusema itageuka kuwa Dog catch your ass instead of you catchin the dog's ass!Sasa badala ya mafisadi kuogopa...Ni wananchi na wawakilishi wao wana unya unya!
 

acha upambe wako wa vyama vya siasa hapa ! alaaa !
 

Yaani hata cha kuongeza sina
 
Zitto, Shukran sana kwa mchango wako ambao umegusia mambo mengi muhimu.
Isipokuwa mkuu wangu kama kwaida yangu nina shindwa kuelewa pale uliposema TUMETOka katika uchumi unaotegemea kilimo tumeenda katika uchumi unaotegemea huduma!..
Mmetoka na nani?... maanake navyoelewa hizi ni sera za CCM, sera ambazo mimi mpiganaji wa JF sikubaliani nazo wala sioni unafuu wake kwa sababu KILIMO ndicho uti wa mgongo wa nchi yetu.. Tutake tusitake!...
kwa nini kumekuwepo na matokeo ya kukua kwa Uchumi wakati wananchi wanaendelea kuwa maskini ni kwa sababu hiyo kwani ni asilimia zaidi ya 80 wanategemea kilimo na ndicho pekee kinachowagusa wengi wetu moja kwa moja.
Hizi huduma ambazo mnakimbilia ni mali za nje malia ambazo uwezo wa kuwekesha hatuna ihivyo vyombo vya nje ndivyo vimejikita na kupewa hizo nafuu za kodi ambazo bila mahesabu ya kina Mkuu Augustine utaona kwamba pato la taifa haliwezi kuongezeka kwa kiwango sawa na ukuaji wa uchumi.
Kisha ikiwa wananchi wakulima, iwe kilimo ufugaji ama uvuvi wataweza kuwa na kipato kizuri kwa mwaka ni rahisi kwao kununua hizo huduma na mali zinazoagizwa toka nje..

Kifupi ni kwamba navyoitazama mimi Tanzania ya leo, mfumo wake ni ule unaogawa wananchi na kuweka makundi mawili kama alivyofanya mkoloni..Tunatazama fungu fulani wa watu hivyo vipaumbele vyetu vinapangwa kuwatazama wao.. Mwananchi ni mtumwa tu atapata ajira ya utumwa na bajeti haiwezi kumtazama hata kidogo..
Hata hayo madini, Utalii na kadhalika hayawezi kumwokoa mwananchi wa kawaida unless mikataba yote ifutwe na mfumo mpya uundwe laa sivyo maombi yenu ama niseme mchango wenu wa hiyo bajiti kivuli hauna maana kabisa kwani hamuwezi kubadilisha MIKATABA haramu iliyokwisha kubaliwa na kuwekewa sahihi..
In all mkuu bajeti yetu inazidi kumkandamiza mwananchi kama bajeti ya Mkoloni Muingereza ambaye naweza kumpa points juu ya serikali hii kwa sababu aliweza kukipa kilimo kipaumbele zaidi..
Nafahamui sana kuwa wakati umebadilika na kwamba sasa hivi huduma ni muhimu lakini hizi huduma haziwezi kabisa kuinua maisha ya mwananchi kjutokana na sisi wenyewe kutokuwa na uwezo wa kifedha na techonologia kiasi kwamba tutategemea sana wawekeshaji toka nje ambao ni lazima watatufunga ktk mikataba migumu...
Ushauri wangu ni kurudi kwenye basics ambako maendeleo ya Tanzania yatakuja tukianza kutoka chini - kutazama nguvu ya wananchi wako na ardhi bora uliyopewa na Mwenyezi ambayo chochote kinaweza kulimwa na kustawi vizuri!... Kupuuza kilimo, ufugaji na uvuvi ni hatua moja nyuma..Hii ndio sera ya CCM na ndio sababu kubwa ya mimi kutokukubali kujiunga ktk kundi hilo!
 

Kwa hiyo hii ndiyo lugha rasmi mnayotumia bungeni? Wananchi wasipowaelewa mnasema wamehongwa T-shirt. Mh. naomba ufafanuzi hapa ulikuwa unamaanisha nini?
Kwa hiyo kuna umuhimu mkubwa sana wa kuweza kuangalia vitu kama hivyo katika hali ya juu na ni suala lile lile la kubadili mindsett.
 
Hansard ya leo bado haijatoka. Ikitoka tu wana JF mtapata nini alisema Cheyo na ni nini alisema Dr. Slaa

Mchango wangu ni wa jana jioni ndio maana hansard yake tumepata

NInavyojua mimi JF ipo hapa kwa manufaa ya taifa siyo chama fulani cha siasa. Tungependa kujua kila mtu amesema nini na tuchambue pumba zipi na mchele ni upi au mtutangazie rasmi kwamba JF ipo kwa manufaa ya chama fulani cha siasa sisi wengine tutafute makao mapya.
 
Is sisal making a comeback? Most people had thought it to be on the verge of being replaced by synthetics.

mzee pundit,
mara yako ya mwisho kwenda maeneo ya tanga ilikuwa lini ?? mbona kuna mashamba mengi tu huko !
 
..Najaribu ku-imagine hivi hata humo bungeni kusingekuwa na mbunge hata mmoja wa chama cha upinzani haya mauchafu yanayoibuliwa yangejulikana kweli?? Maana wabunge wa CCM kwa jinsi walivyo na nidhamu ya unafiki lazima wangenyuti kimya mambo yanaenda " funika kombe mwanaharamu apite" anaenda kusaini anavuta chake siku zinaenda...

Inauma sana.. Kwa kweli wa-tz kuna haja 2010 kuangalia upya huu upepo wa kimaruhani wa CCM vinginevyo nchi itapotea kabisa licha ya kuwa na utajiri pomoni...Lakini umasikini ndio unanzidi kuongezeka.
 

Samahani naomba uliza.
Hivi ni kweli kwamba wabunge wa CCM huwa wanayaona haya madude mfano kama jana hii ya karne aliyo itoa jana Dr Slaa ya tofauti ya biln 130 kwa bajeti ya Mkulo, huwa wanasoma na kuamua kunyamaza kwa nidhamu ya chama? ama kwa vile mzizi wa ufisadi umeshamiri katika chaguzi/teuzi zao basi wabunge wengi wa CCM ni wale ambao japo hutazama hayo makabrasha uwezo wa kuyachambua huwa hawana? yaani nina maana kwamba walio wengi CCM ni Chitarilo type?

Ama kuwa mbunge wa CCM ni kuwa 'Yes man' kwa lolote lile hata kama liko wazi kwamba ni fyongo?
 
Hii serikali mnaoitetea hivi hamuoni aibu jamani au mnaubia katika serikali hii???Tujibuni jamani kuna watu humu JF wapo mstari wa mbele kuitetea sana serikali kila kukicha....watueleze wanaubia na serikali??
 
Well said,ila hao walio kuwa wanacheka bajeti wa wapinzani kweli wehu mbona hawakucheka iliyosomwa na CCM!!! utani umezidi mmle ndani na NS naye eti anasikiliza hata hizo za halfu lela ulela sijui!!!!
Bwana Zitto we kandamiza tu mpaka wajione wako kwenye njozi za mabadiliko..cheers
 

Alafu mbunge mwenyewe aliye ongea hayupo kabisa katika medali za siasa alidandia tu...atuambie ameisadiaje serikali ya CCM katika ubunge wake kama si kusinzia tu bungeni...ndo maana alikurupuka akasema lela ulela kasoma ngumbaru tu huyu...sijui tumhurumie?au tumfanyaje maana maneno mengine watu wanalopoka tu hawajui athari zake.Sasa hata wananchi walio mtuma awawakilishe wakisikia hivyo si aibu jamani>?Ameacha kupigania maendeleo kusini huko ambako kila mtu anakimbia kufanya kazi yeye anaongea utumbo tu bungeni.Wabunge wengine wanaudhi sana itakuwa ilikuwa njia ya kujipatia umaarufu sijui?
 
CCM ilishajisiku nyingi, tunachelewasha maziko tu.Mpaka lini tudanganywe wadanganyika?
 
Zitto nakupa Heko! Kazi nzuri inayofanywa na kambi ya upinzani bungeni inaonekana dhahili kwa watanzania. Nami naipongeza kambi hii.

Serikali ya ccm inabidi ijifunze kubadilika na ianze sasa kufanya kazi kwa manufaa ya watanzania. Kitendo cha kutotoza kodi makampuni ya madini ni ufisadi wa hali ya juu. Kwanini serikali inasita kuyatoza ushuru hayo makampuni ya migodi wakati huohuo inaendelea kutoza ushuru mafuta yote ya petrol na diesel yanayotumiwa na DALADALA zitoazo huduma kwa walala hoi wa nchi hii pamoja na viwanda vinavyozalisha bidhaa mbalambali zitumiwazo na walala hoi watanzania??!! Naishangaa sana hii serikali ya ccm!

Kwa maoni yangu, Serikali yetu inabidi ipunguze kodi kwa mafuta yote ya diesel na petrol ambayo huingizwa nchini kwa ajili ya matumizi ya sector ya transport na viwanda vinavyozalisha bidhaa mbalimbali hapa nchini. Kodi hii kwa sasa ni Tsh 539/liter kwa petrol na Tsh. 514/liter kwa diesel ambayo mwisho wake hulipwa na mlala hoi wa tanzania kila anapolipa nauli na kila anunuapo bidhaa yoyote ile amboyo ni pamoja na chakula chake cha kila siku. Isitoshe, serikali bado inatoza tena ushuru mwingine kwa mafuta hayohayo wa 1.2%FOB kwa mafuta yote yanayotumiwa na viwanda vyetu pamoja na gari zote hapa nchini zikiwemo daladala ambazo ni mkombozi wa huduma ya usafiri kwa wanyonge na masikini wa nchi hii. Anayebebeshwa gharama zote hizi ni mwananchi mlalahoi wa tanzania. Kwanini serikali isipunguze hizi kodi na kuzihamishia migodini??

Serikali yetu inabidi ianze sasa kutoza kodi kwa mafuta ya diesel yanayotumika migodini ili hawa wawekezaji nao waanze kuchangia uchumi wa nchi yetu na wawapunguzie mzigo walala hoi wa nchi hii waliobebeshwa kodi hii ya mafuta wakati mafisadi wenye migodi wakiendelea kutumia mafuta bila kuyalipia kodi yoyote. Hadi lili tutaendelea kuwaruhusu hawa mafisadi wa nje na wa ndani wabebe madini yetu bure???
 
Ahsante sana Zito kwa maelezo yenye uelewa na yaliyojitosheleza.Lakini ....,baada ya yote haya mwisho wake ni nini?????Tatizo langu siku zote ni kuwa hawa wanazi'CCM' wanajua yote haya mabaya lakini wanakanyagia vilevile.....wakati wa kampeni ukifika tutabembelezwa kidogo then watarudi madarakani,full stop!!..waliomo humuhumu na wadanganyika wengine ndio watasimama kutwa nzima kuwapa kula!!!!...
 
Last edited:
mzee pundit,
mara yako ya mwisho kwenda maeneo ya tanga ilikuwa lini ?? mbona kuna mashamba mengi tu huko !

Swali si kwamba kuna mashamba au hamna, sijauliza comeback ya kulimwa.Niko interested kujua kama mkonge unalipa katika soko la dunia.Kuna kipindi hapa kati watu walikuwa wanatumia sana synthetic products ikawa kama mkonge hauna deal, je tunatumia resources zetu vizuri kwa kulima mkonge au tunshindwa tu kuyabadili haya mashamba ya mkonge na kulima mazao mengine yenye faida kubwa zaidi?

Hilo ndilo swali.
 

Hili nalo unauliza? hawakusoma lakini kwa ile wanaita takrima wako mujengo! Sasa watasema nini? wachache walio na uelewa ndiyo hao tunawafahamu kwa jina la mafisadi! Wewe fuatilia tu utasikia michango yao inavyosikitisha. "Oh mh Spika kwetu hakuna barabara.....Naunga hoja asilimia mia moja"😕
 
Kikwete kama ni chakula anapika basi kishakuwa sumu kutokana na hiyo michanganyiko!

Sitta ni shujaa kwasababu alipigania kuwepo uchunguzi wa RICHMOND.
Johnson Mwanyika akawa ni mmoja wapo wa watuhumiwa wa RICHOMD...MKATABA AMBAO HATA LOWASSA ALISHAMWAMBIA YEYE NA MWANYIKA PAMOJA NA DON MAFIOSO TOP MWENYEWE KUWA NI MBOVU NA HAUFAI!

Kikwete akaona ataumbuka hivyo akamuweka Mwanyika kwenye kamati haraka haraka ya kuwachunguza mafisadi wengine ili sasa waje pamoja na kunegotiate namna ya kuua noma pande zote za EPA na RICHMOND...Na huku akimwambia LOWASSA KUWA BADO ANAWEZA KUJITETEA NA KUBAKI KAZINI...

Akageuka upande wa PILI akam TAP Zitto ambaye naye alikuwa akiwaumiza huko Bungeni....Wakamweka kapu moja na MAFISADI kwenye kamati ya MADINI.

Walichozungumza humo ndani ya kamati anayejua ni MKUU MAFIOSO NA SINCLAIR pamoja na Hao kina ZITTO na wanakamati wengine.

Sasa wakaanza kuwazuga wananchi kuwa tusubiri BUNGE likianza kwani watayazungumzia yale ambayo wananchi wanayoyapigia kelele kuwa SASA MAFIA WAWEKWE NDANI...

Kumbe Mafioso ni WOTE na sasa woga ni UCHAWI BUNGENI NA HAKUNA ANAYETAKA KUKAA BUNGENI NA KUJADILI ISSUES ZA WANANCHI.
Baada a kurudi BUNGENI...

Wameanza upya eti wanazungumzia mambo ya ufisadi na namna rasimali za Taifa zitakavyoendelea kutumika ili kuwanufaisha wananchi!?

KUNA MWANANCHI ASIYEJUA KUWA MAFIOSO NI CCM NA SERIKALI YAKE NA KWAMBA HAWAWEZI KUJIKAMATA AMA KUJICHUNGUZA?

Kuna asiyejua kuwa hata wale tunaowaona kama ni wakombozi wetu bado wana maswali ya kutujibu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…