Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Jumatatu, Juni 16, 2008

MHE. KABWE Z. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kunipa nafasi ya kuchangia hotuba hizi mbili hotuba ya bajeti na hotuba ya hali ya uchumi. Ninafahamu ya kwamba sisi kama Kambi ya Upinzani ni Serikali kivuli. Jukumu letu la kidemokrasia ni kuonyesha pale ambapo wenzetu wa Serikali inayoongoza hawapaoni na tumeonyesha katika bajeti yetu kivuli, maeneo ambayo wenzetu hawakuyaona katika bajeti iliyopita, wameyaona katika bajeti ya mwaka huu na wakawa wamepelekea Serikali kuweza kuongeza mapato. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Waheshimiwa Wabunge wanapozungumza na kudhihaki bajeti kivuli ambayo Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed ameitoa kwamba ni alfu lela ulela nashindwa kuelewa sifa zilizowafanya Wabunge hao kuja katika Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaanza na hali ya uchumi.

NAIBU SPIKA: Naibu Spika husikiliza yote tu, alfu lela ulela na mengineyo. (Makofi/Kicheko)

MHE. KABWE Z. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nitaanza na hali ya uchumi. Tuna changamoto kubwa sana kama nchi, kwamba hivi sasa tunaishi katika uchumi unaokuwa lakini umaskini haupungui na hii ndio changamoto ambayo bajeti inapaswa kuijibu na haiwezi kujibiwa kwa bajeti ya mwaka mmoja inajibiwa kwa utaratibu maalumu. Toka tumeingia katika Bunge hili, hii ni bajeti ya tatu, kumekuwa na rekodi za uchumi kukua lakini taarifa mbalimbali za Serikali, kwa mfano Taarifa za hali ya umaskini. Toka tumekuwa Wabunge kumekuwa na taarifa mbili za hali ya umaskini (P&HDR 2005 na 2007), zote zinaonyesha kwamba umaskini kwa wananchi bado ni mkubwa na katika bajeti iliyopita tulizungumzia suala zima la madhara ya kupandisha kodi za baadhi ya vitu kwa maisha ya wananchi na wenzetu (CCM) wakakataa kata kata lakini athari zinaonekana hivi sasa na leo tunaiita bajeti ambayo Mheshimiwa Waziri Mkulo ameitoa kwamba ni bajeti ya wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezi kuwa bajeti ya mwananchi kwa sababu kodi ambazo zilipandishwa mwaka jana hazijashushwa kurudishwa katika viwango vya mwaka 2006/2007, itakuwa ni bajeti ya mwananchi iwapo tu kodi hizo zitakuwa zimeshushwa lakini kitendo cha kuziacha kodi hizo kama zilivyo bado kitaendelea kufanya mfumuko wa bei uweze kuendelea na hili nitaeleza nitaelezea huko chini.
Uchumi wetu umebadilika, tumetoka katika uchumi unaotegemea kilimo tumeenda katika uchumi unaotegemea huduma. Asilimia 47.3 sasa ya uchumi wetu ni huduma na asilimia 28.2 tu ndio kilimo.
Lakini mipango yetu bado ni kana kwamba uchumi unategemea kilimo na tumeonyesha baadhi ya wasiwasi wetu kutokana na takwimu ambazo zimetolewa lakini mipango ya nchi ambayo uchumi wake ambao takriban nusu unategemea huduma ni tofauti na mipango ya nchi ambayo takriban zaidi ya nusu inategemea kilimo. Bajeti hii ni mwendelezo wa bajeti zilizopita ambapo huduma ilikuwa ina mchango mdogo sana katika uchumi, kwa hiyo kwa vyovyote vile kutokana na bajeti hii ni vigumu sana changamoto za sasa za nchi kuweza kujibiwa.


[MHE. KABWE Z. ZITTO]

Mheshimiwa Naibu Spika, sekta ya madini ambayo ndio ilikuwa sekta inayoongoza kwa ukuaji, hivi sasa imekuwa ni sekta ya pili au ya tatu kwa ukuaji, ukuaji wa uchumi sasa unategemea sekta ya mawasiliano na kwa kiasi kikubwa sekta hii bado haichangii vya kutosha katika mapato ya Serikali, kuna baadhi ya maeneo ambayo Waziri wa Fedha ameonyesha ili Serikali iweze kukusanya pesa zaidi lakini wakati anaangalia maeneo hayo bado eneo lenyewe la sekta ya madini bado halikuangaliwa hata kidogo na huwa tunapata wasiwasi mkubwa sana kwamba baadhi ya mapendekezo ambayo Kamati ya Rais ya kuangalia sekta ya madini iliyotoa na si baadhi mapendekezo, yote hayajachukuliwa, matokeo yake ni kwamba bajeti imeangalia zaidi kupandisha kodi za walaji yaani consumption tax na kuacha kabisa kupandisha kodi kwa watu ambao ni wale wazalishaji kwa maana ya wawekezaji na wawekezaji wa ndani na wa nje ya nchi siyo wawekezaji wa nje peke yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tumejikuta tuna chumi mbili ndani ya nchi moja uchumi wa matajiri na uchumi wa maskini, uchumi wa maskini wanauita ni rural economy ambapo ndiko wanakoishi na matokeo yake ni kwamba maskini either bidhaa ambazo yeye analima, (anazozalisha) hazikui lakini bei za bidhaa ambazo yeye anatumia zinakuwa, kwa hiyo maskini anauza kwa bei za vijijini na ananunua kwa bei za mjini. Kwa hiyo hali yake ya kipato ni lazima iendelee kuwa chini, ni tegemeo la bajeti yeyote ile katika nchi yeyote ile iwapo bajeti ikitumika kama sera ya kuangalia ni jinsi gani ambavyo uchumi wa nchi unakwenda wataweza kuangalia ni jinsi gani ya kupunguza gharama hii ambayo mkulima anapata kwa ajili ya kuhakikisha kwamba anabakia na fedha ya kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeelezwa kwamba Serikali imeweka vipaumbele na vipaumbele vimetajwa na pesa zimetajwa kwa ajili ya vipaumbele lakini napata wasiwasi sana kwamba inawezekana kuna ukosefu wa uratibu ndani ya Serikali, taarifa ya hali ya umaskini ya mwaka 2007 ambayo imetolewa mwaka huu imeonyesha changamoto ambazo nchi inazo na ni maeneo gani ambayo yakitiliwa mkazo tutaweza kwenda mbele kiuchumi. Wenyewe wanaita drivers of growth na wameweka maeneo manne ambayo yanapaswa kuangaliwa na kuwekewa mikakati maalum - transport services ambayo ndani yake kuna miundombinu na huduma zingine za usafiri, madini, horticulture kwa Kiswahili nadhani ni masula ya maua ukulima wa maua na kadhalika na utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukiangalia bajeti jinsi ilivyokaa jinsi gani ambavyo tumegawa rasilimali zetu kidogo ambazo tunazipata haikuangalia kabisa vipaumbele hivi ambavyo taarifa ya Serikali imezitoa taarifa ambayo ndio inafanya tathmini ni wapi ambapo tunakwenda kuhusiana na suala zima la kupunguza umaskini.
Nadhani Wizara ya Fedha na Uchumi inabidi iangalie kwa sababu taarifa ya hali ya umaskini inatolewa na idara ndani ya Wizara ya Fedha na Uchumi kwa hiyo ni rahisi sana kwa idara hiyo ya kuondoa umaskini kuwasiliana na Idara ya Sera ya Wizara ya Fedha, kuwasiliana na Idara ya Bajeti ya Wizara ya Fedha ili kuweza kuangalia ni vipi ambavyo tunavyofanya vipaumbele vyetu, tukiamua kuweka vipaumbele kufurahisha wananchi kwa sasa huko tunakokwenda kutakuwa ni kugumu sana kwa sababu utagawa pesa kwa kila sekta lakini zile sekta hazitachochea sekta nyingine. Kwa hiyo kuna umuhimu mkubwa sana wa kuweza kuangalia vitu kama hivyo katika hali ya juu na ni suala lile lile la kubadili mindsett.


[MHE. KABWE Z. ZITTO]

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vipi ambavyo bajeti yetu inaendana na changamoto ambazo tunazo hivi sasa? Kwanza bajeti imeshindwa kabisa kukusanya kodi zinazostahili kwenye madini na ninashindwa kuelewa ni kwa sababau gani, kwa sababu inafahamika wazi kabisa kwamba mwaka 1997 na Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed ameielezea hapa, Bunge hili lilitunga sheria ambayo ilitoa unafuu usio na lazima kwa makampuni ya madini kwa kiasi cha asilimia 15 unafuua mbao umeifanya Taifa lipoteze shilingi bilioni 883 katika kipindi cha miaka 10 toka sekta ya madini ianze kukua katika Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulitegemea kwamba katika finance bill ya mwaka huu Waziri wa Fedha angefuta kabisa sheria hiyo kwa sababu sheria hiyo bado iko kwenye vitabu vyetu vya sheria na inafanya makampuni ya madini ambayo yana mikataba yasiweze kulipa kodi hiyo, kuna mashauriano ambayo Serikali imefanya na baadhi ya makampuni ya madini lakini kama suala hili hatutalitoa kwenye sheria halitaweza kusaidia na mfano mmoja tu wa madhara ya sheria hiyo ni kwamba kampuni ya Bulyanhulu Gold Mine ambayo inangepaswa kuwa imeanza kulipa kodi ya mapato haitalipa kodi ya mapato kutokana na faida yake mpaka mwaka 2019 yaani haitaanza kulipa corporate tax mpaka mwaka wa mwisho wa Rais wa awamu ya tano na hawa wameanza na Rais wa awamu ya tatu. Kwa hiyo unaweza ukaona ni jinsi gani ambayo Taifa linapoteza na mabilioni ya fedha kwa sababu ya sheria ambazo tumezitunga sisi wenyewe na tunao uwezo wa kuweza kuzirekebisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, misamaha, mwaka 2005 wakati tuko kwenye kampeni za uchaguzi Serikali ilitoa misamaha ya kodi miwili wa kwanza ya mafuta kwamba makampuni ya madini hayatalipa kodi ya mafuta mpaka watakapomaliza kama ni dhahabu wanayochimba, kama ni almasi wanayochimba, kama ni Tanzanite wanayochimba na tulishauri kwamba msamaha huo ufutwe kwa sababu ni msamaha ambao hausaidii chochote.

Mheshimiwa Naibu Spika, na msamaha huu ungefutwa ungeweza hata kusaidia kupunguza zile kodi ambazo tulizipandisha mwaka jana kupelekea mfumuko wa bei uweze kutokea. Sisi kama Tanzania hatuna uwezo hata kidogo wa ku-control bei ya mafuta katika soko la Dunia lakini tunao uwezo wa ku-deal na kodi zetu ili kuweza kuhakikisha kwamba tunapunguza ukali wa upandaji wa bei katika soko la Dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ilipaswa kuangalia hizo kodi zetu ili ziweze kupunguza huo ukali wa maisha. Mwaka 2007/2008 aliyekuwa Waziri wa Fedha Mheshimiwa Zakia Meghji alionyesha katika sura ya bajeti kwamba Serikali itakusanya kiasi fulani cha mapato shilingi bilioni 239 kutokana na marekebisho mbalimbali ya kodi, katika bajeti ya mwaka huu Waziri wa Fedha hakuonyesha viwango mbalimbali vya mabadiliko ya kodi vitaifanya Serikali ikusanye kiasi gani? Kwa hiyo ninadhani ni muhimu sana kuwa na mtiririko ulio sawa au consistency ili kuhakikisha kwamba kunakuwa na hali ambayo ni nzuri zaidi.


[MHE. KABWE Z. ZITTO]

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kabisa, bajeti ni vitabu vinne, volume one mpaka volume four, volume one ndio inayo-dill na mapato ya Serikali na ninasikitika kwamba mara nyingi hatuiangali hii volume. Ukiangalia kitabu cha kwanza cha bajeti utagundua mambo mawili la kwanza tunategemea sana kodi za biashara kwa maana ya import, import duties. Mabadiliko ya kodi ambayo Serikal imeyatangaza sasa asilimia 50 itatokana na import duties, hii ni hatari sana katika uchumi wa sasa, tunaokwenda, tuna East African Customs Union tunaenda kwenye common market, tunasaini EPA ambayo itaondoa kodi mbalimbali dhidi ya European Union tutapata tatizo kubwa sana kurekebisha kodi hizi tutajikuta kwamba tunakuja kuumia sana huko baadaye.
Katika revenue book, wakati Waziri wa Fedha anasema kwamba tutakusanya shilingi bilioni 58 kwa mauzo ya hisa za NMB, kwenye revenue book zinaonekana shilingi bilioni 42. Tunapopitisha bajeti tunachoangalia ni revenue book, ni nini ambacho tunakichukua? Ni hotuba ya bilioni 58 au ni revenue book ya bilioni 42, nilikuwa ninaomba Waziri wa Fedha aweze kuliangalia hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kabisa, kama tunataka kuongeza uzalishaji wa kutosha kwenye baadhi ya mazao ambayo tunayo ni lazima tuangalie jinsi gani ya kutoa incentives kwa baadhi ya mazao. Mimi nitatoa mfano mmoja na nilitoa taarifa hii toka mwaka jana kwamba leo India wameweka compulsory usage ya magunia yao ya jute kwa ajili ya mazao yote ya India. Sisi hatujaweka compulsory usage ya maguni yetu ya katani, matokeo yake ni kwamba tunakuwa tuna-export jobs kwenda Bangladeshi na India kwa sababu hatulindi sisal yetu, katani yetu wala hatulindi viwanda matokeo yake ni kwamba baadhi ya wawekezaji wamenunua viwanda havifanyi kazi kwa sababu ya mazingira hayo ya kikodi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa ninaomba Waziri wa Fedha ajaribu kuangalia uwezekano wa angalau mazao mawili, mahindi na korosho ziwe ni compulsory kutumia maguni ya katani ili ku-stimulate uzalishaji wa katani na kufanya viwanda vya katani ambavyo vimekufa hivi sasa viweze kuzalisha magunia ya katani na yaweze kutumika katika nchi, vinginevyo itakuwa ni tatizo ambalo tutaendelea nalo tutaendelea kutegemea kodi kutokana na imports ambazo madhara yake ni makubwa sana kutokana na Dunia ya sasa ya globalization.
Ni lazima kuangalia Serikali isikwepe kazi yake ya distributive role. Ni kazi ya Serikali yeyote Duniani kukusanya kutoka matajiri kuwapeleka maskini ili kuweza kupunguza gharama za maisha yao na ndio kazi ya bajeti kama sera na siyo bajeti kama urari wa mapato na matumizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru sana. (Makofi)

Mh Zitto haya mambo uliyoyazungumzia ni muhimu.Lakini yanajulikana na ulishawahi kuyapigania huko bungeni na wakaku suspend na baadae kamati ikaundwa ya madini ambayo KUNA MAFISADI WALIKUWA NDANI.... Johnson Mwanyika....Mtuhumiwa mkuu wa RICHMOND alikuwepo kwenye kamati EPA.Mafisadi waliwekwa pamoja na wewe ambaye ulinyimwa nafasi ya kupata muafaka utakaotokea kwenye kamati teule ya bunge ili kuweza kuona ni kwa jinsi gani haki huru ya watu huru itapatikana.Tukasema usiingie kwenye kamati!Kuingia kwako kamatini kulisaidia sana kumsafisha kiaina mfisadi na hivyo kupelekea kuyumba kwa haki.Mh Zitto....Kama hutaweza kuja na udhibitisho kuwa wabunge wa CCM hawatakupa tena umaarufu kwa kukufukuza BUNGENI na Kukuundia kamati nyingine zenye mishahara minono...Basi utakuwa umetuweka kwenye njia panda!
 
sio kama serikali haiambiwi. inaambiwa kila mwaka mambo hayo kwa hayo. lakini haitaki kwa kuwa imejificha humo kwenye mikataba mibovu.
mmesikia wapi mtu kutia moto nguo aliyovaa mwilini mwake?
 
sio kama serikali haiambiwi. inaambiwa kila mwaka mambo hayo kwa hayo. lakini haitaki kwa kuwa imejificha humo kwenye mikataba mibovu.
mmesikia wapi mtu kutia moto nguo aliyovaa mwilini mwake?

Tatizo letu tuna mentality ya "kuiambia" serikali.

Sijui kwa sababu tulikuwa protectorate na kupata uhuru bila Mau Mau ndiyo maana kila kitu lelemama na kuambiana mara mia mia. What is the meaning of checks and balances? Whats is the meaning of accountability to voters?

Bunge linatakiwa kuikeep serikali in check.Nafahamu kuna swala la wabunge wa CCM kuleta partisan politics, wananchi wanatakiwa kuwa keep partisan MPs in check.

Kwa hiyo mbunge mmoja machachari anatakiwa kuleta msaada machachari kupinga upuuzi wa serikali na tuone voting records za wabunge, wasioweka maslahi ya taifa mbele tunawatoa regardless ya chama gani wanatoka.

Naelewa kuna ma molasses kibao na ukiritimba kama wa kina Marmo, lakini kwenye molasses hukai na kulalama, unatia maji pole ple kulainisha.
 
ccm wanaharibu bunge letu. mbunge yoyote wa ccm anayejaribu kutetea maslahi ya wananchi utasikia anatengwa na chama, au mara kaekewa uchawi.
ccm ikipeleka wagombea wenye uwezo na moyo wa kusaidia wananchi, basi nchi hii itakwamuka mara moja kutoka maafa yake
 
Tatizo letu tuna mentality ya "kuiambia" serikali.

What is the meaning of checks and balances? Whats is the meaning of accountability to voters?

Bunge linatakiwa kuikeep serikali in check.Nafahamu kuna swala la wabunge wa CCM kuleta partisan politics, wananchi wanatakiwa kuwa keep partisan MPs in check.

Kwa hiyo mbunge mmoja machachari anatakiwa kuleta msaada machachari kupinga upuuzi wa serikali na tuone voting records za wabunge, wasioweka maslahi ya taifa mbele tunawatoa regardless ya chama gani wanatoka.

Ndio maana nikauliza inakuwaje Mbunge aseme anategemea Mkulo alete pendekezo la kufuta sheria ya misamaha ya kodi wakati wao BUnge ndio walitunga hiyo sheria ya misamaha, na wiki iliyopita Serikali ilisema inakerwa na hii Sheria, siku Mkuu wa TRA alipoongea na Wabunge kuhusu wakwepa kodi wa Cocacola? Mnakumbuka?

Tatizo ni kubwa kuliko Checks and balances: Hakuna anaejua nani anatakiwa afanye nini!
 
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kabisa, kama tunataka kuongeza uzalishaji wa kutosha kwenye baadhi ya mazao ambayo tunayo ni lazima tuangalie jinsi gani ya kutoa incentives kwa baadhi ya mazao. Mimi nitatoa mfano mmoja na nilitoa taarifa hii toka mwaka jana kwamba leo India wameweka compulsory usage ya magunia yao ya jute kwa ajili ya mazao yote ya India. Sisi hatujaweka compulsory usage ya maguni yetu ya katani, matokeo yake ni kwamba tunakuwa tuna-export jobs kwenda Bangladeshi na India kwa sababu hatulindi sisal yetu, katani yetu wala hatulindi viwanda matokeo yake ni kwamba baadhi ya wawekezaji wamenunua viwanda havifanyi kazi kwa sababu ya mazingira hayo ya kikodi

Is sisal making a comeback? Most people had thought it to be on the verge of being replaced by synthetics.
 
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kabisa, kama tunataka kuongeza uzalishaji wa kutosha kwenye baadhi ya mazao ambayo tunayo ni lazima tuangalie jinsi gani ya kutoa incentives kwa baadhi ya mazao. Mimi nitatoa mfano mmoja na nilitoa taarifa hii toka mwaka jana kwamba leo India wameweka compulsory usage ya magunia yao ya jute kwa ajili ya mazao yote ya India. Sisi hatujaweka compulsory usage ya maguni yetu ya katani, matokeo yake ni kwamba tunakuwa tuna-export jobs kwenda Bangladeshi na India kwa sababu hatulindi sisal yetu, katani yetu wala hatulindi viwanda matokeo yake ni kwamba baadhi ya wawekezaji wamenunua viwanda havifanyi kazi kwa sababu ya mazingira hayo ya kikodiPia kwanini asiwaulize kuhusu AGOA?Wabunge pia ni wakati wa kuwajulisha wananchi kuhusu opportunities zilizoko na si kuwaachia vigogo mafisadi MAFIOSO na makundi ya wafuasi na familia zao za Ki don!Wananchi waambiwe kuhusu EPZ...Wananchi walifichwa kuhusu ubinafsishaji na wabunge walifumba macho!
 
Halafu MODS naomba tuwekane sawa hapa!Kwanini mumezidis able hizi functions kiasi cha kwamba naonekana kama naandika vituko?Siwezi kuhighlight,kuquote,wala kutumia functions nyingine za maandishi.Tuelezane wakuu maana akufukuzaye hakwambii TOKA!
 
Kuhani Mkuu

Finnance Bill ambayo huwa Act baada ya kupitishwa na sheria inayosimamia utekelezaji wa bajeti.

Alichotegemea zitto hapo ni kuwa katika mjadala wa bajeti wa sasa katika vile vitabu vinne kile cha nne ambacho ni finnance bill kingekuwa na hoja ya serikali ya kufuta hiyo misamaha ili iwe finance act itayaosimamia bajeti ya mwaka huu!

Lakini Mkullo na wenzake hawayakuyaona hayo......wanafikiria kuhusu uchawi tu

Asha

Haya ndiyo maelezo muafaka ya sheria inayozungumziwa hapa. Kila budget huwa inapitiswa kwa hiyo Finance Bill
 
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kabisa, kama tunataka kuongeza uzalishaji wa kutosha kwenye baadhi ya mazao ambayo tunayo ni lazima tuangalie jinsi gani ya kutoa incentives kwa baadhi ya mazao. Mimi nitatoa mfano mmoja na nilitoa taarifa hii toka mwaka jana kwamba leo India wameweka compulsory usage ya magunia yao ya jute kwa ajili ya mazao yote ya India. Sisi hatujaweka compulsory usage ya maguni yetu ya katani, matokeo yake ni kwamba tunakuwa tuna-export jobs kwenda Bangladeshi na India kwa sababu hatulindi sisal yetu, katani yetu wala hatulindi viwanda matokeo yake ni kwamba baadhi ya wawekezaji wamenunua viwanda havifanyi kazi kwa sababu ya mazingira hayo ya kikodiPia kwanini asiwaulize kuhusu AGOA?Wabunge pia ni wakati wa kuwajulisha wananchi kuhusu opportunities zilizoko na si kuwaachia vigogo mafisadi MAFIOSO na makundi ya wafuasi na familia zao za Ki don!Wananchi waambiwe kuhusu EPZ...Wananchi walifichwa kuhusu ubinafsishaji na wabunge walifumba macho!

Kwa mfano hapo juu nilikuwa niki mquote Zitto na ujumbe wangu umeanzia hapo kwenye...Pia kwanini asiwaulize kuhusu AGOA...Sasa ona jinsi ilivyotokea kama kituko flani hivi...!
 
Halafu MODS naomba tuwekane sawa hapa!Kwanini mumezidis able hizi functions kiasi cha kwamba naonekana kama naandika vituko?Siwezi kuhighlight,kuquote,wala kutumia functions nyingine za maandishi.Tuelezane wakuu maana akufukuzaye hakwambii TOKA!

kwi kwi kwi kwi kwi kwi,

yaani hapa sina mbavu jamani, hivi Mushi u-mzima kweli?
 
Is sisal making a comeback? Most people had thought it to be on the verge of being replaced by synthetics.

Nililiona hilo, lakini nikasema ngoja niuchune nisije nikadhaniwa nina mzizi.

Kuhusu katani, lingine analosema Mheshimiwa ni kwamba viwanda (nadhani viwanda vya kamba, hajaeleza) vinakufa kwa sababu ya mazingira ya kodi kwa wawekezaji. Anataka wawekezaji wa viwanda hivi wapewe "incentive" ili "kulinda sisal yetu."

Kwa maneno mengine anataka misamaha ya kodi kwa wawekezaji.

Ilibidi atueleze tofauti ya huu msamaha na ule wa wawekezaji wa migodi. Halafu pia tuelewe kama ni busara kwa Serikali kujaribu kufufua sekta ambayo hata wafanya biashara wameiona haina faida. Kama wafanyabiashara wanadhani hii biashara haistahili hata kuilipia kodi, tungependa kujua kwa nini Serikali iione kwamba ni biashara yenye faida, kama anavyopendekeza Mh. Zitto.
 
Is sisal making a comeback? Most people had thought it to be on the verge of being replaced by synthetics.

Synthetics have proven to be a disaster for an environment, i currrently see that there is a huge possibility of sisal to comeback, i take an example of china which has recently taken some measures to control plastic bags.
so if this opportunity of awareness which has popped to people's minds is well utilized, it is my hope that sisal can make a tremendous comeback, but an immense investment is still needed ofcourse.
 
kwi kwi kwi kwi kwi kwi,

yaani hapa sina mbavu jamani, hivi Mushi u-mzima kweli?

Halafu weka lafudhi ya kichaga kama ile ya katika Rafaeli,

Ni namna gani ah, ni jinsi gani tutawini maishani
mpaka siku tunasema buriani, ah x3

Yerewiiii!
 
Haya ndiyo maelezo muafaka ya sheria inayozungumziwa hapa. Kila budget huwa inapitiswa kwa hiyo Finance Bill

Umefuatilia swali lililofuata baada ya huo utaratibu wa finance bill kuelezwa na Asha Abdalah? Naomba unijibu swali lililofuata baada ya jibu la Asha Abdallah.
 
Jumatatu, Juni 16, 2008

MHE. KABWE Z. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kunipa nafasi ya kuchangia hotuba hizi mbili hotuba ya bajeti na hotuba ya hali ya uchumi. Ninafahamu ya kwamba sisi kama Kambi ya Upinzani ni Serikali kivuli. Jukumu letu la kidemokrasia ni kuonyesha pale ambapo wenzetu wa Serikali inayoongoza hawapaoni na tumeonyesha katika bajeti yetu kivuli, maeneo ambayo wenzetu hawakuyaona katika bajeti iliyopita, wameyaona katika bajeti ya mwaka huu na wakawa wamepelekea Serikali kuweza kuongeza mapato. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Waheshimiwa Wabunge wanapozungumza na kudhihaki bajeti kivuli ambayo Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed ameitoa kwamba ni alfu lela ulela nashindwa kuelewa sifa zilizowafanya Wabunge hao kuja katika Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaanza na hali ya uchumi.

NAIBU SPIKA: Naibu Spika husikiliza yote tu, alfu lela ulela na mengineyo. (Makofi/Kicheko)

MHE. KABWE Z. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nitaanza na hali ya uchumi. Tuna changamoto kubwa sana kama nchi, kwamba hivi sasa tunaishi katika uchumi unaokuwa lakini umaskini haupungui na hii ndio changamoto ambayo bajeti inapaswa kuijibu na haiwezi kujibiwa kwa bajeti ya mwaka mmoja inajibiwa kwa utaratibu maalumu. Toka tumeingia katika Bunge hili, hii ni bajeti ya tatu, kumekuwa na rekodi za uchumi kukua lakini taarifa mbalimbali za Serikali, kwa mfano Taarifa za hali ya umaskini. Toka tumekuwa Wabunge kumekuwa na taarifa mbili za hali ya umaskini (P&HDR 2005 na 2007), zote zinaonyesha kwamba umaskini kwa wananchi bado ni mkubwa na katika bajeti iliyopita tulizungumzia suala zima la madhara ya kupandisha kodi za baadhi ya vitu kwa maisha ya wananchi na wenzetu (CCM) wakakataa kata kata lakini athari zinaonekana hivi sasa na leo tunaiita bajeti ambayo Mheshimiwa Waziri Mkulo ameitoa kwamba ni bajeti ya wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezi kuwa bajeti ya mwananchi kwa sababu kodi ambazo zilipandishwa mwaka jana hazijashushwa kurudishwa katika viwango vya mwaka 2006/2007, itakuwa ni bajeti ya mwananchi iwapo tu kodi hizo zitakuwa zimeshushwa lakini kitendo cha kuziacha kodi hizo kama zilivyo bado kitaendelea kufanya mfumuko wa bei uweze kuendelea na hili nitaeleza nitaelezea huko chini.
Uchumi wetu umebadilika, tumetoka katika uchumi unaotegemea kilimo tumeenda katika uchumi unaotegemea huduma. Asilimia 47.3 sasa ya uchumi wetu ni huduma na asilimia 28.2 tu ndio kilimo.
Lakini mipango yetu bado ni kana kwamba uchumi unategemea kilimo na tumeonyesha baadhi ya wasiwasi wetu kutokana na takwimu ambazo zimetolewa lakini mipango ya nchi ambayo uchumi wake ambao takriban nusu unategemea huduma ni tofauti na mipango ya nchi ambayo takriban zaidi ya nusu inategemea kilimo. Bajeti hii ni mwendelezo wa bajeti zilizopita ambapo huduma ilikuwa ina mchango mdogo sana katika uchumi, kwa hiyo kwa vyovyote vile kutokana na bajeti hii ni vigumu sana changamoto za sasa za nchi kuweza kujibiwa.


[MHE. KABWE Z. ZITTO]

Mheshimiwa Naibu Spika, sekta ya madini ambayo ndio ilikuwa sekta inayoongoza kwa ukuaji, hivi sasa imekuwa ni sekta ya pili au ya tatu kwa ukuaji, ukuaji wa uchumi sasa unategemea sekta ya mawasiliano na kwa kiasi kikubwa sekta hii bado haichangii vya kutosha katika mapato ya Serikali, kuna baadhi ya maeneo ambayo Waziri wa Fedha ameonyesha ili Serikali iweze kukusanya pesa zaidi lakini wakati anaangalia maeneo hayo bado eneo lenyewe la sekta ya madini bado halikuangaliwa hata kidogo na huwa tunapata wasiwasi mkubwa sana kwamba baadhi ya mapendekezo ambayo Kamati ya Rais ya kuangalia sekta ya madini iliyotoa na si baadhi mapendekezo, yote hayajachukuliwa, matokeo yake ni kwamba bajeti imeangalia zaidi kupandisha kodi za walaji yaani consumption tax na kuacha kabisa kupandisha kodi kwa watu ambao ni wale wazalishaji kwa maana ya wawekezaji na wawekezaji wa ndani na wa nje ya nchi siyo wawekezaji wa nje peke yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tumejikuta tuna chumi mbili ndani ya nchi moja uchumi wa matajiri na uchumi wa maskini, uchumi wa maskini wanauita ni rural economy ambapo ndiko wanakoishi na matokeo yake ni kwamba maskini either bidhaa ambazo yeye analima, (anazozalisha) hazikui lakini bei za bidhaa ambazo yeye anatumia zinakuwa, kwa hiyo maskini anauza kwa bei za vijijini na ananunua kwa bei za mjini. Kwa hiyo hali yake ya kipato ni lazima iendelee kuwa chini, ni tegemeo la bajeti yeyote ile katika nchi yeyote ile iwapo bajeti ikitumika kama sera ya kuangalia ni jinsi gani ambavyo uchumi wa nchi unakwenda wataweza kuangalia ni jinsi gani ya kupunguza gharama hii ambayo mkulima anapata kwa ajili ya kuhakikisha kwamba anabakia na fedha ya kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeelezwa kwamba Serikali imeweka vipaumbele na vipaumbele vimetajwa na pesa zimetajwa kwa ajili ya vipaumbele lakini napata wasiwasi sana kwamba inawezekana kuna ukosefu wa uratibu ndani ya Serikali, taarifa ya hali ya umaskini ya mwaka 2007 ambayo imetolewa mwaka huu imeonyesha changamoto ambazo nchi inazo na ni maeneo gani ambayo yakitiliwa mkazo tutaweza kwenda mbele kiuchumi. Wenyewe wanaita drivers of growth na wameweka maeneo manne ambayo yanapaswa kuangaliwa na kuwekewa mikakati maalum - transport services ambayo ndani yake kuna miundombinu na huduma zingine za usafiri, madini, horticulture kwa Kiswahili nadhani ni masula ya maua ukulima wa maua na kadhalika na utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukiangalia bajeti jinsi ilivyokaa jinsi gani ambavyo tumegawa rasilimali zetu kidogo ambazo tunazipata haikuangalia kabisa vipaumbele hivi ambavyo taarifa ya Serikali imezitoa taarifa ambayo ndio inafanya tathmini ni wapi ambapo tunakwenda kuhusiana na suala zima la kupunguza umaskini.
Nadhani Wizara ya Fedha na Uchumi inabidi iangalie kwa sababu taarifa ya hali ya umaskini inatolewa na idara ndani ya Wizara ya Fedha na Uchumi kwa hiyo ni rahisi sana kwa idara hiyo ya kuondoa umaskini kuwasiliana na Idara ya Sera ya Wizara ya Fedha, kuwasiliana na Idara ya Bajeti ya Wizara ya Fedha ili kuweza kuangalia ni vipi ambavyo tunavyofanya vipaumbele vyetu, tukiamua kuweka vipaumbele kufurahisha wananchi kwa sasa huko tunakokwenda kutakuwa ni kugumu sana kwa sababu utagawa pesa kwa kila sekta lakini zile sekta hazitachochea sekta nyingine. Kwa hiyo kuna umuhimu mkubwa sana wa kuweza kuangalia vitu kama hivyo katika hali ya juu na ni suala lile lile la kubadili mindsett.


[MHE. KABWE Z. ZITTO]

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vipi ambavyo bajeti yetu inaendana na changamoto ambazo tunazo hivi sasa? Kwanza bajeti imeshindwa kabisa kukusanya kodi zinazostahili kwenye madini na ninashindwa kuelewa ni kwa sababau gani, kwa sababu inafahamika wazi kabisa kwamba mwaka 1997 na Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed ameielezea hapa, Bunge hili lilitunga sheria ambayo ilitoa unafuu usio na lazima kwa makampuni ya madini kwa kiasi cha asilimia 15 unafuua mbao umeifanya Taifa lipoteze shilingi bilioni 883 katika kipindi cha miaka 10 toka sekta ya madini ianze kukua katika Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulitegemea kwamba katika finance bill ya mwaka huu Waziri wa Fedha angefuta kabisa sheria hiyo kwa sababu sheria hiyo bado iko kwenye vitabu vyetu vya sheria na inafanya makampuni ya madini ambayo yana mikataba yasiweze kulipa kodi hiyo, kuna mashauriano ambayo Serikali imefanya na baadhi ya makampuni ya madini lakini kama suala hili hatutalitoa kwenye sheria halitaweza kusaidia na mfano mmoja tu wa madhara ya sheria hiyo ni kwamba kampuni ya Bulyanhulu Gold Mine ambayo inangepaswa kuwa imeanza kulipa kodi ya mapato haitalipa kodi ya mapato kutokana na faida yake mpaka mwaka 2019 yaani haitaanza kulipa corporate tax mpaka mwaka wa mwisho wa Rais wa awamu ya tano na hawa wameanza na Rais wa awamu ya tatu. Kwa hiyo unaweza ukaona ni jinsi gani ambayo Taifa linapoteza na mabilioni ya fedha kwa sababu ya sheria ambazo tumezitunga sisi wenyewe na tunao uwezo wa kuweza kuzirekebisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, misamaha, mwaka 2005 wakati tuko kwenye kampeni za uchaguzi Serikali ilitoa misamaha ya kodi miwili wa kwanza ya mafuta kwamba makampuni ya madini hayatalipa kodi ya mafuta mpaka watakapomaliza kama ni dhahabu wanayochimba, kama ni almasi wanayochimba, kama ni Tanzanite wanayochimba na tulishauri kwamba msamaha huo ufutwe kwa sababu ni msamaha ambao hausaidii chochote.

Mheshimiwa Naibu Spika, na msamaha huu ungefutwa ungeweza hata kusaidia kupunguza zile kodi ambazo tulizipandisha mwaka jana kupelekea mfumuko wa bei uweze kutokea. Sisi kama Tanzania hatuna uwezo hata kidogo wa ku-control bei ya mafuta katika soko la Dunia lakini tunao uwezo wa ku-deal na kodi zetu ili kuweza kuhakikisha kwamba tunapunguza ukali wa upandaji wa bei katika soko la Dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ilipaswa kuangalia hizo kodi zetu ili ziweze kupunguza huo ukali wa maisha. Mwaka 2007/2008 aliyekuwa Waziri wa Fedha Mheshimiwa Zakia Meghji alionyesha katika sura ya bajeti kwamba Serikali itakusanya kiasi fulani cha mapato shilingi bilioni 239 kutokana na marekebisho mbalimbali ya kodi, katika bajeti ya mwaka huu Waziri wa Fedha hakuonyesha viwango mbalimbali vya mabadiliko ya kodi vitaifanya Serikali ikusanye kiasi gani? Kwa hiyo ninadhani ni muhimu sana kuwa na mtiririko ulio sawa au consistency ili kuhakikisha kwamba kunakuwa na hali ambayo ni nzuri zaidi.


[MHE. KABWE Z. ZITTO]

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kabisa, bajeti ni vitabu vinne, volume one mpaka volume four, volume one ndio inayo-dill na mapato ya Serikali na ninasikitika kwamba mara nyingi hatuiangali hii volume. Ukiangalia kitabu cha kwanza cha bajeti utagundua mambo mawili la kwanza tunategemea sana kodi za biashara kwa maana ya import, import duties. Mabadiliko ya kodi ambayo Serikal imeyatangaza sasa asilimia 50 itatokana na import duties, hii ni hatari sana katika uchumi wa sasa, tunaokwenda, tuna East African Customs Union tunaenda kwenye common market, tunasaini EPA ambayo itaondoa kodi mbalimbali dhidi ya European Union tutapata tatizo kubwa sana kurekebisha kodi hizi tutajikuta kwamba tunakuja kuumia sana huko baadaye.
Katika revenue book, wakati Waziri wa Fedha anasema kwamba tutakusanya shilingi bilioni 58 kwa mauzo ya hisa za NMB, kwenye revenue book zinaonekana shilingi bilioni 42. Tunapopitisha bajeti tunachoangalia ni revenue book, ni nini ambacho tunakichukua? Ni hotuba ya bilioni 58 au ni revenue book ya bilioni 42, nilikuwa ninaomba Waziri wa Fedha aweze kuliangalia hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kabisa, kama tunataka kuongeza uzalishaji wa kutosha kwenye baadhi ya mazao ambayo tunayo ni lazima tuangalie jinsi gani ya kutoa incentives kwa baadhi ya mazao. Mimi nitatoa mfano mmoja na nilitoa taarifa hii toka mwaka jana kwamba leo India wameweka compulsory usage ya magunia yao ya jute kwa ajili ya mazao yote ya India. Sisi hatujaweka compulsory usage ya maguni yetu ya katani, matokeo yake ni kwamba tunakuwa tuna-export jobs kwenda Bangladeshi na India kwa sababu hatulindi sisal yetu, katani yetu wala hatulindi viwanda matokeo yake ni kwamba baadhi ya wawekezaji wamenunua viwanda havifanyi kazi kwa sababu ya mazingira hayo ya kikodi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa ninaomba Waziri wa Fedha ajaribu kuangalia uwezekano wa angalau mazao mawili, mahindi na korosho ziwe ni compulsory kutumia maguni ya katani ili ku-stimulate uzalishaji wa katani na kufanya viwanda vya katani ambavyo vimekufa hivi sasa viweze kuzalisha magunia ya katani na yaweze kutumika katika nchi, vinginevyo itakuwa ni tatizo ambalo tutaendelea nalo tutaendelea kutegemea kodi kutokana na imports ambazo madhara yake ni makubwa sana kutokana na Dunia ya sasa ya globalization.
Ni lazima kuangalia Serikali isikwepe kazi yake ya distributive role. Ni kazi ya Serikali yeyote Duniani kukusanya kutoka matajiri kuwapeleka maskini ili kuweza kupunguza gharama za maisha yao na ndio kazi ya bajeti kama sera na siyo bajeti kama urari wa mapato na matumizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru sana. (Makofi)

Mh. Zitto...

Nimesoma kwa makini... tunashukuru sana lakini kwa wengine kwa kweli hatujaona jipya hapa!
 
kwi kwi kwi kwi kwi kwi,

yaani hapa sina mbavu jamani, hivi Mushi u-mzima kweli?

Nini kinakuchekesha hapa kwenye issue nyeti?Kama unataka kwanini wewe usitoe maelezo kuhusu hii issue ya Mwanyika ambaye ni mtuhumiwa wa RICHMOND aliyewekwa kapu moja na watu wengine kwenye kamati yao ya uchunguzi ya EPA.Halafu Zitto naye kuingia kwenye kamati ya madini na Mafisadi wengine huku ripoti akipewa SINCLAIR kwanza na wakati tukielewa MWK alisema watu wanayo hapa JF lakini maneno yakapindishwa pindishwa tu na sasa tunasahaulishwa kwa awamu nyingine!Kama wananchi hawakuona mavuno kwenye msimu uliopita hawana haja ya kuwa na matumani na msimu ujao kama hali za hewa ni zile zile zenye kuashiria matokeo yale yale yenye mazao hafifu na mabovu!Nilishasema sasa ni kuchoma moto shamba zima na ngedere wote halafu tusahahu mavuno kwa msimu ujao ili tupande mbegu mpya na bora zaidi zenye sumu kali dhidi ya wala mazao wetu ambao ni NGEDERE MAFISADI MAFIOSO NA WACHAWI KULU!
 
Nililiona hilo, lakini nikasema ngoja niuchune nisije nikadhaniwa nina mzizi.

Kuhusu katani, lingine analosema Mheshimiwa ni kwamba viwanda (nadhani viwanda vya kamba, hajaeleza) vinakufa kwa sababu ya mazingira ya kodi kwa wawekezaji. Anataka wawekezaji wa viwanda hivi wapewe "incentive" ili "kulinda sisal yetu."

Kwa maneno mengine anataka misamaha ya kodi kwa wawekezaji.

Ilibidi atueleze tofauti ya huu msamaha na ule wa wawekezaji wa migodi. Halafu pia tuelewe kama ni busara kwa Serikali kujaribu kufufua sekta ambayo hata wafanya biashara wameiona haina faida. Kama wafanyabiashara wanadhani hii biashara haistahili hata kuilipia kodi, tungependa kujua kwa nini Serikali iione kwamba ni biashara yenye faida, kama anavyopendekeza Mh. Zitto.

Halafu mkuu tatizo lingine kubwa kuanzisha na kuendesha kiwanda bongo ni UMEME..Hapo RICHMOND INARUDI!Serikali inatakiwa itoe incentives kwenye gharama za umeme lakini ni MAFIA na MAFIOSOZ DEALZ za wenyewe kwa wenyewe!Wananchi hawaambiwi lolote wao wanaambiwa kuwa ni masikini na Marekani hawajatoa mchele
 
Ndugu Mbunge, naomba uniulizie au ufuatile ile Bill iliyo pitishwa mwaka jana ya kufuta au kupitisha zile fedha ambazo zilikuwa kwenye audit queries, ili zisiendele kutokea katika audit report.
Serekali iliomba wabunge wazipitishe then watazi fuatilia je wamewapa progress report yake, kama zimerudishwa watu wamechukuliwa hatua au ndio basi tena.
 
Ndugu Mbunge, naomba uniulizie au ufuatile ile Bill iliyo pitishwa mwaka jana ya kufuta au kupitisha zile fedha ambazo zilikuwa kwenye audit queries, ili zisiendele kutokea katika audit report.
Serekali iliomba wabunge wazipitishe then watazi fuatilia je wamewapa progress report yake, kama zimerudishwa watu wamechukuliwa hatua au ndio basi tena.

I have only just a minute; just sixty seconds in it … Forced on me, Can’t refuse it, Didn’t seek it, Didn’t choose it but I must suffer if I lose it, give account of it if I abuse it … just a tiny minute but eternity is in it.
 
Back
Top Bottom