Kuna watu wana hela jamani!!

Kuna watu wana hela jamani!!

Kwa mtu mwenye nazo ni bora kupanga kuliko kuwa na nyumba yako. Ni pasua kichwa sana, inaweza kuwa ni rahisi kupanga kuliko kumiliki nyumba yako! Nilikuwa natafakari mfano waziri mwanamama mwenye mtoto mdogo kama angela kairuki, je ana wadada wa kazi minimum wangapi ili na majukumu yake ya kiuwaziri yaende. Si chini ya 3. Mmoja kwa ajili ya kichanga, mwingine kupika na kufanya usafi. Kikubwa tujitahidi kuzitafuta pesa wakati Tukibana matumizi ili siku za usoni tuondokane na janga hili la umaskini uliokithiri.
Mkuu BORA kupanga?? yani kwenye kupanga na kuwa na nyumba yako Uafadhali kwenye kupanga unakujaje?
 
Nimeonyesha screenshot za tangazo tu..
Yap ni tangazo kwenye page yake
Sio mie
Unatumia MasterCard,visa,nettlller,Bitcoin,PayPal,thrller, crytcrrnc n.k nikutumie ukae katika mjengo sipend watoto warembo wapate tabu kabisa mana Mungu hakutaka wapate tabu Wala kula kwa jasho
 
Hiyo ghorofa ina vyumba vingapi? Maana tunaweza kuoiga hesabu tukagundua ni cheap kuliko hotel


Mfano kama ina vyumba 6... wakija wageni maana yake kila mmoja atalipa 50,000 per day
 
Wanayo ila si rahisi kama unavyofikiria. Tatizo la vijana wengi ni kuanza kujadili matokeo baadala ya kujadili chanzo. Mwenyewe hizo nyumba si ajabu ana miaka 80. Alipokuwa umri wako siajabu hakuweza hata kupanda daladala. Wewe leo upo katika maisha ya hali ya juu kuliko yeye! Siajabu ukifika miaka 60 utakuwa na Dreamliner yako. Wenye hayo majumba wakupe morali nawe mbele ya safari uwazidi si kuwaonea gele
Ahsante
 
yani kuna nyumba unatamani kuwa hata house boy kwa jinsi vyuma vilivyokaza...Huyo mke wake juzi kati gari yake imekwama kwenye matope Akashuka akatoa Pochi akalock gari akaliacha pale pale akarudi nyumbani...

Mume wake kurudi kuambiwa ALIMCHEKA MKE WAKE MPAKA kakaachini.. kesho yake asubuhi Gari ikaenda kusukumwa na vijana wa nne Wakaachiwa LAKI eti kuitoa tu pale,imagine!

Tanesco waliwahi kukata umeme kukawa na Mgao ule mtaaa...BABA alichukua watoto wake wote..dada wa kazi wa watoto Akaenda Hotelini kukaa na watoto wake mpaka umeme utakaporudishwa nyumbani..Unaambiwa ile nyumba bila A/C haikaliki.

Baba akirudi akisema washeni A/C mkamwambia umeme hamna...mtamuona huyoooo anabeba nguo anaaga anaenda hotelini Anawambia ukirudi umeme wenu mtaniita.

Akikaa huko siku mbili mfululizo umeme haujarudi siku ya tatu anarudikuchukua watoto wake na dada wa watoto anawapeleka hotelini....

Watu wanaishi hii TANZANIA etiii..tuacheni tu...nyumba matumizi ya umeme ni almost kila mwezi umeme wa LAKI 3 to 4...na wala haimsumbui mtu akili..wana amani BABA Ana amani,mama ana amani Raha full time
Wajenge sasa ya kwao hapo wananufaisha mtu tuu
 
Sawa tupo watu wa vipato tofauti levo tofauti
Lakini kama mlalahoi hiyo hela nkiifikiria nawaza sana..mil 54 si tayari nna nyumba mbezi now!
Inauma mkuu
Milioni 54 nyumba mbezi ipi? Labda Bunyokwa huko Mabondeni😁😁
 
Back
Top Bottom