Kuna la kujifunza kutoka kwa wachuuzi wadogo

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2023
4,695
6,398
Mwanzoni mwa mwaka 2020, nilifanya mazungumzo na kijana mmoja muuza mahindi ya kuchoma Mjini Kahama. Nilitaka kufahamu, pamoja na mambo mengine, manufaa wanayoyapata kutokana na hiyo biashara.

Aliniambia, ni biashara inayomlipa sana. Alipokosa nafasi ya kuenedelea na masomo baada ya kuhitimu kidato cha Nne, aliondoka kwao Tabora na kwenda kutafuta vibarua Kahama. Alifanya vibarua vya ujenzi kwa muda na kisha baadaye kuingia kwenye biashara ya kuchoma mahindi.

Biashara hiyo ilimpa manufaa yafuatayo:
1. Kuihudumia familia yake kwa mahitaji muhimu
2. Kulipa pango la chumba alichokuwa akiishi huko Kahama
3. "Kumwajiri" mtu aliyekuwa akikisimamia "kijiwe" chake kingine cha kuuzia mahindi. Alikuwa na jumla ya vijiwe viwili.
4. Alifanikiwa kujenga "kanyumba kake" nyumbani kwao Tabora.
5. Alikuwa akikusanya faida isiyopungua shilingi elfu thelathini kila siku. Hiyo inamaanisha endapo atafanya kazi kila siku, kwa mwezi atakuwa na wastani wa sh 900,000/=.

Baada ya miezi kadhaa, nilipata tena safari ya kwenda Kahama. Kabla sijaondoka huko, nilimtafuta mtu mwingine mchoma mahindi kwa lengo la kumfanyia usaili kuhusu biashara anayoifanya.

Alikuwa ni Muha kutoka Kigoma. Japo hakuwa amefanikiwa kumaliza shule ya Msingi (lakini alikuwa anajua kusoma na kuandika), lakini biashara ya kuuza mahindi ilimwezesha kuendelea kuwepo mjini.

1. Alikuwa akiishi kwenye nyumba yake mwenyewe, ingawa haikuwa imefanyiwa "finishing". Ni biashara ya mahindi ndiyo iliyomwezesha kununua kiwanja Kahama na kujenga.
2. Alikuwa anamudu kuihudumia familia yake kwa mahitaji muhimu.
3. Alikuwa na jumla ya "vijiwe" viwili vya kuuzia mahindi, ambapo kimoja alikuwa akisimamia mwenyewe na kingine "alimwajiri" mtu
4. Alikuwa anauza mahindi kwa bei ya jumla na rejareja. Alikuwa akiyafuata mahindi shambani, akiishayatenga atakayoyauza kwenye vijiwe vyake, yanayobaki huyauza kwa bei ya jumla kwa wachomaji wengine.
5. Alikuwa na duka la kuuzia bidhaa za nyumbani
6. Aliweza kununua pikipiki aliyokuwa akiitumia kufuata mzigo shambani na kuusamabaza kwa wateja.

Kama hayo waliyoniambia ni kweli, kuna la kujifunza kutoka kwao. Huenda, kwa yanayofanywa na hao wachuuzi wadogo wadogo, mtu akifanya tafakuri yakinifu, anaweza akaibuka na wazo litakalozaa biashara kubwa itakayozaa mafanikio makubwa.

Naamini, kwa kutumia wachuuzi wadogo, mfano, wauza mchicha kama "case study", kupitia tafakuri tunduizi, kampuni kubwa inaweza kuzaliwa. Ubunifu haujafikia ukomo. Unaendelea kila siku iitwayo leo. Na kitu chochote kile kifanywacho na mtu, kiwe kikubwa au kidogo, huanza kama wazo.

Kama "mwewe" alimtia mwanadamu wivu hadi akaamua kutengeneza chombo kitakachomwezesha kuruka angani kama yeye, biashara ya muuza karanga inaweza kumfikirisha mtu hata akamiliki kampuni kubwa ya kibiashara.

Kuna wanaume na wanawake, japo wana Elimu ndogo sana ya darasani, na wakati mwingine, hawajui hata kusoma na kuandika, lakini kwa mtaji usiozidi shilingi elfu hamsini, wameweza kuzihudumia familia zao, alau, mahitaji muhimu.

Kuna wanawake, ambao kwa biashara ya kukaanga samaki na mihogo, wamewasomesha watoto wao hadi Vyuo Vikuu.

Kuna wanaume, ambao kwa biashara ya kuchemsha kahawa, watoto wameendelea kuwa na imani kuwa mahitaji yao yatatimizwa kwa kuwa baba yao anafanya biashara ya kuuza kahawa.

Kwa biashara ya kuuza mchicha, familia nyingi zimeweza kuishi.

Kwa biashara ya kuuza matunda, watu wengi wameweza kulipa kodi ya vyumba vyao.

Kuna watu waliotumia mtaji wa shilingi elfu ishirini kuanzisha kabishara kadogo, na wakafanikiwa kuepuka aibu ya kuwa omba omba.

Ikiwa kwa mtaji usiozidi shilingi elfu hamsini, mtu mwenye Elimu ndogo ya darasani amemudu kuishi, msomi atashindwa "kutoboa" kimaisha kwa shilingi laki moja endapo atafanya tafakuri yadidi?

Tutafakari!
 
Biashara ndogo ndogo hizo hazikuachi mikono mitupu ikifika jioni , sema sehemu nyingi migambo wapo wanasumbu.
 
Niliwahi kufanya biashara hii mwaka 2001 Sinza Dsm, badae nikanunua toroli nikawa nauza maji ya madumu wakati huo sinza maji yalikuwa ya shida sana.

Katika kuuzaji maji nikatokea kupatana na familia Moja, mwisho walinisaidia kurudi shule mpaka ni lipo maliza kidato cha sita yule mama akafariki(Rip).

Aisee niishie hapa tu Ila hizi biashara ndogo ndogo zinalipa sana.
 
Hizo ni nadharia njoo na mtaji huo wa laki mtaani uone kama utafanya kitu
Namfahamu mtu mmoja, ambaye ingawa hakutajirishwa na biashara ndogo aliyokuwa akiifanya, lakini ilimsaidia alau kula yeye na wadogo zake. Ilikuwa ni mwaka 2018. Alikuwa mhitimu wa Chuo na kwa kipindi hicho alikuwa bado hajapata kazi. Kama kutokuwa na kazi ilikuwa haitoshi, alikuwa anategemewa pia na wadogo zake waliokuwa wakisoma Sekondari. Wazazi wake wote walikuwa wameaga dunia, kwa hiyo alikuwa kama mzazi kwa wadogo zake.

Aliponiomba nimkopeshe sh 20,000/= atumie kama mtaji, nilimpatia, na nikamwambia kuwa si mkopo bali nimempa. Siku chache baadaye aliniambia kuwa kaanzisha kibanda cha matunda na mboga za majani. Kwa mtaji wa sh 20,000)=, aliweza kuianzisha biashara ndogo iliyomwezesha yeye na wadogo zake kupata chakula.

Alipopata kazi ya kuajiriwa, aliachana na hiyo biashara. Alilipwa mshahara mzuri, lakini kabla ya mshahara, alikuwa akiishi kwa biashara aliyoianzisha kwa mtaji wa shilingi elfu ishirini.
 
Hizo ni nadharia njoo na mtaji huo wa laki mtaani uone kama utafanya kitu
Kwa maskini wa kipato laki anaiheshimu kama tajiri anavyoheshimu Mali zake.mtaji wa maskini ni nguvu zake waulize wauza kahawa ,wauza matunda, wauza karanga wanaotembeza mitaani uwaulize mitaji yao shs ngapi na kwa siku wanapata faida shs ngapi nimewashuhudia laki wanapata elfu 20 - elfu 30 kwa siku ,Wana mshipa wa kutembea umbali mrefu kwa miguu kusaka wateja wengi wanaosema laki si kitu ubavu wa kutembea tu kutoka Mbagala mpaka mwenge hawawezi wenzio ndio daily life ,ukiwadadisi zaidi watakwambia huko.mikioani Wana mashamba ya mpunga,alizeti,mahindi wamekubali maisha yao Wana familia ,wanasomesha watoto ,wamejenga nyumba na wanategewa .
Au amka alfajiri nenda ferry ukajionee wamama ,wakaka na wababa wakinunua samaki kwenye ndoo za lita 10 ndoo ya samaki lita 10 haizidi elfu 80 ,wanakuja mtaani wanakaanga mfuatilie jioni anapokaanga samaki utakuta wameisha muulize vp biashara yako imekutoa leo atahesabu pesa yake mbele yako utashuhudia utaamini kama mtaji ulikuwa elfu 80, mkaa / kuni na mafuta ya kupikia.

Kwa msomi au watu wenye nafuu ya masha hustling kama hizo utahitajika ujitoe Ufahamu usiwaonee aibu watu wanaokufahamu zaidi ujue hao unaowaonea aibu unapoabika kwa kukosa pesa watakucheka zaidi kukosa pesa na kukosa kazi watukusema hata biashara huna.
Huyu mwenye mtaji wa laki siku akipata mtaji wa 1milioni hufanya wonders.

Maana Siri kuu ya biashara ni biashara yako iwe na wateja aidha wateja wafuate biashara yako au wewe uwafuate wateja walipo ndipo suala la mtaji kiasi gani hufuata
 
Hizo ni nadharia njoo na mtaji huo wa laki mtaani uone kama utafanya kitu
Usibeze mkuu kama haujawahi kulijaribu hilo. Na kama ulishawahi lakini hukufanikiwa, ulipaswa kuwatafuta waliowahi kufanya jambo kama hilo na wakafanikiwa ili wakupe mwongozo.

Kuna watu wana biashara kubwa lakini wakikuambia mtaji walioanza nao unaweza usiamini, ni mdogo sana.

Kuna mwanamke mmoja jirani yangu anayefanya biashara ya kuuza mandazi. Wakati mwingine anachukua unga wa ngano kilo tatu tu. Mtu kama huyo anaweza akatumia mtaji wa shilingi elfu ishirini kwa biashara ndogo na ikamsaidia kupata mahitaji madogo madogo kwa familia yake.

Huyo mama muuza maandazi ana familia inayomtegemea. Kwa biashara yake ndogo ya mandazi, watoto wake wanakula na kusoma.
 
Kwa maskini wa kipato laki anaiheshimu kama tajiri anavyoheshimu Mali zake.mtaji wa maskini ni nguvu zake waulize wauza kahawa ,wauza matunda, wauza karanga wanaotembeza mitaani uwaulize mitaji yao shs ngapi na kwa siku wanapata faida shs ngapi nimewashuhudia laki wanapata elfu 20 - elfu 30 kwa siku ,Wana mshipa wa kutembea umbali mrefu kwa miguu kusaka wateja wengi wanaosema laki si kitu ubavu wa kutembea tu kutoka Mbagala mpaka mwenge hawawezi wenzio ndio daily life ,ukiwadadisi zaidi watakwambia huko.mikioani Wana mashamba ya mpunga,alizeti,mahindi wamekubali maisha yao Wana familia ,wanasomesha watoto ,wamejenga nyumba na wanategewa .
Au amka alfajiri nenda ferry ukajionee wamama ,wakaka na wababa wakinunua samaki kwenye ndoo za lita 10 ndoo ya samaki lita 10 haizidi elfu 80 ,wanakuja mtaani wanakaanga mfuatilie jioni anapokaanga samaki utakuta wameisha muulize vp biashara yako imekutoa leo atahesabu pesa yake mbele yako utashuhudia utaamini kama mtaji ulikuwa elfu 80, mkaa / kuni na mafuta ya kupikia.

Kwa msomi au watu wenye nafuu ya masha hustling kama hizo utahitajika ujitoe Ufahamu usiwaonee aibu watu wanaokufahamu zaidi ujue hao unaowaonea aibu unapoabika kwa kukosa pesa watakucheka zaidi kukosa pesa na kukosa kazi watukusema hata biashara huna.
Huyu mwenye mtaji wa laki siku akipata mtaji wa 1milioni hufanya wonders.

Maana Siri kuu ya biashara ni biashara yako iwe na wateja aidha wateja wafuate biashara yako au wewe uwafuate wateja walipo ndipo suala la mtaji kiasi gani hufuata
Nimewaona watu wa sampuli hiyo. Siyo mmoja wala wawili. Ulichoandika ni kweli kabisa!
 
Usibeze mkuu kama haujawahi kulijaribu hilo. Na kama ulishawahi lakini hukufanikiwa, ulipaswa kuwatafuta waliowahi kufanya jambo kama hilo na wakafanikiwa ili wakupe mwongozo.

Kuna watu wana biashara kubwa lakini wakikuambia mtaji walioanza nao unaweza usiamini, ni mdogo sana.

Kuna mwanamke mmoja jirani yangu anayefanya biashara ya kuuza mandazi. Wakati mwingine anachukua unga wa ngano kilo tatu tu. Mtu kama huyo anaweza akatumia mtaji wa shilingi elfu ishirini kwa biashara ndogo na ikamsaidia kupata mahitaji madogo madogo kwa familia yake.

Huyo mama muuza maandazi ana familia inayomtegemea. Kwa biashara yake ndogo ya mandazi, watoto wake wanakula na kusoma.
Kuna msemo pesa ya biashara hailiki ni pesa ya kuzungushia biashara tu.

Wapemba,wahindi na siku za karibuni wakinga ni wajuzi kwa hilo . Ndilo fumbo la kufanikiwa kwa biashara ndogo hata kubwa, nidhamu ya pesa usipokuwa na nidhamu ya pesa ,kufanikisha biashara yako isonge mbele itakuwa mtihani mzito
 
Kuna msemo pesa ya biashara hailiki ni pesa ya kuzungushia biashara tu.

Wapemba,wahindi na siku za karibuni wakinga ni wajuzi kwa hilo . Ndilo fumbo la kufanikiwa kwa biashara ndogo hata kubwa, nidhamu ya pesa usipokuwa na nidhamu ya pesa ,kufanikisha biashara yako isonge mbele itakuwa mtihani mzito
🙏🙏🙏
 
Fedha nidhamu Tu. Watu wanaishi na biashara ya Karanga za kukaanga Tu. Kama MTU unaingizwa Faida SHS 5000 Kwa siku basi tumia nusu na nusu uweke. Jambo hili wenye malengo wanaweza.
 
Back
Top Bottom