Watu wana hela bwana mi nikiskia watu wakilalamika MAISHA MAGUMU nawaangaliaga halafu sitii hata neno Nanyamaza kimya.
Kuna binti alikua hapa nyumbani kwangu muda tu alikua anatafuta kazi,basi siku moja rafiki angu akanambia ana rafiki ake anatafuta House girl,kwa kua yule bint alikuepo nikamwambia kuna kazi imepatikana ya u house girl nenda kafanye mshahara ni 150,000 Akashangaa sana kama nilivyoshangaa ila kesho yake akapaki vitu akapelekwa huko kwa boss wake.
Kaenda kwa hiyo nyumba ni appartment ya maana Ghorofa na ni wamepanga kuna baba,mama,watoto wao wa 3,house girl wa watoto 1,wa usafi 1 wa chakula 1 so huyu bint aloenda anaenda kuwa house girl wa 4.
Nje kuna house boy m1...Nyumba hiyo ni hatari hizi story alitusimulia huyo binti baada ya kwenda kufanya kazi huko kama mwezi then siku 1 akaambiwa aje atusalimie ndio katika kumuuliza vipi kazi huko ndo akawa anatupa hadithi.
Watoto wawili wote wamenunuliwa smartphone Samsung s6 edge plus za kuangalizia katuni na kuchezea game kila mmoja na yake...Huko ndani maji yanayonyweka ni K.njaro Tu.
Kula hamna ratiba ya pamoja...kila mtu anapikiwa chakula anachotaka SO unakuta mezani baba anataka wali,mama anataka pila,mtoto anataka Chips, mwingine anataka Kuku...vyakula vyote hivyo vitapikwa na vitaletwa mezani.
Soda zimejazwa stooo kama vile wana duka la vinywaji....
kipindi hiki cha mvua nyumba yao imekaa sehemu ambapo gari hazifiki vizuri so Wanachofanya asubuhi wakitoka BABA anatoka na gari Ya juu ya kupita rough road then anafika mbele kule anaipaki kwasababu imechafuka anachukua gari yake ingine NOAH ndio anaenda nayo kazini...akirudi anapaki noah Pale pale kisha anachukua Cruiser lake la juu likiwa lishaoshwa anarudi nalo home.
JMOS NA JPILI nyumbani hapapkwi kitu baba analeta Chakula misosi inayoletwa ni mara 100 wapike wao kina dada unaambiwa maana baba analeta vyakula kama kuna sherehe.
watoto watatu na kila mtoto na room yake hawalali pamoja...kila chumba cha mtoto kina flat ya ukubwa wa 55inch...
dada wakazi wote Hawalali pamoja kila dada wa kazi analala chumba chake peke ake.
Jinsi nilivyokua namsikiliza huyo dada akisimulia nilikua nahisi naangalia MOVIE ila haya maisha ya hivi watu wapo tena tuko nao hapa hapa TANZANIA mnayosema ni nchi maskini.