Kuna vitu vinakera: Viatu vina matope

Kuna vitu vinakera: Viatu vina matope

Si afadhali ya huyo anaonekana katulia,mwingine miguu haitulii akiongea na miguu nayo inaongea,shuguhuli akishuka sasa, utadhani ulitoa lift kwa watu wa tano kumbe mtu mmoja...
 
Hahahaaa. We mwenye gari ndio unakwazika na wao huwa hata hawajali. Akishashuka sasa unaanza kulalamika kimoyo moyo.

Ila huyo mdada kiboko tope lote hilo anaingia nalo pasi hata kujishtukia.
Lkn si ndio maana kuna hilo Carpet hapo la nylon...labda wakati anaingia kulikua na mvua akashindwa kufuta hilo tope.
 
Kumbe ni tope, mie nilidhani ni urembo wa kiatu chake!!!!
 
Lkn si ndio maana kuna hilo Carpet hapo la nylon...labda wakati anaingia kulikua na mvua akashindwa kufuta hilo tope.
Mmh. Ndio kazi yake ila kiustaarabu basi bora hata angelipunguza.

Ikiwa kila anayepanda kwenye gari hawi na ustaarabu sijui kama pangekuwa panatosha kwani sidhani kama kila mwenye gari ana ratiba ya kila leo kuosha hizo carpet.
 
Hahahaaa. We mwenye gari ndio unakwazika na wao huwa hata hawajali. Akishashuka sasa unaanza kulalamika kimoyo moyo.

Ila huyo mdada kiboko tope lote hilo anaingia nalo pasi hata kujishtukia.

Labda huko nje ya gari tope limeshamiri bila kusahau mvua ya haja, hamna hata pa kuyatolea…anafanyaje?

Labda ndio maana akajiandaa na kiatu cha kazi pia….
 
Labda huko nje ya gari tope limeshamiri bila kusahau mvua ya haja, hamna hata pa kuyatolea…anafanyaje?

Labda ndio maana akajiandaa na kiatu cha kazi pia….
Huenda ikawa pia.
 
Si afadhali ya huyo anaonekana katulia,mwingine miguu haitulii akiongea na miguu nayo inaongea,shuguhuli akishuka sasa, utadhani ulitoa lift kwa watu wa tano kumbe mtu mmoja...
Hahahaha, kuna watu wakikaa kwenye gari utadhani wanakata roho,miguu wanarusha rusha hovyo halafu ukute anatope hivyo
 
Back
Top Bottom