Kuna under 30 anayemiliki gari na nyumba?

Kuna under 30 anayemiliki gari na nyumba?

Inawezekana kabisa mkuu. Sema ni watu wachache kwa tanzania yetu hii. Mimi mwenyewe ni moja ya hiyo sample, gari 2 na nyumba nzuri ya kawaida na nina 29 by now na sijaiba cha mtu. Mwombe Mungu na upambane bila kukata tamaa. Ukitegemea mshahara tu hautoshi. Nenda shamba, anzisha na vibiashara hata kama si vikubwa.
 
Jamíiforums kila mtu ni tajiri, kila mtu ana nyumba na gari!!!!

Wengine hata pikipiki hawana lakini nao wamo!!!!!
Lkn ni jukwaa lenye mchango chanya!Kuna siasa,burudani,utani,elimu,dini,mahusiano nk.
 
Inawezekana, ila inabidi uwe single minded kidogo.
Anza kujenga nyumba kabla ya kununua gari.

Kumbuka bia 1 = Tofali 2.
do!bia 1=tofali 2!ina maana chumba kimoja cha tofali 450=bia 225!kumbe mwaka 1 badala ya bia =vyumba 2!
 
Wakuu naomba kuuliza hivi humu jamiiforum kuna kijana yeyote ambaye yupo chini ya miaka 30 ambae anamiliki gari na nyumba.Yani ambae ametafuta kwa jasho lake bila kupewa au kurithi.

Nimeuliza hivi kwa sababu mimi nina miaka 25 na ndoto zangu ni kumiliki gari na nyumba kabla Sijaoa.Lakini kila siku zinavyo sogea naona ndoto inakua ngumu kutimia.

Nikipita barabarani au kwenye kumbi za starehe naona vijana wadogo wamepaki magari yao, basi roho yangu inaumia sana.

Hivi inawezekana kweli au ni ndoto za mchana hizi ninazo ota.
It could be much more better if you had put it more specific. Wako watu at their 25 tayar wameshakuwa na majumba (sio nyumba ) na magari ya kifahari. Lakini swali la msingi ni kuwa "How the heck did they get there?" Mbali na urithi je wametumia njia halali kufika hapo walipofika ?Je nyumba na magari waliyonayo ni matokeo ya kufanya kazi kwa bidii kwa halali ?. Kwa maana in the previous phase government, many young people aged 22 to 30 acquired riches not because of their hard work but as a result of public funds embezzlement and tax avoidance .
 
Inategemea na bahati ya mtu na kikubwa hii bahati isimamiwe na akili zenye utashi kwani umri huo vijana wengi wanawaza starehe zaidi kwa kufikiri maisha yatajiseti baada ya kuanza 30...
Maisha hayana bahati kla mtu kazaliwa na bahati
 
Riz1 anaweza kutusaidia mbinu ya jinsi ya kutajirika kwa haraka haraka
 
Wapo mkuu ila wachache sana. Mimi kati ya umri wa miaka 22 mpaka 25 nilikua tayari nina viwanja vi 3 na baadhi ya biashara za mitaji midogo. at 26 nilioa na kufunga ndoa(sio harusi)pia nilianza ujenzi taratibu. 27 niliendeleza ujenzi na mwaka huo huo nika hamia ingawaje nyumba ilikua haijakamilika baadhi ya vyumba vya ndani.
 
Fafanua nyumba ya kiwango kipi? hata kwa mkopo ni sawa kwa vigezo vyako?
 
Maisha ni malengo. Kamwe usishindane wala kujilinganisha na mwingine. Our struggles are different.

Kwa kijana wa kawaida wa Kitanzania (ambao ndo tuko wengi), ambaye ametoka kijijini akabahatika kuingia University, its is obvious atamaliza degree ya kwanza at the age of 25-27. Baada ya hapo aanze kutafuta address mjini. By the time anaanza kupata sense of stability he is already 30! Na mishahara ya serikali yetu (hata Private sector), you can see that struggle is real. coupled na extended families mambo yanakuwa magumu zaidi.

Hapo linganisha na yule ambaye ni mjasiriamali. Alimaliza form four/six akaingia uraiani. Wengine walifanikiwa. wengine hawajafanikiwa. Wengine unayatamani mafanikio yao. Wengine wanatamani ya kwako. Ilimradi kila mtu anauelewa wake nini maana ya mafanikio.

Ushauri kwa wadogo zetu. Msishindane na wengine. Maisha hayana specific plan. Na mjue kabisa usione vyaelea vimeundwa/tafutwa. Kikubwa muwe na bidii/juhudi na muwe waaminifu katika majukumu yenu. Uaminifu ni silaha.

Ukiona mtu anaendesha gari. Don't panic! ukiona ana nyumba nzuri don't panic! be inspired. Mimi nimenunua gari 10 years after University. Kuna kipindi mpaka jamaa zangu wakawa wananicheka (by then nilikuwa hata naazima IST ya wife). But I knew what I wanted. At the end of the day nimenunua gari ambayo najua ni jasho langu. Its a beautiful car which I dreamed all along! Chuma cha Mjerumani. and that gives me inner satisfaction. Sijaanza kujenga nyumba yangu (nimeshawajengea wazazi though). Lakini some of my friends wamejenga mpaka maghorofa. Nawatembelea, we drink together and we are close as ever.

But I know when time comes, God allowing, I will build house (in a nice place ;-) and friends and foes alike will admire it. Huu utaratibu wa kujenga simply kwa sababu fulani amejenga "anakaa kwake" niliukataa. Au kwenda kununua kiwanja ni the middle of nowhere....kusudi tuu niwe na nyumba...nilikataa..(bora kurudi kujenga kijijini kwetu). Honestly kuna nyumba nyingine unaziangalia mpaka unasema Lord Have Mercy kwa huu ujenzi.......lakini unakuta yote yanafanyika kwa sababu watu wanaishi kwa kufuata pressure za wengine............! I reject this notion..I have got one life to live.

I determine my own pace of movement. Sitaki pressure za walimwengu. At the end of the day sishindani na mtu. Maisha niliyonayo ni haya tuu. I simply want to be happy and fulfilled.
 
Unaweza ukawa na 46 huna nyumba wala gari lakini moyoni una amani na hofu kwa kuamini kwamba utajenga na kununua gari kutokana na strategies ambazo umejiwekea. Hata hizi nyumba ambazo wengi tunasema tumejenga kimsingi ukizifanyia tathimini utagundua bado hazijaisha though kwa vigezo vyetu tunasema zimeisha maana nyumba nyingi ambazo hata tulizowahi kupanga unakuta ni nzuri ndio lakini drishani kuna wavu au ndani imepigwa lipu ndani haina rangi....in this case hata kama mtu hajajenga bado atatukuta tu
Wanasema unahamia site siyo kwenye nyumba ha ha haaaa
 
Umezipata wapi? Isiwe ndio nyinyi mnarithi halafu mnajifanya wapambanaji
Tatizo ukiwa mvivu wa fikra na elimu ndogo ndio utafikiria huko fanya kazi hela mbona ipo nje sina cha urithi hata kimoja na wewe inaonekana ndio kati ya wale wanaokaa kijiweni wanasema maisha magumu raisi hatufai wakati mashamba yapo kibao ya kulima huko kijijini sasa wewe kaa mjini upige porojo hela itakufata tu sawa we kichwa maji
 
Duuh kwa hiyo kama una 30+huna nyumba wala gari na una diploma let's say ya clinical medicine afu unataka ukasome degree MD for 5 years n wa 6 intern you have to think properly,mmmh kaz kwel kwel nna miaka 31 sina hela sina nyumba sina gari sina degree na heslb wanabana mkopo,poor me
 
Back
Top Bottom