Kuna nini Hospitali ya Kairuki?

Kuna nini Hospitali ya Kairuki?

Tulienda pale watu watatu wote wagonjwa wetu wakiwa na tatizo linalofanana kifafa cha mimba, wakaforce operation, mimi nikakataa nikamhamishia mgonjwa wangu Muhimbili, mgonjwa wangu aliponea muhimbili, wale jamaa tuliokutana nao pale wagonjwa wao walifariki baada ya kufanyiwa operation, na waliletwa muhimbili ikiwa too late
 
Why majority of the operations are not sucessful....watu wanapoteza maisha....what the heal is going on??????

Ni hayo tu...kwa anaejua tatizo la pale embu afungue macho na wengine

Watu wengi naowajua waliofanyiwa upasuaji pale they didnt make it...to bad

Inategemea na aina ya ugonjwa wako na hali (stage) yake mgonjwa na ugonjwa. Wagonjwa wanakufa kote Muhimbili, TMJ, India, Uingereza (Nyerere kafia huko), Marekani (Balali kafia huko), n.k. Labda ungetoa takwimu na aina ya operation zinazohusika tungeichangia mada yako kwa ufanisi. Hata hivyo hakuna Hubert Kairuki hospital ila kuna Kairuki Hospital (KH) sijui unasema ipi?
 
Umefanya kazi ya wabunge wa CCM kuitetea serikali yao badala ya kuisimamia. Mtoa uzi inawezekana hana takwimu zinazosadifu hoja yake. Kama kuna mtu yeyote au wa kutoka medical records ya Hulbert Kairuki Hospitala ana weza kukanusha au kukubaliana na mtoa uzi kwa ktupa takwimu zilizochachawizwa. Kwa mfano anaweza kusema ' katika kipindi cha 2011_ 2013 kulifanyika upasuaji wa wagonjwa xxx walitoka salama xxx. Kuna wagonjwa xxx waliokuwa na magonjwa mengine walifanikiwa wagonjwa xxx na wengine xxx hawakufanikiwa kutokana na complication zingine. Kuuliza maswali juu ya maswali ni kukwepa hoja au kutojua unachotakiwa kujibu au kutokuwa na majibu.
Watanzania tumeingiwa na ugonjwa wa kuandaa utetezi hata pale tunapotakiwa kukiri ukweli. Siamini kama mtoa uzi ana nongwa yoyote na hospitali hii, naamini patakuwa na ukweli kwa 100% fulani. Kusema kwake hadharani kunasaidia uongozi wa Hospitali kujitatimini upya badala ya kujitetea kwa maana ya kuficha kasoro zilizopo ili zisirekebishwe.Hoja ya kusema ni Hospitali kubwa, inafundisha madaktari sio ya msingi sana, kinachotakiwa ni matokeo chanya ya kazi ya Taasisi, wanaweza pia wakawa wanafundisha hovyo hovyo kwa sababu hakuna pia standard operating procedures zilizoandaliwa kwa wote. Taasisi nyingi hufuata sops wakati wa kusajiliwa lakini baada ya usajili huachana nazo kabisa na hakuna benchmark zozote zinazofanyika baina ya Hospitali zetu. Unaposema ni Hospitali kubwa hata hatujui ni kwa vigezo gani unasema ni kubwa, je; ni kwa madaktari waliobobea wengi, wamebobea katika nyanja zipi, je; kwa idadi ya wagonjwa wa OPD au wa kulazwa? Na mambo mengine kama haya
Huu Uzi haujatenda haki kwa sababu una 'generalize' bila kutoa takwimu sahihi.

Unaposema majority ni ngapi hizo? Na ni kati ya ngapi? Hii ingetuaaidia.
Hao ambao hazikwenda vizuri hali zao kabla ya operation zilikuwaje?

Hivi walikuwa na shida gani nyingine ukiacha hiyo iliyopelekea kupasuliwa? Mfano kisukari, high blood pressure, ukinwi nk.nk..

Nijuavyo mimi HK Memotial Hosp ni Hosp kubwa na inafundisha madaktari hivyo uwezekano wa kupelekewa kama Rufaa wagonjwa wslio mahututi walitibiwa sehemu nyingine ni mkubwa na hii pia inaongeza uwezekano wa wagonjwa ambao hawataishia vizuri kutokana tu na hali zao.

Ni Kweli hata mmoja Kati ya mia akifariki kwa yule iliyemtokea kwake ni asilimia 100.. Lakini ni vizuri kuwa na background information badala ya kulaumu tu simply kwa kuwa aliyeguswa ana nafasi ya kuandika mtamdaoni ....
 
Ni kweli Hospitali zote duniani huwa wanakufa na hakuna Hospitali isiyokuwa na chumba cha kutunzia maiti, lakini inapotokea alarming sign ndipo watu hushituka. Haitoshi tu kusema maadamu Nyerere kafia huko basi tufanye uzembe kwa kisingizio cha Nyerere kafia ulaya,mawazo kama haya hayapaswi kutolewa na msomi aliyeelimika labda kama amekusanya vyeti tu na kilichomo kichwani hakiendani na cheti chake alichotundika ukutani. Msomi wa kweli ni yule anayefanya kazi kwa weledi kwa mujibu wa taaluma husika bila kutegemea mwenye taaluma mwenzake wa wapi kafanyaje
Inategemea na aina ya ugonjwa wako na hali (stage) yake mgonjwa na ugonjwa. Wagonjwa wanakufa kote Muhimbili, TMJ, India, Uingereza (Nyerere kafia huko), Marekani (Balali kafia huko), n.k. Labda ungetoa takwimu na aina ya operation zinazohusika tungeichangia mada yako kwa ufanisi. Hata hivyo hakuna Hubert Kairuki hospital ila kuna Kairuki Hospital (KH) sijui unasema ipi?
 
Nilishapoteza jamaa yangu pale kwa operation ya moyo dash r.I.p athuman
 
Naomba kuuliza. Kuna hospitali inayofanya operesheni na hakuna mgonjwa aliyewahi kufa kutokana na kufeli kwa operesheni?
 
Naomba kuuliza. Kuna hospitali inayofanya operesheni na hakuna mgonjwa aliyewahi kufa kutokana na kufeli kwa operesheni?

Hakuna na jambo la kawaida na ifanyike operation inapobidi, baada ya njia nyingine zote kushindikana, kwa mfano mtu aliyepata kifafa cha mimba huwezi kukimbilia kumfanyia operation unammaliza, hilo lilinitokea binafsi na watu wengine wawili pale kairuki Mimi nikagoma nikamhamisha mgonjwa kumpeleka muhimbili alipona bila operation wenzangu walipoteza wapendwa wao
 
Km ndio inatia mashaka y kairuki!!!!!kairuki!!!!!! N nt regency,muhimbili,burhan....itakuwa kuna tatizo hebu tuwe makini tusibishe bishe tu
 
Why majority of the operations are not sucessful....watu wanapoteza maisha....what the heal is going on??????

Ni hayo tu...kwa anaejua tatizo la pale embu afungue macho na wengine

Watu wengi naowajua waliofanyiwa upasuaji pale they didnt make it...to bad
Twambie unaongelea operations za tatizo gani?
Acha ubabaishaji na kuharibia watu biashara na kuwatisha...weka hapa ushahidi na takwimu za vifo ukilinganisha na hospitali zilizopo dar na operations zinazofanana ...
Si kila operation hufanikiwa weka hapa takwimu..
 
Twambie unaongelea operations za tatizo gani?
Acha ubabaishaji na kuharibia watu biashara na kuwatisha...weka hapa ushahidi na takwimu za vifo ukilinganisha na hospitali zilizopo dar na operations zinazofanana ...
Si kila operation hufanikiwa weka hapa takwimu..
Yaani wewe unawaza biashara tu
 
Twambie unaongelea operations za tatizo gani?
Acha ubabaishaji na kuharibia watu biashara na kuwatisha...weka hapa ushahidi na takwimu za vifo ukilinganisha na hospitali zilizopo dar na operations zinazofanana ...
Si kila operation hufanikiwa weka hapa takwimu..

Kwa hili jina lako usingebisha ningekushangaa... Lakin pia umenishangaza kuongelea biashara wakati hapa tunajadili uhai wa watu. Kwa mimi hospital ile siwezi kwenda tena nilienda huko mwaka juzi nilikuwa siumwi ila niliamua kwenda kuchek afya ya mke wangu alikuwa na mimba changa, walileta complication vipimo kibao havina maana mwisho wa siku wakaleta bili 180000 nikalipa ila nikaahidi kutorudi tena pale. Mimi kwa magonjwa ya kawaida naenda SANITAS wana huduma nzuri sana na bei za kawaida ishu kama ni kubwa ni Aha Khan au Muhimbili.

Mghosi
 
Naomba kujua kama Aga Khan wameanza tena kupokea wateja wa NHIF.

Tafadhali sana jamani kwa anayejua anisaidie. Nina dharura sana.
 
Amepotoka nadhani 'heal'hakumaanisha ile ya kutibu ila alitaka kusema 'what the hell is going on' 'to bad'nadhani alitaka kuandika 'too bad' hayo ndo marekebisho kama na mimi sijapotoka.

Nashukuru kwa clarification that's what exactly i meant
 
Ndo ivyo kaka. Mmiliki kwa sasa ni RIP lakini alikuwa ni hatari sana kwenye hizo makitu za kula uroda kwa kutumia 'undue influence'



Washwa 2 ...'Undue influence.' Ndio nini..? Na humu yumo mtoto wake mmoja.! Subiria povu la kihaya...!
 
...acha uchawi, one of the best hospitals na chuo cha madaktari hapa nchini kwa sasa. Nimewahi kutibiwa hapo na sasa huduma zao ni bora sanaaa kuliko wasanii wengi hapa mjini....
ningumu kumwita mtu nyo.....hii hospt nizaid yaunyok.....mwambie aliekutuma....
 
Hao washenzi toka waniulie MAMA Sina hamunao.... kunadk anaharufu kamayakinyesi mhindisimhindi
 
Naomba kuuliza. Kuna hospitali inayofanya operesheni na hakuna mgonjwa aliyewahi kufa kutokana na kufeli kwa operesheni?

KAMAMZAZI ALUKUSOMESHA SHULE ZINAZOFELISHA namashaka na uwezowako.....uwezi kuendelea nidili nahospt zinazoua kwa oper kisa lugalo nao wanaua.. hii niangalizo usiangalie nbiasharayamjomba.. mama. shangazi angaliayafuatayo uhaiwawatu nenda kashauri wabadilike wasikimbiliehela za operation kunanjia kibao.....

Ntaruditena
 
Nadhani kuna kitu tumesahau, operation sio ndio inayookoa maisha ya mtu, kuna Mungu juu ya hayo yote na tusiwaaminishe watu kwamba daktari ndiye anayeokoa maisha ya watu ila Mungu humtumia daktari kutuponya. Pili sijaona takwimu hivyo umegeneralize ktk kutoa maamuzi. Ile ni hosp kubwa hivyo hupokea wagonjwa wengi na rate ya vifo lazima iwe juu. Nilikuwa nakwenda sana Muhimbili hosp, wastani wa kila baada ya dk kama 20 unaona maiti nyingi zinapita mbele yako, ningeweza kusema hivyo ila sina uchunguzi niliofanya kusupport my urgument. Pia watanzania huwa tunakwenda hosp tukiwa ktk hali mbaya na kufanya operation kuwa option ya mwisho iliyobaki. Mama yangu mwaka jana alifanyiwa operation hapo tena ya tumbo ila namshukuru Mungu alitoka salama na sasa yupo salama. As said above unaweza ukawa na hoja ya msingi sana na yenye manufaa ila angalau jaribu kuweka takwimu ili tujue wapi tunaanzia kujadili. Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom