Kuna mambo mawili Rais kapotoshwa

Kuna mambo mawili Rais kapotoshwa

Ni kweli umena mkuu. Tatizo la bwana mkubwa apende ushauri ina maana wasaidizi wake hawajaliona hili? Sector ya utalii hawajaliona hili?
 
Unapotosha.

Rais hakuongelea "ada ndogo" na "ada kubwa". Rais Magufuli ameongelea kodi.

Mkisoma hamuelewi basi hata kusikia hamsikii?

Kuna kitu kinaitwa Elasticity of Demand....na biashara ya Utalii in very elastic ongezeko la gharama kidogo linaweza kumuondoa mtumia huduma na kwenda kwa msambazaji mbadala (substitute) mwenye gharama ndogo. Kodi 18% inaongeza gharama za utalii kwa mtalii hivyo ni rahisi kwenda kwenye nchi yenye gharama za chini....kuna economic benefits nyingi tutapoteza watalii wakipungua at a cost of VAT.
 
Haya wewe ndio unaelewa kuliko wengine. Hivi ile Mnayokata kwenye miamala ya simu Pesa na benki ni nani anayetakiwa kulipa!?

TRA ipo kwa ajili yako, unaweza kupitia tovuti yao kuwauliza chochote kuhusu kodi.
 
Kwenye V.A.T ya utalii yaani value added tax. Kwenye utalii wamechemka vizuri na hii athari yake wataiona baadae kabisa wakishaua huo utalii wenyewe
 
Mimi naona tozo hizi kwenye utalii ni moja ya kupunguza pesa za kigeni ambazo tunazihitaji ktk manunuzi ya nje .Pia kwa nn tusinge ongeza tozo kwenye madini ambapo ajira ni za watanazania ni ndogo ukilinganisha na utalii ambao kuna hotel ma tour gud na manunuzi ya vitu vya kiasili na kote huku ndo kuna ajira nyingi za watanzania
 
Ngosha nakupongeza kwa ufafanuzi wako mwema kweli jukwaa likipata wachambuzi wapatao 50 hivi
 
Lipo tatizo mahala fulani tusipopajuwa. Tatizo kubwa haswa.

Ifahamike kwamba miaka hii sekta ya utalii iko very competitive na nchi zenye sera nzuri ndio zitkazofaidika. Uwapo wa vitutio vyakutengenezwa kama disyneland ya Marekani, marineland ya Canada, na kuboreshwa kwa miji ya kitalii duniani kama vile visiwa vya Carebean, Mexico City, Thailand, Madagascar na kwingineko, kuchipuka kwa utitili wa miji ya sinema (film cities) inayovutia zaidi kama India, Nigeria, China na kwingineko, na globalization of international trade inayohamasisha usafirishwaji wa wanyama hai kutoka Africa na Asia kwenda kwenye zoo sehemu watokazo watalii wetu ni sababu tosha sana kwetu kuwa na sera za kuwashawishi watalii kuja Tz badala ya sehemu hizo chache tajwa hapo juu. Sera hizi ni pamoja na kuondoa kodi za ovyo na kufutilia mbali ukiritimba wa aina yoyote.

Ikumbukwe kwamba kodi kubwa katika utalii inaathiri sio tu kiasi cha watalii wanaoingia bali biashara zinazotegemea utalii ikiwamo, usafiri wa maji nchi kavu na angani, tour guide companies, hotels, food production and services, gift shops, car rentals, nk. Kwa maana hii madhara ya kodi katika utalii lazima yaangaliwe kwa mapana yake! Serikali lazima ipime direct monetary gains in terms of government revenue vis-a-vis indirect na direct impacts kwenye sector na biashara nyingine ambazo zina mchango wa moja kwa moja kwenye mapato ya serikali.

Sasa kama tuko tayari kuona watalii wakipungua kwa kutohafiki ongezeko la kodi, je tupo tayari kuona sekta tajwa hapo juu zikiumia? Kama sivyo basi lipo tatizo na vyombo vyetu vya maamuzi, lipo tatizo mahala fulani.
 
Unapotosha.

Rais hakuongelea "ada ndogo" na "ada kubwa". Rais Magufuli ameongelea kodi.

Mkisoma hamuelewi basi hata kusikia hamsikii?
Haha malizia kwa kusema "VAT" na "Bila VAT"
 
Unapotosha.

Rais hakuongelea "ada ndogo" na "ada kubwa". Rais Magufuli ameongelea kodi.

Mkisoma hamuelewi basi hata kusikia hamsikii?
Hii ndio shida ya baadhi ya KLF au HGK scholar kuchambua taarifa ya kiuchumi. Nani kati yenu haelewi?
 
Kwani ka VAT ka asilimia 18 kwa hao wazungu kana hasara gani?
Hata wakikalipa hako bado ni kidogo tu
 
BIASHARA ushawishi
Maneno kuntu kabisa hayo fika pale kipawa na banana uwakute wafanyabiashara ya samaki wabichi utachoka jinsi wanavyovutia wateja samaki mfano aina ya changu huyo yupo karibu meza zote lakini watakushawishi kwa maneno tofauti tofauti mara hawa ni wa leo leo huyu, mwingine hawa hawakuwekwa kwenye frigi,mwingine ukinunua nitakupa mmoja bure hahaaaa hadi unashawishika kununua kwa mmoja wao.Biashara ni mbinu za kuzidiana kete vinginevyo itakudodea,Mleta mada pia imewasilisha hoja yako safi kabisa ubarikiwe,achana na hao nyumbu wa Lumumba kwao wao kila asemacho JPM ni makofi tu hao hawana msaada kwake na kwa vile na yeye hupita humu hahangaiki na michango yao maana haina changamoto.Alichosema MH.raisi mimi binafsi simlaumu ila naelekeza lawama zangu kwa washauri wake wa uchumi hasa waziri wa fedha maana JPM hakuna aliposomea uchumi.Hilo eneo ndilo limekuwa namba moja miaka yote kutupatia pesa za kigeni leo hii tunaongelea kirahisi kabisa kwamba wacha waende,ni kweli wataenda maana twiga aliyeko Serengeti ni sawa na aliyeko Kenya na Afrika kusini pia.wawezaje kuwa na bidhaa sokoni bila kujua wenzio bidhaa hiyo hiyo wanaiuzaje na ufanyeje ile uvute wateja waje kwako na wasiende kwao.NI suala la muda tu watatukuta hapa hapa JF siku mambo hayakwenda kama walivyotegemea.
 
Wanamdanganya vingi tu,
Tutegemee matokeo ya ajabu-ajabu kwa haya maamuzi ya ajabu-ajabu.
 
Kwanza kuna tofauti kubwa sana kwa ujio wa watalii wachache na wengi kwa wananchi wa kawaida mmoja mmoja.
Hili hata akienda kuwauliza wale wakina mama wa kimasai wauza shanga wanaweza kumuelimisha.
Kwa kweli Rais amekosea kusema hivyo .... Watalii wakija hapa faida zake siyo tu kulipa kodi bali wanaleta pesa za kigeni wanazibadilisha na kuzitumia. Kwenye kuzitumia watakula, watakunywa na watanunua vizawadi!!

On the other hand, kinacholalamikiwa siyo watalikulipa au kutokulipa kodi bali ni gharama kubwa za kuja kama Mtalii Tanzania. After all hiyo VAT wanalipa indirect kama Watanzania wengine!!

Tanzania inabidi tujue kuwa pamoja na kuwa na Mbuga nyingi na kubwa lakini bado tujue kuwa siyo peke yetu Africa tulio na hizo mbuga. Sidhani kama kuna wanyama ambo wako Tanzania hawako kwenye nchi nyingine za wenzetu Africa. Wakati sisi tunawasimanga wenzetu wanawaita.

Halafu kitu kingine cha kujua siyo kwamba watalii wote ni matajiri. Wengi wao ni maskini tu kama sisi ila wana hiyo bobby ya kutembea na kuona dunia. Wanakwenda kwenye nchi za wenzetu zaidi kwa vile wameimalisha infrastracture zao mpaka kuna Camping sites ambazo ni malazi ya gharama nafuu kwa watalii.

Nchi kama Botswana au namibia ambazo zina Mbuga moja moja tu zinavuta watalii wengi kuliko sisi.

Kwa kulalizia nakubaliana kabisa na mleta mada ... gharama kubwa kwa watalii zingeelekezwa kwa wale wanaofanya Trophy hunting siyo hawa wa kutembelea mbuga na kukaa pwani!!
 
Wanaopiga kelele waelewe kuwa mzungu anaheshimu sana ulipaji wa kodi. Tena tukijitegemea itakuwa nafuu kwao kwani ziara za kutembeza bakuli zitapungua. Kwa taarifa sahihi ni kwamba tour operators hawataki uwazi katika mapato yao na wanaogopa hizo return za VAT zitawaumbua
Sawa mkuu lakini vipi akisikia kuna wapo wanyama anaweza kuwaona bila VAT bado atakuja kwako kwa vile tu yeye hana tatizo la ulipaji wa VAT??SIO KWELI.
 
Unapotosha.

Rais hakuongelea "ada ndogo" na "ada kubwa". Rais Magufuli ameongelea kodi.

Mkisoma hamuelewi basi hata kusikia hamsikii?
Faidha ni wewe hukumuelewa nini?alichochambua ni maelezo ya ziada ya kiuchumi kuhusu hiyo VAT ambayo ndo inapelekea kupanda kwa malipo jamani of which ni kweli.
 
Kwa kweli Rais amekosea kusema hivyo .... Watalii wakija hapa faida zake siyo tu kulipa kodi bali wanaleta pesa za kigeni wanazibadilisha na kuzitumia. Kwenye kuzitumia watakula, watakunywa na watanunua vizawadi!!

On the other hand, kinacholalamikiwa siyo watalikulipa au kutokulipa kodi bali ni gharama kubwa za kuja kama Mtalii Tanzania. After all hiyo VAT wanalipa indirect kama Watanzania wengine!!

Tanzania inabidi tujue kuwa pamoja na kuwa na Mbuga nyingi na kubwa lakini bado tujue kuwa siyo peke yetu Africa tulio na hizo mbuga. Sidhani kama kuna wanyama ambo wako Tanzania hawako kwenye nchi nyingine za wenzetu Africa. Wakati sisi tunawasimanga wenzetu wanawaita.

Halafu kitu kingine cha kujua siyo kwamba watalii wote ni matajiri. Wengi wao ni maskini tu kama sisi ila wana hiyo bobby ya kutembea na kuona dunia. Wanakwenda kwenye nchi za wenzetu zaidi kwa vile wameimalisha infrastracture zao mpaka kuna Camping sites ambazo ni malazi ya gharama nafuu kwa watalii.

Nchi kama Botswana au namibia ambazo zina Mbuga moja moja tu zinavuta watalii wengi kuliko sisi.

Kwa kulalizia nakubaliana kabisa na mleta mada ... gharama kubwa kwa watalii zingeelekezwa kwa wale wanaofanya Trophy hunting siyo hawa wa kutembelea mbuga na kukaa pwani!!
Wapewape ee vidonge vyao wakimeza wakitema .....................
 
Tatizo kubwa la Serikali yetu, " Wanajua sana namba, lakini hawajui hesabu" Serikali yetu ingekuwa inajua Hesabu, Tanzania tungekuwa mbali sana kiuchumi.
 
Back
Top Bottom