Kumuenzi Baba wa Taifa: CCM, Serikali, Viongozi na Watanzania kwa Ujumla. Je, tunamuenzi kwa Mawazo, Maneno na kwa Vitendo? Tunamuishi?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,498
113,601
Screen Shot 2022-10-09 at 3.39.06 PM.png
Screen Shot 2022-10-09 at 3.39.35 PM.png

Karibuni tena kwenye makala zangu za “Kwa Maslahi kwa Taifa”, zinazozungumzia mada mbalimbali kuhusu taifa letu ziwe ni za kisiasa, za kiuchumi au za Kijamii, baada ya leo ni kuhusu kumuenzi Mwalimu Nyerere, kwa vile Tarehe 14 October ni Nyerere Day, leo naomba tutafakari jinsi sisi Watanzania, tunavyo muenzi Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, jee tunamuenzi kweli, kwa mawazo maneno na matendo?,

Mwalimu Nyerere sio tuu alikuwa ni muasisi wa CCM, mpaka kifo chake aliiamini CCM, hivyo hata baada ya nchi Tanzania, kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi vya siasa ile 1992, bado Mwalimu aliamini kuwa Wapinzani wanaweza kuleta wabunge bora, na hili tumelishuhudia kwa baadhi ya wabunge wa upinzani,walikuwa ni wabunge bora kabisa, lakini kwenye uraisi wa JMT, Mwalimu Nyerere aliamini “Rais bora atatoka CCM pekee”. Jee kuna Wana CCM wanao maishi Baba wa Taifa kwa mawazo, maneno na matendo?, ama watu tunamuenzi Mwalimu kwa mawazo na maneno tuu, lakini matendo na kumuishi....!.

Mimi ni mtu wa mastory mastory, yaani ni story teller, hivyo kama wewe sio mtu wa mastory story, katishia hapa, nenda mwisho, wale wa mastory mastory, tuendelee...

Jinsi Nilivyo Mfahamu Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.
Mimi nimezaliwa miaka ya mwishoni kwa 60s, hivyo nimepata akili za kujitambua nilipoanza Darasa la kwanza, mwaka 1975 Shule ya Msingi ya Nyakahoja jijini Mwanza, kwa kumsikia tuu Rais Nyerere, na kumuona kwenye magazeti baba Mzee Mayalla (RIP) akisoma. Mwaka 1976, baba alipatwa na matatizo kazini, tukahamishwa usiku usiku na landrover 109 za polisi na kupelekwa kijijini Itonjanda huko Tabora, huku ni kwa bibi mzaa baba, babu mzee wa Kusukuma baada ya kuoa mwanamke wa Kinyamwezi, Mwanza tuliishia kuisikia tuu!, akahamia jumla Tabora.

Nimeishuhudia kwa Macho, CCM Ikizaliwa!, Ile Kauli ya Kila Lenye Mwanzo...
Ile mwaka 1977 wakati CCM inazaliwa nilikuwa darasa la 3 Shule ya Msingi ya Itonjanda, siku hiyo shule tulichinja ng’ombe na ndio mara yangu ya kwanza kushuhudia jinsi wanafunzi wanavyogombea nyama!, nikawa nawashangaa maana mimi nilikuwa sipendi nyama ya ng’ombe nilipenda kuku, lakini baada ya kufika kijijini, zile kuku ziliishia Mwanza!, ila niliishuhudia CCM ikizaliwa!. Ule msemo wa kila lenye mwanzo lina mwisho, ni uongo, sio kila lenye mwanzo lina mwisho!, CCM ina mwanzo tuu lakini ....

Kumuona Nyerere kwa Macho kwa Mara ya Kwanza,
Mwaka 1978, nikafuatwa kijijini na baba yangu mdogo, Mzee Mathew Kasanga, na kuja kuishi na familia yake jijini Dar es Salaam, eneo la Drive In, kanisa letu ni St. Peter, hivyo siku ya kwanza napelekwa kanisani, mimi si mgeni kanisa hilo, hivyo tulipoingia, nikashangaa wenzangu wanajazana viti vya nyuma, wakati pale mbele kuna rows za viti vitatu ziko tupu, hivyo mimi na ushamba wangu, nikajiona mjanja ngoja niwahi kukaa siti za mbele, hivyo nikaenda kukaa siti ya kwanza kabisa niko peke yangu!.

Nikaona kama watu wananishangaa shangaa, mara nikafuatwa na mzee mmoja amevaa Kaunda suti nyeusi na kuniuliza, wewe ni nani?, nikamtajia jina, akaniuliza unakaa wapi, nikamjibu, akaniuliza, wewe ni mgeni kanisa hili, hujui hizi siti za nani?, nikajibu mimi ni mgeni na leo ndio mara yangu ya kwanza kuja kanisani!, nikaambiwa nifuate, nikatolewa nje huku kanisa zima wanashangaa!. Kule nje nikaitiwa polisi nikabidhiwe nikahojiwe!, ndipo ndugu zangu wakawafuate wale wazee na kuwasihi nisamehewe, nikasamehewa na kurudi ndani.

Baada ya kurudi kanisani ndipo nikamuona babu mmoja ana nywele nyeusi na nyeupe, ndipo nikamkumbuka ni Nyerere, akaenda kukaa kwenye benchi zima la pili peke yake!. Benchi la kwanza liko tupu, na benchi la mwisho wamekaa watu wawili mwanzo wa benchi na mwisho wa benchi!. Sasa ndio nikaelewa kwanini watu walinishangaa!. Hivyo mimi mwenzenu Nyerere nimemuona live toka mwaka 1978!.

Wakati wa kutoka nikaona watu wanatoka kanisani haraka na kupanga foleni pale nje kwenye ngazi kumsubiri Nyerere atoke, alipotoka akawa anawasalimia watu kwa kuwashika mkono. Jumapili iliofuata na mimi nikafoleni ila mkono sikushikwa, na iliofuta, na iliyofuata, hatimaye nikaacha kufoleni kwa kujua Nyerere hashiki mikono ya watoto.

Baadaye, nikawa mtumishi wa kanisa, nikawa naomba kupangiwa misa ya kwanza, hivyo nikawa namhudumia Mwalimu Nyerere kwa kumshikia kisahani cha hostia, na ndipo pia nikayaona meno yake kwa karibu na kuijua maana ya jina la Mchonga!.

Tangu hapo nikawa namfuatilia sana, ile hotuba yake ya kutangaza vita, nikaikariri baadhi ya vifungu na kumuiga, “Uwezo wa kumpiga tunao, Sababu ya kumpiga tunayo, Nia ya kumpiga tunayo, Tutampiga Amini!.”

Mwaka 1979 kwenye mapokezi ya mashujaa wetu pale uwanja wa Taifa nilikuwepo na kumshuhudia Mwalimu machozi yakimtoka kutokana na lile tukio! .

Baada ya kumaliza shule ya Msingi, familia ya Mzee Kasanga ikahamia Mikocheni opposite na Msasani kwa Nyerere, mimi nikajiunga sekondari ya Tambaza, tulikuwa darasa moja na mmoja wa watoto wa Nyerere akiishi hapo Msasani sasa kwa Nyerere tukawa tunakwenda kucheza!.

Baada ya Tambaza nikaenda Ilboru, nikapelekwa nyumbani kwa Makongoro Nyerere, enzi hizi Mako ni mjeshi. Nilipelekwa pale na Rastafarian mmoja, mdada wa Kijamaica aliyelowea Tanzania akiitwa Gipsy, tukatokee kupatana sana na Mako, maana ndege wafafanao huruka pamoja!, siku za weekend ni usawa wa Cave, kiukweli sijui alikuwa anarudi home saa ngapi!.
Baada ya sekondari nikajiunga na chuo cha Uandishi habari TSJ, ndipo Jumapili moja asubuhi, nikaja kuamshwa na mlinzi wa hostel, kuna nina mgeni!, si unajua tena mambo ya ujana, na hostel, ukisikia tuu una ugeni basi unajua ni ugeni wa type gani, ila asubuhi, tena Jumapili, asubuhi ni hatari!, kunaweza kutokea ajali!.

Kufika nikakuta jamaa fulani mweupe ana bonge la afro na gari sports car nyekundu na kujitambulisha Mimi ni Madaraka Nyerere, mtoto wa Nyerere, anahitajika Msasani kwa Nyerere!.

Naomba niishie hapa, tukutane wiki ijayo mjue niliitiwa nini Msasani kwa Nyerere?, Jee nilikwenda?, Nilimuona Mwalimu Nyerere?.

Nawatakia Nyerere Day Njema.

Paskali.
 
Paskali, nimependa uandishi wako, kweli wewe ulisoma Vipaji, Jamaa wa kijani nimegundua leo ndy saababu hawatakupa uteuzi asilani, sababu ziko mbili ila sitaztaja hapa, moja umeitaja hapa nyingine ni kwa utashi wangu ila Ni ya ukweli. MAYALA KULE KWETU NI NJAA? mimi sikubaliani na usemi ule!!
 
View attachment 2386662View attachment 2386672
Karibuni tena kwenye makala zangu za “Kwa Maslahi kwa Taifa”, zinazozungumzia mada mbalimbali kuhusu taifa letu ziwe ni za kisiasa, za kiuchumi au za Kijamii, baada ya leo ni kuhusu kumuenzi Mwalimu Nyerere, kwa vile Tarehe 14 October ni Nyerere Day, leo naomba tutafakari jinsi sisi Watanzania, tunavyo muenzi Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, jee tunamuenzi kweli, kwa mawazo maneno na matendo?,

Mwalimu Nyerere sio tuu alikuwa ni muasisi wa CCM, mpaka kifo chake aliiamini CCM, hivyo hata baada ya nchi Tanzania, kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi vya siasa ile 1992, bado Mwalimu aliamini kuwa Wapinzani wanaweza kuleta wabunge bora, na hili tumelishuhudia kwa baadhi ya wabunge wa upinzani,walikuwa ni wabunge bora kabisa, lakini kwenye uraisi wa JMT, Mwalimu Nyerere aliamini “Rais bora atatoka CCM pekee”. Jee kuna Wana CCM wanao maishi Baba wa Taifa kwa mawazo, maneno na matendo?, ama watu tunamuenzi Mwalimu kwa mawazo na maneno tuu, lakini matendo na kumuishi....!.

Mimi ni mtu wa mastory mastory, yaani ni story teller, hivyo kama wewe sio mtu wa mastory story, katishia hapa, nenda mwisho, wale wa mastory mastory, tuendelee...

Jinsi Nilivyo Mfahamu Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.

Baada ya sekondari nikajiunga na chuo cha Uandishi habari TSJ, ndipo Jumapili moja asubuhi, nikaja kuamshwa na mlinzi wa hostel, kuna nina mgeni!, si unajua tena mambo ya ujana, na hostel, ukisikia tuu una ugeni basi unajua ni ugeni wa type gani, ila asubuhi, tena Jumapili, asubuhi ni hatari!, kunaweza kutokea ajali!.

Kufika nikakuta jamaa fulani mweupe ana bonge la afro na gari sports car nyekundu na kujitambulisha Mimi ni Madaraka Nyerere, mtoto wa Nyerere, anahitajika Msasani kwa Nyerere!.

Naomba niishie hapa, tukutane wiki ijayo mjue niliitiwa nini Msasani kwa Nyerere?, Jee nilikwenda?, Nilimuona Mwalimu Nyerere?.

Nawatakia Nyerere Day Njema.

Paskali.
Tunamuenzi kwa maneno lakini kumuishi hiyo ni sifuri bin sifur !!
 
tumuenzi na kula ugali wa yanga tumuenzi kwa kugawiwa dawa ya mswaki 1 kila kaya tumuenzi kwa kupewa sabuni ya kuogea 1 na sukari kilo1 kila kaya tumuenzi kwa uhujumu uchumi tumuenzi kwa kutaifisha majumba ya watu
 
Paskali, nimependa uandishi wako, kweli wewe ulisoma Vipaji, Jamaa wa kijani nimegundua leo ndy saababu hawatakupa uteuzi asilani, sababu ziko mbili ila sitaztaja hapa, moja umeitaja hapa nyingine ni kwa utashi wangu ila Ni ya ukweli. MAYALA KULE KWETU NI NJAA? mimi sikubaliani na usemi ule!!
Mtu mkweli huwa hapendwi !!
 
tumuenzi na kula ugali wa yanga tumuenzi kwa kugawiwa dawa ya mswaki 1 kila kaya tumuenzi kwa kupewa sabuni ya kuogea 1 na sukari kilo1 kila kaya tumuenzi kwa uhujumu uchumi tumuenzi kwa kutaifisha majumba ya watu
Tumuenzi pia kwa kutufanya wamoja na tumuenzi kwa kusoma bure na kupewa kila kitu bure huko mashuleni mpaka na warrants za kusafiria za return !! Na pia pamoja na yote watu walikuwa wakiishi kwa furaha bila stress yeyote ile !! Peace of mind ilikuwa imetamalaki !! Kulikuwa hakuna panya rodi wala panya buku. !!
 
View attachment 2386662View attachment 2386672
Karibuni tena kwenye makala zangu za “Kwa Maslahi kwa Taifa”, zinazozungumzia mada mbalimbali kuhusu taifa letu ziwe ni za kisiasa, za kiuchumi au za Kijamii, baada ya leo ni kuhusu kumuenzi Mwalimu Nyerere, kwa vile Tarehe 14 October ni Nyerere Day, leo naomba tutafakari jinsi sisi Watanzania, tunavyo muenzi Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, jee tunamuenzi kweli, kwa mawazo maneno na matendo?,

Mwalimu Nyerere sio tuu alikuwa ni muasisi wa CCM, mpaka kifo chake aliiamini CCM, hivyo hata baada ya nchi Tanzania, kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi vya siasa ile 1992, bado Mwalimu aliamini kuwa Wapinzani wanaweza kuleta wabunge bora, na hili tumelishuhudia kwa baadhi ya wabunge wa upinzani,walikuwa ni wabunge bora kabisa, lakini kwenye uraisi wa JMT, Mwalimu Nyerere aliamini “Rais bora atatoka CCM pekee”. Jee kuna Wana CCM wanao maishi Baba wa Taifa kwa mawazo, maneno na matendo?, ama watu tunamuenzi Mwalimu kwa mawazo na maneno tuu, lakini matendo na kumuishi....!.

Mimi ni mtu wa mastory mastory, yaani ni story teller, hivyo kama wewe sio mtu wa mastory story, katishia hapa, nenda mwisho, wale wa mastory mastory, tuendelee...

Jinsi Nilivyo Mfahamu Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.

Baada ya sekondari nikajiunga na chuo cha Uandishi habari TSJ, ndipo Jumapili moja asubuhi, nikaja kuamshwa na mlinzi wa hostel, kuna nina mgeni!, si unajua tena mambo ya ujana, na hostel, ukisikia tuu una ugeni basi unajua ni ugeni wa type gani, ila asubuhi, tena Jumapili, asubuhi ni hatari!, kunaweza kutokea ajali!.

Kufika nikakuta jamaa fulani mweupe ana bonge la afro na gari sports car nyekundu na kujitambulisha Mimi ni Madaraka Nyerere, mtoto wa Nyerere, anahitajika Msasani kwa Nyerere!.

Naomba niishie hapa, tukutane wiki ijayo mjue niliitiwa nini Msasani kwa Nyerere?, Jee nilikwenda?, Nilimuona Mwalimu Nyerere?.

Nawatakia Nyerere Day Njema.

Paskali.
Mwalimu alikuwa Binadamu sio Malaika,ataenziwa kwa Yale mema na sio kila mawazo yake basi yanafaa zama hizi..

Mfano falsafa yake ya Uchumi ilishindwa kipindi kile na Sasa haiwezekani..

Ila Kwa neno la umoja tutamuenzi daima.
 
Wanabodi,
Kwa maslahi ya Taifa Jumapili hii
Screen Shot 2022-10-17 at 12.12.12 AM.png

Screen Shot 2022-10-17 at 12.12.27 AM.png

Karibu tena, kwenye makala nyingine ya “Kwa Maslahi kwa Taifa”, leo hii ni makala mwendelezo iliyoanzia wiki iliyopita, Kumuenzi Baba wa Taifa:CCM, Serikali, Viongozi na Watanzania kwa Ujumla, Je Tunamuenzi Baba wa Taifa kwa Mawazo, Maneno na kwa Vitendo?, Tunamuishi?. ikizungumzia kumuenzi muasisi wa taifa hili, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Kufuatia kumbukizi ya Baba wa Taifa kila Tarehe 14 October ni Nyerere Day, nikitafakari jinsi sisi Watanzania, Viongozi wetu na Chama chake CCM, tunavyo muenzi Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, na kuuliza tumuenzi vipi Baba wa Taifa?. Jee tuendelee lumuenzi kwa mawazo mazuri tuu na kwa maneno tuu, kwa kupiga blah blah, "Mwalimu alikuwa hivi, Mwalimu alikuwa vile", au sasa tumuenzi kwa matendo kwa kuendelea kutenda kama Mwalimu, na ikiwezekana viongozi wetu wamuenzi Mwalimu kwa kumuishi!, na sio kwa hizi blah blah zinazoendelea sasa?.

Ukiondoa baadhi ya wazee wetu kama kina Ibrahim Kaduma na David Wakati waliotangulia mbele ya haki ambao walimuishi Mwalimu, na wachache waliobakia kama Mzee Joseph Warioba na Mzee Butiku, ni kiongozi gani mwingine yeyote aliye madarakani sasa ana muishi Mwalimu Nyerere?. John Pombe Magufuli angalau angalau Magufuli kama Nyerere: Ni mtu wa watu, hapapasi, hamung'unyi, ni kazi tuu, ila pia sio kama Nyerere!

Mimi ni mtu wa mastori story, hii simulizi ya Mwalimu, niliianza wiki iliyopita na niliishia nikiwa hostel za Chuo cha Uandishi wa Habari, TSJ enzi hizo kiko Ilala Shariff Shamba, nikapata ugeni wa kutembelewa na mtoto wa Mwalimu, Madaraka Nyerere, kunijulisha ninahitajika Msasani nyumbani kwa Mwalimu Nyerere!, wale wa mastori mastori tuendelee, wale wa short and clear, unaweza ku jump into conclusion.

Kwanza nilishtuka!, iweje mtu nobody kama mimi nihitajike nyumbani kwa Mwalimu?!, kuna nini?!. Ndipo Madaraka akanieleza mdogo wake wa kike, amepata mchumba, hivyo familia ya bibi harusi (Familia ya Mwalimu Nyerere na famia ya Bwana harusi, wamenipendekeza mimi kuwa mshereheshaji MC kwenye sherehe ya harusi ya binti Nyerere!.

Nilipokea wito huo kwa furaha, sikukumbuka hata kumuuliza Madaraka nani aliwaelekeza kwangu!, nikakubali moja moja wito huo na nilipo uulizwa gharama zangu, kiukweli siku hizo wala sikujua MC huwa analipwa!, hivyo nikasema nitafanya bure!.

Nikarudi hostel chap kujimwagia maji shaa shaa, kuvaa suruali, maana mwanzo nilitoka na bukta tuu, maana nilidhani ni wale wageni wetu wa ujana ujana kutembeleana hostel, mara nyingi kazi huwa ni moja tuu!. Nikapanda sports car, hadi nyumbani kwa Madaraka, enzi hizo akikaa yale maghorofa ya Sido. Mkewe akanipokea vizuri, kwa staftahi nzito!, Ilikuwa ni siku ya kikao cha mwisho, harusi ni Jumamosi inayofuata. Ile safari ya kwenda Msasani kwa Nyerere, ikaishia hapo Upanga kwa Madaraka. Nikaelezwa kila kitu kimekamilika hakuna haja ya vikao!. Tena sikumbuki kama huyo binti alifanyiwa hata send off, ila mimi ni MC wa harusi, kama alifanyiwa siwezi kujua, maana sikualikwa na siku uliza!.

Siku ya siku ikafika, harusi ikafungwa kanisa la KKKT, Azania front, reception ni ukumbi wa Luther House, sikumbuki hata kama kulikuwa na msafara!.

Tumetoka kanisani ukumbi ni hapo hapo, tukaingia ukumbini, baada ya kutamani sana kumsalimia kwa kumshika mkono Mwalimu, siku hiyo ndio nikamshika mkono!, Mwalimu alikuwa ni mtu mcheshi sana na ana vichekesho sana!, akaniambia MC, usiwe wa blah blah na kuleta habari za uongo uongo ili kuwafurahisha wageni, sipendi utani utani, wewe endesha shughuli vizuri iishe mapema!.

Mwanzo nilikuwa very tense, kuendesha shughuli ya mtoto wa rais!. Baada ya kumsalimia Mwalumu, I was at easy!. Kwa jinsi sherehe hiyo ilivyokuwa simple, binti wa rais ameolewa na mtu wa kawaida tuu, Baba wa bwana harusi ni Baba Mchungaji wa KKKT, hivyo sherehe ilikuwa very simple na down to earth, haina makuu yoyote!.

Funzo hapa ni Mwalimu hakuwalea watoto wake kwa u- spesho wowote kama watoto wa rais, hivyo kijana wa kawaida tuu akampenda mtoto wa rais, harusi ya kawaida sana!, kuonyesha Mwalimu was humble, simple and down to earth!. (Nilipata bahati pia ya kuwa MC harusi ya Binti Lowassa, wakati huo Lowassa ni Waziri Mkuu, nikilinganisha harusi ya binti Nyerere akiwa ni binti wa rais na harusi ya binti Lowassa akiwa ni binti wa Waziri Mkuu!, kiukweli kabisa ni kama mbingu na nchi!).

Nikiwa bado TSJ nilihudhuria kila mkutano wa Mwalimu na waandishi wa habari, hivyo ile mikutano ya Kilimanjaro Hotel na ule ya uzinduzi wa kitabu cha “Nyufa” nilikuwepo.

Nilipomaliza TSJ nikaajiriwa RTD na nikam cover sana Mwalimu kwenye events zake, moja ya event ninayoikumbuka sana ni siku moja alialikwa dinner na Lions Club pale Sheraton, baada ya dinner, the host wakamtaka mwalimu hawezi kuondoka nila kusema neno lolote, hivyo wakamsimamisha Mwalimu auhutubie. Mwalimu aliposimama, akasema, leo niliwaambia kabisa sitaki kuongea!, maadam imeniomba niseme neno lolote, basi nimekubali kusema neno... "asanteni sana kunikaribisha dinner" ... akakaa!, watu hawakuamini!, ila kitu cha cha ajabu ni ukumbi wote ukasimama kumpigia makofi kwa standing ovation!. Sikumbuki lini viongozi we wa sasa wanapata a standing ovation!.
Kazi za Uandishi Kumcover Mwalimu
Mimi ndie mwandishi wa mwisho wa habari kusafiri na Mwalimu safari ya Uswisi kwenye mkutano wa South South Commission uliofanyika jiji la Bern nchini Uswisi. Hivyo mimi ndie mwandishi wa mwisho wa habari kufanya mahojiano na Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere niliyoyafanyia jengo la The Bundes House, mjini Bern

Baada ya kurejea kutoka Uswisi, ndipo akaanza kuugua.

Mwalimu alipozidiwa na kupelekwa kutibiwa hospital ya St. Thomas, jijini London nchini Uingereza, ni mimi tena ndie mwandishi pekee wa Tanzania, aliyemtembelea St Thomas Hospital, nikiwa ndie mwandishi pekee wa Tanzania kutoka private media, aliyeandamana na Rais Mkapa ziarani Marekani kwenye Unga, wakati wa kurejea nchini tukapitia London kumuona Mwalimu na kurejea nyumbani ambapo mwanzoni mwa Octoba na haikupita wiki, Mwalimu akafariki.

Niliandaa a video documentary ya msiba wa Baba wa Taifa, tangu kuwasili kwa mwili, kuagwa uwanja wa taifa, nikamsindikiza mpaka Butiama kwenye makao yake ya milele.

Swali la kumhusu Mwalimu, je viongozi wetu wanamuenzi kwa kumuishi, au wana muenzi kwa mawazo tuu na maneno lakini sio kwa vitendo? Naombeni mnitajie hata kiongozi wetu mmoja tuu anayemuishi Nyerere kwa mawazo, maneno na matendo?

Jee chama alichokiasisi na kukiacha Mwalimu Nyerere, Chama cha Mapinduzi, CCM, kinamuenzi Mwalimu kwa vitendo?, kinamuishi kwa kufuata falsafa yake?, Jee hii CCM ya sasa ndie ile CCM aliyoiacha Mwalimu?.

CCM ya Mwalimu ilikuwa ni chama cha wakulima na wafanyakazi, sifa ya kugombea uongozi ilikuwa ni uwezo wa uongozi na uzalendo wako kwanza kwa nchi yako, kisha kwa chama chako, Jee sasa sifa ya kuchaguliwa kuwa kiongozi CCM bado ni zile zile au sasa ili kuchaguliwa kiongozi sifa kuu ni una mkono mrefu kiasi gani kuwapatia takrima wajumbe?.

Mwalimu aliichukia rushwa kwa dhati, baada ya kufariki, tukaibariki rushwa kwa kuipa jina zuri la “takrima” tukapitisha na sheria kuiruhusu!. Kelele zikapigwa, sheria ile ikafutwa, lakini sasa chama alichokiasisi Mwalimu zile takrima zimegeuzwa ni michango ya lazima ya kuombea fomu ya uongozi, sasa fomu ya kugombea ubunge CCM inauzwa kwa Shilingi milioni 1!, kuna wakulima wangapi na wafanyakazi wanayo hiyo milioni moja ya kujaza fomu ya Ubunge?. Mwalimu Angekuwepo haya yangefanyika?.

Hitimisho

CCM, serikali yetu, viongozi wetu na Watanzania kwa ujumla, tumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, sio tuu kwa mawazo, na maneno, bali kwa matendo na ikibidi kumuishi, tutabarikiwa, na Taifa litabarikiwa!, tukiendelea kumuenzi hivi kwa mawazo tuu na maneno, lakini matendo ni tofauti, taifa letu na chama chetu na viongozi wetu, tutaendelea kupata kichapo cha bakora za kitu kinachoitwa karma.

Wasalaam.

Paskali
 
Naunga mkono hoja

Mkapa aliona hilo akamwambia hayati jpm Kwamba

Tunataka kusikia Serikali ya CCM imefanya HIVI na vile sio mtu kafanya hivi na vile!

Tunajenga majina ya WATU KULIKO Taasisi matokeo yake wanaojengwa hujiona WAKUBWA KULIKO chama na kutengeneza mazingira ya kuimbwa na WATU KWA kutoa Takrima za uteuzi na fedha Ili wasifiwe WAO KULIKO chama na taasisi KWA UJUMLA!

Hata sasa linaimbwa jina KULIKO chama anachotoka mtu!katibu wa chama mwenezi anaimba jina KULIKO CHAMA na kukweza jina KULIKO CHAMA!!

RUSHWA au Takrima tumeitengeza KWA kukuza WATU KULIKO Taasisi! tutarajie sarakasi nyingi ZAIDI KULIKO!!!

Pole pia hata juzi wewe kukosa kale kaubunge ni matokeo yale yale!

Nakuambia live kabisa KWA wewe ulivyo na mchango wako wa uandishi wako Katika jamii sio wa kuwa hivi hivi tu ulipaswa upewe Ili uonyeshe KWA vitendo KWENYE field ya maendeleo na siasa KWA ujumla na sio KWA hukumu ya Moja KWA Moja eti wewe ni timu mamvi kama fimbo ya kukupigia kukosa nafasi!!

Mawazo huru!
 
Mayalla unaonekana kuwa na "connection" huko CCM lakini nashangaa kwanini bado hawakutambui, au ni lile swali lako kwa yule jamaa ndio lilitia doa lisilofutika? don't know!.

Anyway, suala la viongozi wetu wa sasa kushindwa kumuenzi Nyerere linachangiwa na mambo kadhaa, na sidhani kama itakuwa rahisi kuibadilisha hiyo hali, zaidi wataendelea tu kumuimba midomoni.

- Kupenda kwao anasa; kama matumizi yao ya misafara ya magari ya bei mbaya, huku wakiwa wamezungukwa na wananchi masikini, bila kuona aibu yoyote, hawa viongozi wetu wa sasa ni kama vile wanashindana kwa utajiri, na hawawezi kuichukia rushwa, au ufisadi, kwa sababu hivyo ndivyo huwafanya waendelee kuwa matajiri, mfano wa hili ni harusi ya Lowassa ulioutoa.

- Kukosekana sheria madhubuti za kuwabana, na viongozi jasiri wa kuzisimamia; ajabu siku hizi hata sheria zenyewe hazifuatwi, tena viongozi ndio wanaongoza kuvunja sheria, sasa kwenye mazingira haya, ukichanganya na kulindana, ni vigumu sana viongozi wetu kumuenzi Nyerere kwa vitendo.

Kwa mtazamo wangu, hawa viongozi wetu wanatakiwa kulazimishwa kumuenzi Nyerere kwa vitendo, na hilo litafanikiwa endapo tu itapatikana Katiba Mpya, hasa ile Rasimu ya Warioba. Naamini ile ndio itakuja kuwakumbusha kwamba, kuwa kiongozi wa serikali ni kuwatumikia wananchi, na wala sio kujilimbikizia mali wao binafsi.
 
Mwalimu alikuwa muumini wa serikali mbili kuelekea moja. Rasimu ya Warioba inataka serikali tatu. Tunamuenzije kwa kupitia rasimu ya Warioba?
 
Mayalla unaonekana kuwa na "connection" huko CCM lakini nashangaa kwanini bado hawakutambui, au ni lile swali lako kwa yule jamaa ndio lilitia doa lisilofutika? don't know!.

Anyway, suala la viongozi wetu wa sasa kushindwa kumuenzi Nyerere linachangiwa na mambo kadhaa, na sidhani kama itakuwa rahisi kuibadilisha hiyo hali, zaidi wataendelea tu kumuimba midomoni.

- Kupenda kwao anasa; kama matumizi yao ya misafara ya magari ya bei mbaya, huku wakiwa wamezungukwa na wananchi masikini, bila kuona aibu yoyote, hawa viongozi wetu wa sasa ni kama vile wanashindana kwa utajiri, na hawawezi kuichukia rushwa, au ufisadi, kwa sababu hivyo ndivyo huwafanya waendelee kuwa matajiri, mfano wa hili na harusi ya Lowassa ulioutoa.

- Kukosekana sheria madhubuti za kuwabana, na viongozi jasiri wa kuzisimamia; ajabu siku hizi hata sheria zenyewe hazifuatwi, tena viongozi ndio wanaongoza kuvunja sheria, sasa kwenye mazingira haya, ukichanganya na kulindana, ni vigumu sana viongozi wetu kumuenzi Nyerere kwa vitendo.

Kwa mtazamo wangu, hawa viongozi wetu wanatakiwa kulazimishwa kumuenzi Nyerere kwa vitendo, na hilo litafanikiwa endapo tu itapatikana Katiba Mpya, hasa ile Rasimu ya Warioba. Naamini ile ndio itakuja kuwakumbusha kwamba, kuwa kiongozi wa serikali ni kuwatumikia wananchi, na wala sio kujilimbikizia mali wao binafsi.
Kuna doa FULANI wakati akiwa pale TBC,ndilo linalomtafuna!,aliwahi kuandika humu! Mamvi ameponza wengi Sana!!
 
Back
Top Bottom