Kitaani wakijua una MGUU WA KUKU vibaka hawakatizi kabisa mtaani kwako.
ni hatari sana kujulikana mtaani una miliki hicho kifaaa
yani hata uki kimiliki kesho sikushauri uruhusu mtu ajue
Nina rafiki yangu hata mwezi haujaisha ninavyoandika hapa nimetoka kwake
bado anaumwa kwa majeraha na kujeruhiwa na majambazi waliokua wakimfatilia
STORY IKO HIVI
unajua sisi vijana kuna wengine tunapenda sifa za kijinga sana,sasa huyu ndugu yangu kila siku kuu
lazima apige juu tena anapiga kwa fujo sana mtaani kwake wote wanajua jamaaa ana kifaaa
sasa siku moja sijui alijichanganya vipi akawa katoka bila kifaaa kumbe hajui "Anawindwa" akaenda na ki baby walker chake
prrrrrrr kafika sehemu tunayo tuliiaga kauchuna kapaki gari katoa Embassy yake kaanza kupuliza zake mdogo mdogo
ghafla bin vuu majamaaa wakatokea pasipojulikana Kamata roba mbao wakamuingiza ndani ya gari yake
Hawakua na maneno mengi walimwambia sentensi moja Clean and short
Tunahitaji ile bastola unayoitumiaga,tuna kazi nayo hatuhitaji kuku umiza wala kukujeruhi tupe tuondoke zetu
Jamaa akawa anajifanya hana na hajawahi kumiliki, bwana bwana bwana bwana
Alipigwa aliteswa aliumizwa kiasi kwamba ukimuona unaweza anza kulia wewe kabla hajakusimulia ilikuaje
Baada ya kuumizwa hivyo aliachwa akiwa hajitambui ndani ya gari yake na aliletwa hadi kwake na gari lake wakalipaki nnje
wakamuacha hapo wakasepa zao.