Kumiliki bastola ni mzigo na hasara

Kumiliki bastola ni mzigo na hasara

Raha ya Jf ndio hii....
Hapa asilimia zaidi ya 90% wanamiliki silaha, sasa ulete Uzi Wa kuulizia taratibu za kumiliki silaha unaweza kukosa details sahihi kabisaaa ndio utajua humu wote walifika university na ni matajiri wasomi wanajua kila kitu, wapanda bombadia na wasafiri nje ya nchi daily


Aaahhhhh!

Ubarikiwe Maxence na Mushi kwa maono yenu haya tunapunguza stress hapa kila sekunde.
Sijawahi kuona muuza majeneza humu nahisi niko peke yangu
 
Watu wanajiropokesha tu hapa hawajui mziki wake. Na kwa sasa kuipata ni ngumu utahonga ila itaishia Wilayani Mkoani vikao havikai.
Huyo hua anasikia story za vijiweni,hajui lolote kuhusiana na hizo mambo mkuu.
 
Hivi vitu (miguu ya kuku) sio ya kuwapa walevi au mashabiki wa arsenal wanaweza wakaleta maafa makubwa sana
 
Tatizo hizi hapa MIKHAIL KALASHNIKOV 47(AK-47) kwa Tanzania hawaruhusu kwa raia wa kawaida kisheria,I swear ningeweza kuwa nayo tu.Marekani wanaruhusu, tatizo kule watu wanaozimiliki kiholela huwa wanajizuka na kuanza kumiminia risasi watu.Matatizo ya msongo wa mawazo na matumizi ya dawa za kulevya vinachangia kwa kiasi kikubwa watu kumalizana...View attachment 1260892
Marekani hawaruhusu hizi machine mkuu ama nyingine za aina ya kivita (assault rifle) ambazo ni full automatic. Hizo ni kwa matumizi ya jeshi n.k.

Zile unaziziona zinaua sana ni semi auto riffle na ambayo ni common sana ni AR 15 ambayo inapigiwa kelele sana ifungiwe.
 
Marekani hawaruhusu hizi machine mkuu ama nyingine za aina ya kivita (assault rifle) ambazo ni full automatic. Hizo ni kwa matumizi ya jeshi n.k.

Zile unaziziona zinaua sana ni semi auto riffle na ambayo ni common sana ni AR 15 ambayo inapigiwa kelele sana ifungiwe.
Sawa sawa mzee...Nimekupa vizuri...
 
Sijaona uongo wa jamaa. Yes zipo hotel zinapokea na kuhifadhi silaha za wateja kama utapenda. Pia nakubali zipo ambazo hazipokei.

Sema kwa Tanzania sio inshu sana sababu wamiliki ni wachache. Ila kwa wenzetu wapo clear sehemu za mijumuiko kama kanisani, shule unakabidhi chuma yako.
Watu waongo unawakamata kirahisi. Unaiacha mapokezi ikienda tumika kufanya uharifu?
 
Kupata kibali cha bunduki imekua mbinde sana sikuhizi.watu kibao wamewacha bunduki tanganyika arms wanasubiri vibali
 
sina ujuzi juu ya haya mambo. lakini kwa vile wachangiaji wengi wamejitanabahisha kuwa wamiliki na wajuzi kimatumizi (kama walivyo na magari kila mwana jf) subiri hapa hapa watumwagie nondo sisi wenye kutembelea nyota za wengine.

hakika ukitafakari sana maisha ya wana jf unaweza kujidharau kwa kuiona unasindikiza maisha ya wengine.

cc: @kidukulilo
Hahaha.. Ni kweli mkuu
 
Wanabodi.

Wengi ambao wana mguu wa kuku wanapata shida nazo sana. Kuzitunza , kuzibeba na kuzimudu. Wengi wanagongwa wao na hizo machine zao. Hawana mafunzo, hawastahimili na wana misongo mingi ya mawazo.

Sijawahi kusikia kusikia mwenye bastola ameua mharibu kiufasaha. Never. Zinawaponza
Hujawah kusikia maana huna watu wa karibu au watu wanaoweza kukupa hizo info.

Lakini, ulivyosema wengi wao either humiliki kama fashion tu, hawajui tahadhari za matumizi yake, au hata kupiga target vizuri.

Ukijumlisha na kuwa na zero emotional intelligence basi tabu tupu
 
Comment ya kwanza hadi ya 20 wote wana bastola. Haile JF!!!
Acha ujinga bwana mdogo, Mimi ni wapi nimesema namiliki mguu wa kuku? Mie ninezungumzia jamaa yangu aliyekoswakoswa kuuawa na jambazi!
 
Naacha ujinga bro, Usinishoot.
Ha ha haaaaa,, bado unarudia? Ila JF ni kiboko, ukija kwenye pesa kila mtu ana ukwasi wa kutisha, ukija kwa madem kila mmoja anakojolea pazuri, shule kila mtu anamiliki gamba la chuo kikuu! Duuu kazi kweli kweli!
 
Bastola mhimu boss, kamauna kuwezo ka kuilipia kodi basi miliki tu maana kuinunua sio ishu
 
Back
Top Bottom