Kumiliki bastola ni mzigo na hasara

Kumiliki bastola ni mzigo na hasara

Wengi wanapewa umiliki wa silaha ila wengi wao wamezimiliki kimakosa na kwa mihemuko na ndo maana mwisho wa siku wanazitumia vibaya na nyakati nyingine kuishia kuzipoteza ama kuwadhuru wao

Silaha ni muhimu kwa mtu sahihi kwa nyakati sahihi, unakuta mtu anatembea na silaha akipandwa na hasira anaanza toa na kutishia nayo mtu huo ni uwenda wazimu maana siku anaweza ua mtu kisa kapewa tusi,

Ila kwa mtu sahihi ka kapewa mtu sahihi ni swala la msingi sana maana zinawasaidi zaidi katika biashara na mambo yao muhimu ya ulinzi wa mali zao. ila nashauri Jeshi la polisi liangalie sana namna ya utoaji wake ikiwezekana waongeze masharti ya umiliki maana naona watu wasio sahihi wanazimiliki
 
Kwa hiyo walienda muhoji mkeo?
mhh mkuu kupewa silaha sio kama simu,yaani utapelelezwa.hata ikikutwa umegombana na mtu karibuni au kitambo na bado una kinyongo naye hupewi.una mihasira ya kijinga una panick hovyo hupewi,mazingira yako ya utafutaji si salama kwa silaha hupewi(mfano uko machinjioni[emoji1][emoji1]).

ni hivyo,sema rupia inarawiti taratibu nyingi zilizowekwa kwa faida pana.
 
Miaka ya nyuma Sugu a.k.a Mr. 2 alirudi kutoka ughaibuni akiwa vema ki uchumi na kuachia goma linaloitwa Moto chini, na moja ya mistari iliyomo ni hii; 'Sugu sasa namiliki bunduki sihitaji tena amani palipo na deal fake' haikuchukua muda majambazi waliingia kwa Jongwe na kuwamudu walinzi mpaka wakamfikia jamaa na kumshurutisha haraka awape chuma wana shughuli nacho...kumbe jamaa hana kitu ilikuwa ni majigambo ya Hip Hop tu.
 
Muulize Zacharia mguu wa kuku anaushukuru hadi kesho ulimuokoa sana
Naye hajui kulenga shabaha vizuri. Mita3 unakosaje shabaha na kuishia kujeruhi?

Ningelikuwa ni mimi, wote ningeliwamwaga matumbo bila kumkosa hata mmoja kwa kuwapiga risasi mbilimbili kwa usahihi chini ya sekunde8 kwa wote watatu na mbinu za kujigaragaza chini kukwepa ghadhabu zangu zisingewasaidia kwa ukaribu ule.

Kama alivyosema mtoa mada, wamiliki wengi hawazifanyii mazoezi bunduki zao kushindwa kuzoea hata miungurumo ya silaha hizo. vinginevyo nadhani yaweza kuwa ni kwa ajili ya gharama za risasi.

Mazoezi yanatakiwa angalao mara3 kwa mwaka na si chini ya risasi 100 kupoteza kwa mazoezi.

Sasa wamiliki wengine wakishajifunza kulenga na kufyatua, wamemaliza.
 
ongelea kusafiri nje ya nchi, injinia wa ndege na ujuzi wa kitaaluma kama tiba, masuala ya vita, elimu ya anga, siasa na uchumi hapo kila mwana jf ni nguli tena wa kiwango cha phd. aghalabu huwa nakosa pa kuchangia kwa kuogopa kubezwa na wajuzi hawa.

sasa vuta subira baada ya muda kuna nyuzi zinaanzishwa kuomba misaada na mambo kama hayo. id zile 'zile za mambo safi' zikiomba msaada wamedeli ada ya chuo, sijui shemeji kawaje, au pitia jukwaa la ujasiriamali ukute aliyejinadi kaajiriwa ana take home ya 5m anauliza kwa mtaji wa 500,000 naweza kufanya biashara gani. hapo ndio utajua keys za simu /kompyuta ni vichaka tosha kuficha tupu zetu.
Dah aiseee umenichekesha Sana mkuu hi ndio jf 98% tunamiliki magari
 
ongelea kusafiri nje ya nchi, injinia wa ndege na ujuzi wa kitaaluma kama tiba, masuala ya vita, elimu ya anga, siasa na uchumi hapo kila mwana jf ni nguli tena wa kiwango cha phd. aghalabu huwa nakosa pa kuchangia kwa kuogopa kubezwa na wajuzi hawa.

sasa vuta subira baada ya muda kuna nyuzi zinaanzishwa kuomba misaada na mambo kama hayo. id zile 'zile za mambo safi' zikiomba msaada wamedeli ada ya chuo, sijui shemeji kawaje, au pitia jukwaa la ujasiriamali ukute aliyejinadi kaajiriwa ana take home ya 5m anauliza kwa mtaji wa 500,000 naweza kufanya biashara gani. hapo ndio utajua keys za simu /kompyuta ni vichaka tosha kuficha tupu zetu.

Kila mwana JF ni Dr, engineer sio kweli. Ila wapo wenye sifa hizo. Kwani kuna ajabu kuwa na sifa hizo mkuu?
 
Nichokoze nikusambaratishe kichwa, mimi mtaa mzima wanajua kama ninaumiliki moto, kuna vijambazi uchwara vilitaka kureta ujinga kwenye nyumba ya jirani yangu ambae ni mfanya biashara, aisee nilipiga moja juu vile vijambazi vilisambaratika... Nilipata ujiko sana siku hiyo hapa mtaani kwangu, ikawa kila mtu aisee yule bwana sio wa mchezo mchezo yaani huyo bwana ndiye mimi asiyetabirika
 
Nichokoze nikusambaratishe kichwa, mimi mtaa mzima wanajua kama ninaumiliki moto, kuna vijambazi uchwara vilitaka kureta ujinga kwenye nyumba ya jirani yangu ambae ni mfanya biashara, aisee nilipiga moja juu vile vijambazi vilisambaratika... Nilipata ujiko sana siku hiyo hapa mtaani kwangu, ikawa kila mtu aisee yule bwana sio wa mchezo mchezo yaani huyo bwana ndiye mimi asiyetabirika
una mzigo aina gani?
 
Sheria hairuhusu. Hata ndani mwako basically spouse hapaswi kujua ilipo kwa usalama wake na wako pia
Sheria umekariri au unazijua,Hata wiki mbili zilizopita niliacha reception kwenye lodge moja Mwanza.Eti hata spouse anatakiwa asijue ni stori za mitaani tu.
 
Back
Top Bottom