Uchaguzi wa Spika mpya, utafanyika kwenye kikao kijacho cha Bunge, ambapo vyama mbalimbali vya siasa, vitateua majina ya wagombea wake, kila chama mgombea mmoja. Hivyo Mtanzania yoyote, kutoka chama chochote cha siasa, aliyekidhi sifa na vigezo, anaweza kuwa Spika wa Bunge la JMT.
Lakini kwa siasa za Tanzania, tukubali, tukatae, ile kauli ya Mwalimu Nyerere kuhusu urais wa Tanzania, kuwa “rais bora lazima atatoka CCM”, ikingali inaishi hata kwenye Uspika, kuwa Spika bora wa Bunge la JMT, lazima atatoka CCM.
Kama nilivyouanza mwaka huu, katika salamu zangu mwaka mpya, kwa kusema huu ni mwaka wa mabadiliko, na kuwaomba Watanzania tubadilike, kujizulu kwa Spika aliyepita, ni mpango wa Mungu kuleta mabadiliko katika mhimili huu pia, baada ya Mungu kuleta mabadiliko kwenye mhimili wa Serikali, sasa ni zamu ya mabadiliko katika Mhimili wa Bunge, dini zote zinatusisitiza tushukuru kwa yoye, hivyo tushukuru hata kwa mabadiliko haya ya mkuu wa mhimili wa Bunge, baada ya kutokea fursa hii, ni jukumu la Bunge letu kutupatia Spika Bora.
Paskali.