Kujengea makaburi ya Waliotutangulia - Kuna umuhimu wowote?

Kujengea makaburi ya Waliotutangulia - Kuna umuhimu wowote?

charminglady my dia waache wafu wawazike wafu wao. Binadamu anakabiliwa na wimbi kubwa la ignorance na hata ukitaka kutazama jambo hili kwa undani utakuta ya kwamba hizi rabsha zote ni kujiridhisha nafsi zao tu wala aihusiani na marehemu. Binadamu tuna ubinafsi wa ajabu

na wewe ni nani kuhukumu?!!
 
Ni upumbavu na ujinga, Mzoga mzoga tu mnataka kuniambia paka, mbwa, chura nk hawana roho? mbona hao uchimbiwa shimo na maisha yanendele kwa wengine, acheni kukalili.

Hivi kweli ndugu yako kipenzi aliefariki unaweza mfananisha na mnyama na kumuita mzoga!!
Itakua hayajakufika ya kufiwa na mpendwa wako unasikia tu kwa jirani
 
Hakuna.

Au unataka kuwa kama wale jamaa zetu walioambiwa kuwa kabla hujaingia kwenye nyumba ya ibada hakikisha u msafi wenyewe wakajua kumbe wanatakiwa kuoga kwanza?

nilikuwa nauliza tu mkuu. ulishawahi kufiwa na mtu wa karibu mkuu? mlizika bila maiti kuoshwa? hamkumvika sanda? hamkununua jeneza?
 
na wewe ni nani kuhukumu?!!

Kuhukumu tena? Huo ndio ukweli. Ukifiwa unajisikia huzuni utamkosa yule mtu na unajisikia na hofu juu kwahiyo vingi utakavyofanya ni kwa nafsi yako tu including all ceremonial stuff.
Lakini tunaweza kuzungumzia tofauti tukija upande wa Spiritual
 
Hivi kweli ndugu yako kipenzi aliefariki unaweza mfananisha na mnyama na kumuita mzoga!!
Itakua hayajakufika ya kufiwa na mpendwa wako unasikia tu kwa jirani

Yesu alisema waache wafu wazikane wenyewe, wewe unauchungu na huruma kuliko yesu aliyekufa kwa ajili ya ulimwengu? Baada ya dhambi Mungu alisema tuliumbwa kwa udongo mavumbini tutarudi tusiishi kuufata mwili tuishi kwa kanuni za Mungu tunapotea bila kujijua.
 
Wadau mbona mna maneno makali sana... Nazungumzia nakshi jamani yaan inafika mahali watu wanapamba makaburi as if aliyekufa anashuhudia au kutoa shukrani kwa kilichofanyika!

Kuweka kumbukumbu sio issue issue ni kunakshi mpaka inakuwa kufuru. Kwanini ile pesa isitumike kuyaenzi mazuri aliyoyaacha au kusaidia watoto au jamaa zake????

Dada unasahau kuwa duniani tuko tofauti, huko kwenye Makaburi ni mbali sana, hata heri ya hao wanaogawa riziki kwa wengine kwa njia hiyo ya kujenga makaburi ya bei mbaya. Naamini point yako inalenga eneo la uchumi zaidi, mbona hujazungumza mtu mmoja kuwa na gari tatu za kutembelea,hujasema wanaomwaga chakula kwa sababu tu kachoka kula mfululizo. Je umefanya utafiti na kuona kila wanaojenga makaburi vzur sana hawajamueni marehemu? Je wanaofunga ndoa kwa mamilioni na ndoa yenyewe inakufa baada ya week,ilihali kuna watu walichangishwa?

Tunatofautiana dada.
 
umri tu, subiri kidogo ufiwe na mama yako kisha uone mzoga wake, nina imani maiti yake utaifanya kama kama inavyofanyiwa mizoga ya mbwa.

You are too emotional....reality inabaki palepale maiti ni mzoga tu. Nishawahi kufiwa na mzazi btw
 
Dada unasahau kuwa duniani tuko tofauti, huko kwenye Makaburi ni mbali sana, hata heri ya hao wanaogawa riziki kwa wengine kwa njia hiyo ya kujenga makaburi ya bei mbaya. Naamini point yako inalenga eneo la uchumi zaidi, mbona hujazungumza mtu mmoja kuwa na gari tatu za kutembelea,hujasema wanaomwaga chakula kwa sababu tu kachoka kula mfululizo. Je umefanya utafiti na kuona kila wanaojenga makaburi vzur sana hawajamueni marehemu? Je wanaofunga ndoa kwa mamilioni na ndoa yenyewe inakufa baada ya week,ilihali kuna watu walichangishwa?

Tunatofautiana dada.

Wote wapo kundi moja. Wanajenga bondage na vitu vya physical world.......kusema au kutosema hakubadili ukweli
 
Habari za asubuhi ya leo wapendwa wana Jamvi....

Kwanza niombe radhi kwa nitakaowakwaza kwa namna moja ama nyingine.

Kuna suala hili huwa linanitatiza naomba kuelewesha.

Kumezuka tabia ya kujengea makaburi kwa marumaru ya samani za aina tofauti tofauti tena zenye gharama kubwa, Utakuta mtu alikuwa anaumwa kwa muda mrefu lakini watu hawakujitokeza kumhudumia lakini baada ya mtu huyo kufariki dunia wanajitokeza ndugu, jamaa na marafiki wanapanga mipango ya kujengea kaburi lake na kuweka nakshi ya kila aina.

Je watu hawa walikuwa wapi wakati wa ugonjwa??

Je kujengea kaburi hilo kutamsaidia nini yule marehemu??

Kuna watu wanafariki ghafla aidha kwa ajali ama kifo cha aina yoyote ila kwa ghafla... Kuna ulazima gani wa kulinakshi kaburi???

Tena kuna wengine wamekwenda mbali wakaanza kutafuta makaburi haya ya mababu zao na kuanza kuyajengea na kuyaweka katika hali ya unadhifu kana kwamba kilichomo ndani yake kina thamani... Tena na kufanya sherehe sijui ya kujengea makaburi... Ni nini maana yake???

Kwa mtazamo wangu ujenzi huu wa kuweka nakshi ni kugharamika kusiko na faida...


N.B. Ni mtazamo tu naomba nisipondwe mawe....
Subiri siku wanao watakapo uliza kaburi la babu /bibi yao likowapi ndipo utajua umuhimu wake ,na kwa wewe mbona utatafuta ma archaelogist wakusaidie!
 
Ni mtazamo wangu mkuu, naona una maneno makali sana.... Kama angekwua mzima ungemnunulia suti ili kujihifadhi, sasa kumjengea kaburi kutamsaidia nini ilhali ashakuwa marehemu? Hata umejengee kwa dhahabu na lulu haitomsaidia chochote.......
Na akifa usimzike bhana kwani wanini wakati keshakufa ?mtupe jaani huko kama panya,usiishie nusu nusu fika mwisho bint,kitu kama hakina thamani usikipe hadhi nusunusu!
 
Habari za asubuhi ya leo wapendwa wana Jamvi....

Kwanza niombe radhi kwa nitakaowakwaza kwa namna moja ama nyingine.

Kuna suala hili huwa linanitatiza naomba kuelewesha.

Kumezuka tabia ya kujengea makaburi kwa marumaru ya samani za aina tofauti tofauti tena zenye gharama kubwa, Utakuta mtu alikuwa anaumwa kwa muda mrefu lakini watu hawakujitokeza kumhudumia lakini baada ya mtu huyo kufariki dunia wanajitokeza ndugu, jamaa na marafiki wanapanga mipango ya kujengea kaburi lake na kuweka nakshi ya kila aina.

Je watu hawa walikuwa wapi wakati wa ugonjwa??

Je kujengea kaburi hilo kutamsaidia nini yule marehemu??

Kuna watu wanafariki ghafla aidha kwa ajali ama kifo cha aina yoyote ila kwa ghafla... Kuna ulazima gani wa kulinakshi kaburi???

Tena kuna wengine wamekwenda mbali wakaanza kutafuta makaburi haya ya mababu zao na kuanza kuyajengea na kuyaweka katika hali ya unadhifu kana kwamba kilichomo ndani yake kina thamani... Tena na kufanya sherehe sijui ya kujengea makaburi... Ni nini maana yake???

Kwa mtazamo wangu ujenzi huu wa kuweka nakshi ni kugharamika kusiko na faida...

N.B. Ni mtazamo tu naomba nisipondwe mawe....

Ungekuwa karibu yangu ningekunulia soda hahaha!! nakusupport 100%. Hakuna faidia ni kupoteza hela tu
 
Mkuu unajua kujengea hakuna shida ila kuweka nakshi, mara marumaru, mara kuweka kivuli ndio shida! kwani ukijenga kawaida kumbukumbu haibaki???
Kama shida ni sitara tu naamini hata wewe ukijizungushia mabati kama sita tu utalala ,lakini kwanini unajenga nyumba kuubwa twiga anapita bila kuinama?
 
nilikuwa nauliza tu mkuu. ulishawahi kufiwa na mtu wa karibu mkuu? mlizika bila maiti kuoshwa? hamkumvika sanda? hamkununua jeneza?

Tulifanya kwani ni utamaduni tuu kufanya hivyo.
Swali linasema kuwa je kufanya hivyo ni lazima au kuna umuhimu wowote?
Jibu kama nilivyosema,"hakunaga"
 
You are too emotional....reality inabaki palepale maiti ni mzoga tu. Nishawahi kufiwa na mzazi btw

Mtu akifa hapashwi kukumbukwa awe mama, baba, kaka dada etc. Yesu aliposema acha wafu wawazike wafu wenzao hakuropoka alikuwa na maana, Ukishakufa wewe ni mzoga, kinachachobakia ni kukuweka kwenye ardhi tu.
 
Subiri siku wanao watakapo uliza kaburi la babu /bibi yao likowapi ndipo utajua umuhimu wake ,na kwa wewe mbona utatafuta ma archaelogist wakusaidie!

hao watoto wanauliza makaburi ya nini? Jibu ni moja tu. Walitangulia mbele ya haki Period.
 
Yesu alisema waache wafu wazikane wenyewe, wewe unauchungu na huruma kuliko yesu aliyekufa kwa ajili ya ulimwengu? Baada ya dhambi Mungu alisema tuliumbwa kwa udongo mavumbini tutarudi tusiishi kuufata mwili tuishi kwa kanuni za Mungu tunapotea bila kujijua.

My dear sio wote humu Jf wana dini sawa na yako wengine hatuna dini wala imani, na wengine hatuamini katika dini ya waarab wala wazungu bali dini ya kiafrika.
Kwahiyo unapotoa mawazo yako kwa kumquote mtu usiweke swala la imani yako mbele.

Kama unaamini kuhusu wafu kuwazika wafu wenzio kwa tafsiri uliyoitumia hapo juu basi tusingewahifadhi ata kwenye majeneza au kwa nguo hao wapendwa wetu pindi wanapoiacha dunia hii.
 
My dear sio wote humu Jf wana dini sawa na yako wengine hatuna dini wala imani, na wengine hatuamini katika dini ya waarab wala wazungu bali dini ya kiafrika.
Kwahiyo unapotoa mawazo yako kwa kumquote mtu usiweke swala la imani yako mbele.

Kama unaamini kuhusu wafu kuwazika wafu wenzio kwa tafsiri uliyoitumia hapo juu basi tusingewahifadhi ata kwenye majeneza au kwa nguo hao wapendwa wetu pindi wanapoiacha dunia hii.

Ndugu yangu samahan kwa kuonesha upande mmoja wa shilingi lakini pia sikumbuki ni mtume yupi alizikwa na jeneza bali sanda peke yake. Chamsingi hapa hakuna haja ya kulemba kaburi wakati kilicho ndani kitaoza na kuwa udongo .
*Elekeza nguvu na mali zako kwa walio hai kuwafundisha yaliyomema wawe na mahusiano mazuri na Mungu wao wasife na dhambi.
 
Ndugu yangu samahan kwa kuonesha upande mmoja wa shilingi lakini pia sikumbuki ni mtume yupi alizikwa na jeneza bali sanda peke yake. Chamsingi hapa hakuna haja ya kulemba kaburi wakati kilicho ndani kitaoza na kuwa udongo .
*Elekeza nguvu na mali zako kwa walio hai kuwafundisha yaliyomema wawe na mahusiano mazuri na Mungu wao wasife na dhambi.

Sawa ndugu. Ila swala hapa ni kumbukumbu ndio point yangu. Kama waishivyo ndani ya nyoyo zetu na swala la kujengea limekaa kihisia zaidi. Ukiona haina maana kumjengea ni una sababu zako ila kwa kuongelea hii thread basi nitasimamia katika kujengea makaburi kwasababu ya kumbukumbu
 
Mara nyingi ujenzi wa gharama wa makaburi unakidhi zaidi haja ya kuturidhisha sisi wajengaji kuliko haja za waliokufa. Na baadhi ya watu hujisikia va kwamba hawakutoa huduma stahili wakati wa ugonjwa/uhai wa marehemu,hivyo kufidia kwa ujenzi wa gharama. Wengine tunaingia gharama kubwa kwa kufuata mkumbo
 
Back
Top Bottom