Kujengea makaburi ya Waliotutangulia - Kuna umuhimu wowote?

Kujengea makaburi ya Waliotutangulia - Kuna umuhimu wowote?

Kidogo kidogo, unashangaa na wewe kupitia mstari huo unaanzisha kanisa.............mara linakuwa kubwa unakula vichwa, watu kibao wamefanikiwa kwa kutafsiri vifungu katika Biblia...................pambana mdogo wangu..........go......go............gooooooooo!



Wewe Pagija sifikirii huo ujinga Wa kufungua Kanisa km hao wachungaji Wa mishahara! Ntaendelea Kufundisha ukweli tu!
 
Last edited by a moderator:
Hakuna umuhimu wowote wa kujengea makaburi,na wala usidanganyike eti yanajengwa ka ajili ya kutunza kumbukumbu.
Jiulize hivi,hivi bila ya hilo kaburi hutajua au kukumbuka kuwa nduguyo amefariki?!
Hakuna umuhimu wowote!
HAKUNA!...
 
Ata Yesu alisema mnapamba makaburu Lkn ndani kuna mizoga na mifupa tu!

Kwahiyo kupamba Kwa kuyajengea haifai! Muongozo Wa Maandiko unatosha kutuongoza ktk hili!

Ameen... Barikiwa zaidi!!
 
Kwa upande wangu nakubaliana na wewe. Sisi Watanzania tunapenda na kushadadia mambo yasiyo ya msingi sana.

Kwa mfano, kuna haja gani ya kuwa na harusi ya gharama kubwa (wengine wamefika kwenye >40mil) wakati wahusika hawana uhakika wa maisha baada ya harusi?

Kwa hiyo, haya mambo ya msiba pia tumeyaungiza kwenye mkondo huo huo....wa kufikiria mambo ya kutupa maujiko zaidi ya maendeleo!
 
Wadau mbona mna maneno makali sana... Nazungumzia nakshi jamani yaan inafika mahali watu wanapamba makaburi as if aliyekufa anashuhudia au kutoa shukrani kwa kilichofanyika!

Kuweka kumbukumbu sio issue issue ni kunakshi mpaka inakuwa kufuru. Kwanini ile pesa isitumike kuyaenzi mazuri aliyoyaacha au kusaidia watoto au jamaa zake????

Ukitaka kupata jibu la hiyo issue yako ya makaburi kujengwa kwa nakshi jiulize maswali kadhaa....
1. Kwanini kuna nyumba za aina tofauti na nyingine za gharama kubwa! Je, wale waojenga nyumba za gharama kubwa wanakufuru?
2. Kwanini kuna magari ya bei mbali mbali!? Je wale wanaonunua magari ya bei kubwa wanakufuru?
3 Kwanini hata makanisa na misikiti yana thamani tofauti? Je ni kukufuru?
4.....
5.....
1000. Kwa nini kila kitu kwenye maisha kinahitilafiana bei?
 
Hakuna umuhimu wowote wa kujengea makaburi,na wala usidanganyike eti yanajengwa ka ajili ya kutunza kumbukumbu.
Jiulize hivi,hivi bila ya hilo kaburi hutajua au kukumbuka kuwa nduguyo amefariki?!
Hakuna umuhimu wowote!
HAKUNA!...

Kitu kitu kimoja ni dhahiri... watu wasio na uwezo wa fedha siku zote wanapoona wenye uwezo wanafanya mambo wasio na uwezo wa kuyafanya wao hutafuta njia ya kujiliwaza! Nyie mko kwenye hili kundi!
 
Mkuu unajua kujengea hakuna shida ila kuweka nakshi, mara marumaru, mara kuweka kivuli ndio shida! kwani ukijenga kawaida kumbukumbu haibaki???

naona unajichanganya kidogo mkuu wangu! kinacho"mata" hapa ni DHAMIRA YA NAFSI, unapoamua kujengea kaburi la mpendwa wako aliyetangulia ni kwa msukumo upi? je unataka kwa ajili ya ufahari tu kujionesha kwa watu au kuna kitu kinakugusa moyoni? kuna mila za wengine haziruhusu hata kuweka jiwe la kumbukumbu juu ya kaburi, hakuna msalaba, hakuna kupanda hata mauwa;ndugu zangu wajaluo wakizika wanafukia kisha wanacheza disko juu ya kaburi mpaka linapotea, wanafanya hivi ili kujaribu kufuta kumbukumbu ziletazo sononeko la moyo, ni mila zao na wako sahihi kabisa, wengine mtu akifa wanachoma moto na mabaki wanayasaga yanakuwa unga na wanaenda kumwaga baharini, na wao pia wako sahihi. sisi wabantu tunaweka alama kama kumbukumbu, zamani kabla hatujabadilika na kunakili mila za wenzetu tulikuwa tunaweka jiwe, hata hilo jiwe ilikuwa linatafutwa jiwe lililo zuri lenye utofauti na mawe mengine, ukiona tu unajua kuna kaburi hapa hata kama ni porini, tukabadili mila na kuanza kuweka misalaba ya miti, ya chuma, na ya mawe yaliyochongwa vizuri, baadaye tukawa tunajengea, yote sioni ubaya, kikubwani dhamira ya nafsi. Binafsi nina madeni kadhaa kwa wapendwa wangu waliotutoka, nitajitahidi kadri niwezavyo kama nipo hai nitembelee kaburi moja baada ya lingine na kuwakumbuka kwa kuyaboresha, nitatembelea kaburi la rafiki yangu mpendwa wa shule, nitakaa juu ya kaburi, nitalia nitaomboleza mpaka chozi langu likauke, sitataka mtu anishike wala kunipooza kwani ni mimi tu nijuaye machungu ya moyo, nitamtengenezea kumbukumbu, najua haitapoza machungu yangu lakini nafsi yangu ndivyo inavyonituma. :rip:
 
Hakuna umuhimu wowote wa kujengea makaburi,na wala usidanganyike eti yanajengwa ka ajili ya kutunza kumbukumbu.
Jiulize hivi,hivi bila ya hilo kaburi hutajua au kukumbuka kuwa nduguyo amefariki?!
Hakuna umuhimu wowote!
HAKUNA!...

kuna umuhimu wa maiti kuoshwa na kuvishwa sana kabla ya kuzikwa?
 
Kitu kitu kimoja ni dhahiri... watu wasio na uwezo wa fedha siku zote wanapoona wenye uwezo wanafanya mambo wasio na uwezo wa kuyafanya wao hutafuta njia ya kujiliwaza! Nyie mko kwenye hili kundi!

Unafahamu uwezo wangu ?
Iko hivi,wasio na uwezo ndio wanaohaingaika na vitu vya gharama ili kuficha umaskini wao.Chunguza hata simu zao utaona jinsi wanavyo cimplicate.
Wewe upo kwenye kundi hili Sheikh.
 
Ni vizuri kujengea kwa ajili ya kumbukumbu. Fikiria mzazi aliyefariki akaacha watoto wadogo wakija kukua wataonyeshwa kuwa pale ndipo alizikwa mzazi wenu ukiliacha tu ule udongo utasambaratika na kaburi halitoonekana tena.
Nakshi kwenye ujenzi sasa inategemea na uwezo wa familia husika,wakati wewe unaona kuweka tiles ni gharama kuna wanaoona huo ndio ujenzi wa kawaida kabisa. Hata nyumba tunazoishi zinatofautiana thamani kutegemeana na uwezo wa wanafamilia.

Kujengea kama kumbukumbu hakuna tatizo ila isiwe kama kufuru... Inatosha kuwekea sakafu ili lisipotee sio kuweka marumaru mara paa mara uzio n.k!
 
Wadau mbona mna maneno makali sana... Nazungumzia nakshi jamani yaan inafika mahali watu wanapamba makaburi as if aliyekufa anashuhudia au kutoa shukrani kwa kilichofanyika!

Kuweka kumbukumbu sio issue issue ni kunakshi mpaka inakuwa kufuru. Kwanini ile pesa isitumike kuyaenzi mazuri aliyoyaacha au kusaidia watoto au jamaa zake????
Swala bado litabaki uwezo charminglady wenye uwezo watanakshi vile wawezavyo na wasio na uwezo wataweka ata mashahidi ( jiwe kichwani na jiwe miguuni).
Mwenye hela yake huwezi kumwambia aweke tu mashahidi kama kumbukumbu labda swala la imani liwe linakinzana.

Pia tunapowajengea wapendwa wetu tunaamini wanaona bado tunawathamini na kuwapenda ata kama wamefariki. Ni upendo unaokusukuma kufanya hivyo si vinginevyo.
 
Last edited by a moderator:
kuna umuhimu wa maiti kuoshwa na kuvishwa sana kabla ya kuzikwa?

Hakuna.

Au unataka kuwa kama wale jamaa zetu walioambiwa kuwa kabla hujaingia kwenye nyumba ya ibada hakikisha u msafi wenyewe wakajua kumbe wanatakiwa kuoga kwanza?
 
naona unajichanganya kidogo mkuu wangu! kinacho"mata" hapa ni DHAMIRA YA NAFSI, unapoamua kujengea kaburi la mpendwa wako aliyetangulia ni kwa msukumo upi? je unataka kwa ajili ya ufahari tu kujionesha kwa watu au kuna kitu kinakugusa moyoni? kuna mila za wengine haziruhusu hata kuweka jiwe la kumbukumbu juu ya kaburi, hakuna msalaba, hakuna kupanda hata mauwa; ndugu zangu wajaluo wakizika wanafukia kisha wanacheza disko juu ya kaburi mpaka linapotea, wanafanya hivi ili kujaribu kufuta kumbukumbu ziletazo sononeko la moyo, ni mila zao na wako sahihi kabisa, wengine mtu akifa wanachoma moto na mabaki wanayasaga yanakuwa unga na wanaenda kumwaga baharini, na wao pia wako sahihi. sisi wabantu tunaweka alama kama kumbukumbu, zamani kabla hatujabadilika na kunakili mila za wenzetu tulikuwa tunaweka jiwe, hata hilo jiwe ilikuwa linatafutwa jiwe lililo zuri lenye utofauti na mawe mengine, ukiona tu unajua kuna kaburi hapa hata kama ni porini, tukabadili mila na kuanza kuweka misalaba ya miti, ya chuma, na ya mawe yaliyochongwa vizuri, baadaye tukawa tunajengea, yote sioni ubaya, kikubwani dhamira ya nafsi. Binafsi nina madeni kadhaa kwa wapendwa wangu waliotutoka, nitajitahidi kadri niwezavyo kama nipo hai nitembelee kaburi moja baada ya lingine na kuwakumbuka kwa kuyaboresha, nitatembelea kaburi la rafiki yangu mpendwa wa shule, nitakaa juu ya kaburi, nitalia nitaomboleza mpaka chozi langu likauke, sitataka mtu anishike wala kunipooza kwani ni mimi tu nijuaye machungu ya moyo, nitamtengenezea kumbukumbu, najua haitapoza machungu yangu lakini nafsi yangu ndivyo inavyonituma. :rip:

Mie ni mfuasi wa hiyo mila ndio maana naona hakuna haja!
 
Kitu kitu kimoja ni dhahiri... watu wasio na uwezo wa fedha siku zote wanapoona wenye uwezo wanafanya mambo wasio na uwezo wa kuyafanya wao hutafuta njia ya kujiliwaza! Nyie mko kwenye hili kundi!


Mbona kuna michango inapitishwa kama kweli wanaojenga wana uwezo?

Mbona kuna michango ya kukodi magari ya gharama kubeba jeneza??

Unataka kutuaminisha kuwa wanaojengea makaburi kwa bei mbaya wote wana uwezo?
 
msisome maandiko machache mka generalize vitu watu wanajengea ukumbusho wa watu wao sioni kosa mi kwangu lazma yajengewe na ni msomaji mzuri wa biblia

Watu wanajisahau tu...ukisoma Bible kwa makini utagundua wala haikatazi kama wengi wanavyotaka kutuaminisha.

Ila ukijenga kwa lengo la kupaweka pawe SHRINE...hapo ndo utakuwa unatenda kinyume na maandiko!

Turejee wakati wana wa Israel walipokuwa wanatoka Misri...walibeba mpaka mifupa ya mababu zao ili waipeleke Kaanani. This means kuwa waliyatunza makaburi ya hao wapendwa wao ndo maana muda wa kuondoka ulipofika yalikuwa traceable... kwa mtindo wa dunia ya leo ndo sawa na kuyajengea.

Binafsi sioni tatizo...la mamangu nililijengea na la baba nipo mbioni kulijengea pia. If you have a motive behind huko kujengea...hilo ni TATIZO!
 
Charminglady kujengea ni kuweka kumbukumbu kupitia uimara. Makaburi yasipotunzwa vizuri hupotea kabisa. Sisi tunaoishi mbali na miji yetu ya asili na kuwa na makaburi ya wazee ni rahisi sana kupotea maana watunzaji si rahisi kama tunavyofikiria. Hivyo ukilijengea litadumu na vizazi vitajifunzia historia pale. Tena weka na maneno ya jina, mwaka wa kuzaliwa, kufa, kuzikwa etc. Archeologists wanajua maana ya ancestral record keeping.
 
Back
Top Bottom