Kujengea makaburi ya Waliotutangulia - Kuna umuhimu wowote?

Kujengea makaburi ya Waliotutangulia - Kuna umuhimu wowote?

Mkuu unajua kujengea hakuna shida ila kuweka nakshi, mara marumaru, mara kuweka kivuli ndio shida! kwani ukijenga kawaida kumbukumbu haibaki???

Ama kweli jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza. SABABU YA KUJENGA MAKABURI NI KUWEKA KUMBUKUMBU. Kama ni gharama au matumizi waulize wazungu wanaofuatilia ulipozikwa moyo wa Dr. Livingstone hadi leo. Suppose kusingekuwa hakujajengwa mnara kizazi hiki kingejuaje alipofia.

Hata vijukuu vyangu vinatakiwa vijue original yao haswa hao watoto waliozaliwa mijini. Ni muhimu sana mtu kujua original yake na kunapokuwa na evidence ya ancestors inakuwa nzuri zaidi. suppose evidence ya ancestors haipo je uta mshawishije huyu kitukuu au kilembwe aliyezaliwa mjini au Ulaya kama kweli pale ndipo alipoanzia kama hamna Kaburi lililohifadhiwa kwa maana ya kujengwa
 
Moja ya sababu kubwa ni kuonyesha heshima kwa imani ya mjengaji wa kaburi . Kwani kufanya hivyo nafsi huridhika na kujiona imetenda jambo muhimu ambapo inaondoa deni la nafsi.
 
Ata Yesu alisema mnapamba makaburu Lkn ndani kuna mizoga na mifupa tu!

Kwahiyo kupamba Kwa kuyajengea haifai! Muongozo Wa Maandiko unatosha kutuongoza ktk hili!

Yesu alipofufuka aliacha kaburi lake katika utaratibu au mpangilio mzuri kwa vile hakurundika leso ya kichwani pamoja na vitambaa (sanda).

Yohana 20.7 ".....na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake."
 
Yote hayo ni kuridhisha nafsi ya aliye hai . Kwamba sina deni lolote kwa ndugu ama jamaa aliyefariki. Na kuweka kumbukumbu .
 
Kujenga makaburi ni kuonesha udugu, pia kaburi sio lazima lijengwe kulingana na itikadi za kidini na utamaduni.
 
Kwanza fikiria ikiwa ni wew leo hii haupo duniani ukazikwa na kusahauliwa unadhani itakuwa na taswira nzuri? Kwangu mim kuna maana kubwa na kwa mwaka huu nimepanga kuvunja kaburi la Bibi yangu kipenzi Martha Njau(1938-2004) lililojengwa kwa ukawaida sana na kumjengea jingine lenye hadhi nzuri kama Ahsante kwake kwa kuwa alikuwa Moyo wangu alikuwa ni Faraja kwangu na nikumbukumbu ya miaka kumi ya kifo chake. Kwangu kuna maana kwa wapendwa wetu waliotutoka tukiendelea kuwathamini kwa njia hiyo na dua pia.
 
Yesu alipofufuka aliacha kaburi lake katika utaratibu au mpangilio mzuri kwa vile hakurundika leso ya kichwani pamoja na vitambaa (sanda).

Yohana 20.7 ".....na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake."


Kwahiyo Una Maana gani Mkuu!?
 
mi naona kujengea makabr ni vizr ila gharama ziwe za kawaida ili tu kuweka kumbukumbu za ndg zetu walio tangulia mbele za haki kwa sababu kwa wa katoliki wana amini katk maandiko kua petro ndio mwamba na juu yake litajengwa kanisa na ndipo lilipo kanisa kuu zaid la wa RC dunian makai makuu ya papa na waislam waendapo hija lazma wakalitazame kabur la mtume Muhammad (S.A.W) hvo haya mambo si ya kubeza na wengine huenda kupaona mahala ambapo yesu alizukwa na akafufuka ni kila mtu na iman yake na anaejua maandiko vzr ataona ni jinsi gan mungu aliwafundisha wana wa adam namna ya kumzika mtu alie kuga hii nadhan inaonesha picha kua mungu alitaka na antaka tuwakumbuke ndg zetu.waliotangulia tuwaombee na iwe mawaidha kwetu sisi kua ipo siku tutayaonja mauti
 
Habari za asubuhi ya leo wapendwa wana Jamvi....

Kwanza niombe radhi kwa nitakaowakwaza kwa namna moja ama nyingine.

Kuna suala hili huwa linanitatiza naomba kuelewesha.


Madame..you have point..kwani ukieka alama ya kidini au imani yako..hilo kaburi litapotea kama tunahofia
kupotea??
Mimi naona ni mbwembwe tu zizizo na mashiko..sol long you're dead..you're dead..

Kumezuka tabia ya kujengea makaburi kwa marumaru ya samani za aina tofauti tofauti tena zenye gharama kubwa, Utakuta mtu alikuwa anaumwa kwa muda mrefu lakini watu hawakujitokeza kumhudumia lakini baada ya mtu huyo kufariki dunia wanajitokeza ndugu, jamaa na marafiki wanapanga mipango ya kujengea kaburi lake na kuweka nakshi ya kila aina.

Je watu hawa walikuwa wapi wakati wa ugonjwa??

Je kujengea kaburi hilo kutamsaidia nini yule marehemu??

Kuna watu wanafariki ghafla aidha kwa ajali ama kifo cha aina yoyote ila kwa ghafla... Kuna ulazima gani wa kulinakshi kaburi???

Tena kuna wengine wamekwenda mbali wakaanza kutafuta makaburi haya ya mababu zao na kuanza kuyajengea na kuyaweka katika hali ya unadhifu kana kwamba kilichomo ndani yake kina thamani... Tena na kufanya sherehe sijui ya kujengea makaburi... Ni nini maana yake???

Kwa mtazamo wangu ujenzi huu wa kuweka nakshi ni kugharamika kusiko na faida...

N.B. Ni mtazamo tu naomba nisipondwe mawe....


So long you're dead..you're are..what remains its history..
Kwishnei....
 
Ni hulka ya kibinadamu tu..........hata mtu akiugua miaka kumi kitandani watu hawaji wala kumchangia tiba. Akifa wanajazana rundo na michango lukuki!

Safari
Ningetamani mleta hoja angesema kuwa watu wabadilike, wawatunze ndg zao vizuri kabla ya kufa kwao, ili wakija kuwajengea makaburi yao wawe na dhamira njema mioyoni mwao tu.
Hata yeye akifa bado tutamnunulia jeneza kwa fedha yetu, tutamnunulia sanda kwa fedha yetu. Hizo zote ni fadhila kwake japo hawezi kuja kuzilipa tena. Waache wanaotaka kukupamba wakupambe, mbona maiti huoshwa wakati kaokotwa mwenye maji???
 
Ha ha ha, wazee hatukuwasaidia wakiwa hai, hatukuwapamba wakiwa hai. Leo wakifa tunajifanya kupamba makaburi.
 
Ww usijenge sist tutawaenzi marehemu mpk kufa.baba yangu kafariki nikiwa mdogo. Sasa nimekua nna uwezo nisimjengee kaburi lake?angekua hai ningemnunulia suti. Kafariki hela ya suti itamjengea kaburi. We yako kanywee bia bahili wahed

Jitahid kumfanyia mtu mema au mpende akiwa hai akishakufa haina maana tena hata ukihangaika na kabur lake haisaidii lolote km ni mzaz wako ulimkosea na ukashindwa kumuomba msamaha akiwa hai laana ipo palepale hata ujenge kabur la gorofa
 
Kuna watu wanaamini kuwa makaburi yana uwezo wa kimungu, ndo maana wanayajengea na kuyaomba mahitaji yao.
 
Kuna watu wanaamini kuwa makaburi yana uwezo wa kimungu, ndo maana wanayajengea na kuyaomba mahitaji yao.
iman bwana! So wajiopotea kwenye ndege ya malysia ?
 
Hivi hayati tupac alizikwa? Huyu jamaa namkubali sana na wala sihitaji kuliona kabulí lake lakin mziki wake umebaki kwenye roho mpaka kesho
 
Naomba mnitoe porini wana Jf, eti kujenga makaburi au kumbukumbu ya kifo ni Siku ya SHEREHE au HUZUNI?
 
Back
Top Bottom