Kuiper Belt: Behind the certain

Kuiper Belt: Behind the certain

Kwenye kufikiri kuwa hoja yangu msingi wake ni sayansi tu ndipo penye tatizo na kwasababu hii nakuambia hujaelewa nilichokisema na hata ulichokinunuu ...

Mkuu kwanini usirudie kusoma huenda ukaelewa?

By the way,sayansi inadanganya wenye mambo yote au baadhi tu?
Pale uliposema "Hao Aliens wanaweza kuwa ni product ya huyo shetani.....".Hapa ilimaanisha nini ? Sasa unaponiambia wapi sijaelewa unanishangaza sana.Hoja yako hiyo niliijibu kwa kukuonyesha ni jinsi gani huwezi kuonyesha uhusiano kati ya Shetani na hao Aliens.Kama hukuelewa tamko shetani lilisimama kumaanisha Shetani wa kijini,hapa kunaonyesha dhahiri ni jinsi gani usivyokuwa na elimu juu ya tamko hilo la Shetani na jini.Sasa kutokana na kauli yako ya kuniambia kauli zangu zinakinzana,ukweli uko dhidi yako ni kuwa elimu yako haikuwa na uwezo wa kukufikisha kutambua suala la shetani na jini.

Kwahiyo mzee kauli zangu hazipingani aisee.Rudi kusoma hoja vizuri,kisha ujenge hoja.Uchache wa elimu za watu na kutaka kuingilia mambo makubwa na kuyaelezea ndio kumetufikisha hapa.Si kila mtu anapaswa aandike kuhusu jambo fulani,wala si lazima wewe uandike kuhusu jambo fulani na kamwe hautoulizwa kwanini hujaandika kuhusu jambo fulani.Kila mtu anatakiwa kuvaa viatu vyake,viatu vinavyomtosha yeye,si fulani kuvaa viatu vya fulani bila kuwa na sifa anuai za kuvaa viatu hivyo.Ndio maana mimi kwa uchache wangu wa elimu ni kaamua kuwa mwanafunzi,na kuhoji jambo kielimu.

Ukiandika makala nyingine usisahau kuni tag mzee.
 
Kwenye kufikiri kuwa hoja yangu msingi wake ni sayansi tu ndipo penye tatizo na kwasababu hii nakuambia hujaelewa nilichokisema na hata ulichokinunuu ...

Mkuu kwanini usirudie kusoma huenda ukaelewa?

By the way,sayansi inadanganya wenye mambo yote au baadhi tu?
Kiongozi kamwe huwezi kuukataa ukweli huo kama kweli wewe ni mtu wa elimu.Hoja yako msingi wake ni wa sayansi ndio maana pale ulipo anza kuleta stori za Kuiper belt na nadharia zake.Ndio maana kuna jamaa mmoja alikuuliza swali moja la msingi sana juu ya maelezo,akionyesha ya kuwa maelezo yako hayajaonyesha uwepo wa Mola aliyeumba,yaani kuhusu hizi ngano mbona Mola haonekani nafasi yake.Sasa unapotaka kukanusha hoja yako na kukataa ya kuwa haija mili kisayansi,basi twambie hoja yako msingi wake ni upi.Ila kaa ukijua hoja yako msingi wake ni sayansi.

Nimezisoma sana hoja mzee,ndio maana nikaamua kukujibu,bali nimezielewa sana.
 
1;Unachokifanya hapa ni kutaka kuonesha kuwa wanasayansi ni watu waongo na ambao hawajawahi kufanya jambo lolote la maana kiasi kwamba ni wa kupuuzwa sana.hii siyo kweli hata kidogo na inawezekana labda kwako ni waongokwa kiwango hiki.Unaweza kutueleza kuwa ni waongo kwenye mambo yote?

2;Kimsingi watoto huwa wanasema kweli kabisa na ushahidi wao huwa unakubalika sana mahakamani hadi ithibitishwe walirubuniwa au kulazimishwa kwa njia mbali mbali kusema waliyosema.Dhana yako ya ushahidi wa mtu hadi abalehe ni dhana ya wapi sijui....

Bado sijaona sababu ya kufuatilia maelezo yako kwa kina hadi sana labda ukinipa maelezo ya kueleweka....
Umeuliza swali zuri sana mzee,ukweli unabaki pale pale.Umejaribu kugusia nukta moja ya utoto na ghafla ukafikia hitimisho lisilo la kielimu kwa kuegemeza kwenye mahakama.Sisi hatuangalii mahakama sisi tunaangalia utoto na suala la ushahidi na tunaangalia vipi tutaupata ukweli kama ulivyo si kama unavyojitokeza kwa watu.

Ukimuangalia mtoto kwa umbile bila kaungalia silika yake ni vigumu sana kunielewa,ila tunaelekea kuzuri sasa.Niliposema mtoto sikuacha kuzungumzia jambo la msingi sana liitwalo kupambanua mambo.

Turudi katika ukweli muhimili,hii umeshawi kusikia kuna mtume alipewa utume akiwa mtoto au nabii aliyekuwa nabii akiwa mtoto,ukitaka kuukataa ukweli utaruhusu madudu mengi sana katika kupata habari ya uhakika.Mfano wa hili ni sawa sawa na kuchukua ushahidi wa mtu mlevi au mtu muovu.

Sijasema watoto hawasemi kweli mzee,mfano mtoto ukimuuliza huyu ni baba yako,kama kweli ni baba yake atakwambia ni baba yake lakini mtoto hawezi kung'amua mambo na kuyapembua na kutofautisha kweli kutokana na uongo.Embu hapa jaribu kufikiri kidogo kisha nitakuja na mifano juu ya hilo.
 
Unaniambiaje nirejee misingi ya sayansi wakati wewe huitaki hiyo sayansi?

Sina ushahidi namna gani?

Haya maelezo yako yanakinzana na maelezo yako hapo juu,hebu rejea uone namna unavyo0jikinza....

Nani amesema kuwa hao Aliens wanawezekana kuwa ni majini?

Unasoma ninachoandika vizuri mkuu?

Hili swali lako halina mashiko kutokana na msingi wa swali hili ambalo ni hiyo kauli yako hapo juu kuwa siyo ya kweli...

Kutawala maana yake nini kwa namna unavyoelewa wewe?

tuanzie hapo halafu uone namna unavyokuna kushindwa kutetea hiki unachoandika hapa...

Akili yangu iko huru sana,tatizo ni kwamba matatizo yako unayaonea kwangu kitu ambacho ni tatizo zaidi....

Wewe peke yako ndiye unasema umegusa mambo muhimu bila kujua kuwa unaweza kuona ni muhimu wakati kiuhalisia ikawa siyo....
Tamko kutawala lina maana ya kilugha na maana ya kisheria.Ndio maana nahisi naongea mambo mepesi sana kiasi ambacho akili yako haikuweza kuyafikia.Kutawala si mpaka uwe katika mfumo fulani,yaani kutawala kidemokrasia au mfano wake katika kutawala kwa kifedhuli.Kutawala hapa nazungumzia kutawala kwa ujumla kwa kiludha na kimatendo.Binadamu ana akili kuliko viumbe wengine na amepewa akili kwa ajili ya kutahiniwa na kuwatawala viumbe wengine,kwa kuwajua tabia zao na kuweza kuwahudumia.Huu ni mfano mwepesi sana juu ya utawala wa binadamu dhidi ya viumbe wengine.

Leo tembo hawezi kumfuga binadamu na kumzidi maarifa lakini,leo binadamu anamfuga tembo na kumfundisha.Hivi hata hili linataka tuminyane mzee ? Embu jitahidi kuelewa isee.
 
Nimekumbuka ile series ya falling skies jinsi wale alien walivyokuwa wanawasiliana na binadam
 
Tamko kutawala lina maana ya kilugha na maana ya kisheria.Ndio maana nahisi naongea mambo mepesi sana kiasi ambacho akili yako haikuweza kuyafikia.Kutawala si mpaka uwe katika mfumo fulani,yaani kutawala kidemokrasia au mfano wake katika kutawala kwa kifedhuli.Kutawala hapa nazungumzia kutawala kwa ujumla kwa kiludha na kimatendo.Binadamu ana akili kuliko viumbe wengine na amepewa akili kwa ajili ya kutahiniwa na kuwatawala viumbe wengine,kwa kuwajua tabia zao na kuweza kuwahudumia.Huu ni mfano mwepesi sana juu ya utawala wa binadamu dhidi ya viumbe wengine.

Leo tembo hawezi kumfuga binadamu na kumzidi maarifa lakini,leo binadamu anamfuga tembo na kumfundisha.Hivi hata hili linataka tuminyane mzee ? Embu jitahidi kuelewa isee.
Unaposema binadamu ana akili kuliko viumbe wengine una maana gani?

Hao viumbe wengine ni wapi/wako wapi?
 
Sijasema watoto hawasemi kweli mzee,mfano mtoto ukimuuliza huyu ni baba yako,kama kweli ni baba yake atakwambia ni baba yake lakini mtoto hawezi kung'amua mambo na kuyapembua na kutofautisha kweli kutokana na uongo.Embu hapa jaribu kufikiri kidogo kisha nitakuja na mifano juu ya hilo.
Kuna mambo mtoto hawezi kuhusishwa hasa mambo yanayohusu tafakuri ambapo mtoto anakuwa hana.Ili binadamu aweze kujitambua anahitaji kufikia umri fulani ambao utamfanya awe na uwezo wa kutafakari kwasababu ubongo wake unakuwa umekomaa vya kutosha.Huu ndiyo muktadha wa hoja yako kuhusu utoto.Tatizo huo siyo muktadha wa hiki tunachokijadili hapa....

Suala la utume na mengine ya kufanana na hayo hawezi kupewa mtoto kwasababu yanahitaji fikra zilizokomaa na tafakuri hivyo mfano wako huu una matege....

Hapa tunazungumzia kitendo cha kuona kitu na kukielezea namna kilivyo bila kupindisha.Katika muktadha huu mtoto anaweza kuwa kwenye nafasi kubwa na nzuri zaidi kuaminika kwasababu mtoto hana namna ya kupindisha kwa maslahi yoyote labda tu atishwe.....

Katika kushuhudia jambo,wakiwa wameona watu wa wili mmoja ni mtoto na mwingine ni mtu mzima kisha wakapaswa watoe ushahidi wa jambo lile ushahidi wa mtoto utachukuliwa kwa uzito zaidi kutokana na utoto wake.Jambo lililo hapa linafanana na hilo,ni suala la kuona na kusema ulichokiona na siyo zaidi ya hapo na hapa mtoto anakuwa na uzito zaidi....
 
Pale uliposema "Hao Aliens wanaweza kuwa ni product ya huyo shetani.....".Hapa ilimaanisha nini ? Sasa unaponiambia wapi sijaelewa unanishangaza sana.Hoja yako hiyo niliijibu kwa kukuonyesha ni jinsi gani huwezi kuonyesha uhusiano kati ya Shetani na hao Aliens.Kama hukuelewa tamko shetani lilisimama kumaanisha Shetani wa kijini,hapa kunaonyesha dhahiri ni jinsi gani usivyokuwa na elimu juu ya tamko hilo la Shetani na jini.Sasa kutokana na kauli yako ya kuniambia kauli zangu zinakinzana,ukweli uko dhidi yako ni kuwa elimu yako haikuwa na uwezo wa kukufikisha kutambua suala la shetani na jini.
1;Unaposoma maandiko zingatia sana kila mwandishi anachokuwa anaandika na kujua muktadha wa jumla na muktadha wa kila sentensi ili uelewe mkuu.Kwenye sentensi yamngu nimetumia neno "inawezekana",hapa nilikuwa sijamaanisha iko hivyo isipokuwa nilimaanisha kuwa "kuna uwezekano" nilichokisema kikawa hivyo lakini siyo kama unavyodhani wewe...

2;Niliposema product nadhani nilikuchanganya.Nilitumia neno hilo nikimaanisha kuwa "hao niliowataja wanaweza kuwa ni matokeo ya 'akili' ya Shetani",nitakupa mfano maana naona una shida ya kuelewa haraka....

Mtu akisema kwamba tarakilishi [Computer] ni matokeo ya binadamu hana maana ya kwamba hiyo tarakilishi ni binadamu pia bali matokeo ya kufikiri au akili ya binadamu.Sasa maana hii ndiyo niliyoimaanisha nilipoandika kuwa inawezekana Aliens ni product ya huyo huyo Shetani...

Ukiandika makala nyingine usisahau kuni tag mzee
Haina tatizo kiongozi.....
 
Kiongozi twende taratibu sasa,naona unaelekea kunielewa.Nimekwambia urejee misingi ya sayansi ili ujue ni yapi mapungufu ya sayansi na usiendelee kujadili matokeo ya sayansi sababu mafikio yako yatakuwa ni kubebeshwa uongo ulio mwepesi na kushindwa kuujua uongo huo.Misingi ndio asasi ya kujua hatima ya jambo husika,misingi imara huleta natija madhubuti.Sayansi siikubali hasa sayansi ya mambo ya anga kutokana na misingi yake.Natilia mkazo urejeetena na tena kwenye misingi ya sayansi ili ujue uozo wa sayansi.
Nilikuuliza kwamba,kwako wewe sayansi ni uongo yote au kuna mambo inasema kweli?

Sijaona mahali umejibu hili swali....
Maelezo yangu kamwe hayapingani na ukiona yanapingana basi tambua kuna mambo mawili juu yako.

1.Kwanza ituhumu akili ya kuwa imeshindwa kuyadiriki mawazo na kuyaelewa ndio maana ukafikia hitimisho la kusema ya kuwa yana kinzana.Hapa naweza kukupa mfano juu ya kauli kwayo kwa uelewa mdogo utaweza kusema ya kuwa kauli hizi zina kinzana.Tazama kwa makini kauli hizi.

a) Nilijifunza shari niijue ili nisifanye shari na

b) Haifai mtu kujifunza kufanya mambo maovu.

Mwenye uchache wa kufikiri na kung'amua mambo hapo lazima atasema kauli hizi mbili zinakinzana.Swali la msingi litakuja ni wapi zinakinzana kauli hizo.Tusipende mteremko lazima tuzishughulishe kauli zetu.
1;Siyo kweli kuwa napaswa kuituhumu akili yangu kwasababu tu ya kutoyaelewa maelezo yako nitakueleza hili nikiwa najibu maelezo yako hapa chini....

2;Mfano wako pia siyo sahihi na hili linaendelea kuonesha shida kwenye tafakari yako..

Kujifunza jambo ili ulielewe siyo sawa na kujifunza ili ulifanye.Kinachotofautisha hayo mawili ni dhumuni la kujifunza na sentensi yako ya pili inakataza dhumuni la kujifunza jambo ili ulifanye na siyo kwamba unakatazwa kujifunza jambo kwa ujumla wakeHii ndiyo tofauti iliyoko kwenye mfano wako...

Wewe ulichokisema ni tofauti na hiki.Nakubali kwamba ukikagua msingi wa kitu unaweza kujia tatizo la kitu hicho lakini hili linategemea na muundo wa hoja na muktadha mzima wa jambo lenyewe...

Kama jambo ni uongo kwa ujumla wake itakuiwa sahihi kurejea misingi yake lakini kama siyo uongo lote misingi haiwezi kukusaidia chochote,hapa rejea swali langu kwako kama unaamini [sijatumia neno amini kwa bahati mbaya] sayansi yote ni uongo au inadanganya kwenye baadhi ya maeneo tu....
2.Pili kuona kwako kauli zangu kama zinakinzana,lazima uituhumu elimu yako kuwa haina uwezo kung'amua mawazo yangu au hoja nilizo zihudhurisha hapo juu.
Hapana,jambo kutokueleweka linakuwa na mambo mawili...

1;Mtoa maelezo kuhusu jambo haeleweki
2;Anayesikiliza maelezo hana uwezo wa kuelewa

Hapa ninachokiona mimi ni tatizo la kwanza na linaongezewa nguvu na kauli yako ya kudhani moja kwa moja kuwa mimi ndiye mqwenye tatizo na siyo wewe.Nasema hivi kwasababu mtu yoyote mwenye tafakari hawezi kujihesabia haki kwanza isipokuwa anaweka nafasi ya kukosolewa [room of doubt] kwasababu anajua uwezekano wa yeye kutokuwa sahihi upo....

Wewe hujafanya hivi,unanirushia tu tuhuma japokuwa nakuonesha mara nyingi tu namna unavyokosea kwenye maelezo yako bila wewe kuonesha ni namna ipi hukosei....

Jaribu kuangalia upya kiongozi...
 
Kiongozi kamwe huwezi kuukataa ukweli huo kama kweli wewe ni mtu wa elimu.Hoja yako msingi wake ni wa sayansi ndio maana pale ulipo anza kuleta stori za Kuiper belt na nadharia zake.Ndio maana kuna jamaa mmoja alikuuliza swali moja la msingi sana juu ya maelezo,akionyesha ya kuwa maelezo yako hayajaonyesha uwepo wa Mola aliyeumba,yaani kuhusu hizi ngano mbona Mola haonekani nafasi yake.Sasa unapotaka kukanusha hoja yako na kukataa ya kuwa haija mili kisayansi,basi twambie hoja yako msingi wake ni upi.Ila kaa ukijua hoja yako msingi wake ni sayansi.

Nimezisoma sana hoja mzee,ndio maana nikaamua kukujibu,bali nimezielewa sana.
Ndiyo maana nakuambia kuwa hujaelewa....

Base ya hoja yangu siyo sayansi pekee na ndiyo maana nimemtaja huyo mama wa ki-Japan anayetoka familia ya kifalme,sijui ni kwa vipi unashindwa kuelewa mambo rahisi kama haya....

Unapotaka kuleta ishu ya Mola ndiyo unazidi kuingia machakani kabisa.Unataka nimtaje hapo kwasababu ipi haswa? Yaani unaweza kujadili kuhusu uwepo wa vyura wenye macho 20 kwenye mapango ya Amboni na wapo watu waliowaona vyura hao halafu unamtaja Mola kwa misingi ipi?

Kama nilikuwa nazungumzia chanzo cha uwepo wa Aliens hapo sawa ningetakiwa kuonesha kwamba base ya hoja zangu ni uwepo wa Mungu au kinyume chake,lakini nazungumzia uwepo wa viumbe ambavyo kuna watu wamewaona,sasa hapo unataka nitaje/nimtaje Mungu kwa misingi ipi?

Hii ni shida sana....
 
nashindwa kusema kama ni kweli ama ni uongo!,lkn nikiangalia mazingira ndio naweza sema huenda kukawa na viumbe wengine zaidi yetu,sidhani kama hizo nyota zipo angani kama mapambo tu.. ila uhakika wa kusema "ndio" kuna viumbe wengine nje ya dunia hilo ndilo nalositia!.
Ktk upande wa pili kama kuna watu wanatambua kuna alien hlf wanaficha lzm tuwaangalie ktk jicho la ulakini either wana yao ajenda 1.yakutawala
hili ndilo limebeba dhana kuu ya lengo lao ama ktk ukweli au udanganyifu!.

chengine kama watu hao wanashirikiana na alien ili kuangamiza wengine basi watakuwa wamepotoka either kwa kudanganywa ama kuambiwa ukweli!
inaniwia vigumu kusema kwamba sayari hii ilikuwa ni ya alien! na kwa kusema hivyo kutakuwa kumeharibu historia mbalimbali zinazoaminika kama ndio mwanzo wa maisha ktk dunia..

kipi kiliwaondosha hao alien hapa duniani..?
na kipi kinawarudisha hao alien hapa duniani..?
wapi mwanadamu na viumbe wa hapa duniani chanzo chake..?
 
Nilikuuliza kwamba,kwako wewe sayansi ni uongo yote au kuna mambo inasema kweli?

Sijaona mahali umejibu hili swali....

1;Siyo kweli kuwa napaswa kuituhumu akili yangu kwasababu tu ya kutoyaelewa maelezo yako nitakueleza hili nikiwa najibu maelezo yako hapa chini....

2;Mfano wako pia siyo sahihi na hili linaendelea kuonesha shida kwenye tafakari yako..

Kujifunza jambo ili ulielewe siyo sawa na kujifunza ili ulifanye.Kinachotofautisha hayo mawili ni dhumuni la kujifunza na sentensi yako ya pili inakataza dhumuni la kujifunza jambo ili ulifanye na siyo kwamba unakatazwa kujifunza jambo kwa ujumla wakeHii ndiyo tofauti iliyoko kwenye mfano wako...

Wewe ulichokisema ni tofauti na hiki.Nakubali kwamba ukikagua msingi wa kitu unaweza kujia tatizo la kitu hicho lakini hili linategemea na muundo wa hoja na muktadha mzima wa jambo lenyewe...

Kama jambo ni uongo kwa ujumla wake itakuiwa sahihi kurejea misingi yake lakini kama siyo uongo lote misingi haiwezi kukusaidia chochote,hapa rejea swali langu kwako kama unaamini [sijatumia neno amini kwa bahati mbaya] sayansi yote ni uongo au inadanganya kwenye baadhi ya maeneo tu....

Hapana,jambo kutokueleweka linakuwa na mambo mawili...

1;Mtoa maelezo kuhusu jambo haeleweki
2;Anayesikiliza maelezo hana uwezo wa kuelewa

Hapa ninachokiona mimi ni tatizo la kwanza na linaongezewa nguvu na kauli yako ya kudhani moja kwa moja kuwa mimi ndiye mqwenye tatizo na siyo wewe.Nasema hivi kwasababu mtu yoyote mwenye tafakari hawezi kujihesabia haki kwanza isipokuwa anaweka nafasi ya kukosolewa [room of doubt] kwasababu anajua uwezekano wa yeye kutokuwa sahihi upo....

Wewe hujafanya hivi,unanirushia tu tuhuma japokuwa nakuonesha mara nyingi tu namna unavyokosea kwenye maelezo yako bila wewe kuonesha ni namna ipi hukosei....

Jaribu kuangalia upya kiongozi...
Sasa kiongozi kama umeshindwa kuona usawa wa hizo kauli mbili.Unazidi kunipa mashaka na kunifanya nitoke kifua mbele kwa wewe kushindwa kung'amua kauli hizo mbili.

Niliposema "Nilijifunza shari ili niijue nisifanyeshari" na kauli "Haifai kujifunza shari".Hapa ulitakiwa kwanza ujue nini maana ya shari,pili kwanini sitakiwi kujifunza shari na kwanini nilijifunza shari ili nisiifanye shari.Kauli zote mbili zime mili katika kuelewa jambo.Kitu ambacho wewe umekitoa katika kauli moja.

Kiongozi naposema akili haina uwezo wa kung'amua haya ninayo yasema nimemaanisha hivyo.
 
Ndiyo maana nakuambia kuwa hujaelewa....

Base ya hoja yangu siyo sayansi pekee na ndiyo maana nimemtaja huyo mama wa ki-Japan anayetoka familia ya kifalme,sijui ni kwa vipi unashindwa kuelewa mambo rahisi kama haya....

Unapotaka kuleta ishu ya Mola ndiyo unazidi kuingia machakani kabisa.Unataka nimtaje hapo kwasababu ipi haswa? Yaani unaweza kujadili kuhusu uwepo wa vyura wenye macho 20 kwenye mapango ya Amboni na wapo watu waliowaona vyura hao halafu unamtaja Mola kwa misingi ipi?

Kama nilikuwa nazungumzia chanzo cha uwepo wa Aliens hapo sawa ningetakiwa kuonesha kwamba base ya hoja zangu ni uwepo wa Mungu au kinyume chake,lakini nazungumzia uwepo wa viumbe ambavyo kuna watu wamewaona,sasa hapo unataka nitaje/nimtaje Mungu kwa misingi ipi?

Hii ni shida sana....
Hilo ndio tatizo kubwa uliokuwa nalo.Mzee mambo ya kiulimwengu na yasiyokuwa hayo huwezi kuyajadili bila kuzungumzia uwepo wa yule alieviweka kutafakari kwa mtindo huo ni kutafakari kwa kitoto na ndio huko kulikowafanya watu wawe wazito wakufikiri kuliko tukuka.
 
Sasa kiongozi kama umeshindwa kuona usawa wa hizo kauli mbili.Unazidi kunipa mashaka na kunifanya nitoke kifua mbele kwa wewe kushindwa kung'amua kauli hizo mbili.

Niliposema "Nilijifunza shari ili niijue nisifanyeshari" na kauli "Haifai kujifunza shari".Hapa ulitakiwa kwanza ujue nini maana ya shari,pili kwanini sitakiwi kujifunza shari na kwanini nilijifunza shari ili nisiifanye shari.Kauli zote mbili zime mili katika kuelewa jambo.Kitu ambacho wewe umekitoa katika kauli moja.

Kiongozi naposema akili haina uwezo wa kung'amua haya ninayo yasema nimemaanisha hivyo.
hivi ulielewa utofauti niliouzungumzia kwenye hayo maelezo ni upi?

Mkuu inaonekana kama tunazungushana kwenye jambo ambalo hatuwezi kuelewana na shida kubwa ni namna ya kufikiri iliyopo hapa....

Na hilo ndilo tatizo kubwa....
 
Hilo ndio tatizo kubwa uliokuwa nalo.Mzee mambo ya kiulimwengu na yasiyokuwa hayo huwezi kuyajadili bila kuzungumzia uwepo wa yule alieviweka kutafakari kwa mtindo huo ni kutafakari kwa kitoto na ndio huko kulikowafanya watu wawe wazito wakufikiri kuliko tukuka.
Unafahamu maana ya neno muktadha?

Maana hili ndilo tatizo lako kubwa mkuu...
 
Back
Top Bottom