Kuiper Belt: Behind the certain

Mkuu wangu Eiyer Saluti.

H
izi habari zamani sana Babu yangu amewahi nisimulia kwamba miaka mingi nyuma, wamerekani wamewahi waokota binadamu wawili wasio wa kawaida, wanaoaminika kutoka sayari nyingine, walipojaribu kuwakamata mmoja akakimbia kwa kupaa kwenye kitu kama kisosa kikubwa hivi na mwingine wakamkamata. ss inasemekana huyu waliemkamata wakagundua ana akili isiyo ya kawaida, hivyo basi inaaminika mpk leo huyo kiumbe yupo na wanamtumia katika mambo ya tekinolojia. umewahi kusikia hii?? na hapo eneo linaitwa Area 51 unalizungumziaje mkuu, nini haswa area 51?

Humbly With Regards.
 
Mkuu wangu Eiyer Saluti.

H
izi habari zamani sana Babu yangu amewahi nisimulia kwamba miaka mingi nyuma, wamerekani wamewahi waokota binadamu wawili wasio wa kawaida, wanaoaminika kutoka sayari nyingine, walipojaribu kuwakamata mmoja akakimbia kwa kupaa kwenye kitu kama kisosa kikubwa hivi na mwingine wakamkamata. ss inasemekana huyu waliemkamata wakagundua ana akili isiyo ya kawaida, hivyo basi inaaminika mpk leo huyo kiumbe yupo na wanamtumia katika mambo ya tekinolojia. umewahi kusikia hii?? na hapo eneo linaitwa Area 51 unalizungumziaje mkuu, nini haswa area 51?

Humbly With Regards.
Mkuu

Habari za Wazungu kumkamata Aliens huwa ni uongo tu,huwezi kukikamata kiumbe ambacho unakinadi kuwa kina uwezo mikubwa kuliko wewe,hilo haliwezekani kabisa...

Kinachoendelea ni kwamba hawa viumbe wao wenyewe wameamua kushirikiana na binadamu katika maeneo fulani tu kwa madhumuni maalum lakini siyo kwamba eti wamewakamata...

Kuhusu Area 51 ni kwamba hiyo ni mada inayojitegemea mkuu,huwezi kuelezea eneo hilo haraka haraka namna hii.Ni jambo ambalo linahitaji utafiti mzuri na mkubwa zaidi mkuu...

Tuombe uzima iko siku tutalijadili hapa...
 
Hii ni sayansi Kali sana maana kuupata ukweli sometimes mpaka ufanye assumption,, lakini hao wanaotambua unachowaza wakija Africa watuua sana,,
 
binafsi yangu siwezi kudhibitisha uwepo WA Hawa viumbe na PIA siwezi kukataa kama hawapo....japo theory Ni nyingi kuwahusu.thread Ni nzuri Sana ILA unataka upembuzi yakinifu kuendana na vielelezo...my take,I think hizi Ni Hoax Tu japo sina sababu maalumu ya kupinga Hilo.naamin humu wapo wajuzi zaidi WA mambo watakuja kuweka mambo sawa..asante Sana mkuu Eiyer
 
Mkuu Eiyer kwanza lazima nikuambie ukweli, mimi ni mmoja kati ya watu ninao kuheshimu sana, na kuheshimu mawazo yako, huwa ninapoona bandiko lako popote lazima nilisome kwa umakini maana najua lazima kutakua na nondo. Salute mkuu.
sasa tuje kwenye mada.

nimesoma hili bandiko lako kwa umakini, ila kuna vitu vinaonekana vinapingana vyenyewe au laba mimi kuna mahali unaniacha.

kwanza wakati unaelezea hiyo kuiper belt, kwa maelezo yako ni kwamba ni "vimawe ambavyo ni kama barafu au vinauwezekano wa kuwa na barafu" kwa jinsi unavyosema ni kitu ambavyo hata hao wataalamu hawana ukakika navyo, hawajui kama ni barafu kabisa au vina hali ya ubarafu kwa asilimia fulani. na pia wanahisi/wanadhani kuwa kuna uwezekano wa kuwa na uhai. Hawana uhakika sana labda pengine hawajawahi kufika au kukaribia eneo hilo.

Lakini kitu cha kustaajabisha sana ni kuwa wameweza kueleza kwa ufasaha sana vitu vinavyoishi ndani ya hiyo kuiper belt, hadi kufikia ku-categorize aina ya hao aliens na tabia zao hadi mission zao na jinsi wanavyotuchukulia sisi.
kila aina na mipango iliyonayo kuhusu binadamu, as if kama hao wataalamu walikaa meza moja na hao aliens na kupia story.

Sasa inakua vigumu kidogo mtu kuelewa kwa kweli maana kama huo ukanda tu bado hawaujui kwa asilimia mia unawezaje kujua kilichopo ndani yake na kukielezea kwa ufasaha namna hiyo.

kwa mafano mtu ameona nyumba kwa mbali na kwa sababu ya umbali hawezi kujua rangi ya bati la hiyo nyumba kuwa ni blue au kijani, lakini hapo hapo anakuelezea kwa ufasaha kuhusu mazingira ya ndani ya nyumba jinsi yalivyo.

inakua na ukakasi sana kuelewa
 
Nimekua observer wa hii thread. Nimetambua jambo. Eiyer una upeo mkubwa na unajibu kwa facts na hukurupuki. Wengi humu hamtaki kushughulisha fikra zenu na mnaamini kile wengi wanachofikiri ndiyo ukweli. Kuna m/falsafa(nimemsahau jina) aliwahi kusema, mambo mengi yanayoendelea duniani katika nyanja tofauti tofauti ukweli wake ni tofauti na wakazi wa duniani wanavyoaminishwa.
 
Back
Top Bottom