Kuiper Belt: Behind the certain

Man you cant beat the bold! That guy is special. He was born to do do what he does. Baki msomaji kama mimi. Sio lazima wote tuandike. Makala ndeeefuu hadi usingizi. Acha kujaza server kwa nonsensical threads
Wakati mwingine ni aibu sana hata kuangalia ulichokiandika na naimani ww huna tofauti na wale wafuasi wa Mange istagram ambao kazi yao ni kusifia tu bila ya kuhoji wala kuuliza ukweli na uhakika wa taarifa anazowapatia. lakini akili na ufahamu wao huko kwa mtu aliye zaidi ya 13987 km sawa na 8691 miles kutoka pale walipo
 
Kuna sifa za walizovikwa hao aliens zinatatanisha kukubaliana kwamba uwepo wao ni wa kuogofya kiasi hicho.

1. Ujio wao kutoka sehemu fulani na si wenyeji wa hapa hapa duniani.

Ukweli ni kwamba kadri teknolojia inavyokua ndivyo tunaweza kugundua vitu. Vitu vinavyotoka huko kwenye ulimwengu huwa vikitua katika uso wa dunia kuna havina mwendelezo mf. Vimondo. Kwamba wao wameweza kuishi hapa na sisi hatuna uwezo wa kuishi huko, kama nia yao kutumaliza wangetumaliza kirahisi sana labda kama lengo lao si hilo.
Kwangu inasomeka vizuri kama wao ni wenyeji wa hapa ila sisi hatukuwa tunafahamu uwepo wao. Mf. Awali hatukujua uwepo wa virus kabla ya hadubini. Na vyote viishivyo duniani tuvionavyo kwa macho na tusivyoviona vinapambana na mazingira yao ikiwa pamoja na kujitengenezea mazuri viendelee kuwepo kama wafanyavyo nyumbu kuzaa wakati mmoja.

2. Uwezo wao kulinganisha na sisi.

Duniani hakuna vitu tata hasa vilivyo vya asili vilinganavyo sawia. Hata mawe yanatofautiana. Mimi binafsi kwa ushahidi wa kibaiologia na kijamii mimi ni binadamu. Lakini nimeshuhudia watu weusi binadamu wenye mazingira kama yangu tukitofautiana sana ufahamu, kumbukumbu na hata utendaji. Pengine katika kundi la watu wenye uwezo wa chini sana naweza nisionekane wa kawaida. Hivi ndivyo niwaonavyo hao kina einstein na wengine. Sioni tofauti ya kijamii na kibaiolojia kuwatenga na binadamu wengine nnaowashangaa inakuwaje wanashindwa kung'amua vitu rahisi sana. Ni asili ya viumbe kutofautiana, hata mapacha wafananao huwa wana tofauti zao.

Kwangu ni rahisi kukubali kuna wanadamu wanaofanya vitu vikubwa kuliko kuwanasabisha na aliens.

3. Usiri, mafumbo, kutawala

Ukweli ni kwamba wanadamu tuna ubinafsi au tuna asili ya kujipenda na kujipendelea.
Tunachagua kila siku nini kukiweka wazi kwa nani tukiangalia usalama wa maslahi yetu. Mf. Kuna mambo sijawahi mwambia hata mtu mmoja. Kuna mambo nimewahi kuwaeleza watu fulani kwa sababu fulani. Kuna mambo nayaweza kuyaeleza kwa watu wengi zaidi.

Haya ndiyo yanafanya dunia ijae kila aina ya fujo. Mambo ya kufichana fichana. Unaweza kuona athari zake katika maingiliano ya shughuli zetu za kila siku na mahusiano.

Tukirudi kwenye mada, kwamba hao aliens wapo wanajulikana na baadhi ya wanadamu ila wameficha si jambo la kujiuliza kwa nini wafiche, ni maslahi yao tu kama vikundi au kikundi. Na kutawala ni ujanja wa kuwahi ili kufanikisha yale uwazayo muhimu sana kufikia maslahi yako ya kimtazamo. Sitashangaa kusikia binadamu wamekodi aliens kuwatumia kama wapo. Kama ambavyo wanatumia bacteria au madawa ya kulevya kwa faida zao.

Hitimisho;
Sifa za hao alien kuna binadamu wengi wanaweza bila kuwa na uhusiano na hao alien.

Na kama hao aliens wapo kwa sifa hizo si wa kuogofya kama inavyosemekana au la hatujawapatia kuwasoma vyema.

Mpaka sasa katika dunia hii binadamu amedhihirika ni hatari zaidi kwa ustawi wa viumbe wengine wanaojulikana katika uso wa dunia. Kama alien wameshtukia dili kutushughulikia sisi tu watakuwa wamefanya kazi kubwa.
 
Man you cant beat the bold! That guy is special. He was born to do do what he does. Baki msomaji kama mimi. Sio lazima wote tuandike. Makala ndeeefuu hadi usingizi. Acha kujaza server kwa nonsensical threads

Ivi Mungu kweli alikumbuka kuweka ubongo ndani ya fuvu lako au ndio nyinyi mliletwa ili mje kua mifano na ili tuwe na ma-Dr na vitengo vya afya ya akili..?
Nakushauri jaribu kupitia thread za kitambo umu utawakuta watu ambao leo haujui wako wapi walikua wabobezi wa hizi kazi ila walionekana kua juniors itakua hiki kizazi kipya naaamini haumfahamu Eiyer na umetawaliwa msukumo wa timu x na y,JF ni forum huru kwa kupeana na kupata habari nikupe hongera kwa kuchezea umeme.
 
umeandka vzuri bro nmeshawah kusoma nakala flan la NASA wakikanusha uwepo wa viumbe wakati huohuo baadh ya mashuhuda kuptia majarida balmbal wameelezea uwepo wa aliens ila umechambua vizur sana sana nmependa na endelea kutupa uzi za kigeographia coz mm n mtaalam wa anga meteorologist so napenda hiz nakala na uchunguzi.
 
Hongera mkuu Eiyer kwa makala nyingine nzuri na ya kusisimua.
Hawa aliens unaowaongelea wana uhusiano wa moja kwa moja na wanefili uliokuwa ukiwasimulia kwenye makala zako za nyuma? Je,kama hawahusiani ajenda zao,utendaji wao unakinzana na shughuli za Mungu juu ya mwanadamu? Je,inawezekana hawa viumbe ni tokeo la malaika waasi? La mwisho na la msingi kabisa,naomba uwe unanitag kwenye posti zako maana zinanivutia.
 
Kwa ninavyoona USA ina mipango ya kiovu juu ya binadamu, wanachofanya ni kutufanya tuamini kuwa Aliens ni viumbe toka space ili vikianza kuleta uharibifu tukose cha kulalamikia. Mi nionavyo USA imelenga nchi za kimaskini hasa huku Africa ambapo teknolojia ni duni waweze kutufanyia ukatili wa kupora mali zetu kwa kutumia "Robots" afu waseme aliens. Hakuna mambo ya viumbe, sijui aliens, zote hizo ni hila za wazungu, mara utasikia Aliens kaonekana Zimbabwe kabeba Ng'ombe! Kumbe ni roboti linaloendeshwa na Mitambo. Tujichunge sana wakati ndo huu wa vita.
 
Kwanini unaweweseka sana?

Unataka kuonesha nini kwenye post zako za ajabu kwenye thread za watu?

Siyo vyema kumjadili mtu kwenye thread za watu,jaribu kufanya mambo ya maana na haya uachane nayo..
Wakati mwingine naanza kufikiria vibaya kidogo na kwenda mbal..najaribu kuwaza kwamba kwani huku JF kuna watu wamechaguliwa kua wao tuu ndio wakuandika kitu fulan??? Alafu huyu anaesema kazi hii muachie fulan....ni kwel ni third party ama ni huyo huyo ambae anajidai ni shabiki kuongeza kick??
 
Hao alliens wanaonekana nchi za mbele tu huko?

Viongozi mashuhuri duniani wamewaona ila viongozi wa Afrika sijaona aliekutana nao!

Umesema kuna kundi la binadamu wachache wenye nia ovu Juu ya wengi. Yes ni kikundi cha watu wachache..waoga na makatili kupindukia.

Wanaua watu kupitia mifumo ya afya, mazingira(global warming), uchumi, vita etc..sasa wametumia njia zote na bullet yao ya mwisho ni hiyo ya alliens baada ya ile ya secret society kufeli.

Hao aliens, kama wapo ni viumbe tu wa kutengeneza maabara through cross breeding. Kama walivyo robots.

Tunajua kikundi hicho cha wachache kinakazana kufanya depopulation, psyco operations, mind control hadi tunapoteza WILL power na kuanza kuogopa vitu vya ajabu.

Na NWO ndio inaelekea kufeli sasa .
 
Kwa kweli mleta mada amenifanya nifikiri nje ya box.

Hawa viumbe kwa maelezo ya mleta mada na utafiti alioeleza vizuri kuwa enanyika na unaendelelea kufanyika bila aha hwa viumbe wapo.

Mimi nakubaliana na mleta mada kuwa hawa viumbe wanaishi humu dunia ni na huenda walikuwepo enzi na enzi.

Hebu tujiulize maswali yafuatayo:
Inakuwaje binadamu wa kawaida anakula vipande vya chupa na misumari?

Inakuwaje binadamu wa kawaida anakunywa petroli kama maji?

Inakuwaje binadamu wa kawaida anajisokota kama nyoka na kujigeuza utadhani hana mifupa?

Kuna maeneo ambayo yana nyayo juu ya miamba zinazofanana na za binadamu. Hii inathibitisha kuwa kuna viumbe waliishi karne nyingi duniani!

Je ile michoro kwenye mapango ya amboni ilibuniwa na nani na ni kwa nini inaleta mfanano na teknolojia ya leo?

Je ,nani alijenga mapiramidi kule misri?
Wajenzi wa mipiramidi walinyanyuaje tofali lenye uzito wa tani 150?

Mazingaumbwe na uchawi vinatokana na nini!?
Ni viumbe gani wanaosimamia utendaji na matokeo ya uchawi na mazingaumbwe?

Ni viumbe gani vinavyosimamia nguvu ya laana?
Mfano mtu amempiga mama yake halafu mama yake akamlaani inakuaje laana inampata?



Kuna maswali mengi sana yakujiuliza ambayo bila shaka yoyote kuna viumbe visivyoonekana vinavyocheza na akili ya binadamu au kujifanya binadamu ili vifanye baadhia ya mambo humu duniani.

Pia nikitafakari na kurejea kwenye imani za dini naona kuwa hawa viumbe wapo na ni hatari kwa binadamu mida wote ndio maana wale watu wa kiroho wanatuambia kuwa kuna vita kubwa sana katika ulimwengu wa roho. Binadamu inabidi amombe sana rehema za mwenyezi Mungu.
 
Kiukweli kama Mungu alituumba na aliumba ulimwengu wote, alafu akatuumba binadamu peke yetu tu na hakuna binadamu au viumbe wengine sehemu nyingine ya ulimwengu, basi Mungu atakua alifanya kazi chini ya kiwango.

Haiwezekani ulimwengu wote huu tuwe peke yetu tu.It doesn't make sense
 
Binafsi ninaamini ktk uumbaji wa aina mbili, vinavyoonekana na visivyoonekana.

Yaani namaanisha ktk Roho na Mwili. Katika hivi vyote, roho vinakuwa powerful kuliko mwili.

Ninaamini Mungu kaumba vinavyoonekana au kuhisika kama Binadamu, wanyama, upepo n.k Ninaamini pia uumbaji wa Malaika, roho chafu n.k maana hizo zote ni Mungu aliumbaga huko zamani.

Ikiwa hao Aliens mnawaweka ktk kundi la Malaika wale wachafu walioasi basi nnaweza nikawa na wewe kwa 100% lakini sio mbali na hapo.

Ninaamini sn ktk maandiko matakatifu na hizi zama ni zama ambazo zinajadili sn uweza wa Mungu, mara hayupo, mara ametokea wapi, mara amefanya hiki n.k. Tunajadili kumhusu Mungu tunaona kama tunajadili wazazi wetu vile
 
hapa comment haziruhusiwi au ?? maana kwa tafiti na mambo fikirishi yaliyomo kwenye hii thread na jukwaa iliyopo ni imani yangu kubwa sana isingewezekana kufika siku mbili bila comment yoyote
There must be something wrong..

My take :
Naanza kuona yaliyotabiriwa yanatokea kwakua sisi kwenye imani ambayo naamini tumeambiwa nyakati za mwisho vitakuja viumbe vya ajabu ambavyo vina uwezo mkubwa kuliko binaadam na vitafanya uharibifu mkubwa na hivi viumbe vyenyewe nahisi ni hawa aliens ambao unawazungumza mkuu

amsr
Lete hilo andiko Mkuu, Biblia inasema usizidishe wala kupunguza maneno yake. Nipe reference kwa hayo uliyoseama.
 
Jamaa anasemaje kuhusu hao viumbe mkuu?
Kifupi ni kuwa kuna chombo kilianguka huko milimani uswis,ambapo watu 11 watalii wa kizungu walikiishuhudia na Mmoja kupiga picha,baada ya muda kiliondolewa hicho chombo kwa siri kubwa lkn ktk hicho chombo kulikua na viumbe hao watatu ila walikuta wawili mmoja kaenda wapi yukp wapi haijulikani,mchezo unaanzia hapo na wale mashuhuuda wote 11 wanatakiwa kuuwawa haraka mmno kabla hawajamhadithia MTU.... In SIRI inawezekana wapo kweli hapa duniani unaweza kukitafuta mie ninacho
 
Man you cant beat the bold! That guy is special. He was born to do do what he does. Baki msomaji kama mimi. Sio lazima wote tuandike. Makala ndeeefuu hadi usingizi. Acha kujaza server kwa nonsensical threads
Hivi hiki ulichokiandika hapa ulikusudia au hiyo post ilipotea njia kwa bahati mbaya??
 
Back
Top Bottom