Kuiper Belt: Behind the certain

Niliiona halafu ghafla ikapotea nikajiuliza kulikoni?ahsante Eiyer huu Uzi unanirudisha nyuma kdg ila ktk upande ule wa akina Pindar na wenzake,je Pindar na hawa aliens wako pamoja
Mkuu,humu duniani kuna mambo mengi kweli kweli ambayo hayasemwi na ukiyatazama kwa jicho la tatu utaweza kuunganisha dots na ukapata kitu...

Nitakuwa naandika haya masuala kila nikipata wasaa ili kila mmoja aweze kuunganisha dots yeye mwenyewe na kupata jibu....

Mkuu wewe kuwa mpole kwa sasa na utakuwa unaunganisha mwenyewe tu....
 
Mkuu,humu duniani kuna mambo mengi kweli kweli ambayo hayasemwi na ukiyatazama kwa jicho la tatu utaweza kuunganisha dots na ukapata kitu...

Nitakuwa naandika haya masuala kila nikipata wasaa ili kila mmoja aweze kuunganisha dots yeye mwenyewe na kupata jibu....

Mkuu wewe kuwa mpole kwa sasa na utakuwa unaunganisha mwenyewe tu....
Tuko pamoja mkuu
 
Kwanza me naamini alien are myth hivyo hakuna MTU aliyemuona hata baadhi ya picha zako ni za kutengenezwa hakuna exactly alien picture so there is no proof of their existence
 
Mkuu,humu duniani kuna mambo mengi kweli kweli ambayo hayasemwi na ukiyatazama kwa jicho la tatu utaweza kuunganisha dots na ukapata kitu...

Nitakuwa naandika haya masuala kila nikipata wasaa ili kila mmoja aweze kuunganisha dots yeye mwenyewe na kupata jibu....

Mkuu wewe kuwa mpole kwa sasa na utakuwa unaunganisha mwenyewe tu....
mkuu nijumlishe kwenye kumbukumbu kila unapotoa bandiko hapa kwamaana mimi ni muumini sana wa haya mambo. asante sana
 
grey-882x750.jpg
 
Man you cant beat the bold! That guy is special. He was born to do do what he does. Baki msomaji kama mimi. Sio lazima wote tuandike. Makala ndeeefuu hadi usingizi. Acha kujaza server kwa nonsensical threads
kwani nani kasema mkuu eiyer anashindana na the bold? Ni ukweli ambao uko wazi kua the bold ni mzuri kwenye fasihi simulizi kama sio andishi ila kilakitu kina mahala pake mkuu huwezi kua na mkeo ukaanza kuzungumzia habari za mchepuko ingawa kwa marafiki zako ni stori poa,ila hata hivo kwani umeshikiwa bunduki usome post ya mkuu ya eiyer? kama unaona the bold ndie anaefaa kuandika makala ndefu peke yake basi subiri aandike halafu utasoma.

amsr
 
Mkuu

Hii thread ilikaa huko mafichoni kwa siku karibia tano na sijui mods walikuwa wanaifanyia nini lakini nadhani leo au usiku wa jana ndiyo wameiachia...

Karibu sana mkuu tufikirishe ubongo wetu....
kwahiyo nayo ilitekwa ?? hahaha
lakini afadhali imerudishwa bila ya yale mabango na hashtag za bringback...

asante sana ila mada kama hizi hua zinahitaji akili iliyo huru ndio mtaenda sawa otherwise mapovu bila sabuni...

pamoja sana mkuu hua nafuatilia mabandiko yako kimyakimya ila leo nimejishindia kutoa volume na nahisi ushakutana sana likes zangu,cheers boss.

amsr
 
Imeanza vizuuuri, lakini baadaye zikaanzwa kuingizwa story za "wataalam", wataalam wa maneno ambao sifa yao ni kuzusha conspiracies ambazo hazina ushahidi wa kisayansi wala mashiko.
 
Kimsingi ninavyojua ni kwamba hawa Aliens wapo hapa duniani na wamekuwa wakiishi na binadamu tangu enzi hizo na najua wanahusika na mambo mengi anayokutana nayo binadamu....

Binadamu yupo siyo kwa sababu ya bahati mbaya mkuu,kuna nguvu inayosimamia uwepo wake na kuhakikisha anaendelea kuwepo...
Mkuu twende kwa hoja na ushahidi, jibu maswali hapo chini:

1. Umesema aliens wapo duniani, je wanaishi eneo gani, wanakula nini, wanavaa nini, wanazaliana? na wanafanya shughuli gani? Ikiwezekana weka picha yao wakiwa duniani.

2. Je, hao aliens waliopo duniani wanatumia njia gani kuwasiliana na binadamu?

3. Hao watafiti wamejuaje aliens wanataka kumuangamiza binadamu?

Nitarudi...
 
kwahiyo nayo ilitekwa ?? hahaha
lakini afadhali imerudishwa bila ya yale mabango na hashtag za bringback...

asante sana ila mada kama hizi hua zinahitaji akili iliyo huru ndio mtaenda sawa otherwise mapovu bila sabuni...

pamoja sana mkuu hua nafuatilia mabandiko yako kimyakimya ila leo nimejishindia kutoa volume na nahisi ushakutana sana likes zangu,cheers boss.

amsr
Hahahahaa....

Eti ilitekwa....

Ni kweli mkuu hii inahitaji akili iliyohuru kuitafakari,taratibu tutakuwa tunaelewa tu mkuu....

Pamoja sana mkuu,wewe ni miongoni wa watu ninaokutana na pongezi [likes] kibao na kimsingi ni faraja tosha kabisa...

Tupo pamoja mkuu....
 
Kwanza me naamini alien are myth hivyo hakuna MTU aliyemuona hata baadhi ya picha zako ni za kutengenezwa hakuna exactly alien picture so there is no proof of their existence
Kila mmoja ana haki ya kuamini chochote mkuu....

Unaweza kuamini kuwa nyekundu ni kijani na hakuna atakayeweza kukuhoji...

Labda hapo uliposema kuwa "hakuna aliyewahi kumuona Alien" ndipo penye jambo kubwa na la kukuuliza...

Umewafanyia utafiti watu wote wa duniani hadi kufikia kujua kuwa "watu wote" hawajaona Aliens?
 
Imeanza vizuuuri, lakini baadaye zikaanzwa kuingizwa story za "wataalam", wataalam wa maneno ambao sifa yao ni kuzusha conspiracies ambazo hazina ushahidi wa kisayansi wala mashiko.
Hao hao wataalam ndiyo wanategemewa kwenye sayansi kuleta tafiti ambazo zitasaidia maendeleo ya kisayansi,sasa nashindwa kukuelewa unaposema kwamba hao wataalamu ndiyo wanaoleta mambo yasiyokuwa na ushahidi wa kisayansi.....

Kivipi?
 
Mkuu twende kwa hoja na ushahidi, jibu maswali hapo chini:

1. Umesema aliens wapo duniani, je wanaishi eneo gani, wanakula nini, wanavaa nini, wanazaliana? na wanafanya shughuli gani? Ikiwezekana weka picha yao wakiwa duniani.
1;Kwa mujibu wa taarifa nilizonazo ni kwamba Aliens wanaishi kwenye underground bases [D.U.M.Bs] zilizoko maeneo tofauto tofauti chini ya ardhi....

2;Sijui chochote kuhusu kula yao,lakini kufikiria kuwa kuna "kula" kwa kila kiumbe ni dhana potofu mkuu...

3;Ishu ya kuvaa ni kama kula tu,unadhani kila kiumbe kinahitaji kuvaa kwanini? Hebu fikiria tu uwe hujawahi kumuona Tembo halafu ukakutana na mtu akakupa taarifa kuwa kuna mnyama mkubwa mwenye sifa kama za Tembo halafu wewe kwasababu hujawahi kumuona ukaanza kuingiwa na wasi wasi halafu ukamuuliza kuhusu kuvaa kwao,swali lako litakuwa na mantiki kweli?

Swali lako halina mantiki mkuu....

4;Sijui ni namna ipi wanayotumia kuongezeka,lakini,kama maswali yako mengine hili nalo ni swali linalotoka kwa mtu ambaye ana upungufu wa taarifa tu maana kama ungejua kuwa kuna viumbe havihitaji kuzaliana ili viongezeke wala usingeuliza swali hili...

5;Aliens wanachokifanya hapa duniani ni kuwasaidia binadamu katika eneo la maendeleo ya kiteknolojia ili aweze kuishi maisha rahisi zaidi lakini wana ajenda zao ambazo baadhi zimeelewa kwenye makala hii kwa sehemu....

6;Sijawahi kukutana na picha yao halisi lakini kutokuwepo kwa picha siyo sababu ya kuona ni uongo..
2. Je, hao aliens waliopo duniani wanatumia njia gani kuwasiliana na binadamu?
Namna ambayo wanaitumia ni ya kuzungumza,wana uwezo mkubwa wa kuongea ligha yoyote lakini wao kwa wao hawazungumzi isipokuwa wanawasiliana kwa kusoma mawazo ya wengine.Wanaweza kusoma mawazo ya binadamu pia lakini kwakuwa binadamu hawezi kusoma mawazo yao inabidi waongee ili kuwasiliana na binadamu....
3. Hao watafiti wamejuaje aliens wanataka kumuangamiza binadamu?
Taarifa za jambo hili ni ndogo sana lakini ni kwamba hao hao Aliens walishakutana na binadamu na kusema kwa nyakattofauti tofauti na jambo hili halisemwi ndiyo maana taarifa ni ndogo....

Tatizo ni kwamba jambo hili ni miongoni mwa mambo ambayo yanafichwa sana lakini siyo jipya maana hata binadamu wa kale walishawahi kukutana na hawa viumbe....
 
Back
Top Bottom