Kufanya masters, phd ni uoga wa maisha.

Kufanya masters, phd ni uoga wa maisha.

Kuna watu wanapenda sana maisha ya uanafunzi, utafikiri walizaliwa ili wasome.

Shule ya msingi ========= 7 years.

O-Level ========== 4 years.

A- Level =========== 2 years.

Degree ya kwanza =========3 au 4 years.

Jumla : Miaka 16 au 17.

Umekaa shuleni kwa muda wa miaka kumi na saba lakini bado hauna uwezo wa kutumia elimu na maarifa uliyo yapata shuleni kukabiliana na changamoto za maisha? Still unataka kwenda kufanya masters, miaka miwili, after masters, unataka tena PHD miaka 3, we vipi wewe?

Ukiniambia nimuelezee mtu wa namna hii kwa maneno machache , nitasema ' MUOGA WA MAISHA ". Anaogopa ugumu wa maisha, anashindwa kuzi face changamoto za maisha ( e.g ukosfu wa ajira ). Anataka aendelee kuonekana mwanafunzi ili kuutumia uanafunzi wake kama excuse ya kuwa broke. Let me tell you brother, the only excuse of being broke is to be in jail. Achana na hizo bla blah za masters na PHD, piga kazi mjomba tujenge taifa letu. GPA yenyewe ya 2.1, masters mpaka ukafanye post graduate kwanza, dah watu wanajua kuua muda. Ukomboe wakati bro, siku ya mwisho utahukumiwa kwa kosa la ku ua muda. Nyambaff, unasoma hadi PHD halafu ukimaliza unaanza kutembea kwenye ofisi za watu na bahasha za kaki.

Kuna watu wanapenda kusoma mkuu. Hata wakikuta plain paper wanaipitia pitia japokua wengi wao katika hao wanaopenda kusoma ukifatilia kwa undani utagundua unachosema ni sahihi kabisa kuwa wanaogopa maisha na hawataki kujishughulisha kwenye mambo mengine kutafuta ugali wao wa kila siku.
Wanategemea kuajiriwa kwenye taasisi kubwa duniani wapate hela kiulaini. Kuna Prof mmoja namjua pale UD nahdhani yule jamaa anafundisha basi tu. Anapiga biashara balaa na ameinvest sana kwenye real estate yuko CoET kule anaitwa Prof Mayo. Katika vitu vinavyomuudhi nadhani kwa sasa ni kushika chaki. Nasikia PhD yake Tanzania nzima ni ye na Mwandosya ndo walivuruga vuruga balaa (namaanisha kwa kufaulu kiwango cha juu)
 
Mimi ndio kwanza najiandaa kwenda ng'ambo kuchukua jiwe lingine.
 
mdau ulisahau kuanza na chekechea(Montessori /kindergarten) miaka 2- 3 , certificate mwaka 1, diploma miaka 2, Hivyo jumla kuu mpaka shahada ya kwanza ni kuanzia miaka 23+ , bila kujumuisha kama bahati nzuri unafanikiwa kupitia mchakato aliopitia "bwana Tamimu /mulugo -kuunga unga vidato kwa spagluu /ulimbo) kwani utavuna miaka kadhaa zaidi.
hakika mleta mada nakuunga mkono , tuchape kazi "kusoma mbwembwe tu cha msingi kufaulu maisha" bingo ndo mpango bila kujalisha madegree yako kichwani. e;g:ushamuona tajiri wa maana duniani prof ??
 
kula 5 mkuu,kama unataka kuwa academician au researcher it's ok kuendelea kusoma hadi elimu za juu zaidi,ila kiukweli digrii inatosha sana kukabiliana na changamoto nyingi za lyf nashangaa mijitu mingi kufuata mikumbo tu

Elimu si pesa, ni ujuzi. Wewe kama umeshindwa kaa kimya.
 
Kusoma Masters na PhD ni sehemu ya mapambano ya maisha. Kama mtu hakusumbui na wewe unaendelea na maisha yako, hakuna haja ya kuhoji kwanini anasoma sana. Kila mtu aishi maisha anayotaka na afanye anachoona kinafaa maishani ili maradi havunji sheria na hawakwazi wengine kufanya mambo yao au yale anayoyafanya yeye. Vitabu vya dini vinatuhimiza kuitafuta sana elimu
 
Kuna watu wanapenda sana maisha ya uanafunzi, utafikiri walizaliwa ili wasome.

Shule ya msingi ========= 7 years.

O-Level ========== 4 years.

A- Level =========== 2 years.

Degree ya kwanza =========3 au 4 years.

Jumla : Miaka 16 au 17.

Umekaa shuleni kwa muda wa miaka kumi na saba lakini bado hauna uwezo wa kutumia elimu na maarifa uliyo yapata shuleni kukabiliana na changamoto za maisha? Still unataka kwenda kufanya masters, miaka miwili, after masters, unataka tena PHD miaka 3, we vipi wewe?

Ukiniambia nimuelezee mtu wa namna hii kwa maneno machache , nitasema ' MUOGA WA MAISHA ". Anaogopa ugumu wa maisha, anashindwa kuzi face changamoto za maisha ( e.g ukosfu wa ajira ). Anataka aendelee kuonekana mwanafunzi ili kuutumia uanafunzi wake kama excuse ya kuwa broke. Let me tell you brother, the only excuse of being broke is to be in jail. Achana na hizo bla blah za masters na PHD, piga kazi mjomba tujenge taifa letu. GPA yenyewe ya 2.1, masters mpaka ukafanye post graduate kwanza, dah watu wanajua kuua muda. Ukomboe wakati bro, siku ya mwisho utahukumiwa kwa kosa la ku ua muda. Nyambaff, unasoma hadi PHD halafu ukimaliza unaanza kutembea kwenye ofisi za watu na bahasha za kaki.

Naunga mkono hoja 100% !mtu sio academician or researcher utashangaa linazeekea tu shule badala ya kufanya mambo mengine ya kujenga taifa!
kwa nchi kama yetu tunatakiwa tuwekeze kwenye elimu ya ufundi ili vijana waweze kujiajiri wenyewe naomba nifanye case study ya singapore ambayo techncal instition/elimu ya ujuzi ni nyingi sana hata tatizo la ajira hakuna maana wamewekeza sana kwenye elimu ya chini,ambayo sisi wa tanzania tunaikimbia technical college siku hizi hazitoi mafundi mchundo , siku hizi kila mtu anataka kuwa meneja. sasa hivi tutafurahi kuwa tuna wasomi wengi lakini baada ya miaka 10 tutakuja kulia kwa kuwa elimu ya chini hatutakuwa na wataalamu wa kutosha

kitu kingine ninachokiona kuwa siku hizi watu wengi wanasomea mkumbo hawajui malengo yao ni nini? mfano mtu ana master ya finance au MBA lakini utamkuta bado anafanya kazi za operation au technical lakini sio kwamba anaonewa ni kutokana na elimu yetu ya knowledge based badala ya competent based! ndio maana utaona multinational companies wakija tanzania yanaongozwa na CEO ambaye ana degree wakati customer care officer ana mtanzania ana MBA ya mzumbe jioni!ambayo haijabadilisha ufanisi wake

 
Elimu si pesa, ni ujuzi. Wewe kama umeshindwa kaa kimya.

kaka wengi mnaokimbilia kusoma elimu za juu zaidi wengi wenu hata hamuwi ma-academician au maresearcher, wengi mnataka vyeo tu makazini kwa kuwa elimu yenu haijawakomboa kuwa na fikra zaidi za kutoka kivingine kama kuwa wajasiriamali n.k ndo maana kwa kuwa mimi sihitaji kuwa mtumwa wa hzo shule,nilichokipata kinanitosha na kinaniwezesha kufanya chochote nachotaka kwa njia halali na maisha yanakwenda kama kawa,we kama unaona degree yako haijakukomboa hadi uwe PHD holder ndo maisha kwako yawe malaini ujue elimu yako ilikuwa fake Mkuu,samahani lakini!!
 
kama wote wakiishia digrii moja hao wa kuwafundisha hiyo degree moja watatoka wapi kama wote tukiwa na mawazo mgando kama yako!!!

yayeyushe basi ili yawe laini kama yako.
 
Unajuaje mkuu kama hata hao unaowasema ni wenzako na wewe kama wana mpango wa kwenda kuwa Lecturers kule vyuoni? Nina jamaa yangu kamaliza PhD yake juzi sasa hivi ananyatiwa na Nelson Mandela pale Arusha! Sasa wewe utatujazaje ujinga na akili yako ya kushikiwa na mkeo hiyo? Wewe kama kitabu hakipandi pigwa kimya mkuu usitake kusumbua watu hapa. Unafikri wote tukiishia kuwa na ka-degree kamoja ka ki-Mulugo tutakuwa Taifa gani sisi?

Mawazo ya kusoma sana ili uajiriwe kama uliyo nayo wewe, yalikuwa valid kuanzia mwaka 1985 kushuka chini. We are in 2013 brother! Think again
 
Sina tatizo na waalimu wa vyuo vikuu, kwa sababu inabidi wasome hizo masters na phds, hapa nawazungumzia hawa weenzangu na mimi, G.P.A haisomi, yupo mtaani, haajariwa na taasisi yote ya kitaaluma, ameshindwa kupambana na changamoto za maisha, then anakuja na proposal ya kufanya masters and all that.

Aah ah ah...eti wanasema wanatafuta added advantage. Mi nafikiri elimu ya kuanzia masters lazima ifanyike kama mtu anaona kuna knowledge gap ya kile anachofanya, otherwise ni uoga tu. Mi niliamua kujifanyia zangu kacertificate ili kukidhi haja ya majukumu yangu.
 
Badili mtazamo ndugu,sio wote wanafanya hivyo,wana huo woga unaousema...unatarajia mwenye degree akafundishe level ya masters,au mwenye masters akafundishe phd?
Think big mkuu,unaweza ukawa sahihi kiasi fulani,but do not generalize....
Au kuna mtu umekuja kumpa makavu live huku...
 
LIKUD, mbona huu uzi umeandika kwa hasira sana? Yaani mtu kwenda shule tu anakukasirisha namna hii?! By the way masters na PhD zinahitajika sana katika Taifa hili. Kila mtu ana akili yake ya maisha, mwingine form 4 tu inamtosha kuwa na maisha mazuri na kuna mwingine PhD ndio itakayomtoa kwenye umaskini. Binaadam tumetofautiana sana mkuu, mwanafunzi anaweza kumsikiliza mwalimu mara moja tu na akamwelewa, kuna mwingine mpaka aweke miguu kwenye karai la maji ili asisinzie ndio aweze kuelewa alichofundishwa, na mtu kama huyu unaweza kumpa mtaji na kumfungulia biashara na bado akashindwa kuindeleza. So, sio makosa yao ni kwa jinsi mtu alivyozaliwa.
 
Basi rekebisha kichwa cha habari, vinginevyo watake radhi madocta na maprofesa wote, kwa kuwaita waoga wa maisha..!!

ni waoga wa maisha ndo maana maprofesa na madokta walio wengi wanakimbilia kwenye siasa ili wale nchi na si kutumia elimu kujikomboa na kulikomboa taifa, maprofesa hao hao ndo wamekuwa vibaraka vya wanasiasa kila wanachoelezwa na wanasiasa ambao wameishia form 4 wanaitikia ndio bila hata kuhoji
 
Daaaa adi nimeogopa!
wa TZ tuna kazi kweli kweli
lakini haya yoote ni matokeo ya sera mbovu za CCM!
 
Kutofanya Masters, PhD ni uoga wa masomo

Si uoga wa masomo baling hofu ya kupoteza muda,but bado na-support watu wakajipigie masters na PHD zao ili tujipatie wakufunzi na maprofesa wa kutosha
 
I boast in not failing myself and my creator.do I have any education really? watu wamesoma wakamaliza vitabu, mie ni survivor tu. na elimu sio ya darsani tu, sio?:bored:
So you mean you also boast about your level of education?
 
Back
Top Bottom