Kufanya masters, phd ni uoga wa maisha.

Kufanya masters, phd ni uoga wa maisha.

Tanzania haitakaa ikombolewe unless watu wake kama hawa wakombolewe kwanza.

Kwa akili zake kidogo anadhani masters zote lazima usome miaka miwili.

Kwamba ukiwa na GPA ya 2.1 lazima ukafanye post graduate kwanza ili usome masters.

Sijui hata kama anajua maana ya post graduate.

Kwamba huwezi kufanya kazi huku ukiwa unasoma.

Hata hivyo mtu akiamua kusoma ni hiari yake, sijui kwa nini ikuwashie wewe?

Probably, hapo ulipo cheo chako kipo mashakani baada ya mwezio kwenda kupiga shule.



we nawe mshambaa...bado unawaza mambo za cheo? mfyuuuuu
 
Kifupi wewe huna ufahamu kabisa


BEST BUSINESS MAN THAT EVER LIVED......YOU KNOW WHY?ALIISHIA DARASA LA SABA BABANGU TENA KIJIJINI HUKO .LESS THAN 10 YRS AFTER MOVING TO DASLAMHE OWNED A CONSTRUCTION COMPANY -HIRED HIGHLY EDUCATED ENGINEERS, EDUCATED ACCOUNTANTS , ETC.I MEAN, A MAN FROM A POOR FAMILY UPARENI HUKO WAS HIRING MEN 1,000 TIMES MORE EDUCATED THAN HIM AND THEY NEVER FOOLED HIM.......MY DAD WAS A GENIUS......
R.I.P

Source : http://www.u-turn.co.tz/
 
Sio kila anayeenda shule anakwrnda kusoma ili kuboresha maisha. Some wants expertism and not high scale salary.
 
We unashangaa hiyo?

7yrs Msingi
5yrs Secondary (O- level)
2yrs Secondary (A-level)
1yr Come and See
3 yrs Philosophy (Dip or Baccalaureate)- Bachelor
4yrs Theology (Dip & Baccalaureate)- Bachelor
1 yr Probation
Jumla mingapi? 23

Then baadaye niende
2yrs Masters degree in a different discipline
3yr PHD
Jumla mingapi? 5

Jumla kuu 23 + 5 = 28yrs niko shule. Huo ndo ukweli!!!!!
 
mimi bado naipenda shule aisee.......degree moja tu...graduates ndo hawa wanamwagwa karibia elfu 10 kila mwaka,tofauti yao na sisi itaonekana wapi kama tusipojiendeleza?....kama umeamua kuridhika ni wewe....shule tamu jamani.
 
Unajuaje mkuu kama hata hao unaowasema ni wenzako na wewe kama wana mpango wa kwenda kuwa Lecturers kule vyuoni? Nina jamaa yangu kamaliza PhD yake juzi sasa hivi ananyatiwa na Nelson Mandela pale Arusha! Sasa wewe utatujazaje ujinga na akili yako ya kushikiwa na mkeo hiyo? Wewe kama kitabu hakipandi pigwa kimya mkuu usitake kusumbua watu hapa. Unafikri wote tukiishia kuwa na ka-degree kamoja ka ki-Mulugo tutakuwa Taifa gani sisi?

haina mashiko hii mkuu..we umeona kuajiriwa na nelson mandela ndio peak enh! it is a greater honor to employ yourself and others at an earlier time....one's intelligence should shine at any level...get that
 
waajiriwa watakuchapa wewe. ujue ndugu zangu katika jamii ya kuku kuna "kuku wa kienyeji (happy chikens) alafu kunakuku "wa kisasa" (unhappy chikens)

kuku wa kienyej ukimtoa kwenye banda lake hata kama ni jangwani jion akirud anakuwa ameshiba na kama kawaida anafuraha...

huyu wa KISASA ye kwanza hata uache banda wazi hatoki alipokua amelala,, anaogopa jua, upepo, vumbi, kelele n.k...

( WENYE DEGREE HAPA WASHANIELEWA ILA WA MASTERS NA P.H.D BADO WANATAFUTA LOGIC) utalala hapo.:smile-big: :wave:
 
Endeleeni kujifariji hivyo hivyo wenzenu mataifa yote yanayowazunguka vijana wao wanakimbilia masters na PhD tena wala sio academicians...shule haina mwisho ukipata nafasi kasome kaka.Kusoma ni njia nyingine ya kutafuta maisha
 
We ni kama pacha na mm kimawazo na kimtazamo mkuu.... Ata nipate nafasi ya kwenda kusoma sayari nyingine siendi.... Ila mwenye kutaka kusoma zaidi c mbaya waache..
 
Watu wanashindwa kuelewa kuwa unavyozidi kusoma ndo unavyozidi kuwa mjinga au?!
 
Kuna watu wanapenda sana maisha ya uanafunzi, utafikiri walizaliwa ili wasome.

Shule ya msingi ========= 7 years.

O-Level ========== 4 years.

A- Level =========== 2 years.

Degree ya kwanza =========3 au 4 years.

Jumla : Miaka 16 au 17.

Umekaa shuleni kwa muda wa miaka kumi na saba lakini bado hauna uwezo wa kutumia elimu na maarifa uliyo yapata shuleni kukabiliana na changamoto za maisha? Still unataka kwenda kufanya masters, miaka miwili, after masters, unataka tena PHD miaka 3, we vipi wewe?

Ukiniambia nimuelezee mtu wa namna hii kwa maneno machache , nitasema ' MUOGA WA MAISHA ". Anaogopa ugumu wa maisha, anashindwa kuzi face changamoto za maisha ( e.g ukosfu wa ajira ). Anataka aendelee kuonekana mwanafunzi ili kuutumia uanafunzi wake kama excuse ya kuwa broke. Let me tell you brother, the only excuse of being broke is to be in jail. Achana na hizo bla blah za masters na PHD, piga kazi mjomba tujenge taifa letu. GPA yenyewe ya 2.1, masters mpaka ukafanye post graduate kwanza, dah watu wanajua kuua muda. Ukomboe wakati bro, siku ya mwisho utahukumiwa kwa kosa la ku ua muda. Nyambaff, unasoma hadi PHD halafu ukimaliza unaanza kutembea kwenye ofisi za watu na bahasha za kaki.


mmmh mapoyoyo wengi kweli nimeamini, afu nimegundua huna uwezo wa kusoma masters ndo maaana umeleta maada hii, si unajua ya sungura Sizitaki mbichi hizi. Poleeeeeee, acha wenzio tukomae kaka, kama ni uoga wa maisha au laaa poa, tunakomaa tuu, utaishia kuwa ......
 
Hii inaukweli upande flan kwan kati ya wanaoenda fanya masters na phd wapo walofata mkumbo na wengne ni uoga wa maisha kwa kuzani degree zaid ztawarahisishia maisha yao!
 
Sorry to say,mi kwangu kusoma ni sehemu ya kazi,huwa nahakikisha napata scholarship kabisa kupata mshahara wa mwezi.So ni muono wako tu ndio hasi.Na kama kungkuwa na uwezekano, kazi ingekuwa kutafuta scholarship na kusoma tu.
 
ni waoga wa maisha ndo maana maprofesa na madokta walio wengi wanakimbilia kwenye siasa ili wale nchi na si kutumia elimu kujikomboa na kulikomboa taifa, maprofesa hao hao ndo wamekuwa vibaraka vya wanasiasa kila wanachoelezwa na wanasiasa ambao wameishia form 4 wanaitikia ndio bila hata kuhoji
Hapa ndio umepotea kabisa ndugu yangu. Bilashaka kukimbilia kwenye siasa ndio wanatumia elimu yao kujikomboa, na kama watakua wawakilishi wazuri zaidi hao wana uwezo zaidi wa kulikomboa taifa kuliko wengine. Issue ya kusema wamekua vibaraka, hio ni issue binafsi wala haihusiani na elimu yao..!!
 
Soma,tena soma sana.Ukimaliza tengeneza ajira na sio kutafuta ajira,hapo utakuwa umeelimika.Dunia ya sasa,wabunifu ndio wanaoifaidi.
 
daaaah!

Nimesoma hii post kwa hisia kali sana na imenigusa kwa namna moja au nyingine. Naona kuna ukweli humu, but take a minute a think a bit wider, kwa mfano kwa wale wenzetu wanaoitwa madaktari.

Namchukulia mfano mdogo wangu daktari:
7yrs primary + 6 yrs secondary + 5 yrs degree ya kwanza ya udaktari + 1 yr internship + 4 yrs masters + 2 (udaktari bingwa sijui bobezi kwenye anga kama figo etc) + 5 yrs PhD.

Jumla hiyo miaka hapo juu = 30yrs!!!!!!
Huwa namuuliza dogo kwanini umeamua kufanya au kuchukua uamuzi mzito hivi? Jibu lake siku zote ni hili 'je nisingesoma ungepata wapi kuwa na daktari bingwa/bobezi?' na hapa nabaki kumwambia sawa, endelea.

Sasa kina sisi wenziwe tunaweza kuuuza mayai ya kuku au mboga mboga na tukapata 'fweza' za ukwee, lakini ukweli uko pale pale kusoma, tena kufikia highest level ni muhimu sana kwa faida pana ya jamii na taifa more than than an an individual or personal gain.

Mtoa mada si kila asomaye anataka kuwa tajiri, wengine wanataka kuwa part of the problem solvers katika jamii.

Wewe unataka kuwa tajiri na kuajiri 'wasomi' kuliko wewe, that's well and good ila support wengine wasome otherwise
utakosa hata wa kumwajiri

asante
 
Whether ni academician or not, mtu kaamua kujisomea mwenyewe, hela ya ada hajakuomba, kama ni faida au hasara ni ya kwake sasa wewe inakuhusu nini? fanya unachoamini ni sahihi kwako na waache wengine wafanye wanayoona ni sahihi kwao ilimradi hawavunji sheria.
 

BEST BUSINESS MAN THAT EVER LIVED......YOU KNOW WHY?ALIISHIA DARASA LA SABA BABANGU TENA KIJIJINI HUKO .LESS THAN 10 YRS AFTER MOVING TO DASLAMHE OWNED A CONSTRUCTION COMPANY -HIRED HIGHLY EDUCATED ENGINEERS, EDUCATED ACCOUNTANTS , ETC.I MEAN, A MAN FROM A POOR FAMILY UPARENI HUKO WAS HIRING MEN 1,000 TIMES MORE EDUCATED THAN HIM AND THEY NEVER FOOLED HIM.......MY DAD WAS A GENIUS......
R.I.P

Source : http://www.u-turn.co.tz/

Kwa hii post umejidhihirisha ulivyo mweupe kwa hoja.....unakiri mtu kaajiri wasomi then kapata mafanikio ya kutosha then wewe unapinga umuhimu wa elimu za kueleweka. Unajua unachokitetea kweli wewe? au ndo stimu za kulanduka?
 
Back
Top Bottom