Kua uyaone, weka mkasa wako hapa ulipogundua pesa si kila kitu

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,034
Yes, Pesa sio kila kitu, ni mpaka ikosekane kabisa ndio kila kitu ila ukiwa nayo hata kiasi sio kila kitu. Najua kuna msemo siku hizi kila mara "Tafuta Pesa" ila ukichunguza ni athari za watu walioishi katika umaskini tangu wadogo hivyo kisaikolojia wanaamini pesa ni kila kitu, siwezi kuwalaumu.

Ok tukija kwenye lengo la hii post ni wazi kabisa kwamba pesa sio kila kitu.

Rafiki yangu alikuwaga wa kishua sana miaka ya 2006 tu hapo simu haikosi anawekewa vocha za laki na mzee wake, pesa ya matumizi ya kutosha. Simu yake ndio niliitumia sana mzee ananipigia simu kwa namba yake kujua hali yangu, nikichelewa nyumbani anaona wazazi wananigombeza, akija nyumbani tuna mkaribisha chakula, anaona namna tunapiga stori na mzee. basi kuna siku akaniambia hawezi kujifikiria hata mara mbili tubadilishane nafasi za wazazi sababu wazazi wake hawana time nae kabisa zaidi ya kutuma pesa.

Niliwahi kuwa na mbwa wangu nimemkuza tangu mdogo, kuna mtu alikuwa anamtaka aliniletea hadi shilingi laki 5 lakini wapi, nilimwambia hata aje na milioni 5 huyo mbwa siuzi, huyu mbwa kuna kipindi mtoto alitoka nje kuna mbwa sijui aliruka fensi akataka kumshambulia mtoto, alimtoa nduki huyo mbwa koko.
 
Mwezi wa saba 2022 nilipotea porini mafinga ndani ndani huko msituni. Baridi ilikuwa kali kichizi. Nilikuwa na million mia saba kwenye begi . Uvumilivi ukanishinda ikabidi tu nichome noti ili kuota moto nipate joto. Nikabakiwa na laki sita tu nilipoweza kufika kijiji jirani.
 
Mwezi wa saba 2022 nilipotea porini mafinga ndani ndani huko msituni. Baridi ilikuwa kali kichizi. Nilikuwa na million mia saba kwenye begi . Uvumilivi ukanishinda ikabidi tu nichome noti ili kuota moto nipate joto. Nikabakiwa na laki sita tu nilipoweza kufika kijiji jirani.
Hahaha

Hio ni muvi ya Narcos, yule Pablo muuza madawa mkubwa alipoanza kusakwa na polisi akakimbilia moja ya nyumba zake za maficho aliyojenga porini, wamefika huko usiku na kuna baridi kali sana, hakuna kuni za kuotea moto ikabidi achome maburungutu ya pesa ili watoto wapate joto.
 
Ngoja mkuu nipate Kwanza pesa ndipo nitajua ndio Kila kitu au ni uongoo..

Ila pesa bhana ni tamu ukiwa nayo mkuu
 
Unaweza ukamtaka posh au pisi yoyote unayodhani ni kali na pesa inaweza fanya ukaipata ila mwisho wa siku na pesa zako hiyo pisi haizimikii na wewe unashangaa tu muhuni au mtu wa kawaida anakula.

Mfano mimi kuna demu kanielewa mimi wa kawaida mpaka sasa huwa najiuliza why hakumuelewa jamaa yule mwenye nazo na jamaa aliniambia anamuelewa sema kumpata ndiyo hawezi nikimwambia demu mbona humtaki jamaa na ana ukwasi fresh, demu anakuambia sina time naye.

Nimeshindwa kujua why kanielewa zaidi kuliko jamaa na demu hana muda naye yaani mimi nacheka na kuwa naye huru ila jamaa akimuona demu kwa mbali anatetemeka na kumwaza sana, sielewi nimependewa nini, demu yuko na uwezo wa kawaida ila ni mtafutaji kiaina.
 
Ni kweli ziko familia ni za kishua kwelikweli ila amani hamna, japo sio zote ila zipo lakini, pia kuna baadhi ya familia tia maji tia maji ila zina upendo balaa. Unakuta Baba na Mama wanapiga stori na watoto wao tena kwa amani na furaha kabisa licha ya financial crisis wapitiayo.

Ndo maana kuwa na pesa ni jambo moja na unaweza ukawa nazo na mkaishi vizuri sana kama familia tena kwa upendo ulotukuka na pengine ikawa kinyume chake. Binafsi naamini kwenye kumtegemea Mungu kwenye kila hali ndani ya familia.
 
Hahaha

hio ni muvi ya Narcos, yule Pablo muuza madawa mkubwa alipoanza kusakwa na polisi akakimbilia moja ya nyumba zake za maficho aliyojenga porini, wamefika huko usiku na kuna baridi kali sana, hakuna kuni za kuotea moto ikabidi achome maburungutu ya pesa ili watoto wapate joto.
Hapana ilinitokea kweli
 
Niko zangu mawindo nimetoka na chawa wangu wananiambia we point dem afu mengine tuachie sisi.
Basi katika kupiga ulabu umekolea bili zote kwangu jamaa wanagida atari.
Mbele yangu ikakatiza pisi yaani ile pisi ya kwenda iko na haga flani hivi hapo nikawaamuru chawa wangu kazi ile pale.
Asee waliimbisha mpaka mida mibaya mzee baba wakatoka kapa.
Niliumia sana siku ile.
 
Niko zangu mawindo nimetoka na chawa wangu wananiambia we point dem afu mengine tuachie sisi.
Basi katika kupiga ulabu umekolea bili zote kwangu jamaa wanagida atari.
Mbele yangu ikakatiza pisi yaani ile pisi ya kwenda iko na haga flani hivi hapo nikawaamuru chawa wangu kazi ile pale.
Asee waliimbisha mpaka mida mibaya mzee baba wakatoka kapa.
Niliumia sana siku ile.
Tufanye ilikuwa na UTI sugu
 
Kwenye huu mjadala nimeupenda huo msemo wa "Tafuta Pesa" kuwa unatumiwa zaidi na watu walioishi kimaskini na sasa wamezipata pesa ukubwani.
Hao wanaona jinsi ambavyo pesa inawapa yale waliyoyakosa kabla.

Watu waliokulia kwenye ukwasi ukiongea nao wanajua pesa si kila kitu maana wameona nyakati ambazo pesa zao hazikuwapa walivyovitaka.
 
Yes, Pesa sio kila kitu, ni mpaka ikosekane kabisa ndio kila kitu ila ukiwa nayo hata kiasi sio kila kitu. Najua kuna msemo siku hizi kila mara "Tafuta Pesa" ila ukichunguza ni athari za watu walioishi katika umaskini tangu wadogo hivyo kisaikolojia wanaamini pesa ni kila kitu, siwezi kuwalaumu.

Ok tukija kwenye lengo la hii post ni wazi kabisa kwamba pesa sio kila kitu.

Rafiki yangu alikuwaga wa kishua sana miaka ya 2006 tu hapo simu haikosi anawekewa vocha za laki na mzee wake, pesa ya matumizi ya kutosha. Simu yake ndio niliitumia sana mzee ananipigia simu kwa namba yake kujua hali yangu, nikichelewa nyumbani anaona wazazi wananigombeza, akija nyumbani tuna mkaribisha chakula, anaona namna tunapiga stori na mzee. basi kuna siku akaniambia hawezi kujifikiria hata mara mbili tubadilishane nafasi za wazazi sababu wazazi wake hawana time nae kabisa zaidi ya kutuma pesa.

Niliwahi kuwa na mbwa wangu nimemkuza tangu mdogo, kuna mtu alikuwa anamtaka aliniletea hadi shilingi laki 5 lakini wapi, nilimwambia hata aje na milioni 5 huyo mbwa siuzi, huyu mbwa kuna kipindi mtoto alitoka nje kuna mbwa sijui aliruka fensi akataka kumshambulia mtoto, alimtoa nduki huyo mbwa koko.
Pesa sio kila kitu maana pesa inakupa furaha lakin haiwez kukupa raha. Mungu ndio kila kitu maana kwake utapata raha ukiwa nae unakuwa na amani kias upendo nk
 
Kwa maisha ya sasa tusijidanganye, pesa ndio kila kitu. Siku hizi pesa inanunua haki, pesa inanunua heshima, pesa inanunua maisha, pesa inanunua mpaka uhai!
 
Kwa maisha ya sasa tusijidanganye, pesa ndio kila kitu. Siku hizi pesa inanunua haki, pesa inanunua heshima, pesa inanunua maisha, pesa inanunua mpaka uhai!
Pesa ni muhimu lakini sio kila kitu. Wewe bado mdogo, ukiwa mkubwa ndio utaelewa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom