Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,504
- 113,618
Wanabodi,
Hizi ni salamu zangu za Makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa kwa ajili ya Krisimasi kwa Wanabodi wetu.
Merry Christmas And Happy New Year!.
Japo makala hizi ni za lugha yetu adhimu ya Kiswahili, kwa vile kesho ni sikukuu ya Krisimasi ni sikukuu ya kutoa, ili kuwezesha na wengine tusherehekee sikukuu ya Krimasi pamoja na Jumapili siku ya Boxing Day, nasi pia tuwe na maxi ya zawadi za kufungua, ambapo Boxing Day ni siku ambayo huifuatia sikukuu ya Krisimasi, hivyo bado tuko kwenye kitu kinachoitwa “festival mood” or “holiday mood” yaani mudi ya sikukuu au ya kisherehe sherehe au ya kushereheka, tena nimekumbuka zile enzi za Mzee Rukhsa, Rais Ali Hasaan Mwinyi, sikukuu ya siku mbili, ikiangukia siku za mapumziko, Jumamosi na Jumapili, mapumziko hayo yanafidiwa kwa mapumziko siku ya Jumatatu na Jumanne, kazini ingekuwa ni Jumatano ijayo!.
Sasa kufuatia hii mudi ya kisherehe sherehe na kushereheka, na kwa vile sikukuu yenyewe ya Krisimasi ni sikukuu ya Kizungu, iliyoletwa Afrika na ujio wa Wamisionari wa Kizungu walioleta dini ya Kikiristo Afrika, kwenye kichwa cha habari cha makala hii kwa leo, nimeamua kuwatakia heri ya sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya kwa kuitumia lugha yake ya asili iliyokuja nayo, yaani Kiingereza, kwasababu kuna vitu ikivitamka kwa lugha yake ya asili, vinanoga zaidi, kupendeza zaidi na kukolea zaidi kuliko ukivitamka kwa lugha ya tafsiri.
Japo Krisimasi ni sikukuu ya kuadhimisha kuzaliwa kwa Masiha, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa sisi Wakristu, lakini sikukuu hii inaadhimishwa dunia nzima na watu wa dini zote na mataifa yote, hata nchi za Kiislam, maana hata kwenye Dini ya Kiislamu, wanamtambua Masiha, Bwana wetu Yesu Kristo, ila kule wanamtambua kwa majina mengine. Kiislam wanamtambua kama Nabii Issa Bin Maryam, ukisoma sifa za huyo Nabii Issa bin Maryam, utakubalia na mimi mtu huyo ni Yesu Kristo, ila kwa vile kila dini iko huru kuamini imani yake, kuna dini zinamkubali Yesu ndiye Nabii Issa, hivyo kuzaliwa kwake kunasherehekewa dunia nzima, hivyo sikukuu ya Chrismas ni sikukuu ya wote.
Hata simulizi za mwanzo wa ulimwengu kwa dini kuu mbili za Wakristo na Waislamu, sote tunakubaliana dunia iliumbwa na Mungu, mwanzo Mungu aliumba dunia na vyote vilivyomo, ndio kisha akamuumba binadamu, Adam na Eva, (Kikristu) au Adam na Hawa, (Kiislamu) hivyo sisi binadamu wote ni watoto wa baba mmoja. Adam, hata neno Mwanadamu, au Binadamu, maana yake ni Mwanadamu. Hata sisi nembo yetu ya Taifa yenye mwanamke na mwanaume, Bibi na Bwana, wengine wanawaita Adam na Hawa.
Kwa dini zote mbili, tunaamini kisa cha Nabii Abraham (Kikristo) Ibrahimu, (Kiislamu) na mkewe Sara (Kikristu), Sarai (Kiislamu), waliishi muda mrefu kwenye ndoa yao bila kubahatika kupata mtoto. Baada ya uzee kuwanyemelea na mkewe Sara siku zake kukoma, hivyo kutokuwa na uwezo tena wa kuzaa mtoto, ndipo akamtoa mjakazi wake wa Kimisri, Hagai (Kikiristu), Hagir (Kiislamu), kushiriki na mumuwe Ibrahim, ili kuweza kupata mrithi.
Somo hapa ni familia ambazo hazikujaaliwa kupata watoto kutokana na tatizo la uzazi kwa mke, wanawake msiwe wachoyo kwa waume zenu, waruhusuni waume zenu kupata watoto kwa wanawake wengine. Hii ni endapo tatizo la uzazi ni kwa mwanamke, linapokuwa tatizo ni kwa mwanaume, hili mtanisamehe bado sijajua utaratibu wake, kwasababu hata kwenye vitabu vya dini, haijasemwa.
Huyo mjakazi akashika ujauzito, akamzaa mwana wa kwanza wa Ibrahimu akaitwa Ishamel (Kikirstu) Ismail (Kiislamu), aliyemzaa na huyo mjakazi wake wa Kimisri Hajiri (Kikiristu), Hagir (Kiislamu). Familia nzima ilifurahi kupa mtoto, Baba, mama na mjakazi. Baadaye kwa muujiza wa Mungu, mke wa Ibrahimu Sara, akiwa mzee wa umri wa miaka 90, alishika ujauzito, na kumzaa mtoto aliyeitwa Isaka (Kikristu), Isihaka (Kiislamu). Ismaili ndio Baba wa Waislamu wote, na Isaka ndio baba wa Wakisto wote.
Ni katika ukoo huu ndio alikuja kuzaliwa Nabii Musa, na aliyewakomboa Waisraeli kutoka utumwani Misri, nan die aliyepewa Amri Kuu za Mungu, ni zile zile amri alizopewa Musa, kupitia Torati. Ni katika ukoo huu ndio Yesu alizaliwa na hata Yesu alipokuja, bado amri za Mungu ni zile zile za Musa, Yesu hakuja kuitengua Torati bali kuikamilisha. Hata Mtume ni kutoka Ukoo wa Ismail, hivyo Wakristu na Waislamu ni watoto wa baba mmoja na wamwamini Mungu mmoja, hivyo tusherekee Krismasi pamoja kwa jinsi ile ile Wakristo tunavyo sherehekea Iddi pamoja au Maulid.
Kwa vile Krismasi ni sikukuu ya kizungu, wenzetu wazungu wanaisherehekea kwa kitu kinachoitwa “The Christmas Spirit” ambacho ni kusherehekea by “Giving” and not “Receiving”, kumaanisha Chrismasi ni sikukuu ya kutoa, na sio kupokea, ila kila ukitoa, unabarikiwa nawe utapokea.
Kuna Watanzania wengi wanajiandaa kwa Krisimasi kwa mwaka mzima, ikiwemo kuweka akiba ya fedha za kutumia kula Krismasi, na baadhi wanajikuta wanaisherehekea kinyume cha malengo, badala ya kutoa, wao ndio kwanza wanatumia kwa kutanua kwa kujipenda, kufanya matumizi makubwa na sherehe, anasa, kustarehe na kuponda raha kwa kula, kunywa, kusafiri, kustarehe, kununua vitu anasa na mapambo na kujipa zawadi wenyewe badala ya kuwapa zawadi wengine haswa wahitaji.
Mimi mwenyewe nimejikuta huwa ninatuma kadi tuu za kirismasi kwa watu na salamu za heri ya Krismasi kavu kavu bila kutoa chochote au zawadi yoyote kwa wahitaji, hujiwekea akiba kwa mwaka mzima ili Krisimasi nitumbue kwa kutanua, kwa ajili ya kusafiri na familia, kuinunulia familia nguo mpya za Krismasi, kula vizuri, kunywa kwa sana na kufurahi kwa kujifurahisha sisi na familia zetu, na ndugu zetu na jamaa zetu na marafiki zetu, lakini jee tumewakumbuka wahitaji?.
Naomba japo sikukuu tuisherekee kitofauti kidogo kwa kuwakumbuka wengine ambao ni wahitaji. Na kwa vile watu hatufanani uwezo, kipato na kuyawezea maisha, kwa vile sikukuu hii ni sikukuu ya wote, na spirit yake ni kutoa, hebu nasi basi kwa siku hii na wiki hii, tuwaangazie na wenzetu tukianzia na majirani zetu walio tuzungunguka ni watu wenye hali gani kiuchumi, jee watashereheka kama tunavyoshereheka sisi?. Unaonaje ukiwashika japo mkono nao washereheke. Tuwakumbuke wagonjwa mahospitalini, wafungwa magerezani, yatima kwenye nyumba za mayatima au watu wengine wowote wenye uhitaji, hebu jitoe uwashike mkono kwa kidogo chochote kitu ili kudumisha “the Christmas Spirit, to give”, kwa kujitoa kuwatolea chochote ili na wao pia washerekee sikukuu ya Krismasi ni sikukuu ya wote.
Its by giving, you will receive.
Malizia kwa kuangalia kisa hiki
Ukiguswa do something
I wish You A Merry Christmas, Christmas and Prosperous New Year.
Paskali.
Rejea za Mwandishi kuhusu Christmas
1. Je, wajua Wakristo na Waislamu ni watoto wa baba mmoja? Kuwa Yesu ndiye Nabii Issa, hivyo X Mass ni sikukuu ya wote? I wish you a Merry Christmas!
2. Amri Kuu Kuliko Zote ni Upendo! Mpende Mungu, Ipende Nchi, Wapende Viongozi, Mpende Jirani Yako Kama Nafsi Yako!. Jirani yako ni Nani?, Unampenda?