Krismasi ni sikukuu ya wote, tutoe kwa wengine na tushereheke pamoja. Merry X-Mas!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,504
113,618
Makala ya Krismasi-.png

Wanabodi,
Hizi ni salamu zangu za Makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa kwa ajili ya Krisimasi kwa Wanabodi wetu.
Merry Christmas And Happy New Year!.

Japo makala hizi ni za lugha yetu adhimu ya Kiswahili, kwa vile kesho ni sikukuu ya Krisimasi ni sikukuu ya kutoa, ili kuwezesha na wengine tusherehekee sikukuu ya Krimasi pamoja na Jumapili siku ya Boxing Day, nasi pia tuwe na maxi ya zawadi za kufungua, ambapo Boxing Day ni siku ambayo huifuatia sikukuu ya Krisimasi, hivyo bado tuko kwenye kitu kinachoitwa “festival mood” or “holiday mood” yaani mudi ya sikukuu au ya kisherehe sherehe au ya kushereheka, tena nimekumbuka zile enzi za Mzee Rukhsa, Rais Ali Hasaan Mwinyi, sikukuu ya siku mbili, ikiangukia siku za mapumziko, Jumamosi na Jumapili, mapumziko hayo yanafidiwa kwa mapumziko siku ya Jumatatu na Jumanne, kazini ingekuwa ni Jumatano ijayo!.

Sasa kufuatia hii mudi ya kisherehe sherehe na kushereheka, na kwa vile sikukuu yenyewe ya Krisimasi ni sikukuu ya Kizungu, iliyoletwa Afrika na ujio wa Wamisionari wa Kizungu walioleta dini ya Kikiristo Afrika, kwenye kichwa cha habari cha makala hii kwa leo, nimeamua kuwatakia heri ya sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya kwa kuitumia lugha yake ya asili iliyokuja nayo, yaani Kiingereza, kwasababu kuna vitu ikivitamka kwa lugha yake ya asili, vinanoga zaidi, kupendeza zaidi na kukolea zaidi kuliko ukivitamka kwa lugha ya tafsiri.

Japo Krisimasi ni sikukuu ya kuadhimisha kuzaliwa kwa Masiha, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa sisi Wakristu, lakini sikukuu hii inaadhimishwa dunia nzima na watu wa dini zote na mataifa yote, hata nchi za Kiislam, maana hata kwenye Dini ya Kiislamu, wanamtambua Masiha, Bwana wetu Yesu Kristo, ila kule wanamtambua kwa majina mengine. Kiislam wanamtambua kama Nabii Issa Bin Maryam, ukisoma sifa za huyo Nabii Issa bin Maryam, utakubalia na mimi mtu huyo ni Yesu Kristo, ila kwa vile kila dini iko huru kuamini imani yake, kuna dini zinamkubali Yesu ndiye Nabii Issa, hivyo kuzaliwa kwake kunasherehekewa dunia nzima, hivyo sikukuu ya Chrismas ni sikukuu ya wote.

Hata simulizi za mwanzo wa ulimwengu kwa dini kuu mbili za Wakristo na Waislamu, sote tunakubaliana dunia iliumbwa na Mungu, mwanzo Mungu aliumba dunia na vyote vilivyomo, ndio kisha akamuumba binadamu, Adam na Eva, (Kikristu) au Adam na Hawa, (Kiislamu) hivyo sisi binadamu wote ni watoto wa baba mmoja. Adam, hata neno Mwanadamu, au Binadamu, maana yake ni Mwanadamu. Hata sisi nembo yetu ya Taifa yenye mwanamke na mwanaume, Bibi na Bwana, wengine wanawaita Adam na Hawa.

Kwa dini zote mbili, tunaamini kisa cha Nabii Abraham (Kikristo) Ibrahimu, (Kiislamu) na mkewe Sara (Kikristu), Sarai (Kiislamu), waliishi muda mrefu kwenye ndoa yao bila kubahatika kupata mtoto. Baada ya uzee kuwanyemelea na mkewe Sara siku zake kukoma, hivyo kutokuwa na uwezo tena wa kuzaa mtoto, ndipo akamtoa mjakazi wake wa Kimisri, Hagai (Kikiristu), Hagir (Kiislamu), kushiriki na mumuwe Ibrahim, ili kuweza kupata mrithi.

Somo hapa ni familia ambazo hazikujaaliwa kupata watoto kutokana na tatizo la uzazi kwa mke, wanawake msiwe wachoyo kwa waume zenu, waruhusuni waume zenu kupata watoto kwa wanawake wengine. Hii ni endapo tatizo la uzazi ni kwa mwanamke, linapokuwa tatizo ni kwa mwanaume, hili mtanisamehe bado sijajua utaratibu wake, kwasababu hata kwenye vitabu vya dini, haijasemwa.

Huyo mjakazi akashika ujauzito, akamzaa mwana wa kwanza wa Ibrahimu akaitwa Ishamel (Kikirstu) Ismail (Kiislamu), aliyemzaa na huyo mjakazi wake wa Kimisri Hajiri (Kikiristu), Hagir (Kiislamu). Familia nzima ilifurahi kupa mtoto, Baba, mama na mjakazi. Baadaye kwa muujiza wa Mungu, mke wa Ibrahimu Sara, akiwa mzee wa umri wa miaka 90, alishika ujauzito, na kumzaa mtoto aliyeitwa Isaka (Kikristu), Isihaka (Kiislamu). Ismaili ndio Baba wa Waislamu wote, na Isaka ndio baba wa Wakisto wote.

Ni katika ukoo huu ndio alikuja kuzaliwa Nabii Musa, na aliyewakomboa Waisraeli kutoka utumwani Misri, nan die aliyepewa Amri Kuu za Mungu, ni zile zile amri alizopewa Musa, kupitia Torati. Ni katika ukoo huu ndio Yesu alizaliwa na hata Yesu alipokuja, bado amri za Mungu ni zile zile za Musa, Yesu hakuja kuitengua Torati bali kuikamilisha. Hata Mtume ni kutoka Ukoo wa Ismail, hivyo Wakristu na Waislamu ni watoto wa baba mmoja na wamwamini Mungu mmoja, hivyo tusherekee Krismasi pamoja kwa jinsi ile ile Wakristo tunavyo sherehekea Iddi pamoja au Maulid.

Kwa vile Krismasi ni sikukuu ya kizungu, wenzetu wazungu wanaisherehekea kwa kitu kinachoitwa “The Christmas Spirit” ambacho ni kusherehekea by “Giving” and not “Receiving”, kumaanisha Chrismasi ni sikukuu ya kutoa, na sio kupokea, ila kila ukitoa, unabarikiwa nawe utapokea.

Kuna Watanzania wengi wanajiandaa kwa Krisimasi kwa mwaka mzima, ikiwemo kuweka akiba ya fedha za kutumia kula Krismasi, na baadhi wanajikuta wanaisherehekea kinyume cha malengo, badala ya kutoa, wao ndio kwanza wanatumia kwa kutanua kwa kujipenda, kufanya matumizi makubwa na sherehe, anasa, kustarehe na kuponda raha kwa kula, kunywa, kusafiri, kustarehe, kununua vitu anasa na mapambo na kujipa zawadi wenyewe badala ya kuwapa zawadi wengine haswa wahitaji.

Mimi mwenyewe nimejikuta huwa ninatuma kadi tuu za kirismasi kwa watu na salamu za heri ya Krismasi kavu kavu bila kutoa chochote au zawadi yoyote kwa wahitaji, hujiwekea akiba kwa mwaka mzima ili Krisimasi nitumbue kwa kutanua, kwa ajili ya kusafiri na familia, kuinunulia familia nguo mpya za Krismasi, kula vizuri, kunywa kwa sana na kufurahi kwa kujifurahisha sisi na familia zetu, na ndugu zetu na jamaa zetu na marafiki zetu, lakini jee tumewakumbuka wahitaji?.

Naomba japo sikukuu tuisherekee kitofauti kidogo kwa kuwakumbuka wengine ambao ni wahitaji. Na kwa vile watu hatufanani uwezo, kipato na kuyawezea maisha, kwa vile sikukuu hii ni sikukuu ya wote, na spirit yake ni kutoa, hebu nasi basi kwa siku hii na wiki hii, tuwaangazie na wenzetu tukianzia na majirani zetu walio tuzungunguka ni watu wenye hali gani kiuchumi, jee watashereheka kama tunavyoshereheka sisi?. Unaonaje ukiwashika japo mkono nao washereheke. Tuwakumbuke wagonjwa mahospitalini, wafungwa magerezani, yatima kwenye nyumba za mayatima au watu wengine wowote wenye uhitaji, hebu jitoe uwashike mkono kwa kidogo chochote kitu ili kudumisha “the Christmas Spirit, to give”, kwa kujitoa kuwatolea chochote ili na wao pia washerekee sikukuu ya Krismasi ni sikukuu ya wote.
Its by giving, you will receive.

Malizia kwa kuangalia kisa hiki

Ukiguswa do something

I wish You A Merry Christmas, Christmas and Prosperous New Year.

Paskali.
Rejea za Mwandishi kuhusu Christmas
1. Je, wajua Wakristo na Waislamu ni watoto wa baba mmoja? Kuwa Yesu ndiye Nabii Issa, hivyo X Mass ni sikukuu ya wote? I wish you a Merry Christmas!
1703610474256.png

2. Amri Kuu Kuliko Zote ni Upendo! Mpende Mungu, Ipende Nchi, Wapende Viongozi, Mpende Jirani Yako Kama Nafsi Yako!. Jirani yako ni Nani?, Unampenda?
1703610659537.png
 

Attachments

  • 1703610399347.png
    1703610399347.png
    277.3 KB · Views: 1
Wanabodi,
Hizi ni salamu zangu za Makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa kwa ajili ya Krisimasi kwa Wanabodi wetu.
Merry Christmas And Happy New Year!.

Japo makala hizi ni za lugha yetu adhimu ya Kiswahili, kwa vile kesho ni sikukuu ya Krisimasi ni sikukuu ya kutoa, ili kuwezesha na wengine tusherehekee sikukuu ya Krimasi pamoja na Jumapili siku ya Boxing Day, nasi pia tuwe na maxi ya zawadi za kufungua, ambapo Boxing Day ni siku ambayo huifuatia sikukuu ya Krisimasi, hivyo bado tuko kwenye kitu kinachoitwa “festival mood” or “holiday mood” yaani mudi ya sikukuu au ya kisherehe sherehe au ya kushereheka, tena nimekumbuka zile enzi za Mzee Rukhsa, Rais Ali Hasaan Mwinyi, sikukuu ya siku mbili, ikiangukia siku za mapumziko, Jumamosi na Jumapili, mapumziko hayo yanafidiwa kwa mapumziko siku ya Jumatatu na Jumanne, kazini ingekuwa ni Jumatano ijayo!.

Sasa kufuatia hii mudi ya kisherehe sherehe na kushereheka, na kwa vile sikukuu yenyewe ya Krisimasi ni sikukuu ya Kizungu, iliyoletwa Afrika na ujio wa Wamisionari wa Kizungu walioleta dini ya Kikiristo Afrika, kwenye kichwa cha habari cha makala hii kwa leo, nimeamua kuwatakia heri ya sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya kwa kuitumia lugha yake ya asili iliyokuja nayo, yaani Kiingereza, kwasababu kuna vitu ikivitamka kwa lugha yake ya asili, vinanoga zaidi, kupendeza zaidi na kukolea zaidi kuliko ukivitamka kwa lugha ya tafsiri.

Japo Krisimasi ni sikukuu ya kuadhimisha kuzaliwa kwa Masiha, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa sisi Wakristu, lakini sikukuu hii inaadhimishwa dunia nzima na watu wa dini zote na mataifa yote, hata nchi za Kiislam, maana hata kwenye Dini ya Kiislamu, wanamtambua Masiha, Bwana wetu Yesu Kristo, ila kule wanamtambua kwa majina mengine. Kiislam wanamtambua kama Nabii Issa Bin Maryam, ukisoma sifa za huyo Nabii Issa bin Maryam, utakubalia na mimi mtu huyo ni Yesu Kristo, ila kwa vile kila dini iko huru kuamini imani yake, kuna dini zinamkubali Yesu ndiye Nabii Issa, hivyo kuzaliwa kwake kunasherehekewa dunia nzima, hivyo sikukuu ya Chrismas ni sikukuu ya wote.

Hata simulizi za mwanzo wa ulimwengu kwa dini kuu mbili za Wakristo na Waislamu, sote tunakubaliana dunia iliumbwa na Mungu, mwanzo Mungu aliumba dunia na vyote vilivyomo, ndio kisha akamuumba binadamu, Adam na Eva, (Kikristu) au Adam na Hawa, (Kiislamu) hivyo sisi binadamu wote ni watoto wa baba mmoja. Adam, hata neno Mwanadamu, au Binadamu, maana yake ni Mwanadamu. Hata sisi nembo yetu ya Taifa yenye mwanamke na mwanaume, Bibi na Bwana, wengine wanawaita Adam na Hawa.

Kwa dini zote mbili, tunaamini kisa cha Nabii Abraham (Kikristo) Ibrahimu, (Kiislamu) na mkewe Sara (Kikristu), Sarai (Kiislamu), waliishi muda mrefu kwenye ndoa yao bila kubahatika kupata mtoto. Baada ya uzee kuwanyemelea na mkewe Sara siku zake kukoma, hivyo kutokuwa na uwezo tena wa kuzaa mtoto, ndipo akamtoa mjakazi wake wa Kimisri, Hagai (Kikiristu), Hagir (Kiislamu), kushiriki na mumuwe Ibrahim, ili kuweza kupata mrithi.

Somo hapa ni familia ambazo hazikujaaliwa kupata watoto kutokana na tatizo la uzazi kwa mke, wanawake msiwe wachoyo kwa waume zenu, waruhusuni waume zenu kupata watoto kwa wanawake wengine. Hii ni endapo tatizo la uzazi ni kwa mwanamke, linapokuwa tatizo ni kwa mwanaume, hili mtanisamehe bado sijajua utaratibu wake, kwasababu hata kwenye vitabu vya dini, haijasemwa.

Huyo mjakazi akashika ujauzito, akamzaa mwana wa kwanza wa Ibrahimu akaitwa Ishamel (Kikirstu) Ismail (Kiislamu), aliyemzaa na huyo mjakazi wake wa Kimisri Hagai (Kikiristu), Hagir (Kiislamu). Familia nzima ilifurahi kupa mtoto, Baba, mama na mjakazi. Baadaye kwa muujiza wa Mungu, mke wa Ibrahimu Sara, akiwa mzee wa umri wa miaka 80, alishika ujauzito, na kumzaa mtoto aliyeitwa Isaka (Kikristu), Isihaka (Kiislamu). Isumaili ndio Baba wa Waislamu wote, na Isaka ndio baba wa Wakisto wote.

Ni katika ukoo huu ndio alikuja kuzaliwa Nabii Musa, na aliyewakomboa Waisraeli kutoka utumwani Misri, nan die aliyepewa Amri Kuu za Mungu, ni zile zile amri alizopewa Musa, kupitia Torati. Ni katika ukoo huu ndio Yesu alizaliwa na hata Yesu alipokuja, bado amri za Mungu ni zile zile Musa, Yesu hakuja kuitengua Torati bali kuikamilisha. Hata Mtume ni kutoka Ukoo wa Ismail, hivyo Wakristu na Waislamu ni watoto wa baba mmoja, tusherekee Krismasi pamoja.

Kwa vile Krismasi ni sikukuu ya kizungu, wenzetu wazungu wanaishehekea kwa kitu kinachoitwa “The Christmas Spirit” ambacho ni kusherehekea by “Giving” and not “Receiving”, kumaanisha Chrismasi ni sikukuu ya kutoa, na sio kupokea.

Kuna Watanzania wengi wanajiandaa kwa mwaka mzima, ikiwemo kuweka akiba ya fedha za kutumia kula Krismasi, wanajikuta wanaisherhekea kinyume cha malengo, badala ya kutoa, wao ndio kwanza wanatumia kwa kujipenda, kufanya matumizi makubwa na sherehe, kula, kunywa, kusafiri, kustarehe, kununua vitu na kujipa zawadi wenyewe badala ya kuwapa zawadi wengine haswa wahitaji.

Mimi mwenyewe nimejikuta huwa ninatuma kadi tuu za kirismasi kwa watu na salamu za heri ya Krismasi kavu kavu bila kutoa zawadi yoyote kwa wahitaji, hujiwekea akiba nzuri, kwa ajili ya kusafiri na familia, kuinunulia familia nguo mpya za Krismasi, kula vizuri, kunywa kwa sana na kufurahi kwa kujifurahisha sisi na familia zetu, na ndugu zetu na jamaa zetu na marafiki zetu, lakini jee tumewakumbuka wahitaji?.

Naomba japo sikukuu tuisherekee kitofauti kwa kuwakumbuka wengine ambao ni wahitaji. Na kwa vile watu hatufanani uwezo, kipato na kuyawezea maisha, kwa vile sikukuu hii ni sikukuu ya wote, na spirit yake ni kutoa, hebu nasi basi kwa siku hii na wiki hii, tuwaangazie na wenzetu tukianzia na majirani zetu walio tuzungunguka ni watu wenye hali gani kiuchumi, jee watashereheka kama tunavyoshereheka sisi?. Unaonaje ukiwashika japo mkono nao washereheke. Tuwakumbuke wagonjwa mahospitalini, wafungwa magezani, yatima kwenye nyumba za mayatima au watu wengine wowote wenye uhitaji, hebu jitoe uwashike mkono kwa kidogo chochote kitu ili kudumisha “the Christmas Spirit, to give”, kwa kujitoa kuwatolea chochote ili na wao pia washerekee sikukuu ya Krismasi ni sikukuu ya wote.
Its by giving, you will receive.

I wish You A Merry Christmas, Christmas and Prosperous New Year.

Paskali.
Dunia nzima unamaanisha hawa ADF, ISIL,BOKO HARAM nao tunasheherekea nao kuzaliwa kwa yesu kristo


USSR
 
Mkuu Pascal Mayalla asante sana Heri ya Christmas na Kwako pia.

Ila umesema maana ya Christmas ni kutoa na siyo kupokea... vitendo hivyo viwili vinakwenda pamoja....kwani utakuwa unamtolea nani kama hakuna wa kupoea ?
The Christmas Spirit is giving ule moyo wa kutoa na ni kwa kutoa ndipo utapokea. Lengo ni wenye nacho, who are very fortunate wawakumbuke the unfortunate ones wawape chochote ili krisimasi tusherehekee wote.
P
 
Wanabodi,
Hizi ni salamu zangu za Makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa kwa ajili ya Krisimasi kwa Wanabodi wetu.
Merry Christmas And Happy New Year!.

Japo makala hizi ni za lugha yetu adhimu ya Kiswahili, kwa vile kesho ni sikukuu ya Krisimasi ni sikukuu ya kutoa, ili kuwezesha na wengine tusherehekee sikukuu ya Krimasi pamoja na Jumapili siku ya Boxing Day, nasi pia tuwe na maxi ya zawadi za kufungua, ambapo Boxing Day ni siku ambayo huifuatia sikukuu ya Krisimasi, hivyo bado tuko kwenye kitu kinachoitwa “festival mood” or “holiday mood” yaani mudi ya sikukuu au ya kisherehe sherehe au ya kushereheka, tena nimekumbuka zile enzi za Mzee Rukhsa, Rais Ali Hasaan Mwinyi, sikukuu ya siku mbili, ikiangukia siku za mapumziko, Jumamosi na Jumapili, mapumziko hayo yanafidiwa kwa mapumziko siku ya Jumatatu na Jumanne, kazini ingekuwa ni Jumatano ijayo!.

Sasa kufuatia hii mudi ya kisherehe sherehe na kushereheka, na kwa vile sikukuu yenyewe ya Krisimasi ni sikukuu ya Kizungu, iliyoletwa Afrika na ujio wa Wamisionari wa Kizungu walioleta dini ya Kikiristo Afrika, kwenye kichwa cha habari cha makala hii kwa leo, nimeamua kuwatakia heri ya sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya kwa kuitumia lugha yake ya asili iliyokuja nayo, yaani Kiingereza, kwasababu kuna vitu ikivitamka kwa lugha yake ya asili, vinanoga zaidi, kupendeza zaidi na kukolea zaidi kuliko ukivitamka kwa lugha ya tafsiri.

Japo Krisimasi ni sikukuu ya kuadhimisha kuzaliwa kwa Masiha, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa sisi Wakristu, lakini sikukuu hii inaadhimishwa dunia nzima na watu wa dini zote na mataifa yote, hata nchi za Kiislam, maana hata kwenye Dini ya Kiislamu, wanamtambua Masiha, Bwana wetu Yesu Kristo, ila kule wanamtambua kwa majina mengine. Kiislam wanamtambua kama Nabii Issa Bin Maryam, ukisoma sifa za huyo Nabii Issa bin Maryam, utakubalia na mimi mtu huyo ni Yesu Kristo, ila kwa vile kila dini iko huru kuamini imani yake, kuna dini zinamkubali Yesu ndiye Nabii Issa, hivyo kuzaliwa kwake kunasherehekewa dunia nzima, hivyo sikukuu ya Chrismas ni sikukuu ya wote.

Hata simulizi za mwanzo wa ulimwengu kwa dini kuu mbili za Wakristo na Waislamu, sote tunakubaliana dunia iliumbwa na Mungu, mwanzo Mungu aliumba dunia na vyote vilivyomo, ndio kisha akamuumba binadamu, Adam na Eva, (Kikristu) au Adam na Hawa, (Kiislamu) hivyo sisi binadamu wote ni watoto wa baba mmoja. Adam, hata neno Mwanadamu, au Binadamu, maana yake ni Mwanadamu. Hata sisi nembo yetu ya Taifa yenye mwanamke na mwanaume, Bibi na Bwana, wengine wanawaita Adam na Hawa.

Kwa dini zote mbili, tunaamini kisa cha Nabii Abraham (Kikristo) Ibrahimu, (Kiislamu) na mkewe Sara (Kikristu), Sarai (Kiislamu), waliishi muda mrefu kwenye ndoa yao bila kubahatika kupata mtoto. Baada ya uzee kuwanyemelea na mkewe Sara siku zake kukoma, hivyo kutokuwa na uwezo tena wa kuzaa mtoto, ndipo akamtoa mjakazi wake wa Kimisri, Hagai (Kikiristu), Hagir (Kiislamu), kushiriki na mumuwe Ibrahim, ili kuweza kupata mrithi.

Somo hapa ni familia ambazo hazikujaaliwa kupata watoto kutokana na tatizo la uzazi kwa mke, wanawake msiwe wachoyo kwa waume zenu, waruhusuni waume zenu kupata watoto kwa wanawake wengine. Hii ni endapo tatizo la uzazi ni kwa mwanamke, linapokuwa tatizo ni kwa mwanaume, hili mtanisamehe bado sijajua utaratibu wake, kwasababu hata kwenye vitabu vya dini, haijasemwa.

Huyo mjakazi akashika ujauzito, akamzaa mwana wa kwanza wa Ibrahimu akaitwa Ishamel (Kikirstu) Ismail (Kiislamu), aliyemzaa na huyo mjakazi wake wa Kimisri Hagai (Kikiristu), Hagir (Kiislamu). Familia nzima ilifurahi kupa mtoto, Baba, mama na mjakazi. Baadaye kwa muujiza wa Mungu, mke wa Ibrahimu Sara, akiwa mzee wa umri wa miaka 80, alishika ujauzito, na kumzaa mtoto aliyeitwa Isaka (Kikristu), Isihaka (Kiislamu). Isumaili ndio Baba wa Waislamu wote, na Isaka ndio baba wa Wakisto wote.

Ni katika ukoo huu ndio alikuja kuzaliwa Nabii Musa, na aliyewakomboa Waisraeli kutoka utumwani Misri, nan die aliyepewa Amri Kuu za Mungu, ni zile zile amri alizopewa Musa, kupitia Torati. Ni katika ukoo huu ndio Yesu alizaliwa na hata Yesu alipokuja, bado amri za Mungu ni zile zile Musa, Yesu hakuja kuitengua Torati bali kuikamilisha. Hata Mtume ni kutoka Ukoo wa Ismail, hivyo Wakristu na Waislamu ni watoto wa baba mmoja, tusherekee Krismasi pamoja.

Kwa vile Krismasi ni sikukuu ya kizungu, wenzetu wazungu wanaishehekea kwa kitu kinachoitwa “The Christmas Spirit” ambacho ni kusherehekea by “Giving” and not “Receiving”, kumaanisha Chrismasi ni sikukuu ya kutoa, na sio kupokea.

Kuna Watanzania wengi wanajiandaa kwa mwaka mzima, ikiwemo kuweka akiba ya fedha za kutumia kula Krismasi, wanajikuta wanaisherhekea kinyume cha malengo, badala ya kutoa, wao ndio kwanza wanatumia kwa kujipenda, kufanya matumizi makubwa na sherehe, kula, kunywa, kusafiri, kustarehe, kununua vitu na kujipa zawadi wenyewe badala ya kuwapa zawadi wengine haswa wahitaji.

Mimi mwenyewe nimejikuta huwa ninatuma kadi tuu za kirismasi kwa watu na salamu za heri ya Krismasi kavu kavu bila kutoa zawadi yoyote kwa wahitaji, hujiwekea akiba nzuri, kwa ajili ya kusafiri na familia, kuinunulia familia nguo mpya za Krismasi, kula vizuri, kunywa kwa sana na kufurahi kwa kujifurahisha sisi na familia zetu, na ndugu zetu na jamaa zetu na marafiki zetu, lakini jee tumewakumbuka wahitaji?.

Naomba japo sikukuu tuisherekee kitofauti kwa kuwakumbuka wengine ambao ni wahitaji. Na kwa vile watu hatufanani uwezo, kipato na kuyawezea maisha, kwa vile sikukuu hii ni sikukuu ya wote, na spirit yake ni kutoa, hebu nasi basi kwa siku hii na wiki hii, tuwaangazie na wenzetu tukianzia na majirani zetu walio tuzungunguka ni watu wenye hali gani kiuchumi, jee watashereheka kama tunavyoshereheka sisi?. Unaonaje ukiwashika japo mkono nao washereheke. Tuwakumbuke wagonjwa mahospitalini, wafungwa magezani, yatima kwenye nyumba za mayatima au watu wengine wowote wenye uhitaji, hebu jitoe uwashike mkono kwa kidogo chochote kitu ili kudumisha “the Christmas Spirit, to give”, kwa kujitoa kuwatolea chochote ili na wao pia washerekee sikukuu ya Krismasi ni sikukuu ya wote.
Its by giving, you will receive.

Malizia kwa kuangalia kisa hiki

Ukiguswa do something

I wish You A Merry Christmas, Christmas and Prosperous New Year.

Paskali.

Sijakuelewa hata kidogo kada wa CCM!
 
Dunia nzima unamaanisha hawa ADF, ISIL,BOKO HARAM nao tunasheherekea nao kuzaliwa kwa yesu kristo
USSR
Wote sisi ni watoto wa baba mmoja Adam, na Mungu mmoja, God, Father, The Lord!. Siku yako ikifika, ukifika hukumuni, unaweza kushangaa kuwakuta Osama, Saadam na Ghadafi peponi, halafu Bush, Blair na Obama...ndio wanaogelea kwenye lile ziwa la jehanum ya moto wa milele!.
P
 
Wanabodi,
Hizi ni salamu zangu za Makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa kwa ajili ya Krisimasi kwa Wanabodi wetu.
Merry Christmas And Happy New Year!.

Japo makala hizi ni za lugha yetu adhimu ya Kiswahili, kwa vile kesho ni sikukuu ya Krisimasi ni sikukuu ya kutoa, ili kuwezesha na wengine tusherehekee sikukuu ya Krimasi pamoja na Jumapili siku ya Boxing Day, nasi pia tuwe na maxi ya zawadi za kufungua, ambapo Boxing Day ni siku ambayo huifuatia sikukuu ya Krisimasi, hivyo bado tuko kwenye kitu kinachoitwa “festival mood” or “holiday mood” yaani mudi ya sikukuu au ya kisherehe sherehe au ya kushereheka, tena nimekumbuka zile enzi za Mzee Rukhsa, Rais Ali Hasaan Mwinyi, sikukuu ya siku mbili, ikiangukia siku za mapumziko, Jumamosi na Jumapili, mapumziko hayo yanafidiwa kwa mapumziko siku ya Jumatatu na Jumanne, kazini ingekuwa ni Jumatano ijayo!.

Sasa kufuatia hii mudi ya kisherehe sherehe na kushereheka, na kwa vile sikukuu yenyewe ya Krisimasi ni sikukuu ya Kizungu, iliyoletwa Afrika na ujio wa Wamisionari wa Kizungu walioleta dini ya Kikiristo Afrika, kwenye kichwa cha habari cha makala hii kwa leo, nimeamua kuwatakia heri ya sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya kwa kuitumia lugha yake ya asili iliyokuja nayo, yaani Kiingereza, kwasababu kuna vitu ikivitamka kwa lugha yake ya asili, vinanoga zaidi, kupendeza zaidi na kukolea zaidi kuliko ukivitamka kwa lugha ya tafsiri.

Japo Krisimasi ni sikukuu ya kuadhimisha kuzaliwa kwa Masiha, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa sisi Wakristu, lakini sikukuu hii inaadhimishwa dunia nzima na watu wa dini zote na mataifa yote, hata nchi za Kiislam, maana hata kwenye Dini ya Kiislamu, wanamtambua Masiha, Bwana wetu Yesu Kristo, ila kule wanamtambua kwa majina mengine. Kiislam wanamtambua kama Nabii Issa Bin Maryam, ukisoma sifa za huyo Nabii Issa bin Maryam, utakubalia na mimi mtu huyo ni Yesu Kristo, ila kwa vile kila dini iko huru kuamini imani yake, kuna dini zinamkubali Yesu ndiye Nabii Issa, hivyo kuzaliwa kwake kunasherehekewa dunia nzima, hivyo sikukuu ya Chrismas ni sikukuu ya wote.

Hata simulizi za mwanzo wa ulimwengu kwa dini kuu mbili za Wakristo na Waislamu, sote tunakubaliana dunia iliumbwa na Mungu, mwanzo Mungu aliumba dunia na vyote vilivyomo, ndio kisha akamuumba binadamu, Adam na Eva, (Kikristu) au Adam na Hawa, (Kiislamu) hivyo sisi binadamu wote ni watoto wa baba mmoja. Adam, hata neno Mwanadamu, au Binadamu, maana yake ni Mwanadamu. Hata sisi nembo yetu ya Taifa yenye mwanamke na mwanaume, Bibi na Bwana, wengine wanawaita Adam na Hawa.

Kwa dini zote mbili, tunaamini kisa cha Nabii Abraham (Kikristo) Ibrahimu, (Kiislamu) na mkewe Sara (Kikristu), Sarai (Kiislamu), waliishi muda mrefu kwenye ndoa yao bila kubahatika kupata mtoto. Baada ya uzee kuwanyemelea na mkewe Sara siku zake kukoma, hivyo kutokuwa na uwezo tena wa kuzaa mtoto, ndipo akamtoa mjakazi wake wa Kimisri, Hagai (Kikiristu), Hagir (Kiislamu), kushiriki na mumuwe Ibrahim, ili kuweza kupata mrithi.

Somo hapa ni familia ambazo hazikujaaliwa kupata watoto kutokana na tatizo la uzazi kwa mke, wanawake msiwe wachoyo kwa waume zenu, waruhusuni waume zenu kupata watoto kwa wanawake wengine. Hii ni endapo tatizo la uzazi ni kwa mwanamke, linapokuwa tatizo ni kwa mwanaume, hili mtanisamehe bado sijajua utaratibu wake, kwasababu hata kwenye vitabu vya dini, haijasemwa.

Huyo mjakazi akashika ujauzito, akamzaa mwana wa kwanza wa Ibrahimu akaitwa Ishamel (Kikirstu) Ismail (Kiislamu), aliyemzaa na huyo mjakazi wake wa Kimisri Hagai (Kikiristu), Hagir (Kiislamu). Familia nzima ilifurahi kupa mtoto, Baba, mama na mjakazi. Baadaye kwa muujiza wa Mungu, mke wa Ibrahimu Sara, akiwa mzee wa umri wa miaka 80, alishika ujauzito, na kumzaa mtoto aliyeitwa Isaka (Kikristu), Isihaka (Kiislamu). Isumaili ndio Baba wa Waislamu wote, na Isaka ndio baba wa Wakisto wote.

Ni katika ukoo huu ndio alikuja kuzaliwa Nabii Musa, na aliyewakomboa Waisraeli kutoka utumwani Misri, nan die aliyepewa Amri Kuu za Mungu, ni zile zile amri alizopewa Musa, kupitia Torati. Ni katika ukoo huu ndio Yesu alizaliwa na hata Yesu alipokuja, bado amri za Mungu ni zile zile Musa, Yesu hakuja kuitengua Torati bali kuikamilisha. Hata Mtume ni kutoka Ukoo wa Ismail, hivyo Wakristu na Waislamu ni watoto wa baba mmoja, tusherekee Krismasi pamoja.

Kwa vile Krismasi ni sikukuu ya kizungu, wenzetu wazungu wanaishehekea kwa kitu kinachoitwa “The Christmas Spirit” ambacho ni kusherehekea by “Giving” and not “Receiving”, kumaanisha Chrismasi ni sikukuu ya kutoa, na sio kupokea.

Kuna Watanzania wengi wanajiandaa kwa mwaka mzima, ikiwemo kuweka akiba ya fedha za kutumia kula Krismasi, wanajikuta wanaisherhekea kinyume cha malengo, badala ya kutoa, wao ndio kwanza wanatumia kwa kujipenda, kufanya matumizi makubwa na sherehe, kula, kunywa, kusafiri, kustarehe, kununua vitu na kujipa zawadi wenyewe badala ya kuwapa zawadi wengine haswa wahitaji.

Mimi mwenyewe nimejikuta huwa ninatuma kadi tuu za kirismasi kwa watu na salamu za heri ya Krismasi kavu kavu bila kutoa zawadi yoyote kwa wahitaji, hujiwekea akiba nzuri, kwa ajili ya kusafiri na familia, kuinunulia familia nguo mpya za Krismasi, kula vizuri, kunywa kwa sana na kufurahi kwa kujifurahisha sisi na familia zetu, na ndugu zetu na jamaa zetu na marafiki zetu, lakini jee tumewakumbuka wahitaji?.

Naomba japo sikukuu tuisherekee kitofauti kwa kuwakumbuka wengine ambao ni wahitaji. Na kwa vile watu hatufanani uwezo, kipato na kuyawezea maisha, kwa vile sikukuu hii ni sikukuu ya wote, na spirit yake ni kutoa, hebu nasi basi kwa siku hii na wiki hii, tuwaangazie na wenzetu tukianzia na majirani zetu walio tuzungunguka ni watu wenye hali gani kiuchumi, jee watashereheka kama tunavyoshereheka sisi?. Unaonaje ukiwashika japo mkono nao washereheke. Tuwakumbuke wagonjwa mahospitalini, wafungwa magezani, yatima kwenye nyumba za mayatima au watu wengine wowote wenye uhitaji, hebu jitoe uwashike mkono kwa kidogo chochote kitu ili kudumisha “the Christmas Spirit, to give”, kwa kujitoa kuwatolea chochote ili na wao pia washerekee sikukuu ya Krismasi ni sikukuu ya wote.
Its by giving, you will receive.

Malizia kwa kuangalia kisa hiki

Ukiguswa do something

I wish You A Merry Christmas, Christmas and Prosperous New Year.

Paskali.

Kaka heshimu dini ya kiislamu na imani yetu, why unafanya comparison ambayo inadhalilisha imani ya kiislamu, acha kupotosha ,dini hii imekamilika kupitia mtu Muhammad (s. a.w.) hakuongolezwi kitu kipya, dini hii imeletwa kwa wahyi ktoka kwa Allah kuputia jibril ikamfikia mtume, kwa mujibu wa mafundisho ni haramu kwa muislamu tena ni shirki kubwa kusherehekea krismas pia ni haramu kupokea chakula, zawadi au kitu chchte ambacho msingi wake ni kusherehekea sikukuu hii,pia haifai kwa musilamu ku mu wish asie kuwa muislam heri ya krismas,kwani katika Quran Allha ameweka wazi bila kificho kuwa Issa hakuteswa,hakusulibiwa lkn Allah kwa uwezo wake wa kimungu aliwabadilishia wale waliokuwa wanataka kumdhuru akamfanya miongoni mwao afanane na Issa kisha wao wakamuua nakudhani wamemuua Issa,allha alimpandisha Issa mbinguni na atarud kabla ya kiama kusimama kama ishara ya mwisho wa dunia.
Pia kwa mujibu wa Quran tukufu mitume wte uliowataja, Ibrahim, Ishaka, Ismaili, Issa na Musa hao wote ni mitume walioletwa na Allah kwa watu wao kueneza mafundisho ya dini ya kiislamu, hakuna mkristo hapo,
Pia Allah kwenye Quran amekanusha bila kificho kwa kusema Ibrahim hakua mkristo wala myahudi Bali alikuwa muislam yy na kizazi chake,
Hivyo tunakuomba mwanajamvi mwenzetu kabla ya kuandika jambo linalohusu dini nyengine fanya utafiti wa kutosha kujua wenye dini yao wamefundishwa nini na kitabu chao ilikuepuka upotoshaji Kwani ww ni member mwenye kufatliwa unachokiandika, pia ni Aibu kwa hadhi yako kusema muislam washerehekee krismas kwa hoja ambazo hazina mashiko,
Swali:Je tufuate mtazomo wako juu ya jambo hili au mafundisho ya kitabu cha Quran.
Acha upotoshaji na usome uislamu, pia nachkuwa nafasi hii kukutaka uingie kwenye uslamu kwani ndio dini ya haki na nasra kwa Allah itapatikana kwa kuwa muislamu tu.
 
Kaka heshimu dini ya kiislamu na imani yetu, why unafanya comparison ambayo inadhalilisha imani ya kiislamu, acha kupotosha ,dini hii imekamilika kupitia mtu Muhammad (s. a.w.) hakuongolezwi kitu kipya, dini hii imeletwa kwa wahyi ktoka kwa Allah kuputia jibril ikamfikia mtume, kwa mujibu wa mafundisho ni haramu kwa muislamu tena ni shirki kubwa kusherehekea krismas pia ni haramu kupokea chakula, zawadi au kitu chchte ambacho msingi wake ni kusherehekea sikukuu hii,pia haifai kwa musilamu ku mu wish asie kuwa muislam heri ya krismas,kwani katika Quran Allha ameweka wazi bila kificho kuwa Issa hakuteswa,hakusulibiwa lkn Allah kwa uwezo wake wa kimungu aliwabadilishia wale waliokuwa wanataka kumdhuru akamfanya miongoni mwao afanane na Issa kisha wao wakamuua nakudhani wamemuua Issa,allha alimpandisha Issa mbinguni na atarud kabla ya kiama kusimama kama ishara ya mwisho wa dunia.
Pia kwa mujibu wa Quran tukufu mitume wte uliowataja, Ibrahim, Ishaka, Ismaili, Issa na Musa hao wote ni mitume walioletwa na Allah kwa watu wao kueneza mafundisho ya dini ya kiislamu, hakuna mkristo hapo,
Pia Allah kwenye Quran amekanusha bila kificho kwa kusema Ibrahim hakua mkristo wala myahudi Bali alikuwa muislam yy na kizazi chake,
Hivyo tunakuomba mwanajamvi mwenzetu kabla ya kuandika jambo linalohusu dini nyengine fanya utafiti wa kutosha kujua wenye dini yao wamefundishwa nini na kitabu chao ilikuepuka upotoshaji Kwani ww ni member mwenye kufatliwa unachokiandika, pia ni Aibu kwa hadhi yako kusema muislam washerehekee krismas kwa hoja ambazo hazina mashiko,
Swali:Je tufuate mtazomo wako juu ya jambo hili au mafundisho ya kitabu cha Quran.
Acha upotoshaji na usome uislamu, pia nachkuwa nafasi hii kukutaka uingie kwenye uslamu kwani ndio dini ya haki na nasra kwa Allah itapatikana kwa kuwa muislamu tu.
Kwa hiyo bibi ushungi amekosea alivyotutakia Merry x-mas?
 
Kaka heshimu dini ya kiislamu na imani yetu, why unafanya comparison ambayo inadhalilisha imani ya kiislamu, acha kupotosha
Mkuu Ikahalasi , uzi huu unazungumzia watu, Wakisto na Waislamu ni watoto wa baba mmoja, na Mungu wao ni mmoja, sijazungumzia dini hapa. Katika bandiko hili, wapi nimedhalilisha dini yoyote?.
kwa mujibu wa mafundisho ni haramu kwa muislamu tena ni shirki kubwa kusherehekea krismas pia ni haramu kupokea chakula, zawadi au kitu chchte ambacho msingi wake ni kusherehekea sikukuu hii,pia haifai kwa musilamu ku mu wish asie kuwa muislam heri ya krismas,
Duh, kiukweli kuna vitu sisi ambao sio Waislamu, hatuvijui kuhusu Uislamu. Kama hiki ndio nimekijua leo.
kwani katika Quran Allha ameweka wazi bila kificho kuwa Issa wamemuua, Allha alimpandisha Issa mbinguni na atarud kabla ya kiama kusimama kama ishara ya mwisho wa dunia.
Hili ni zuri kuwa kuna Nabii alipalizwa mbinguni na atarudi tena siku ya mwisho, siku ya kiama, kuja kuwahukumu wazima na wafu.
Pia kwa mujibu wa Quran tukufu mitume wte uliowataja, Ibrahim, Ishaka, Ismaili, Issa na Musa hao wote ni mitume walioletwa na Allah
Hapa tuko pamoja na sio mitume tuu na manabii bali binadamu wote ni watoto wa baba mmoja, Adam, na sisi wote ni wa kwake na kwake tutarejea.
Kwani ww ni member mwenye kufatliwa unachokiandika, pia ni Aibu kwa hadhi yako kusema Muislam washerehekee krismas kwa hoja ambazo hazina mashiko,
Swali:Je tufuate mtazamo wako juu ya jambo hili au mafundisho ya kitabu cha Quran.
Sisi Wakristo tunasherekea Iddi pamoja nanyi.
Acha upotoshaji na usome uislamu, pia nachkuwa nafasi hii kukutaka uingie kwenye uslamu kwani ndio dini ya haki na nasra kwa Allah itapatikana kwa kuwa muislamu tu.
Hili la mimi kuingia Uislamu ni suala la muda tuu, tena nitasilimia Zanzibar. Ninachosubiri ni malipo yangu tuu ya mafao yangu yao kustaafu, niende Zanzibar nikajitwalie jiko moja matata sana!.
P.
 
Back
Top Bottom