Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
Ni usiku wa baridi kali sana , vijana na vikundi mbali mbali vya sanaa viko hapa uwanjani , uwanja umerembwa kidogo katika baadhi ya maeneo haswa yale ya watu kuingilia na sehemu ya wageni maarufu
Watu kwa makundi wanapiga picha na vijana hawa wanaopiga ngoma na kuonyesha sanaa zingine za mtandao , kila mtu anafuraha yake moyoni
furaha hizi hazijaletwa na kingine bali ni ujio wa ndege nyingine toka kwa shirika la ndege la uholanzi aina ya Boeng 777 , ndege hii safari zake ndio zinazinduliwa usiku huu katika uwanja wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere .
Baada ya serikali kuamua kuitupa ATCL kwa Wachina na kusikika tetesi za shirika la ndege la Community kurudi tena hewani KLM wakaamua watuletee vitu vya uhakika na sasa kuna 777 ambayo ndio itaanza safari zake katika ya Tanzania na sehemu zingine za dunia kuanzia usiku wa leo