Janeth Thomson Mwambije
Member
- Apr 11, 2024
- 13
- 37
Nilifanikiwa Kushiriki Kwenye Mapokezi Ya Ndege Mpya (Boeing 737 - Max 9) Ya Shirika La Air Tanzania (Air Tanzania Company Limited) Ambapo Mgeni Rasmi Katika Mapokezi Hayo Alikuwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaaliwa, Kwa Niaba Ya Mheshimiwa Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kutokana na Mheshimiwa Rais Kutingwa na Majukumu.
Katika Mapokezi Haya, Mheshimiwa Waziri Mkuu Aliweza Kumpongeza Mheshimiwa Rais Kwa Juhudi Anazozifanya, Hususani Ndani Ya Miaka Hii Mitatu, Kwa Kuimarisha Sekta Mbalimbali Ikiwemo Sekta Ya Uchukuzi, Na Kutekeleza Ilani Ya Uchaguzi Ya Chama Cha Mapinduzi Ya Mwaka 2020-2025.
Pia Mheshimiwa Waziri Mkuu, Aliweza Kutujuza Mafanikio, na Umuhimu wa Sekta Ya Uchukuzi Nchini Kwa Maendeleo Ya Taifa Letu, Ikiwa Ni Pamoja Na, Kuwa Mchango Katika Kuhakikisha Ukuaji wa Uchumi Wetu Na Kuzalisha Ajira Nchini. Kuongeza Uwezo wa Taifa Kujitegemea Kiuchumi. Kuchochea Uzalishaji, na Kutumia Vyema Fursa za Rasilimali Zilizopo Hapa Nchini. Kuchochea Upatikanaji wa Fedha za Kigeni, Nchini. Na Ongezeko La Mnyororo wa Thamani Ya Mazao Ya Kilimo, Pamoja na Biashara, Na Kadhalika.
Lakini Pia Ameweza Kusema Ndege Ambazo Zimenunuliwa Kwa Kipindi Cha Miaka Mitatu Ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ambapo Tayari Ndege Tano Zimeshawasili Ikiwemo Ndege Ya Mizigo, Ndege Ya Sita Ikiwa Ni Boeing 737-9 Max Iliyowasili Leo, Na Ndege Nyingine Moja (Boeing 787-8 Dreamliner) Ambayo Inategemewa Kuwasili Hivi Karibuni.
Na Mpaka Sasa. Kuna Endelea Na Maboresho Ya Viwanja Vya Ndege Kwenye Mikoa Mbalimbali. Kubwa Zaidi Ni Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa, Msalato - Dodoma, Pamoja na Uboreshwaji wa Uwanja wa Pili wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius K. Nyerere, Utaosaidia Kuifanya Tanzania Kuwa Kitovu Cha Anga, Afrika Mashariki.
Lakini Pia, Aligusia Mafanikio Ya Sekta Ya Uchukuzi Kwenye Reli (Ukamilisho wa Reli Ya SGR), na Usafiri wa Maziwa-Bahari (Ujenzi wa Meli Zinazokaribia Kukamilika Hivi Karibuni), Pamoja na Maboresho Ya Bandari. Kisha Akatoa Maelekezo Ya Usimamizi wa Shirika La Ndege, Ambalo Limetumiwa Fedha Nyingi Katika Uwekezaji.
Ulikuwa Wakati Mzuri.
#KaziIendelee 🇹🇿
Katika Mapokezi Haya, Mheshimiwa Waziri Mkuu Aliweza Kumpongeza Mheshimiwa Rais Kwa Juhudi Anazozifanya, Hususani Ndani Ya Miaka Hii Mitatu, Kwa Kuimarisha Sekta Mbalimbali Ikiwemo Sekta Ya Uchukuzi, Na Kutekeleza Ilani Ya Uchaguzi Ya Chama Cha Mapinduzi Ya Mwaka 2020-2025.
Pia Mheshimiwa Waziri Mkuu, Aliweza Kutujuza Mafanikio, na Umuhimu wa Sekta Ya Uchukuzi Nchini Kwa Maendeleo Ya Taifa Letu, Ikiwa Ni Pamoja Na, Kuwa Mchango Katika Kuhakikisha Ukuaji wa Uchumi Wetu Na Kuzalisha Ajira Nchini. Kuongeza Uwezo wa Taifa Kujitegemea Kiuchumi. Kuchochea Uzalishaji, na Kutumia Vyema Fursa za Rasilimali Zilizopo Hapa Nchini. Kuchochea Upatikanaji wa Fedha za Kigeni, Nchini. Na Ongezeko La Mnyororo wa Thamani Ya Mazao Ya Kilimo, Pamoja na Biashara, Na Kadhalika.
Lakini Pia Ameweza Kusema Ndege Ambazo Zimenunuliwa Kwa Kipindi Cha Miaka Mitatu Ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ambapo Tayari Ndege Tano Zimeshawasili Ikiwemo Ndege Ya Mizigo, Ndege Ya Sita Ikiwa Ni Boeing 737-9 Max Iliyowasili Leo, Na Ndege Nyingine Moja (Boeing 787-8 Dreamliner) Ambayo Inategemewa Kuwasili Hivi Karibuni.
Na Mpaka Sasa. Kuna Endelea Na Maboresho Ya Viwanja Vya Ndege Kwenye Mikoa Mbalimbali. Kubwa Zaidi Ni Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa, Msalato - Dodoma, Pamoja na Uboreshwaji wa Uwanja wa Pili wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius K. Nyerere, Utaosaidia Kuifanya Tanzania Kuwa Kitovu Cha Anga, Afrika Mashariki.
Lakini Pia, Aligusia Mafanikio Ya Sekta Ya Uchukuzi Kwenye Reli (Ukamilisho wa Reli Ya SGR), na Usafiri wa Maziwa-Bahari (Ujenzi wa Meli Zinazokaribia Kukamilika Hivi Karibuni), Pamoja na Maboresho Ya Bandari. Kisha Akatoa Maelekezo Ya Usimamizi wa Shirika La Ndege, Ambalo Limetumiwa Fedha Nyingi Katika Uwekezaji.
Ulikuwa Wakati Mzuri.
#KaziIendelee 🇹🇿