ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Hapa Watanzania ni kama tunamtafuta mchawi nani wakati wote tunajua kuwa haya yote yanayotokea yanafanywa na watanzania wenzetu ambao tunaishi nao hapa hapa nchini na tunaweza kuwawajibisha kwa nia moja au nyingine kutokana na dhamana walizinazo. Kama kweli hawana hisa yoyote kwa Dowans, ya nini kuonekana wakiumiza vichwa vyao kutaka Dowans ilipwe? Ni makampuni mangapi ya kizalendo au ya kigeni ambayo yameshinda kesi dhidi ya Serikali na mpaka leo hayajalipwa? Kuna nini kwa hili la Dowans?
(i) Inawezekanaje Kampuni ya Kigeni au raia wa nje akasajili kampuni hapa nchi pasipokuwa na mkono wa Mtanzania eti hata wakili tu wa kugonga mihuri nyaraka hayupo kiasi cha kutufanya tusijue Dowans ni ya kina nani?
(ii) inawezekanaje Msajili wa Makampuni akawa kimya na kumwachia mtu kama Mhe. Ngeleja kutuziba mdomo watanzania kwa kujifanya anajua wamiliki wa Dowans wanati yeye si Bosi wa BRELA??
(iii) Iweje Mhe. Ngeleja akasimama na kuwaeleza wananchi tuilipe Dowans kutokana na kesi ambayo inaihusu Tanesco wakati Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco yupo??
(iv) Imekuwaje Mwanasheria Mkuu wa Serikali akawa kimya na kuwaachia mawakili binafsi wa Rex Attorney kulishauri na kuliwakilisha Mahakamani shirika la Umma ilihali ikijulikana tokea mwanzo kuwa kesi husika ni nyeti kwa Serikali?? (tukumbuke kuwa Taarifa ya Dr. Mwakyembe ilibainisha mapungufu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhusu usimimizi wa Suala la Umeme wa dharura na mkataba na kampuni ya Richmond LC. Hata hivyo, uzembe huo umeendelea kujitokeza mpaka sasa ambapo Mwanasheria Mkuu badala ya kuitetea Serikali analazimisha tuliilipe Dowans mabilioni ya shilingi.)
(v) Mawakili kama akina FUngamtama wanahisa gani kwenye Dowans mpaka wakadiriki kusimama mbele ya wanatanzania na kuda tuilipe Dowans wakati yapo makampuni kibao ya kizalendo ambayo yameshinda kesi dhidi ya Serikali muda mrefu na hayajalipwa (Ikumbukwe kesi kama ile ya Valambia, Ubomoaji wa Maghorofa ya Masaki nk).
(vi) Kama kuna uhalali wowote wa kuilipa Dowans, kwa nini uwepo wa kesi hii haukufahamisha kwa watanzania kabla hukumu haijatolewa ili kuwezesha haki kutendeka kwa fedha za walipa kodi kama ilivyokuwa katika kesi ya BIWATER/CITY WATER??.
(i) Inawezekanaje Kampuni ya Kigeni au raia wa nje akasajili kampuni hapa nchi pasipokuwa na mkono wa Mtanzania eti hata wakili tu wa kugonga mihuri nyaraka hayupo kiasi cha kutufanya tusijue Dowans ni ya kina nani?
(ii) inawezekanaje Msajili wa Makampuni akawa kimya na kumwachia mtu kama Mhe. Ngeleja kutuziba mdomo watanzania kwa kujifanya anajua wamiliki wa Dowans wanati yeye si Bosi wa BRELA??
(iii) Iweje Mhe. Ngeleja akasimama na kuwaeleza wananchi tuilipe Dowans kutokana na kesi ambayo inaihusu Tanesco wakati Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco yupo??
(iv) Imekuwaje Mwanasheria Mkuu wa Serikali akawa kimya na kuwaachia mawakili binafsi wa Rex Attorney kulishauri na kuliwakilisha Mahakamani shirika la Umma ilihali ikijulikana tokea mwanzo kuwa kesi husika ni nyeti kwa Serikali?? (tukumbuke kuwa Taarifa ya Dr. Mwakyembe ilibainisha mapungufu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhusu usimimizi wa Suala la Umeme wa dharura na mkataba na kampuni ya Richmond LC. Hata hivyo, uzembe huo umeendelea kujitokeza mpaka sasa ambapo Mwanasheria Mkuu badala ya kuitetea Serikali analazimisha tuliilipe Dowans mabilioni ya shilingi.)
(v) Mawakili kama akina FUngamtama wanahisa gani kwenye Dowans mpaka wakadiriki kusimama mbele ya wanatanzania na kuda tuilipe Dowans wakati yapo makampuni kibao ya kizalendo ambayo yameshinda kesi dhidi ya Serikali muda mrefu na hayajalipwa (Ikumbukwe kesi kama ile ya Valambia, Ubomoaji wa Maghorofa ya Masaki nk).
(vi) Kama kuna uhalali wowote wa kuilipa Dowans, kwa nini uwepo wa kesi hii haukufahamisha kwa watanzania kabla hukumu haijatolewa ili kuwezesha haki kutendeka kwa fedha za walipa kodi kama ilivyokuwa katika kesi ya BIWATER/CITY WATER??.