Kituo cha Polisi Kitunda Mkoani Tabora kimechomwa moto na wananchi wenye hasira

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
12,830
21,460
Mkuu wa Kituo cha Polisi Kitunda amekimbia baada ya kunusurika kuuawa na wananchi wenye hasira.

Katika tukio hilo la Septemba 18, gari la askari Polisi na Kituo cha polisi kimechomwa moto.

IGP hana habari!

==============

POLISI YAKIRI KUTOKEA KWA TUKIO HILO
Alipoulizwa na JamiiForums kuhusu kituo kuchomwa moto, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao amesema “Taarifa ni za kweli na hakuna madhara yoyote yaliyotokea kwa binadamu."

Ameongeza "Nipo katika shughuli za Mwenge siwezi kutoa taarifa kamili kuhusu tukio hilo lakini hadi sasa tunawashikilia watuhumiwa 28, wanaendelea kuhojiwa ili kujua chanzo ya kukichoma moto kituo hicho kidogo na upelelezi unaendelea."
 
Back
Top Bottom