Dr bila digree. ujinga na wizi. wanachukua dawa za hospitali zikiwe ARV s na kuchanganya na miti shamba. ubatili mtupuWizara ya Afya imekifunga kwa mda usiojulikana kituo cha Fore plan Clinic kilichopo ilala Bungoni. Kituo hiki kinamilikiwa na Dr J.J Mwaka mtaalam wa magonjwa ya kinamama akitibu kwa kutumia tiba mbadala.Wizara imesema kituo hakijatimiza vigezo na masharti yanayotakiwa na serikali ikiwemo kutokuwa na wataalam wenye sifa na elimu stahiki.Dr J.J Mwaka amekuwa akionyesha kazi nzuri za kituo chake kwenye vyombo vya habari ikiwemo kutibu ugumba na upungufu wa nguvu za aina mbalimbali.Watu wengi wamekua wakifurahia sana tiba hii mbadala itolewayo na Dr Mwaka na mpaka kituo kinafungwa wagonjwa wengi walikua wakisubilia huduma.
Kuna maduka ya dawa mbadala dawa za asili,wengi Wenye maduka Hawa,hawana elimu ya tiba mbadala,pia wangetizamwa kwa jicho LA tatu,afya ni muhimu,wanawapa watu dawa bila vipimo na maelekezo ya kubahatisha,wako kibiashara zaidi,sio kuwasaidia wagonjwa.Dr bila digree. ujinga na wizi. wanachukua dawa za hospitali zikiwe ARV s na kuchanganya na miti shamba. ubatili mtupu
Kuhusiana na hili la kufungiwa kwa muda, mwenye ufahamu kwa UNDANI SANA juu ya kitengo hiki TFDA atujuze, hata pamoja na kwamba kazi yake ni kuthibiti but what's extra authority about natural remedies?
Ambayo weeengi naona tunaikataa kwamba si dawa salama na ina garama kubwa?
ni kweli, sio msabato ni mwislam anaitwa Juma (J). yeye nilimsikia kwenye tv anasema amesoma degree ya kwanza hapa nchini na ya pili alisoma ya mambo ya kienyeji india. nilimsikia kwa masikio yangu kwenye tv anasema hivyo. alisema amesomea udaktari wa kawaida, akamaliza akaenda kusomea huu wa mimea, hivyo anajua vitu vyote na ni dr halisi. ninyi mnaposema alikuwa anauza mitumba, siamini kwasababu anapoelezea utakuta ni mtu ambaye at least amefika form four au form six and above. pamoja na kwamba, anapoelezea mambo mengine utakuta ni ya layman, si ya daktari bingwa.
all in all, amekusanya hela nyingi sana, ni bilionea, hata wakifunga wanajisumbua kwasababu ameshapata hela nyingi, ataweza kuwekeza kwingine. kama kuchuma ameshachuma za kutosha. jamaa ndi mganga wa tiba asili aliyejimarisha kuliko wote na aliyepata hela nyingi kuliko wote. pale appointments unaenda siku mbili kabla, siku nyingine zote hizi watu wameshabook, na dawa zake ni garmaa sana. malaki. miaka yote hii kila siku amekuwa akikusanya mamiilioni. zaidi ya yote, hawa tfda wanaompinga, huyo jamaa ana hela, atawapa hela kesho tu hapa kituo kitafunguliwa na ataendelea kutoa dawa.
rai yangu ni kwamba, kama kweli hawa watu wawe ni wasababu au waislam, kama wanatoa dawa wakati hawajasomea udaktari, wakamatwe wafungwe kabisa. mke wangu alishawahi kupata tatizo fulani, kaenda sana kwa hao wasababu, kuna msabato mmoja alikuwa kule tabata alikufa tayari, wife alienda sana na kwa hao wote wanaolisha watu malimao na machungwa mia, matokeo yake nilitoa sana hela hakuna kupona, waifu alikuja kuponea kwenye maombi ya kanisani hadi leo mzima. hao majamaa ni waongo ajabu, na wanatisha watu kwa maelezo ya magonjwa wanawapa matumaini ya uongo na kuwapiga hela na kwasababu watu wako kwenye shida mfano ya kupata watoto etc, anaweza kutoa hela yeyote na kwasababu wao wanajua kupata watoto na matatizo ya wanawake ndio mtu anaweza kutoa chochote, basi wanashikilia hapohapo na kuchuma hela za watu.
Hahaha sawa mwalimu wa Kiswahili, nifundishe
Vyovyote tu utakavyotaka mwalimu. Yeah nimeshanunua daftari la mistari mikubwa na midogoUnaaandika lakini? Acha kulialia, kwani wee umejipangaje?
walewale madokta wa kisabato walinipa dawa niliharisha siwezi sahau!
Sikutarajia kituo kama hiki kufungiwa sababu dk Mwaka amekuwa akijatangaza sana kwenye radio na tv na niliamini kituo kina vigezo vyote vya kitaalamu vinavyotakiwa
Afadhali waziri wa afya kidogo umefanya kazi binafsi mimi na familia yangu t7nakupongeza hongera sana waziri wa afya,huyo jamaa ni tapeli wa kufa mtu hafai hata kidogo kisifungiwe tu kifutwe kabisa!
Wizara ya Afya imekifunga kwa mda usiojulikana kituo cha Fore plan Clinic kilichopo ilala Bungoni. Kituo hiki kinamilikiwa na Dr J.J Mwaka mtaalam wa magonjwa ya kinamama akitibu kwa kutumia tiba mbadala.
Wizara imesema kituo hakijatimiza vigezo na masharti yanayotakiwa na serikali ikiwemo kutokuwa na wataalam wenye sifa na elimu stahiki.
Dr J.J Mwaka amekuwa akionyesha kazi nzuri za kituo chake kwenye vyombo vya habari ikiwemo kutibu ugumba na upungufu wa nguvu za aina mbalimbali.
Watu wengi wamekua wakifurahia sana tiba hii mbadala itolewayo na Dr Mwaka na mpaka kituo kinafungwa wagonjwa wengi walikua wakisubilia huduma.
mkuu ww acha tu.😀😀😀😀 kama nakuona vile ulivokimbiza
Sina shaka we mleta uzi ndio Mwaka mwenyewe maana ni dr bingwa wa kujipiga prömo. Jamaa amekariri kila vipindi vyake utasikia homonal imbalance na UTI. Hata ukiumwa kichwa atakwambia homon imbalansi.