Kitabu cha "dr. Slaa mjenzi makini wa taifa" kinawakawaka channel ten leo jioni

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Channel ten leo jioni imeonyesha uzinduzi wa kitabu kiitwacho "Dr. Slaa mjenzi makini wa Taifa."

Kitabu hicho kinazungumzia mchango wa Dr. Slaa katika ujenzi wa taifa hili changa.

Utoaji wa vitabu vya aina ya "memoirs" ni jambo la kawaida sana ikumbukwe Barrack Obama alitoa kitabu cha "Dreams from My father" na "The Audacious of Hope" ambavyo vilisaidia sana kumweka kwenye chati katika chaguzi za nchi hiyo.


Kwetu hapa watu hawana tabia ya kujisomea vitabu, hivyo ufanisi wake kwenye kampeni hii unatarajiwa kuwa ni kiduchu ukilinganisha na mchango mkubwa utakaojitokeza kwenye kampeni zake ambazo zinakwenda vizuri mno kuliko matarajio ya wengi.

Kama kitabu hicho kitawekwa kwenye internet basi wengi tutaweza kukisoma kabla ya uchaguzi au kama watakisambaza mapema mikoani itasaidia kwa haswa sisi wapashaji watu wengine habari.

Kitabu hicho kimehaririwa na mwandishi wa siku nyingi Bw. Henri Muhanika.

Mara nitakapokisoma kama itakuwa kabla ya uchaguzi nitakichambua kwa manufaa ya wale ambao hawataweza kukisoma kwa sababu moja au nyingine
 
Jk Hana hat a mawazo ya kuandika kitabu..nimemuona mpaka kitambi kimeyeyuka
 
Big up Dr wa ukweli. Tunataka kiongozi wa kutuongoza siyo wa kujineemesha kama and family + CCM.
 
Kuna kitabu kingine kuhusu Dr Slaa nimekinunua kina title ''Mambo usioyajua kuhusu Dr Slaa'' kinaelezea maisha Dr Slaa, na michango yake katika Taifa.
 
Kuna kitabu kingine kuhusu Dr Slaa nimekinunua kina title ''Mambo usioyajua kuhusu Dr Slaa'' kinaelezea maisha Dr Slaa, na michango yake katika Taifa.

kitakuwa na majibu ya maswali magumu, kitolewe haraka wakati huu kuelekea okt 31 ili zile 12% ziongezeke hadi 7%
 
nimekisikia bbc leo jioni inaonekana ni kitabu kizuri, jk na wabunge wao wameandika vitabu pia kuelezea litania za mafanikio ikiwamo kujenga minara ya simu
 
Kisambazwe mikoani haraka sana, niwanunulie ndugu zangu walioko vijijini.
 
ccm na redet yao wameumbuka.wanajibaraguza eti wamepunguziwa asilimia naona hela waliyotoa haikutosha kuongeza zaidi ya hapo.kama wanataka aslimia 100 waongeze hela kwani kwa ccm nini kinashindikana kwa rushwa hata kama wanataka 200% ni hela yao tu mbona Miraji anafungu la kutosha?

tuharakishiwe hicho kitabu ili tuweze kupiga kampeni za kisomi kama za Obama.
 
WanaJF tunaomba mzalendo apost soft kopi kwenye mtandao. Jamani tunakitaka sana. Au tuambiwe kinapatikana wapi. Pia mwenye complete kopi ya ilani ya chadema anisaidie mana mi nina summary peke ake.
 
NO NO NO wazalendo wakinunue, waongeze
na watoe moyo kwa mwandishi, ni wandishi wachache hawa wasiojipendekeza kwa wakubwa waungwe mkono, naenda kukitafuta nitanunua copy nyingi niwagawie
na wengine wasiotaka kuelewa upepo wa mabadiliko. This is similar to audacity of hope. Pls no pyrating to this book
 
NYOTA ya mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, imeendelea kung’ara baada ya mmoja wa wasomi maarufu nchini, Henry Muhanika, kuzindua kitabu kinachoeleza maisha ya mgombea huyo. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kitabu hicho, mjini Dar es Salaam jana, mtunzi wa kitabu cha “Dk. Willibrod Slaa, Mjenzi Makini wa Taifa”, Henry Muhanika, alisema kama viongozi wakiweka misingi imara na kuwa waadilifu michango yao itaendelea kuthaminiwa.
Alisema, kuandika kitabu hicho, kumetokana na msukumo katika mchango wake kwa taifa; kusimamia maslahi ya Watanzania na kuchukia vitendo vya ufisadi vinavyolitafuna taifa.
Alisema kitabu cha Dk. Slaa, kimejikita zaidi katika mambo ambayo ameyafanya katika nyanja zote kwa uadilifu na uwazi kwa wananchi katika kusimamia maendeleo na kupambana na vita dhidi ya umaskini.
Alisema kitabu hicho, kamwe hakikuzinduliwa kwa ajili ya kumsadia Dk. Slaa wakati huu wa kampeni za uchaguzi mkuu.
Alisema kitabu hicho ni mfululizo wa vitabu ambavyo ataviandika kwa viongozi waliofanya vizuri katika nyanja mbalimbali kwa faida ya Watanzania na sio kwa maslahi binafsi.
Alisema akiwa mbunge wa Karatu, aliweza kutatua kero za maji na elimu ambazo zilikuwa changamoto kwa wananchi wake kuweza kujikomboa.
“Kuandika kitabu hicho sio kila mtu ataandikwa, tutaangalia uadilifu wake kwa wananchi na kuamua kuandika na haombi mtu aandikwe katika mwendelezo huu wa vitabu vya kuwakumbuka kwa michango yao,” alisema Muhanika.
Alisema katika sera zake, anaonekana kutaka kujenga Tanzania yenye mabadiliko ambayo yatawakomboa wananchi kutoka dimbwi la umaskini ambao umewafanya kuwa tegemezi.
 
God Bless you Professor Mhanika, ueanika ukweli usiopingika, tulidhani wetu alikataa kununua nyba za serikali ya 3 kumbe naye ni walewale, tunakutakia maisha mema Professor, mwaka huu hapatoshi hatudanganyaikiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiimpaka magogoni, hatutki kulipiza kisasi ila ubadili mfumo dume wa ccm na kamba za minazi tuweke huru waliofungwa na kupapa afya bora na eliu bure kwa TZ wote.
 
vipo posta mpya na kariakoo nimechukua kopi kadhaa na vinakwenda kwa kasi sana, mnunuzi nilimdadisi akasema vinatoka vingi sana na wana mawasiliano na dalali wa vitabu vikiisha wanaletewa. Nilichoshihudia ni bango la CCM AMESHAURIWA ATUPE MBALI KAMA ANATAKA KUENDELEA NA KAZI YAKE VEMA MAANA WANAONA KICHEFUCHEFU WAKIONA RANGI YA KIJANI NA PICHA YA JK. Wajumbe kitabu ni sh 3,500 tshs tu kanunue NO PYRATES
 
Safi sana profuu wangu.wewe ndo unajua nini maana ya elimu..sio Yale majizi ya redet
 
Back
Top Bottom