Kisiwa cha Ukara (Ukara Island)

Kisiwa cha Ukara (Ukara Island)

mweeh basi tena mamba huyu anayeishi majini ama mamba gani?
Mamba huyo anayeishi majini.
Wakara ni watu poa sana, waliosoma wako njema sana kichwani, hasa kwenye science. Hizi myth za uchawi ni majo a jamii ya zamani, japo yanaweza kuwepo kwa uchache siku hizi. Zamani jamii nyingi zilikuwa na uchawi wa hatari, ndio maana unaweza kuta watu wakipata maendeleo kidogo wanakimbia Ukara na hawarudi kujenga kwao wakiogopa ndumba.
 
Ahsante sana ndugu kwa kunipeleka nansio coz toka nitoke huko almost 30 years cjakanyaga huko shukrani sana pia nitafurahi zaidi ukituletea na picha za ukara
Nyehunge wanaendelea rahisisha safari ya Nansio. Hiyo ni VIP Class ya ferry yao mpya.
Nyehunge VIP Class-1.jpg
 
PAZURI HUKO SANA. WAPI.
1. BWISYA.
2. NYANG'OMBE.
3. KOME.
4. CHIBASI.
5. MALELEMA (CITY OF UKARA).
6. BUKUNGU.
7. BUKIKO.
8 NYAMANGA.

I WILL BACK THERE SOON.
Mkuu umesahau na Kisiwa cha"GHANA"
 
Zamani miaka ya 80 walikuwa wanatisha kwa uchawi bt nowadays hakuna kitu kama hicho kama wapo basi ni wachache nakumbuka maza alikuwa akienda likizo cku ya kuondoka alikuwa haagi anakwambia ukiaga tu kuwa unaondoka jua watarudisha maiti yako
Vipi kuhusu dancing stones kama mleta mada alivyosema, ni kweli hiyo?
 
Ni safari ya masaa mangapi kutoka Mwanza?
masaa 3 kutoka Mwanza hadi Nansio, Ukerewe. nauli ni elfu 6, elfu 7 na elfu 15. hii ni ferry ya mtu binafsi, maarufu kama Nyehunge.
Tax kutoka Nansio hadi Bugorola ni sh 2,500.00 kama mtaunganishwa watu watano hadi sita au sh 15,000 ukiichukua mwenyewe. inatumia roughly 20 minutes.
Kutoka Bugorola hadi Bwisya,Ukara ni mwendo wa saa moja, nauli sh 800. hii ni ferry ya serikali.
 
masaa 3 kutoka Mwanza hadi Nansio, Ukerewe. nauli ni elfu 6, elfu 7 na elfu 15. hii ni ferry ya mtu binafsi, maarufu kama Nyehunge.
Tax kutoka Nansio hadi Bugorola ni sh 2,500.00 kama mtaunganishwa watu watano hadi sita au sh 15,000 ukiichukua mwenyewe. inatumia roughly 20 minutes.
Kutoka Bugorola hadi Bwisya,Ukara ni mwendo wa saa moja, nauli sh 800. hii ni ferry ya serikali.
Nani mmiliki wa hiyo ferry binafsi?
 
Mkuu huko ndio kwetu ukifika ulizia kijiji kinaitwa nyamanga
Pale karibu na uwanja wa mpira kuna soko la samaki , zahanati pia kuna kanisa la kihistoria la roman ..babu yangu alikuwa ni padre hapo anaitwa father bwile alifariki miaka miwili iliyopita. Ndiye kwenye ukoo wetu mungu alimjalia kupata daraja takatifu..
 
Nyerere alishawahi kupataja huko katika hotuba yake moja.

Alikuwa anasema Tanzania hatuchagui rais kwa ukabila. Hata Mkara anaweza kuwa rais. Hata watu wakiuliza "lakini huyu mbona Mkara?" (inaonekana kabila linadharaulika sana) Nyerere akasema kama ana sifa anakuwa rais tu.

Kwa nini Wakara wanadharaulika sana?
 
Nimefika kwenye hilo jiwe, ni usanii mtupu, hakuna kitu kinachoitwa miujiza. Jiwe hilo linacheza kwa sababu za kisanyansi na sio miujiza. Kwa ufipa wangu nilitaka niwachallenge kwa sayansi ya ufipa, nikakuta watupu mnoooo!
Position ya hilo jiwe ni sababu kuu ya lenyewe kucheza...
Jiwe lenyewe lazima lisukumwe ndipo licheze!
Sijui kwa nini watu wanaaminishwa tofauti na wanakubali!
Naomba unijibu kwa nini wale wazungu ambao walifunga hilo jiwe na minyororo lianguke ziwani walishindwa na mnyororo ulikatika.
 
Back
Top Bottom