Kisiwa cha Ukara (Ukara Island)

Kisiwa cha Ukara (Ukara Island)

Jamaa anaelichezesha huwa hataki msimame upande wake... Na watu kwa vile wameaminishwa ni miujiza, hukubali bila kuhoji.. Bahati mbaya wengine tumetokea kwenye Jamii ya watenda miujiza....kwetu kamati za ufundi ni kama Wacongo na muziki!!
hahahahhaha, ati wacongo kwa music
 
Jamaa anaelichezesha huwa hataki msimame upande wake... Na watu kwa vile wameaminishwa ni miujiza, hukubali bila kuhoji.. Bahati mbaya wengine tumetokea kwenye Jamii ya watenda miujiza....kwetu kamati za ufundi ni kama Wacongo na muziki!!
wewe utakuwa mtu wa 3 kusema hivyo kuwa ni usanii tu ule,
 
Wakerewe hawaongei kikara wao huongea kikerewe ambayo lugha yao inaweza kufanana na lugha ya wahaya. Mfano ,kwa kihaya wanasema wabhonaki na wakerewe wanasema wabhokiha. Kwa kiswahili (Umeona nini)
 
Kabila la wakara waishio ukara ni kabila linalodharauliwa kuliko makabila yote Tanzania

Sidhani kama kuna kiongozi wa nchi hii aliwahi kutoka huko...hata kama ametoka huko hatajitambulisha kama Mkara.
Mongela je?, msekwa je?
 
Jamaa anaelichezesha huwa hataki msimame upande wake... Na watu kwa vile wameaminishwa ni miujiza, hukubali bila kuhoji.. Bahati mbaya wengine tumetokea kwenye Jamii ya watenda miujiza....kwetu kamati za ufundi ni kama Wacongo na muziki!!
Aisee!
 
Dah ukaraaa? Nilipataga demu kule. Chumba guest self kabisa buku tano tu
bado guest chache zinachaji elfu tano self contained rooms, guest ambazo hazijaunganishwa na umeme bado, na sasa kuna guest mpya chumba ni elfu kumi na tano, ni nzuri haswa kwa level ya Ukara, ina vyumba vikubwa, chini tiles, chooni tiles, imeungwa na umeme. sasa ukiwa Ukara huwezi ona tofauti na mjini.
 
ukara ndo naisikia leo.. endelea kutujuza kisiwa kilivyo.hali ya uchumi
Hali ya uchumi Ukara sio nzuri sana, uvuvi umekuwa wa shida siku hizi, wengi walipiga ela sana wakati samaki wako wengi majini, wakatimkia kujenga mijini, sasa Ukara haikuendelezwa wakati huo, bado uvuvi upo ila sio ule wakufanya dreams come true, upo uvuvi wa kuendesha maisha ya watu kila siku.
Kijiji cha Malelema ndio kinasifika kwa uvuvi katika kisiwa cha Ukara.
 
Kabila la wakara waishio ukara ni kabila linalodharauliwa kuliko makabila yote Tanzania

Sidhani kama kuna kiongozi wa nchi hii aliwahi kutoka huko...hata kama ametoka huko hatajitambulisha kama Mkara.
Sina hakika na hilo, ila mbunge wa sasa wa Ukerewe anatokea Ukara, ni mbunge toka CHADEMA, nashangaa kwa nini yupo kimya sana bungeni.
 
Wewe kuna kitu unakitafuta sio kuja hapa na vijistori vya "Ukara".
Sema unachotafuta usaidiwe kama ni Stori za yule Mkuu pale, Shauri zako!

"KISIWA CHA UKARA"
Mkuu yupi tena, nipe intro nikifika nitafute stori za huyo mkuu nije kuweka hapa kama zinafaa kuwekwa hapa.
 
PAZURI HUKO SANA. WAPI.
1. BWISYA.
2. NYANG'OMBE.
3. KOME.
4. CHIBASI.
5. MALELEMA (CITY OF UKARA).
6. BUKUNGU.
7. BUKIKO.
8 NYAMANGA.

I WILL BACK THERE SOON.
Nimegundua Wakerewe na Wakara ni wengi sana Jf, hata wewe?
 
umetembelea visiwa vipi na vipi mkuu,
Nishaenda Irugwa (Ukerewe), Rukuba (Musoma Rural), Maisome (Buchosa, zamani Sengerema), Kerebe (Muleba), Goziba (Muleba), Bumbure/Mahaiga (Muleba), Ikuza/Kasenyi (Muleba) na Iramba/Murumo (Muleba).

katika visiwa vyote hivyo, Goziba, Kerebe na Iramba vina mandhari nzuri sana.
 
Huyo mtalii akifika Ukara, ajaribu kufanya utafiti kuhusu kabila hili na akiweza ayalinganishe maisha yao na Wahadzabe wanaoishi maisha ya Ujima, ya kutafuta asali, wadudu na kuwinda wanyama wadogo wadogo, na pia maisha ya kuhamahama.
Wakara wameendelea mkuu, huwezi wafananisha na makabila kama ya wahadzabe.
 
Mkuu huko ndio kwetu ukifika ulizia kijiji kinaitwa nyamanga
Pia ufike pahala panaitwa Kome, ns ufikie G/house inaitwa Parachichi hapo Bwisha
Leo nasafiri kwenda katika kisiwa cha Ukara, nmeona ni vyema ningewajuza kuhusu kisiwa hiki kilichopo ndani ya mipaka ya Tanzania. Kabla sijaja Mwanza kikazi nlikuwa nasikia kuhusu kisiwa cha Ukerewe tu, kutokana na kazi yangu nimeweza fika katika visiwa nane tofuti na Ukerewe vyote vikiwa ndani ya mipaka ya Tanzania. Hivyo leo tutaiongelea Ukara tu.

Ukara ni kisiwa cha pili kwa ukubwa ndani ya ziwa Victoria kwa upande wa Tanzania, kisiwa kinachoongoza kwa ukubwa ndani ya ziwa ni kisiwa cha Ukerewe.

Wenyeji wa kisiwa cha Ukara wanaitwa Wakara, hawa wanaongea lugha inayoingiliana na wajita wa Musoma, pia wakerewe huongea lugha hiyo hiyo.

Kisiwa cha Ukara kina mawe yaliyopachikwa jina la "the dancing stones", kwamba mawe yanayocheza. Sijawahi kwenda yatembelea bado, japo ntajitahidi fika huko kwa siku za usoni. Pia inasemekana kuna mti ambao majani yake yakiingia ndani ya ziwa, yakitoka anatoka mambo na sio majani tena.

Kufika Ukara kwa kutokea Mwanza inakubidi upande ferry kutoka Mwanza hadi Nansio Ukerewe, baada ya hapo utapanda Tax kutoka Nansio hadi Bugorora, kutoka Bugorora utapanda tena ferry hadi Ukara, Ferry inafikia katika kijiji cha Bwisya.

Ntaendelea wajusa safari ya Ukara step kwa step.
View attachment 478574
 
Niliwahi kufika hapa. Eneo la kisiwa biashara ya ngono inafanyika Kama biashara ya pipi.
Katika kisiwa cha Ukara, nadhani ni malelema tu ndio kutakuwa na ngono zembe, huko kwingine sidhani kabisa.
Kwa ujumla vijiji/visiwa vinavyojihusisha na uvuvi, pombe na ngono ndio habari yao, ukiona makreti ya bia yanayoingizwa kila siku na idadi ya watu utashangaa. malaya walioshindikana mijini huko ndio machaka yao, yani wavuvi wanaondoka na ukimwi hatari.
 
10312639_10152462565319605_6114804141846738089_n.jpg
 
Mongela ni Mkerewe wa murutunguru, msekwa ni mluli na sio mjita wala mkerewe, ila kakulia ukerewe, na kasomea akiwa ukerewe, ila sio mkerewe
Nyumba ya Mongela ipo barabarani tu, katumia interlocking bricks, imetoka poa sana, kanyanyua na bendera ya chama chake. Nyumba ya Msekwa sijawahi iona, ila naambiwa ndio nyumba inayotumiwa kama kulaza maraisi wakifika Ukerewe.
 
Back
Top Bottom