Kisbo imepitwa hapa mapema tu!

Kisbo imepitwa hapa mapema tu!

Nauli kutoka Mwanza hadi dar Kwa basi ni elfu 60, Chakula njiani 20, tax kufika standi 10, ( masaa 14hrs road) ukishuka ubungo either ulale gest 30000 au uchukue tax elf 30, kama kuna ndugu Wa kukupokea (hasara na usumbufu Wa kukufuata stand tumpe naye elf 30) haya uchofu Wa safari utakupasa upumzike ambapo hasara ya kulala siku nzima inayofuata elf 30 n.k let's say imekucost laki mbili kupanda bus,
Ungefanya mipango ya FASTJET 150000 /= AU Ungefanya mpango Wa precision Air 360000/= Ungefika chap na Kwa haraka ukaendeleza majukumu yako ya kuingiza Pesa nyingine ;
Mi ninafikiri siku nyingine panda ndege kupunguza gharama ( Note; gharama zingine hazionekani direct)
SAFARI ZA BUS MASAFA MALEFU IFIKE MAHALI TUACHANE NAZO zimepitwa na wakati ( Tutumie bus safar fupi fupi)
==========================
NI SAWA NA KUNUNUA KIWANJA KWENYE KILIMA AU BONDENI 2MIL HALAFU MSINGI WA NYUMBA IKAKUCOST 15MIL pamoja risk za Maji na bomoabomoa! Wakati kuna viwanja flat saafi vinauzwa 8mil na mzingi only 3mil na ni sehemu salama


Wote hatunufaiki na utawala huu kama wewe.

Hapo kwenye tax 30,000 weka 400 daladala ,chakula 30,000 weka 5000 , gesti 30,000 weka 10,000 .

Mwisho ndege tunaogopa viberiti vyetu vya moyo.

Acha waswahili tufurahie ligi ya mabus njiani ,ndo raha yake ya kututolea stress ,mtasema ajali hata ndege zinapata ajali au unaweza fika airport ukapanda tax yako na mkapata ajali vile vile .

Vipi route ya Dar to Mbeya bado Newforce wanakimbiza?
 
cku hizi kuna mghamba ya MWZ_Dar?? Najua za arusha na moshi na wao mnaachania Singida wao wanaelekea kateshi_Bahati nyie mnasonga Dom
Sijamaanisha inaenda dar. Sina uhakika km ipo ya kwenda. Nilichokuwa namaanisha ukimbiaji wa gari haijalishi inaenda dar au la km ni njia moja hata km inaishia shinyanga, itawaacha mbali. Kuna kipind nilipanda kutoka singida to mwanza.
 
Tarehe za kufunga mahesabu ya mwaka unalilia gari inayosindikizwa na ziraili, mbona ndege zipo
 
Jamani nilishauriwa humuhumu JF ili nifike dar kutoka Mwanza kwa siku moja nipande basi la kisbo, wanaJF wakasisitiza hakuna basi linalokimbia kama Kisbo, nami kweli nikakata tiketi ya hilo basi.

Sasa ajabu leo tumetoka Nyegezi stand tumevuka tu Buhongwa Kisbo ikapitwa basi fulani linaitwa master, sasa nimeanza kupata wasiwasi kama kweli nitafika leo make uongo umeanza kudhihirika.
Mkuu kama vipi piga chini hilo subiri Mohamed Trans au Hood kama lipo! Hapo Dar kufika ni keshokutwa kwa raha zako yaani hata rushwa hawatoi wale jamaa na ujiandae kufaulishwa muda wowote kabla ya kufika sekenke. Bon voyage
 
Kifo kinakunyemelea kwa ushabiki, mwambie dereva aongeze mafuta, halafu mpenyezee konyagi ya kupima kwenye maji ya kilimanjaro
 
Back
Top Bottom