Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,895
Kwema Wakuu!
Kisa cha Lowasa na Rafikiake na usaliti mkubwa uliotokea ni kisa kitakachoishi kwenye taifa hili kwa karne na karne.
Huwaga visa vya usaliti na mapenzi vinadumu sana. Historia na Historia zitapita lakini visa vya usaliti havipiti kwani ni visa vya maisha.
Kisa cha Yesu na Yuda ni maarufu na kitaendelea kudumu miaka na miaka kwa sababu kinahusisha. Usaliti.
Kisa cha Adamu na Hawa dhidi ya kumsaliti Mungu kipo mpaka hivi Leo.
Kisa cha Samsoni na Delilah halikadhalika.
Legacy pekee ambayo mwanadamu ataacha ni kuishi kwa wema na Upendo na watu.
Madaraja, mahospitali, viwanda, na miundombinu yoyote unayoiona hivi leo haijawahi na haitakuja kuwa Legacy na kumbukumbu ya maana kwa sababu miaka miambili ijayo vyote vitakuwa vimepitwa na wakati. Vitabomolewa na kujengwa upya na vitaitwa kwa majina mengine na kutumiwa na wahusika wengine.
Visa vya usaliti vinadumu sana kwa sababu vinahusu nafsi na maumivu ya mwanadamu.
Unapofanya usaliti mkubwa sio tuu utamuumiza yule uliyemsaliti bali utaumiza mioyo ya wanadamu wengine ambao hata ambao hawajawahi kukuona. Vile kusikia stori ya usaliti wenu jina lako linakuwa limeharibika.
Utakuwa na jina moja tuu, alikuwa mtu mbaya, msaliti.
Miaka ijayo tukiwa hatupo, kisa hiki cha Lowasa na Rafikiake kitaigizwa na vijana na zama hizo. Sio ajabu hata majina ya waigizaji yatakayotumika yakawa majina ya wahusika wa sasa waliokatika maisha yetu.
Ukishakuwa msaliti tayari wewe ni mtu aliyepata hasara kubwa ya maisha. Hasa unapomsaliti mtu wako wa karibu aliyekuamini na aliyekupenda.
Tatizo la usaliti Mkubwa ni ngumu sana kuomba msamaha.
Ni kama shetani na Mungu. Usaliti Mkubwa unajikuta unaamua tuu kuwa msaliti na kiburi cha kushindwa kuomba toba kinakuwa ndio maisha yako.
Jumapili njema
Kisa cha Lowasa na Rafikiake na usaliti mkubwa uliotokea ni kisa kitakachoishi kwenye taifa hili kwa karne na karne.
Huwaga visa vya usaliti na mapenzi vinadumu sana. Historia na Historia zitapita lakini visa vya usaliti havipiti kwani ni visa vya maisha.
Kisa cha Yesu na Yuda ni maarufu na kitaendelea kudumu miaka na miaka kwa sababu kinahusisha. Usaliti.
Kisa cha Adamu na Hawa dhidi ya kumsaliti Mungu kipo mpaka hivi Leo.
Kisa cha Samsoni na Delilah halikadhalika.
Legacy pekee ambayo mwanadamu ataacha ni kuishi kwa wema na Upendo na watu.
Madaraja, mahospitali, viwanda, na miundombinu yoyote unayoiona hivi leo haijawahi na haitakuja kuwa Legacy na kumbukumbu ya maana kwa sababu miaka miambili ijayo vyote vitakuwa vimepitwa na wakati. Vitabomolewa na kujengwa upya na vitaitwa kwa majina mengine na kutumiwa na wahusika wengine.
Visa vya usaliti vinadumu sana kwa sababu vinahusu nafsi na maumivu ya mwanadamu.
Unapofanya usaliti mkubwa sio tuu utamuumiza yule uliyemsaliti bali utaumiza mioyo ya wanadamu wengine ambao hata ambao hawajawahi kukuona. Vile kusikia stori ya usaliti wenu jina lako linakuwa limeharibika.
Utakuwa na jina moja tuu, alikuwa mtu mbaya, msaliti.
Miaka ijayo tukiwa hatupo, kisa hiki cha Lowasa na Rafikiake kitaigizwa na vijana na zama hizo. Sio ajabu hata majina ya waigizaji yatakayotumika yakawa majina ya wahusika wa sasa waliokatika maisha yetu.
Ukishakuwa msaliti tayari wewe ni mtu aliyepata hasara kubwa ya maisha. Hasa unapomsaliti mtu wako wa karibu aliyekuamini na aliyekupenda.
Tatizo la usaliti Mkubwa ni ngumu sana kuomba msamaha.
Ni kama shetani na Mungu. Usaliti Mkubwa unajikuta unaamua tuu kuwa msaliti na kiburi cha kushindwa kuomba toba kinakuwa ndio maisha yako.
Jumapili njema