hearly
JF-Expert Member
- Jun 19, 2014
- 51,629
- 74,037
nimeshangaa mnooo baada ya kuona umepata like moja...wakati umetoa hoja yenye mashiko mnooo"" aisee..kweli maisha bila ya unafiki hayaendi ""Wasema atheist ni yule asiyejua lolote kumhusu Mungu ama miunngu. Lakini ili tupate tofauti halisi ya nonbeliever na atheist ni lazima tuangalie engo mbalimbali, kama vile; Elimu ya mtu, jamii alimozaliwa, uwezo wa kiuchumi wa mtu au taifa atakapo, upatikanaji wa machapisho ya kidini n.k.
Sasa ukija kuangalia vigezo hivyo utagundua kua kuna watu wanaamini uwepo wa Mungu pasipo kuwa na elimu yoyote kumhusu Mungu na hawana hoja imara za kutetea uwepo wa Mungu.
Hawa ni wale wanaoishi chini ya umaskini mkubwa katika maeneo maskini ambayo wakati fulani yaliwahi kufikiwa na waeneza dini ambao walipata wafuasi fulani lakini baadaye mawasiliano yale yakakata hivyo wafuasi waandamizi wakakosa elimu ya kile walichoridhi toka kwa wazazi wao, na wao kubaki tu na majina yanayoashiria dini ile hivyo kuendelea kuitwa waamini.
Vilevile utaona pia kuna watu wamezaliwa kwenye mataifa ya kidini ambamo dini ni sehemu ya maisha katika jamii husika, lakini wao hawaamini katika hizo dini bila kujali kama walipata elimu ya dini ama la na hawapingani na yeyote kumhusu Mungu. Hivyo wanasalia kuitwa waamini pasipo wao kuamini.
Pia kuna wengine wamesoma kanuni na miongozo mbalimbali ya kidini, lakini wao wakaichukulia kama vitabu na machapisho mengine ya kutoa elimu wakashika maarifa yaliyomo na wasifuate njia za kuabudu za kundi lile. Mfano mzuri ni Japan nchi inayoongoza kuwa na maatheist wengi lakini bado hua wanasoma authoritative books ambazo zimeandaliwa na watu wa dini kwa lengo la kuwaelimisha waamini wao.
Mtazamo mwingine dhidi ya nonbeliever na atheist waweza kuangaliwa kupitia wale wanaojiita waamini ama wenye dini. Kwa miaka mingi kumekua na matamshi kutoka kundi fulani la wanaojiita wenye dini kuwaita wafuasi wa kundi jingine kama wasioamini (nonbelievers) kwa sababu tu, wanatofautiana katika imani zao kumwelekea Mungu. Na hii inatokana na ubinafsi wa kila mwenye dini kuamini kuwa dini yake ni sahihi kiliko mwingine.
Hitimisho, kwa hayo machache waweza kuona namna ilivyo vigumu kupata kategoria rahisi za kuwatofautisha nonbelievers na maaatheists. Kwa sababu dunia ya sasa yenye teknologia bora kabisa ya kewezesha watu kipata machapisho mbalimbali yahusuyo dini na miongozo yake imekua ikishuhudia kuongezeka kwa kasi kwa kundi la wale wanaoitwa wakana Mungu.
hapa kakimbia